01-07-2022, 09:29 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'AFADHALI'
Neno *afadhali* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. *Nomino: [Ngeli:i-/i-]* hali yenye unafuu; hali bora zaidi.
2. *Kivumishi:* tamko la kuonesha hali bora na ya kufaa zaidi ikilinganishwa na hali zingine.
3. *Kielezi:* bora kuliko; nafuu kidogo.
*Kuna methali:* Afadhali ya Musa kuliko ya Firauni.
*Kuna msemo:* Afadhali mchawi kuliko mfitini.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *afadhali* (soma: *afdhwalu/afdhwala افضل)* lina maana zifuatazo:
1. *Kitenzi:* Amefanya bora.
2. *Nomino:* Amekuwa mbora zaidi.
3. *Nomino:* Ziada na wingi.
4. *Nomino:* Kichobaki, salio.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *afadhali* ( *soma: afdhwalu/afdhwala افضل*) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *afadhali* halikubadili maana yake ya msingi katika lugha ya asili - Kiarabu.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *afadhali* katika lugha ya Kiswahili lina maana zifuatazo:
1. *Nomino: [Ngeli:i-/i-]* hali yenye unafuu; hali bora zaidi.
2. *Kivumishi:* tamko la kuonesha hali bora na ya kufaa zaidi ikilinganishwa na hali zingine.
3. *Kielezi:* bora kuliko; nafuu kidogo.
*Kuna methali:* Afadhali ya Musa kuliko ya Firauni.
*Kuna msemo:* Afadhali mchawi kuliko mfitini.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *afadhali* (soma: *afdhwalu/afdhwala افضل)* lina maana zifuatazo:
1. *Kitenzi:* Amefanya bora.
2. *Nomino:* Amekuwa mbora zaidi.
3. *Nomino:* Ziada na wingi.
4. *Nomino:* Kichobaki, salio.
Kinachodhihiri ni kuwa neno *afadhali* ( *soma: afdhwalu/afdhwala افضل*) lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *afadhali* halikubadili maana yake ya msingi katika lugha ya asili - Kiarabu.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*