MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SHAIRI : KUFA KUFAANA

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SHAIRI : KUFA KUFAANA
#1
SHAIRI : KUFA KUFAANA
———————–

Kweli kufa kufaana, nimeyaelewa haya,
nikayapata tokana, na msiba ulikuwa,
upo kwa Bwana Njuguna, tajiri huko Iwawa,
kafiwa na mtu wake, ikawa kufa kufaana.
______

Jamaa na marafiki, na wandugu walifika,
nyumbani hapakaliki, watu walimiminika,
wengi ja kundi la nyuki, sehemu zote kutoka,
msibani walikaa, kwa Njuguna pakajaa.
_____

Wapo walilia sawa, kwa ndimi zote kulia,
na macho wakavimbiwa, kwa kukesha wakilia,
pilau walipogawa, hapo ndo wakatulia,
walipotafuna yote, wak’endeleza kulia.
_____

Kumbe hao walikuwa, walala miferejini,
na njaa kwao ikiwa, ni wa daima mwandani,
hata hawakuelewa, huo msiba wa nani?
kweli kufa kufaana, sasa nimeshaelewa.
_____

Rwaka rwa Kagarama,
Mshairi Mnyarwanda.

Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)