MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO 'AILA' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA NENO 'AILA' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA NENO 'AILA' (/showthread.php?tid=2287)



ETIMOLOJIA YA NENO 'AILA' - MwlMaeda - 01-24-2022

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AILA'

Neno aila katika lugha ya Kiswahili ni nomino: [Ngeli: a-/wa-] yenye maana ya ndugu wa familia moja; familia.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili aila( soma: aailatun/aailatan/aailatin عائلة ) ni nomino ya Kiarabu yenye maana zifuatazo:

1. Neno la jinsi ya kike kwa neno la Kiarabu aail (soma: aailun/aailan/aailin عائل) lenye maana zifuatazo:
a)  Mtu mwenye watoto wengi.

b) Mtu anayeishi katika lindi la ufukara.

c) Mmea unaotegemewa na mmea mwengine kwa makuzi na kupata chakula.

d) Familia: Kundi linalokusanya mume, mke, watoto na ndugu wanaowategemea; ndugu wanaoishi nyumba moja.

2. Watu wa nasaba ya babu wa kwanza mmoja; ukoo.

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili aailatun/aailatan/aailatin عائلة lilipoingia katika  Kiswahili na kutoholewa kuwa neno la Kiswahili ' aila ' lilichukua maana moja inayohusu familia/ukoo na kuacha maana zingine zilizo katika lugha asili - Kiarabu.

Shukran sana.

Khamis S.M. Mataka.