MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
LUGHA YA KISWAHILI ILITOKA WAPI ?

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
LUGHA YA KISWAHILI ILITOKA WAPI ?
#1
  • Lugha ya Kiswahili ilitoka wapi?
Katika fasihi simulizi ya Waswahili, wazee wa pwani wanadai kwamba walitoka sehemu za kaskazini ya pwani ya Kenya mahali panapoitwa Shungwaya karibu na mji wa Lamu. Kutoka Shungwaya, Waswahili walihamia sehemu mbalimbali za pwani ya Afrika Mashariki kwa sababu walikumbwa na matatizo mbalimbali. Matatizo hayo ni pamoja na njaa, vita, magonjwa na ongezeko kubwa la idadi yao.
Wazee hawa wa pwani wanasema kuwa zamani waliitwa ‘Wangozi’, na Waswahili ni jina la kubandikwa tu. Aidha wanadai kuwa Kiswahili cha asili ni Kingozi. Kulingana na mapokeo ya Waswahili, asili ya kuitwa ‘Wangozi’ ni kwamba zamani watu hao walikuwa wakipima mashamba yao kwa kutumia kanda za ngozi na walivaa nguo zilizotengenezwa kutoka kwa ngozi (Mbaabu, 1985:1–5).
Hata hivyo, miongoni mwa Waswahili wenyewe hakuna makubaliano kuhusu asili ya jina ‘Waswahili’ na ‘Kiswahili.’ Kuna wale wanaodai kuwa jina Waswahili lilitolewa na kijana wa Kingozi alipoulizwa na wasafiri wa Kiarabu kuwa wao ni kina
nani? Akawaambia kuwa ‘sisi ni Wa-ziwa-hili au Wa-siwa-hili,’ yaani wenyeji wa pwaa hizi au wenyeji wa kisiwa hiki kikubwa. Inaaminika kuwa jina hili liliendelea kubadilika na wakati jinsi lilivyotumiwa hadi tukawa na neno ‘Waswahili.’
Kuna wengine wanaosema kuwa neno Swahili lina asili ya neno la Kiarabu. Wanasema kwamba Waarabu walikuja na kuwakuta watu wakiishi pwani na wakawaita watu hao Sahil na wingi wake ni Sawahil, yaani watu wa pwani au ufuo. Waarabu waliokuja pwani waliita sehemu hii ya Bara Afrika Al-Sahil (Pwani maalum). Kwa hivyo neno ‘Wa-swahili’ lina maana ya watu wanaoishi pwani. Kiambishi Ki– katika neno ‘Ki- swahili’ ni cha asili ya Kibantu na kina maana ya lugha. Kwa hivyo hii ni lugha ya watu wanaoishi pwani. Wana-elimu-chimbo wanasema kuwa jina ‘Kiswahili’ lilianza kutumika katika sehemu ya kaskazini ya pwani ya Kenya karibu na mji wa Lamu kati ya mwaka 700 na 800 baada ya Kristo (Mbaabu, 1978:3).
BOGYA HAPA CHINI KUFUNGUA YOTE KATIKA PDF>>>>> 
.pdf   KISWAHILI-HISTORIA-NA-MAENDELEO-YA-KISWAHILI.pdf (Size: 1.05 MB / Downloads: 5)
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)