MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI : KUFA KUFAANA - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
SHAIRI : KUFA KUFAANA - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Fasihi simulizi (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=6)
+---- Forum: Ushairi (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=50)
+---- Thread: SHAIRI : KUFA KUFAANA (/showthread.php?tid=1965)



SHAIRI : KUFA KUFAANA - MwlMaeda - 01-03-2022

SHAIRI : KUFA KUFAANA
———————–

Kweli kufa kufaana, nimeyaelewa haya,
nikayapata tokana, na msiba ulikuwa,
upo kwa Bwana Njuguna, tajiri huko Iwawa,
kafiwa na mtu wake, ikawa kufa kufaana.
______

Jamaa na marafiki, na wandugu walifika,
nyumbani hapakaliki, watu walimiminika,
wengi ja kundi la nyuki, sehemu zote kutoka,
msibani walikaa, kwa Njuguna pakajaa.
_____

Wapo walilia sawa, kwa ndimi zote kulia,
na macho wakavimbiwa, kwa kukesha wakilia,
pilau walipogawa, hapo ndo wakatulia,
walipotafuna yote, wak’endeleza kulia.
_____

Kumbe hao walikuwa, walala miferejini,
na njaa kwao ikiwa, ni wa daima mwandani,
hata hawakuelewa, huo msiba wa nani?
kweli kufa kufaana, sasa nimeshaelewa.
_____

Rwaka rwa Kagarama,
Mshairi Mnyarwanda.