MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: KANUNI ZA HISABATI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: KANUNI ZA HISABATI
#1
1. Kalamu yangu nashika, kuelezea kanuni,
Hisabati kuishika, tuweze kuwa makini,
Eneo mzingo fika, nataka mufahamuni,
Kanuni kuelezea, za maumbo ya hesabu.
2. Tukianza na mraba, Duara mstatili,
Pembetatu msambamba, tuweze kuyajadili,
Na trapeza si haba, la sita si la awali,
Za maumbo ya hesabu, kanuni kuelezea.
3. Awali hapa MRABA, eneo lake sikia,
Pande mara pande kiba, jibu utajipatia,
Mzingo wake mraba, pande mara nne pia,
Kanuni kuelezea, za maumbo ya hesabu.
4. Pili ni MSTATILI, Tujue eneo hili,
Refu mara pana jali, ni rahisi afadhali,
Pana ngeza refu pili, uzidishe mara mbili,
Mzingo wake hakika, hapo unamalizia.
5. PEMBETATU pia limo, tusije kulisahau,
Nusu uzidishe kimo, zidisha kitako dau,
Utapata vyema humo, eneo sio nahau,
Kanuni za hisabati, majibu kujipatia.
6. Tuende mzingo huo, kanuni ipi jamani,
Tajumlisha vipimo, vilivyo umboni,
Ei, B, na C kikomo, jumlisha vyote hani,
Majibu kujipatia, kanuni za hisabati.
7. MSAMBAMBA eneo lake, ni urefu mara kimo,
Muhimu mzingo wake, kanuni kuijuamo,
Refu ngeza kimo chake, uzidishe kwa mbilimo,
Kanuni za hisabati, majibu kujipatia.
8. TRAPEZA fuatilia, eneo kukujulisha,
Nusu mabano sikia, A na B jumlisha,
Kisha mabano wekea, pia kimo kuzidisha,
Majibu kujipatia, kanuni za hisabati.
9. Mzingo wa Trapeza, tunakuja kukujuza,
A, B, C, na D kuweza, hizo pamoja ongeza,
Jumlisha ni ongeza, hilo muhimu kuwaza,
Kanuni za hisabati, majibu kujipatia,
10. Sasa DUARA kanuni, Ya eneo angalia,
Chukua pai jamani, kipenyo kuzidishia,
Zidisha kwa umakini, fanya kipenyo skwea,
Kanuni za hisabati, majibu kujipatia.
11. Duara mzingo wake, sio mgumu jamani,
Sikiliza kanuni yake, pai mara kipenyoni,
Naomba fanya makeke, kujikumbusha kanuni,
Kanuni za hisabati, Majibu kujipatia.
12. Anaomba msamaha, iwapo amekosea,
Mwalimu wetu Twaha, Shairi katutungia,
Kanuni kwa ufasaha, kuweza kujifunzia,
Majibu kujipatia, Kanuni za hisabati.
MANENO MBADALA
1. Ngeza = Kujumlisha
2. Pande= upande
3. Refu= urefu
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)