MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MFANANO NA TOFAUTI KATI YA RIWAYA PENDWA NA RIWAYA DHATI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
MFANANO NA TOFAUTI KATI YA RIWAYA PENDWA NA RIWAYA DHATI
#1
Swali :
Linganisha na linganua riwaya pendwa na riwaya pevu kwa kurejeleaRiwaya ya Nyota ya Rehema na Kufa na Kupona .
Masebo (2008) anasema riwaya ni hadithi ndefu ya kubuni yenye mawanda mapana ,lugha ya kinathari ,mchanganyiko wa visa na dhamira ,wahusika kadhaa na matukio yaliyosukwa Kimantiki yenye kufungamana na wakati na kushabihiana na maisha halisi.
 
Msokile (1992) ,anasema kuwa riwaya ni kazi ya sanaa ya kubuni yanye maandishi ya kinathari yanayosimulia hadithi ambayo ina uzito ,upana, na urefu wa kutosha ina wahusika mbalimbali wenye tabia za aina nyingi vilevile huwa na migogoro mingi ,mikubwa na midogo ndani yake.
 
Madumulla (2009) ,riwaya pendwa ni riwaya ambayo inajihusisha na masuala ya mapenzi ,upelelezi, na ujasusi ambapo mara nyingine katika ufuatiliaji wake kuna mapigano makali ya kimwili au kiakili kati ya mtu mmoja au wachache na watu wengi.
 
Masebo (2008) ; riwaya pevu ni riwaya yenye kuchimbua matatizo au masuala mazito ya kijamii ,kutafuta sababu zake ,athali zake na ikiwezekana ufumbuzi wake. Ni riwaya inayokusudiwa kumkera na kumfikirisha msomaji,sio kumstarehesha tu.
 
Riwaya pendwa ni kufa na kupona iliyoandikwa na E. Musiba na Riwaya pevu ni Nyota ya Rehema iliyoandikwa na iliyoandikwa na M.S Mohammed.
 
Riwaya pendwa na riwaya pevu hufanana na hutofautiana.Kwa kutumia kitabu cha riwaya ya “ Nyota ya Rehema” iliyoandikwa na M.S Mohammed na riwaya ya “Kufa na Kupona” iliyoandikwa na E .Musiba .
 
Ufuatao ni ufanano uliopo kati ya riwaya pendwa na riwaya pevu kwa kutumia riwaya ya “Nyota ya Rehema” na riwaya ya “Kufa na Kupona.”
 
Riwaya hizi zimetumia mandhari halisi ,mandhari kama eneo ambalo tukio la kifasihi kutendeka .riwaya pevu na riwaya pendwa waandishi wake mara nyingi hutumia mandhari ambazo ni halisi na zidhihilikazo katika mazingira halisi. Kwa mfano katika riwaya ya “Nyota ya Rehema “mwandishi ametumia mandhari kama vile Mwembeshomari (uk 31)
 
“Unakwenda mwembeshomari? Rehema aliulizwa.
 
‘Mwembeshomari’ aliitika upesi upesi.”
 
Vilevile katika riwaya ya “kufa na Kupona” mwandishi mandhari kama vile
 
“nikaingia kwenye gari langu huyoo upanga” uk 12
 
Riwaya hizi zinaelimisha jamii ;riwaya pevu na pendwa zote zinaelimisha jamii katika mambo mbalimbali kwa mfano riwaya ya “Nyota ya rehema “ mwandishi amewatumia Rehema na Sulubu kuelimisha jamii suala la kutokata tamaa, baada ya wahusika hawa kufukuzwa katika shamba la Ramwe wakapata kijieneo kidogo huko pakani ambapo hapakuwa na rutuba lakini hawakukata tamaa na jitihada za kilifanya shamba kuwa na rutuba kwa kulitilia moto na kuanza kulima kwa juhudi (uk -155 -159 ).
 
Pia katika riwaya ya Kufa na Kupona mwandishi amewatumia wahusika Sammy na Joe Masanja konesha suala la kutokata tama ambapo wapelelezi wenzao wanauwawa mmoja mmoja kwa vifo vya kutisha na kikatili lakini wao wanaendelea na upelelezi wa nyaraka za siri pasi kuto kukata tamaa mfano Wiilly Gamba anasema
 
“lazima mumkamate na kumuua mimi mwenyewe kama nitakuwa mzima wakati wote wa madhira kama yao………… (uk 24)
 
Zote zinaonyesha uhalisia wa matukio katika jamii, riwaya pendwa na riwaya pevu zote huonyesha uhalisia wa matukio yaliyo katika jamii . mfano katika riwaya ya “ kufa na kupona” mwandishi anaonyesha matukio ya rushwa,usaliti ,mauaji ya kiharifu na upelelezi ambapo mwandishi anamtimia mhusika piter mpigania uhuru aliyewasaliti wenzake kwa kuiba “nyaraka za siri “ Uk 91.
 
Pia DR Dikson Njoroge aliyeahidiwa kupewa rushwa na wareno ili kufanikisha wizi wa karatasi za siri (uk 99 ). Pia Benny anayefanya mauwaji ya kiharifu ili kulinda “nyaraka za siri walizoziiba (uk 53). Hivyo hivyo katika riwaya ya “Nyota ya Rehema” mwandishi anaonyesha matukio kama vile Dhuruma ambapo mwandishi anaonyesha rehema anadhurumiwa shamba la Ramwe aliyopewa na Baba yake (Fuad ) enzi za uhai wake na akina salma na karim (uk -150).
 
.Zifuatazo ni tofauti kati ya riwaya pevu ya “Nyota ya Rehema “ na ile ya “Kufa na Kupona” unadhihirika katika mambo yafuatayo ;-
 
Mtindo ,huu ni upekee wa mwandishi ambao hutofautisha kazi ya mwandishi mmoja na mwingine katika riwaya ya “Nyota ya Rehema”mwandishi ametumia mtindo wa wimbo. Kwa mfano pale Rehema alipoanza kukalili nyimbo za kubembelezea wototo.
 
“ukimpenda mwanao
 
Na wa mwenzio mpende,
 
Wako ukimpa chenga
 
Wamwezio chenjegere
 
Humjui akufaaye
 
Akupaye maji mbele……………”
“Nyamaa mama nyamaa
 
Nyamaa usilie ,
 
Ukilia waniliza
 
Wanikumbusha ukiwa
 
Ukiwa wa baba na mama” (uk 49 na 50)
 
Vilevile mwandishi ametumia mtindo wa nafsi ya tatu umoja na pia nafsi ya kwanza umoja, mfano “Mansuri alimtazama Rehema aliyekuwa akingojea jawabu kwa hamu “ (nafsi ya tatu umoja ) (UK 43). Na matumizi madogo ya nafsi ya nafsi ya kwanza mfano “ningependa kwenda huko rakwe nikakuona kulivyo “ alisema Rehema (uk 86). Na katika riwaya ya “Kufa na kupona” mwandishi ametumia matumizi ya simu.mfano ni pale polisi walipompigia willy kumjulisha Benny aliwasiliana na nani. Kama vile :
 
Hello ,Joe huyu “ “polisi stesheni hapa”
 
Basi hii simu ilikuwa inapigwa huko laving green ,kwenye nyumba ya Dr. Dickson Njoroge “ . uk 80.
 
Vilevile kuna matumizi ya nafsi ya kwanza umoja “nilipiga simu kwa chifu saa hiyohiyo nikimweleza kuwa awashauri maofisa polisi wasishugulike sana na mauaji mengi yatakayotokea “.
 
Katika riwaya pendwa mhusika mkuu ni mkwezwa ilhali katika riwaya pevu mhusika mkuu ni wakimapinduzi. Mfano katika riwaya yaKufa na kupona mhusika Willy Gamba amekwezwa na mwandishi kwa kumpalia sifa kama ,mwenye nguvu ,jasiri na mwenye uwezo mkubwa wa kupambana ,mfano mwandishi anamwinyesha mhusika Gamba akipambana na kundi la watu kumi na tatu na bado akawashinda anasema …
 
“..walipotaka kuanza kunifyatulia risasi haraka nikawafyatulia mfululizo.sita tayari chini nilipiga risasi mkono wa pita risasi ikaanguka chini bila ya kuwa nayo bastolla,ksha nikawamalizia wale wane waliobaki”………(uk 93). Pia katika riwaya ya “Nyota ya Rehema”mwandishi anamwonyesha mhusika mkuu Rehema kama mwanamapinduzi pale ambapo moja alipotoroka nyumbani kukataa mateso ya mama yake wa kambo (uk 22) pia kujiepusha kuingiliwa kimwili na mansuri kwa kumuuma meno na kupata nafasi ya kujiokoa (uk 65) tatu ,kupitia jitihada ya kufanya kazi kama ufugaji na kilimo ili kupambana na maisha yake na mmewe aliyemchagua kuishi naye (uk 104)
 
Riwaya imetumia lugha rahisi na inayoeleweka ilihali riwaya pevu imetumia lygha ngumu. Kwa mfano katika riwaya ya nyota ya rehema mwandishi ametumia misamiati ambayo si rahisi kuelewa maana yake mfano bigija,dhiyaa,ghila (uk 170) pia mwandishi ametumia mafumbo kama ubwebwe wa shingo haujamtoka………(uk 45) lakini, katika riwaya Kufa na kupona mwandishi ametumia lugha rahisi na inayoeleweka na iliyo na methali mfano mtaka cha sharti ainamen (uk 44).
 
Matumizi ya taharuki taharuki kama hamu ya msomaji kujua matokeo ya kitu Fulani katika riwaya pevu matumizi ya taharuki hutumika kwa kiasi kidogo mfano katika riwaya ya Nyota ya Rehema,taharuki imejitokeza ktika (uk 12) mwandishi anasema
 
“jina lako nani ? Faud alijisikia akiuliza kwa sauti iliyokuwa si yake
 
Adili ; alisikia jawabu akija
 
Aligeuka kumtazama na macho yao yakakutana ,roho zao zikaumana …………milele. Baada ya hapo hakuna chochote kilichoendelea baada ya hapo mwandishi ametuacha kwenye taharuki. Ilhali katika riwaya pendwa taharuki hujitikeza kiasi kikubwa mfano katika riwaya ya kufa na kupona wandiishi anathibitsha katika ukurasa wa 7 kama ifuatavyo “Amani lete madebe ya petrol na kiberiti”. Hii ni baada ya Sammy na willy kukamatwa na benny hivyo basi msomaji anapata hamu ya kujua nini kitatokea baadaa ya kuletwa petrol na kiberiti.
 
Pia katika ukurasa 45 taharuki imejitokeza pale willy aliposema “alinivuta akaanza kufungua tai yangu,kasha shati langu , halafu suruali yangu……….. tukajilaza . pia hapa msomaji atataka kuelewa kitu gani kiliendelea baada ya hapo.
 
Pia katika ( uk 67 ) ni pale ambapo willy anamkuta lina amechomwa kisu na mtu aliyemfahamu na anataka kumuuliza bila mafanikio. Hivyo msomaji Napata maswali je? Lina atakufa au atapona baada ya kujeruhiwa vibaya na mtu asiyefahamika
 
Vilevile taharuki nyingine imejitokeza pale ambapo willy Gamba alivyokamatwa na benny na akaambiwa asali sala yake ya mwisho kabla sijammiminia risasi kama mwenzake (uk 89 ).hivyo msomaji anapata taharuki kuwa je? Anaweza kufa au kunusulika? Lakini hata Gamba mwenyewe anakuwa yuko kwenye taharuki je? Anaweza kunusulika.
 
Wahusika katika riwaya pevu huakisi hali halisi ya maisha ilhali wahusika katika riwaya pendwa hupewa uwezo mkubwa usio wa kawaida wa kutenda matukio yanayosawiriwa Wahusika katika riwaya pevu huakisi hali halisi katika jamii riwaya hizi waandishi wametumia wahusika wao ambao ni tofauti dhidi ya uwakilishaji wao wa uhalisia wa mambo. Riwaya ya “Nyota ya Rehema” kama Rehema alipokuwa akipambana kupata mali yake ya urithi wa mali ya baba yake Faud, ambaye alifariki.hali hii ya urithi wa mali kwa mtu aliyefariki ni hali halisi kwa sababu yanatokea. katika jamii . mwandishi anathibitisha katika (uk 143) “ konde zilizomo na shamba lenyewe ni mali ya yangu bwana muridi na mimi ndiye motto wa maarehemu bwana Faud………………….. . Na katika riwaya ya “KUFA NA KUPONA “ mwandishi ameonyesha hali isiyo halisi kwa kumtumia mhusika Gamba aliyepewa uwezo mkubwa pale anapopambana na watu kumi na watatu na kuwashinda . hali hii si ya kawaida katika jamii.Katika (uk 93) walipotaka kuanza kunifyatulia risasi haraka nikawafyatulia mfululizo.sita tayari chini nilipiga risasi mkono wa pita risasi ikaanguka chini bila ya kuwa nayo bastola ,kisha nikawamalizia wale wakiobaki”
 
Katika riwaya pendwa mwanamke
amechorwa kama chombo cha anasa na katika riwaya pevu mwanamke amechorwa kama
mlezi na mzazi. Mwandishi wa riwaya ya Kufa
na Kupona anaonesha ambavyo Lina na Lulu wanavyojihusisha na masuala ya
anasa kama vile kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mhusika Benny aliyekuwa
mhalifu katika wizi wa nyaraka za siri (uk. 3) lakini mwandishi wa riwaya ya
Nyota ya Rehema, anamwonesha Bi. Kiza katika nafasi ya mlezi kwa kumlea Rehema
baada ya kifo cha mama yake (Aziza) pia Rehema anachorwa kama mzazi na mlezi wa
mwanae aliyeitwa Faud baada ya kuoana na Sulubu mume aliyemchagua mwenyewe (uk.
44)
Suluhu ya matatizo katka Riwaya pevu hutolewa hali ambayo ni tofauti na riwaya pendwa . suluhu ya matatizo katika riwaya ya “Nyota ya Rehema “ imedhihirika pale ambapo mhusika Rehema baada ya kupiia mikasa mingi katika maisha ambayo ilimfedhehesha, mfano kufa kwa mama yake (Aziza ) safari yake ya kutoroka nyumbani kwao ,maisha magumu aliyokuwa nayo mjini ,kudhurumiwa haki ya urithi lakini badi hakukata tama,hatimaye akampata sulubu ambaye kwake alimuona ni mume mchapakazi na chaguo lake katika maisha. Ilhali katika riwaya pendwa, suluhisho la matatizo haijaonyeshwa , kwani mwandishi wa riwaya ya kufa na kupona anaonyesha mwisho wa riwaya kuwa Lulu anawapigia simu
Tofauti nyingine ni riwaya pevu imejikita katika mkondo wa kihalisia ilihali riwaya pendwa imejikita katika mkondo wa kipelelezi, mkondo wa kiuhalisia ni aina ya mkondo ambao hueleza jambo katika uhalisia wake. Katika riwaya ya nyota ya rehema mwandishi amejaribu kueleza matatizo mbalimbali yanayoakisi jamii zetu. Mfano; ugumu wa maisha ,watu kunyimwa haki zao mwandishi katika (uk 143) anathibitisha
“ Konde zilizomo na shamba lenyewe ni mali yangu bwana Mudiri na mimi ndiye mototo wa marehemu bwana Faud……………” . Hapa mhusika Rehema alikuwa akijitetea pindi alipokuwa anataka kudhurumiwa shamba wakati ni haki yake kabisa. Hivyo basi haya ni masuala ya kihalisia kabisa katika jamii zetu. Lakini mkondo wa kipelelezi ni aina ya mkondo ambao hujikita kuzungumzia masuala ya mapenzi, upelelezi na ujasusi katika riwaya ya Kufa na kupona tunaona mwandishi ameeleza na kuonyesha vya kutosha masuala ya upelelezi na mapenzi mfano katika (uk 66) mwandishi anasema
“ kwa hiyo kazi kubwa sasa ni kutafuta kwa kila njia tumjue huyo “ bosi mi nani. Na habari nilizozipata kwa James hizo karatasi zinabadilishwa kesho usiku………. .Hapa ni Willy alikuwa anazungumza na Sammy.hivyo basi hapa inasibitisha kuwa hawa wanajihusisha na vitendo vya upelelezi. Pia masuala ya mapenzi katika riwaya hii pia yapegusiwa kama sifa mojawapo mwandishi katika (uk 105)
“Oh Willy,nilikuwa nakuota sasa hivi umenikumbatia ,kumbe ni kweli .Oh ,sasa nimepona kabisa ,nibusu Willy nirejewe na uhai”. Hapa ni lina baada ya kukutana na Willy.hivyo basi hii inathibtisha riwaya pendwa imejikita katika mkondo wa kipelelezi.
Kwa kumalizia riwaya pendwa na riwaya pevu zote kwa ujumla hubeba dhima za fasihi nia na madhumuni ni kufikisha ujumbe mzito uliokusudiwa kwa jamii lengwa ,mfano wa dhima hizo ni kuelimisha ,kukosoa ,kuburudisha kuonya ,kutunza historia ya jamii hivyi basi fasihi ya riwaya inamchango mkubwa katika jamii.
  1. Madumulla, J.A. (2009),Riwaya ya Kiswahili,Nadharia Historia na Misingi ya Uchambuzi Dar-es-Salaam:Mture Education Publishers.
  1. Masebo, J.A.(2007), Nadharia ya Fasihi (Fasihi kwa Ujumla).Dar-es- Salaam: Nyambari Nyangwine Publishers.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)