MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
JIFUNZE KISWAHILI - SHAIRI: SAFARI YANGU

JIFUNZE KISWAHILI

Full Version: SHAIRI: SAFARI YANGU
You're currently viewing a stripped down version of our content. View the full version with proper formatting.
SAFARI YANGU

1. Anongozile Mtume,
Na Masihi Mfalme,
Nitunge tenzi niseme,
Waisome nchi hizi. 

2. Ninakuomba Wadudi,
Masihi na Muhamadi,
Mnitieni juhudi,
Beti nitunge mashazi.

3. Beti mashazi mashazi,
Nizinene waziwazi,
Zenee habari hizi,
Wazaliwa na Wazazi.

4. Wazaliwa na Wazazi,
Wazisome wasihizi,
Kumbe tele kuzihozi,
Zenye raha na machozi.

5. Nataka niwambe waja,
Ingawa kwao si hoja,
Basi mie Mara moja,
Wakanipe masikizi.

6. Moyoni linanipwita,
  Nabaki kutwetatweta,
Kooni likinipita,
Moyo wangu tabarizi.

7. Katika maisha yangu,
Yalinifika machungu,
Nami niliwaza tangu,
Kueleza waziwazi.

8. Nitapata afueni,
Hadhira waelezeni,
Likibakia moyoni,
Laniletea maradhi.

9. Leo nimedhamiria,
Ili nibaki sawia,
Ya sadiri tawambia,
Kwa kina bahari zi.

10. Zi ndo kina bahari,
Nizitunge beti nzuri,
Na watunzi mashuhuri,
Wazisifu beti hizi.

11.
(09-13-2021, 11:12 AM)MwlMaeda Wrote: [ -> ]SAFARI YANGU

1. Anongozile Mtume,
Na Masihi Mfalme,
Nitunge tenzi niseme,
Waisome nchi hizi. 

2. Ninakuomba Wadudi,
Masihi na Muhamadi,
Mnitieni juhudi,
Beti nitunge mas
3. Beti mashazi mashazi,
Nizinene waziwazi,
Zenee habari hizi,
Wazaliwa na Wazazi.

4. Wazaliwa na Wazazi,
Wazisome wasihizi,
Kumbe tele kuzihozi,
Zenye raha na machozi.

5. Nataka niwambe waja,
Ingawa kwao si hoja,
Basi mie Mara moja,
Wakanipe masikizi.

6. Moyoni linanipwita,
  Nabaki kutwetatweta,
Kooni likinipita,
Moyo wangu tabarizi.

7. Katika maisha yangu,
Yalinifika machungu,
Nami niliwaza tangu,
Kueleza waziwazi.

8. Nitapata afueni,
Hadhira waelezeni,
Likibakia moyoni,
Laniletea maradhi.

9. Leo nimedhamiria,
Ili nibaki sawia,
Ya sadiri tawambia,
Kwa kina bahari zi.

10. Zi ndo kina bahari,
Nizitunge beti nzuri,
Na watunzi mashuhuri,
Wazisifu beti hizi.

11.

Ninatamani uendelee maana utenzi ni mzuri mno.