MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MIKAKATI YA UTEKELEZAJI WA SERA YA KISWAHILI KWA KUFUNDISHIA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
MIKAKATI YA UTEKELEZAJI WA SERA YA KISWAHILI KWA KUFUNDISHIA
#1
Mikakati ya utekelezaji wa sera ya Kiswahili kwa kufundishia
Dkt. Z.S.M Mochiwa
TANGU kuanzishwa kwa shule na mitalaa ya kigeni nchini mwetu matumizi ya lugha ya kufundishia yalikuwa yanalingana na makusudi ya elimu yenyewe. Kwa sababu kubwa makusudi ya elimu ya kikoloni na/au ya kimisheni yalikuwa kujenga stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu. Kwa msingi huo, shule zilitazamiwa zitoe watekelezaji wa mambo ambayo yanapangwa na watu wengine.
WAHITIMU wa shule hizo hawakutizamiwa kuwa chimbuko la fikra mpya. Wahitimu waliofuzu walikuwa na stadi hai za kukumbuka na kuiga.
Tanzania ilipopata uhuru, Nyerere (1967) alifanya tathmini ya kina ya elimu nchini. Dhima ya elimu, kwa mujibu wa Nyerere, ni kumuwezesha mpokeaji ajitambue na ajijengee stadi za akili na mwili za kumfanya ajitegemee, atanzue tata na awe na fikra angavu. Mhitimu wa elimu hii ni mweledi wa vipawa vyake na pia hujiamini. Elimu hii humpa ujasiri wa utangulizi badala ya kuwa mlunguzi. Msisitizo wa elimu hii umo katika kumpa changamoto mpokeaji kiakili na kimwili ili amudu kujisawiri na kuyasawiri mazingira yake.
Mtalaa unaokidhi malengo ya elimu ya namna hii ni ule unaoibukia ndani ya utamaduni wa mpokeaji na ambao unazingatia mahitaji yake katika viwango vyote.
Kasoro kubwa iliyojitokeza, na tukabaki nayo hadi leo, ni kwamba falsafa iliyomo katika elimu ya kujitegemea haikutoa msimamo kuhusu matumizi ya lugha madarasani.
Badiliko lililotokea baada ya kutangazwa kwa falsafa hiyo ni matumizi ya Kiswahili kwa kufundishia elimu ya msingi tu. Badiliko hilo lilileta athari maradufu. Mosi, limeifanya elimu ya msingi ‘kupungua thamani’ machoni mwa Watanzania. Elimu hiyo ilionekana kuwa ya kienyeji kwa kuwa inafundishwa kwa lugha ya ‘kienyeji’: Kiswahili. Ni elimu ya kila Mtanzania aliye, na asiye na akili. Kwa mtazamo huo, ilihisika kuwa elimu ya kweli kweli haifafanuki kwa lugha ya kienyeji. Aidha, moja ya sababu zilizoifanya Tanzania isibadili lugha ya kufundishia elimu ya sekondari na vyuo ni kuamini kuwa Kiswahili hakiwezi kufafanua mambo makubwa ya kisayansi.
Athari ya pili ya badiliko la lugha ya kufundishia elimu ya msingi tu ni kukatika kwa mfululizo wa usawiri wa mpokeaji. Kwa maneno mengine, matumizi ya lugha mbili za kufundishia: Kiswahili katika shule ya msingi na Kiingereza katika sekondari na vyuo vya juu, kunasababisha mgawanyiko wa mtalaa kiakili au kisaikolojia.
Mwanafunzi wa shule ya msingi anayebahatika kuliona darasa la kidato cha kwanza hujigundua kuwa mbumbumbu kutokana na kushindwa kuelewa Kiingereza. Dhana alizozizoea hazionekani kwa kuwa zimemezwa na lugha mpya ya kufundishia. Kwa msingi huo, kuingia kidato cha kwanza si kuendeleza uzoevu uliopatikana katika elimu ya msingi bali ni kuanza mtalaa mpya na kusahau wa zamani.
Katika umri wake wote, Jamhuri ya Tanzania iliendelea kufumbia macho kasoro hii kwa kukosa ujasiri wa kuikabili uso kwa macho. Badala yake, Jamhuri ikaendelea kuliundia tume suala hili na wakati mwingine kuviagiza vyombo vya ukuzaji wa lugha ‘kukiandaa’ Kiswahili ili kimudu majukumu mapya.
Katika hatua ya kushangaza zaidi, Jamhuri imepata kuwaalika wananchi wote katika mjadala wa kufaa/kutofaa kwa Kiswahili na/au kuweza/kutoweza kwake jukumu la kufundishia.
Mtaalam anayefuatilia mwenendo wa sera ya lugha nchini Tanzania atagundua dosari kadhaa. Dosari ya kwanza ni uelewa tofauti wa suala linaloikabili nchi. Ni kwa kiasi gani wale waliopata kulichangia wanajua nafsi ya suala lenyewe? Je wanajua kinachowalema wanafunzi ndani ya Kiingereza cha kufundishia? Wanaohoji uwezo wa Kiswahili wa kukidhia haja ya elimu ya juu wanajua lugha ni nini? Laiti wangejua wangethubutu kuuliza swali hili? Aidha, maelekezo ya kuandaa Kiswahili kwa majukumu mapya hayatokani na ujuzi wa dhati ya lugha. Ni kwa vipi lugha ya Kiswahili ikuzwe na kikundi cha watu nje ya matumizi? Aidha, maelekezo haya yanaifanya lugha katika jamii kuwa gwanda ambalo, mara baada ya kushonwa na fundi maalumu, linamtosha kila mwanajamii. Hii ni miongoni mwa fikra ambazo tumedumu nazo hadi sasa.
Makusudi ya makala hii ni kuonesha, hatua kwa hatua, utekelezaji wa sera ya kuleta maendeleo ya elimu nchini Tanzania. Katika azma hiyo, makala itatoa kwa muhtasari lugha zilizopo nchini na manufaa yake, baada ya kufafanua suala lililopo. Baada ya hapo, makala itafafanua uhusiano utakaokuwepo baina ya lugha zilizopo pindi sera itakapoanza kutekelezwa. Makala itajadili maandalizi muhimu yatakayoandamana na utekelezaji huo. Tuanze na suala lenyewe.
Suala la msingi
Mfumo wa elimu nchini Tanzania huanza na Kiswahili katika kufundishia shule za msingi. Wakati wanafunzi wanajiunga na shule hizo wanalazimishwa kuacha lugha za mama zao. Kutokana na lazima ya shule, wanafunzi hao hujifunza Kiswahili hadi ya kukimiliki (ang. Mochiwa 1999). Kwa kuwa lugha za mama zao zilizo nyingi ni za Kibantu, changamoto ya kubadili lugha hubebeka bila ya maumivu na bila ya uwezekano wa mwanafunzi kushindwa.
Anapoingia katika shule ya sekondari, mwanafunzi hulazimika tena kubadili lugha ya kufunziwa. Safari hii, lugha hiyo haina nasaba yoyote na lugha ya mama zao wala Kiswahili. Nasaba inayokusudiwa hapa ni ile inayoziunganisha lugha kisarufi na si nasaba ya kimsamiati. Kikwazo kilicho mbele ya mwanafunzi na ambacho kitaukilia mafanikio yake endapo atakishinda ni sarufi ya lugha ya Kiingereza.
Kwa muda wote huu wa mdahalo wachangiaji wanaounga mkono kuendelea kwa matumizi ya Kiingereza katika kufundishia, wameshikilia kidinindi kuwa Kiswahili hakina msamiati wa kutosheleza mahitaji ya elimu ya juu. Tatizo hili – na ni lazima sote tukiri kuwa liko – linaweza kupungua uzito endapo kihalisi cha nafsi ya lugha kitakuwa sehemu ya uzoevu wa Watanzania. Kihalisi chenyewe ni kwamba lugha ni sarufi. Wanaoshindwa kumiliki Kiingereza wanashindwa kumiliki sarufi yake. Kwa mantiki hiyo, badiliko la lugha ya kufundishia shule za sekondari na elimu ya juu linatokana na kukiri kuwa wanafunzi wanashindwa kuimudu sarufi ya Kiingereza. Aidha, tunapoliangalia tatizo hili kwa mwanga huo, itakuwa vyepesi kuona kuwa msamiati wa lugha yoyote huweza kuingizwa katika lugha yoyote. Kw msingi huo, kama ilivyokuwa katika Kiingereza, Kiswahili kitavuna msamiati ndani ya matumizi yake. Laiti nafsi ya lugha ingalikuwa ni msamiati wake, Kiingereza kisingepata sifa ya kuwa kubwa duniani kwa sababu asilimia ya msamiati wake asilia ni ndogo kuliko ile ya mkopo.
Kutokana na kutoelewa nafsi ya tatizo hili la elimu, baadhi ya wanaounga mkono kuendelea kwa Kiingereza kwa kufundishia, wanaelewa kuwa pendekezo la badiliko ni la kuking’oa Kiingereza hapa nchini. Watu hao wanafikiri kuwa Kiswahili kinapoingia sekondari, Kiingereza hakitakuwa na nafasi kabisa. Kutoelewa huko kumelifanya badiliko linalokusudiwa kuleta kitisho kwa kila mtu anayejua nafasi ya Kiingereza katika zama hizi. Kiswahili kina vitabu vya rejea? Kwa kuwa jibu la swali hili si “ndiyo”, ndipo wakapendekeza vitafsiriwe vitabu vya kiada na vya ziada. Kwa ufupi, wataalam wanapendekeza ijengwe maktaba ya Kiswahili kwanza kabla ya kuliingiza badiliko hilo la lugha ya kufundishia.
 
Mara inapochukuliwa kuwa kweli kwamba hatua muhimu za utekelezaji wa sera hii ni ujenzi wa maktaba ya Kiswahili, kila mtu huona kuwa badiliko hilo haliwezekani. Aidha, itaonekana dhahiri kuwa badiliko hilo litasababisha maafa makubwa kielimu na kiuchumi. Sasa tujipe fursa ya kuabiri lugha zilizopo kabla ya kuratili badiliko linalofikiriwa.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)