MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: WALIMU SHIKENI HAYA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: WALIMU SHIKENI HAYA
#1
WALIMU SHIKENI HAYA
walimu zingatieni, kushika habari hizi,
mwenendo mwema shikeni, kuifanya yenu kazi,
tena kuweni makini, hasa kwenye siku hizi,
leo nawambia wazi, hasira zipunguzeni.

Leo nawaambia wazi, ushauri ushikeni,
atayeona upuzi, huyo bwana muacheni,
siku madhara kihozi, nitajiweka pembeni.
Hasira zipunguzeni, leo nawambia wazi.

Bakora sawa chapeni, Ila siwe kwa mashazi,
Si kucharaza mwilini, ukamzidisha dozi,
tabia hiyo acheni, huu utungo ni kozi,
Leo nawambia wazi, hasira zipunguzeni.

Jua wageuka mbuzi, kujitia hasirani,
kujiuzuia huwezi, upige namna gani,
sawa amekosa kwizi, lake kosa tathimini,
hasira zipunguzeni, leo nawambia wazi.

Kiwa  si leo mwakani, taniweka kumbukizi,
Kuna huyu Athumani, yupo jela siku hizi,
niliposema acheni, yeye kajitia chizi,
hasira zipunguzeni, leo nawambia wazi.

chanzo Cha habari hizi, sijui likuwa nini,
Kama anapiga mwizi, huku kiwa darasani,
kupumua akasizi, mwanafunzi kijijini,
hasira zipunguzeni, Leo nawambia wazi.

Athumani matatani, huku atokwa machozi,
akatiwa gerezani, mwalimu loenda kozi,
kifungo cha maishani, kutoka huko hawezi,
Leo nawambia wazi, hasira zipunguzeni.

Kuna walimu jamani, zao kauli maudhi,
kumwita mtoto nyani, au ngedere na chizi,
Hilo halileti shani, ulienda wapi kozi?
leo nawambia wazi, hasira zipunguzeni.

Kumwambia mwanafunzi, maneno ya kisirani,
kusema hili hawezi, unamtia tamani,
Ila waambie wazi, jitihada ongezeni,
hasira zipunguzeni, Leo nawambia wazi.

Sasa natoka shuleni, pokeeni yangu dozi,
ingawa yangu kwinini, chungu peke huimezi,
naomba badilikeni, walimu muwe walezi,
Leo nawambia wazi, hasira zipunguzeni.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)