09-14-2021, 02:31 PM
HADITHI
1. Mbiu ninawapigia, wa mbali mkaribie,
Nia kuisimulia, hadithi muisikie,
Yale yalotukia, na ninyi myatambue,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
2. Alikuwepo aazi, baba asiye na inda,
Mwenye kupenda uwazi, si mambo yaliyopinda,
Aliyeboresha makazi, familia ikampenda,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
3. Ilikuwa ni adhama, familiye kuongoza,
Maana alijituma, hewani kuipepeza,
Imara ikasimama, wema wakampongeza,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
4. Alivipenda vya ndani, kuliko ughaibuni,
Vikaipata thamani, vilivyoonwa ni duni,
Wageni wakatamani, wawenavyo dalihini,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
ITAENDELEA....
Mtunzi: John L. John
Mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya elimu katika lugha na utwala chuo kikuu Mzumbe.
Simu; 0788514751/0747225775.
Email: johnlucasjohn074@gmail.com
1. Mbiu ninawapigia, wa mbali mkaribie,
Nia kuisimulia, hadithi muisikie,
Yale yalotukia, na ninyi myatambue,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
2. Alikuwepo aazi, baba asiye na inda,
Mwenye kupenda uwazi, si mambo yaliyopinda,
Aliyeboresha makazi, familia ikampenda,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
3. Ilikuwa ni adhama, familiye kuongoza,
Maana alijituma, hewani kuipepeza,
Imara ikasimama, wema wakampongeza,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
4. Alivipenda vya ndani, kuliko ughaibuni,
Vikaipata thamani, vilivyoonwa ni duni,
Wageni wakatamani, wawenavyo dalihini,
Hadithi nahadithia, yale nilojionea.
ITAENDELEA....
Mtunzi: John L. John
Mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya elimu katika lugha na utwala chuo kikuu Mzumbe.
Simu; 0788514751/0747225775.
Email: johnlucasjohn074@gmail.com