ETIMOLOJIA YA NENO 'ASHERATI' - Printable Version +- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz) +-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1) +--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16) +--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO 'ASHERATI' (/showthread.php?tid=2557) |
ETIMOLOJIA YA NENO 'ASHERATI' - MwlMaeda - 05-11-2022 HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'ASHERATI' Neno *asherati* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: a-/wa-*] yenye maana ya *mtu mwenye tabia ya kujamiiana na mtu au watu wasiokuwa na uhusiano wa kindoa.* Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *asherati* linatokana na nomino ya Kiarabu *ashiirah (soma: ashiiratun/ashiiratan/ashiiratin عشيرة)* lenye maana zifuatazo: 1. Rafiki. 2. Jamaa wa karibu. 3. Mke, *haadhihii ashiiratii هذه عشيرتي* huyu ni mke wangu, *haadhaa ashiirii هذا عشيري* huyu ni mume wangu. Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *ashiirat* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *asherati* lilichukua maana mpya ya mtu mwenye tabia ya kujamiiana na mtu au watu wasiokuwa na uhusiano wa kindoa. *Shukran sana.* *Khamis S.M. Mataka.* |