MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: ZAMU YETU BADO

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: ZAMU YETU BADO
#1
ZAMU YETU BADO
Nasibu sio awamu, ilivyokuwa ghafla,
Sasa tunangoja zamu, kuushika utawala,
Na hapo ndipo patamu, kushindwa semeni wala,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola. 

Miaka imesalia, michache muimaizi,
Umoja wetu sawia, tuujenge tusihizi,
Kiti kuking'ang'ania, wasemaje hatuwezi?
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Samia tunamtaka, imbeni tena imbeni,
Naye hatuna mashaka, wacha abaki kitini,
Hatuwezi kubanduka, wanawake simameni,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Limelia la mgambo, vita hivi tupigeni,
Walitupiga vikumbo, tukabaki Kama nyani,
Duniani Kuna mambo, nafasi hiyo shikeni,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Tunataka kampeni, vijiji na vitongoji,
mwendo mmoja nchini, wa mijini na majiji,
Tunarejea kitini, na walidhani hatuji,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Asitokee mmoja, kusema yeye hawezi,
Na pasiwe ngojangoja, tumepata mtetezi,
Sasa tumpe pambaja, aliye wetu mlezi,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Wakati ukiwadia, wakutafuta Raisi,
Sisi tunaye Samia, kutushinda si rahisi,
Kura tutawakombea, tusiwe na wasiwasi,
Ni imara Wana wanawake, twendeni kushika dola.

Tunaomba CCM, Samia huyo tupeni,
Hili ni jambo muhimu, nasema mrudisheni,
Sasa tutimize zamu, Wana'ke kuwa kitini,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Tuondoa tofauti, chama na zetu imani,
Tuipange mikakati, siye kutinga ngomeni,
Ni mipango madhubuti, mafarakano acheni,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Tuunganeni wa bara, pamwe huko visiwani,
Sisi ni jeshi imara, wingi wetu hamuoni?
Tukijaza zetu kura, atushinde mtu gani?
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Beti kadha nimegonga, nasihi tuunganeni,
Yetu mambo kuyapanga, Ni jambo lenye thamani,
Wetu umoja kuchunga, awamu kuishikeni,
Ni imara wanawake, twendeni kushika dola.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)