MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JANDONI KUNA MENGI YA KUJADILI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
JANDONI KUNA MENGI YA KUJADILI
#1
JANDONI KUNA MENGI YA KUJADILI

Dada mmoja alinipigia simu, kabla hata sijamuuliza sababu alianza kunielezea matatizo ya mume wake.

Alinielezea mambo mengi mabaya ambayo mume wake alikua akimfanyia.

Nilimsikiliza sana lakini kwa namna alivyokua anaongea nilihisi kuna kitu.

Niliamua kumsikiliza mpaka mwisho ambapo aliniambia “Kaka mimi nimeamua kuondoka huyu si mwanaume wa kuishi naye!.”

Baada ya kumaliza kuongea nilimuambia sasa hembu niambie mazuri ya mume wako.

Alikaa kimya kwa muda kisha akaniambia “Mimi sikukupigia ili kumzungumzia yeye nilitaka tu unipe ushauri kuwa niondokeje maana nimechoka.”

Niliendelea kumsisitiza aniambie angalau zuri moja la mume wake.

Aliniambia zuri nikwakua tu labda anamsomesha mdogo wake sekondari lakini hakuna kingine.

Nilimuambia wala sihitaji mengi, hilo moja tu linatosha, nilimuuliza unasema mume wako hakujali, hajawahi kukununulia nguo hata siku moja au kukutoa out kama wanawake wengine?

Akanijibu ndiyo, nikamuuliza mshahaara wake ni Shilingi ngapi, akaniambia ni kama laki saba kwa mwezi.

Nikamuuliza chakula anatoa akaniambia ndiyo, nikamuuliza kodi ya nyumba kwa mwezi mnalipa Shilingi ngapi akaniambia laki moja na nusu,  kwa mwaka ni Shilingi ngapi?

Akanijibu milioni moja na laki nane.

Nikamuuliza umeme na maji analipa nani?

Akanijibu mlipaji ni  mume wake.

Nikamuuliza kwa mwezi vinaweza fika shilingi ngapi?

Akasema kama elfu ishirini.

Nikamuuliza kwa mwaka ni shilingi ngapi? Akajibu ni kama laki mbili na arubaini, ukichanganya na kodi ni kama milioni mbili.

Nikamuuliza ada ya mdogo wako Shilingi ngapi?

Akaniambia kwakuwa anasoma shuke binafsi ni kama milioni tatu na laki tano kwa mwaka.

Nikamwambia ukichanganya na zile milioni mbili unapata ngapi?

Tukapiga hesabu ikaja kama milioni tano na laki tano.

Nikamuuliza kwa siku chakula anakuachia Shilingi ngapi?

Akaniambia elfu kumi.

Kwa mwezi ni kama ngapi?  Akasema ni laki tatu kwa mwaka ni  kama milioni tatu na laki sita.

Nikamwambia ukijumlisha na zile tano inakuja kama ngapi?

Tukakuta inakuja kama milioni tisa na laki moja.

Nikamwambia haya sasa tuangalie mshahaara wa mume wako ni Shilingi laki saba kwa mwezi, ambayo kwa mwaka ni Shilingi ngapi?

Tukakuta ni milioni nane na laki nne, nikamwambia kama mnatumia milioni tisa na zaidi tena hapo hamjaumwa, sijajumlisha na ndugu zake, sijajumlisha nauli, sijajumlisha na michango ya harusi na bado unalalamika hakutoi out, wakati matumizi yenu tu ni ziadi ya mshahara wake unataka nini, unataka awe anakupa na damu yake.

Alibaki kimya na kukata simu. Baada ya siku mbili alinipigia simu na kuniambia “Kaka nimeelewa sitaki kuondoka tena kwani nimeona nilikua namchanganya tu mume wangu.
Sikua na shukurani na sikuona mazuri yake kwakua akili yangu niliielekezea katika mabaya tu.”

SOMO
Watu wengi tunawachukia wenza wetu kwakua akili zetu tumezipeleka katika mabaya yao tu na si mazuri hivyo tunajikuta tunawachukia na kudhani kua hawatupendi.

Hebu leo amua kuangalia angalau zuri moja tu la mwenza wako...

Hujachelewa.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)