MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'ADUI' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA NENO 'ADUI' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO 'ADUI' (/showthread.php?tid=2456)



ETIMOLOJIA YA NENO 'ADUI' - MwlMaeda - 03-15-2022

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'ADUI'

Neno *adui* katika lugha Kiswahili lina maana zifuatazo:

1. *Nomino [Ngeli: a-/wa- wingi: maadui]* mtu, mnyama au kiumbe chochote kinachofanyia kiumbe kingine uovu; mtu aliye dhidi yako, kitu kibaya unachopambana nacho kwa mfano: magonjwa, njaa, chuki, wivu, ujinga na kadhalika.

*Methali* : adui wa mtu ni mtu, adui mpende, adui aangukapo mnyanyue.

2. *Nomino [Ngeli: a-/wa-]* mtu unayekabiliana naye katika mchezo; *mshindani* .

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *adui*( *soma: aduwwun/aduwwan/aduwwin عدو)*  ni nomino ya Kiarabu  yenye maana ya mtu aliye dhidi yako; hasimu wako, mgomvi wako.

Waarabu wana msemo: *aduwwun aaqilun khayrun min swadiiqin jaahilin عدو عاقل خير من صديق جاهل* adui mwerevu ni bora kuliko rafiki mjinga.

Katika Qur'aan Tukufu, Sura ya 2 (Surat Al-Baqarah), Aya ya 168 shetani ametangazwa kuwa adui wa mwanadamu. Imeandikwa: *Walaa Tattabiu Khutwuwaatish Shaytwaani Innahuu Lakum Aduwwum Mubiin. ولا تتبعوا خطوات الشيطان إنه لكم عدو مبين* Wala usifuate nyendo za shetani, hakiki yeye ni adui aliye wazi.

Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu  *aduwwun/aduwan/aduwwin عدو)* lilipoingia katika Kiswahili  na kutoholewa kuwa neno *adui* maana yake katika lugha yake ya asili - Kiarabu haikubadilika bali iliongezeka maana ya mtu unayekabiliana naye katika mchezo; *mshindani* .

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*