11-23-2021, 07:35 AM
SWALI: Onesha viunganishi katika sentensi zifuatazo na taja maneno na vipashio vinavyoungwa.
(a) Mama na mwanawe wameondoka
(b) Baba anachimba mashimo na mama anapanda mahindi
© Sitaongea naye hadi utakaporudi
(d) Mlipoondoka tu, mama yake alikuja kumtafuta
(e) Watoto waliofaulu wamechaguliwa kwenda sekondari
(f) Aliadhibiwa kwa sababu hana heshima.
Jaribu kujipima kwa kujibu maswali hayo na ukipata ugumu wasiliana nami kwa njia zilizopo.
Mwl Maeda