MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI: NAVAA JEZI YA SIMBA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI: NAVAA JEZI YA SIMBA
#1
NAVAA JEZI YA SIMBA
Jezi yenye misukule, siivai asilani,
Kuchorwa watu wa kale, inachekesha jamani,
Nisipigiwe kelele, sivai jezi kwa nini,
Jezi yenye mikule, kuvaa Ina udhia.

Jezi ina watu watu, kama wapo msibani,
Kununua sithubutu, hata ningepewa nini,
Nasema sivai katu, habari mziamini,
Jezi zenye misukule, kuvaa Ina udhia.

Ninaogopa kuota, madudu yaje ndotoni,
Yaanze kunifuata, na mapanga mikononi,
Ndio Mana ninasita, kujitundika mwilini,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Nahisi ikinigusa, nitalegea mwilini,
Na siyafanyi makosa, kujitia madharani,
Wavaaji medodosa, jezi zatisha jamani,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Yake njano hunichosha, kuniumiza machoni,
Wengine wamejivisha, Kama nyoka wa kijani,
Kweli zinaogopesha, wenyewe angalieni,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Lakini jezi za Simba, mithili upo peponi,
Kuvaa ni kujipamba, tamu kutia mwilini,
Kuvaa kupiga pamba, alo vaa hushaini,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Nivae nipate raha, Ya Simba jezi nipeni,
Wala haina karaha, naota nipo mbinguni,
Nasema nataka raha, msimbazi nivisheni,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Sasa namaliza jambo, mtunzi mniacheni,
Msinipige kikumbo, sitaki Yanga jueni,
Timu iendayo kombo, kuwa nayo ni ya nini?
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704
Mwl Maeda
Reply
#2
(09-06-2021, 09:00 AM)MwlMaeda Wrote: NAVAA JEZI YA SIMBA
Jezi yenye misukule, siivai asilani,
Kuchorwa watu wa kale, inachekesha jamani,
Nisipigiwe kelele, sivai jezi kwa nini,
Jezi yenye mikule, kuvaa Ina udhia.

Jezi ina watu watu, kama wapo msibani,
Kununua sithubutu, hata ningepewa nini,
Nasema sivai katu, habari mziamini,
Jezi zenye misukule, kuvaa Ina udhia.

Ninaogopa kuota, madudu yaje ndotoni,
Yaanze kunifuata, na mapanga mikononi,
Ndio Mana ninasita, kujitundika mwilini,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Nahisi ikinigusa, nitalegea mwilini,
Na siyafanyi makosa, kujitia madharani,
Wavaaji medodosa, jezi zatisha jamani,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Yake njano hunichosha, kuniumiza machoni,
Wengine wamejivisha, Kama nyoka wa kijani,
Kweli zinaogopesha, wenyewe angalieni,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Lakini jezi za Simba, mithili upo peponi,
Kuvaa ni kujipamba, tamu kutia mwilini,
Kuvaa kupiga pamba, alo vaa hushaini,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Nivae nipate raha, Ya Simba jezi nipeni,
Wala haina karaha, naota nipo mbinguni,
Nasema nataka raha, msimbazi nivisheni,
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Sasa namaliza jambo, mtunzi mniacheni,
Msinipige kikumbo, sitaki Yanga jueni,
Timu iendayo kombo, kuwa nayo ni ya nini?
Jezi yenye misukule, kuvaa ina udhia.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704

Sawa mtunzi. Mimi nitavaa jezi ya Yanga.
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)