MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: TITI LA MAMA LITAMU

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: TITI LA MAMA LITAMU
#1
Titi la mama litamu, hata likiwa la mbwa,
kiswahili naazimu, sifayo inayofumbwa,
kwa wasiokufahamu, niimbe ilivyo kubwa,
toka kama chemchemu, furika palipozibwa,
titi la mama litamu, jingine halishi hamu.
Toka kama mlizamu, juu kwa wingi furika,
Mfano wa zamzamu, yenye rutuba Makka,
Uonyeshe na muhimu, kwa wasiokutamka,
Hata waanye hamu, mapajani kukuweka,
Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.
Lugha yangu ya utoto, hata leo nimekua,
Tangu ulimi mzito, sasa kusema najua,
Sawa na manukato, moyoni mwangu na pua,
Pori bahari na mito, napita nikitumia,
Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.
Sababu ya kupenda, lafidhi yangu natoa,
Natumia toka ganda, na kiini chanelea,
Lugha nyingine nakonda, wakati nikitumia,
Mbele nikitaka kwenda, ulimi wangu hukwaa,
Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.
Ujira mwema napewa, kwa lugha za kigeni,
Na bidii natoa, nyingi nisiwekwe chini,
Lakini juu ya haya, nawaza mwangu moyoni,
Mwasi wa kutumia, lugha yake maskini,
Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.
Usemi na akili, nip ambo vikilingana,
Kwa lugha ya Kiswahili, sina cha kunibana,
Kama natoa kauli, na fikira hufanana,
Lugha nyingine bahili, ujima kwangu hazina,
Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.
Lugha kama kiarabu, kirumi na kingereza,
Kwa wingi zimeratibu, mambo ya kupendeza,
Na mimi nimejaribu, kila hali kujifunza,
Lakini sawa na bubu, nikizisema nabezwa,
Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)