MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - ETIMOLOJIA YA MANENO 'DHAMBI' NA 'DHUNUBU

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: ETIMOLOJIA YA MANENO 'DHAMBI' NA 'DHUNUBU
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO 'DHAMBI' NA 'DHUNUBU'

Neno *dhambi* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino [Ngeli: i-/zi-]*  yenye maana zifuatazo:

1. Tendo la kufanya kinyume na amri za Mwenyeezi  Mungu.

2.  Kufanya makosa katika michezo aghalabu mpira wa miguu.

Neno *dhunubu* katika lugha ya Kiswahili ni *Nomino*  iliyo iliyo wingi wa neno dhambi na aghalabu hutumika katika tenzi na mashairi. Maana ya dhunubu ni uovu tele, dhambi nyingi.

Wingi wa neno *dhambi* katika lugha ya kawaida ni *madhambi*.

Katika lugha ya Kiarabu, neno *dhambi* limetoholewa kutoka neno la Kiarabu ' *dhanbu' (soma: dhanbun/dhanban/ dhanbin ذنب)* lenye maana ya kilicho kinyume cha Sharia/Sheria.

Na neno *dhunubu* limetoholewa kutoka neno la Kiarabu *dhunuubun (soma: dhunuubun/dhunuuban/dunuubin ذنوب)* lenye maana ya dhambi nyingi.

Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *dhanbun ذنب* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *dhambi* maana yake katika lugha yake asili Kiarabu haikubadilika bali iliongezwa maana ya kufanya makosa katika michezo aghalabu  mpira wa miguu.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*