MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : “MAPIGO YA MOYO ” **SEHEMU YA 07*

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : “MAPIGO YA MOYO ” **SEHEMU YA 07*
#1
SIMULIZI : “MAPIGO YA MOYO “
**SEHEMU YA 07*
Mapenzi ni hisia za ajabu sana, ukimpenda mtu kwa dhati utajikuta ukifanya kila jambo uweze kumpata. Pengine hata kutoa uhai wa binadamu mwenzio ili tu moyo wako uweze kupata furaha. Hilo ndilo jambo pekee ambalo lilimkuta msichana mrembo Rose ,alikuwa kama mtumwa wa mapenzi.
Hakuwa tayali kulala bila kuiona sura ya Peter, mvulana pekee aliyetokea kumpenda siku zote alizokuwa akisoma chuo kikuu cha Sokoine mkoani Morogoro.
Kusema ukweli Peter na Rose waliendana sana ,na wote walikuwa maarufu sana chuoni. Ungeonekana mshamba sana kama ulikuwa unasomea SUA na hukuwa unamfahamu Rose. Vivyo hivyo kwa Peter, wale tu waliopenda kuvaa na kuendana na fasheni chuoni ndio waliokuwa wakimfahamu Peter, kijana pekee aliyeshinda mataji ya ubunifu wa mavazi ya kiume chuoni.
“Naitwa Rose Jastin, bila shaka mwenzangu unaitwa Peter Mathew ……”,yalikuwa ni maneno ambayo Rose  aliweza kuyaongea mwaka mmoja uliopita,mwaka ambao ulikuwa wa mwisho chuoni wa masomo yake.Bila kujali ugumu wa kozi ya Biotechnology aliyokuwa akisoma, hakusita kushiriki mashindano ya urembo chuoni, na siku zote aliibuka mshindi wa taji hilo, na kuvunja rekodi kuwa msichana wa kwanza kubeba taji hilo la  umisi chuoni miaka yote ya masomo yake huku akisoma kozi ngumu.
“Bila shaka ndiye mimi ……”,Peter aliongea huku akijifanya kama ndiyo ilikuwa mala yake ya kwanza kumuona Rose, japokuwa alipokea kadi nyingi pamoja na sms za kimapenzi kutoka kwa msichana huyo, lakini hakumpenda. Yeye aliridhika na maisha ya kiplay boy, maisha ya kuwatumia wanawake kama chombo cha starehe ndio maisha pekee ambayo Peter aliweza kuyachagua. Pesa haikuwa tatizo kwake, kwani baba yake alimiliki hoteli nyingi za kitalii pamoja na mabasi mengi ya abiria yaendayo mikoani. Hivyo basi, akaunti ya Peter ilikuwa na pesa nyingi kumtimizia kila alichokitaka kama kijana.
“In short, sikupendi! mpende sana Robert kwani anakupenda na sio mimi “,ni maneno ambayo mshindi wa kiume katika ubunifu wa mavazi, kijana mtanashati aliyekuwa akipendwa sana na wasichana chuoni aliongea kumjibu Rose kuhusu ombi lake la kuwa wapenzi, ombi ambalo Rose aliahidiwa kupatiwa jibu na Peter katika part hiyo. Siku zote Rose  hakuweza kumtamkia hisia zake Peter uso kwa uso, bali alimtumia kadi za kimapenzi, hakuishia hapo alitafuta namba ya Peter na alipoipata hakusita kuwasilisha hisia zake kwa kijana huyu mtanashati.
“Kwanini lakini hutaki kunipenda, familia zetu zote zina pesa, harafu pia mimi na we ……”Rose alitaka kumalizia sentesi yake, lakini alishangaa sana Peter akiondoka huku akimtamkia kauli ya mwisho ambayo ilimfanya Rose kuumia sana na kuapa kulipiza kisasi, kwa yule aliyesababisha aweze kumkosa mwanaume aliyempenda sana.
“Robert ndiye mtu pekee unayepaswa kumpenda, kafeli mala nyingi sana mitihani yake sababu yako, kaaibika sana sababu ya kukupenda…
Kuanzia leo ukinifuatilia tena nitakuua …”,Peter aliongea huku akiwa ana hasira sana ,hakuwa tayali kuniona nikiendelea kuteseka mimi kama rafiki yake, urafiki ambao ulinifanya na mimi nionekane kama miongoni mwa watu kati ya watu.
Urafiki wetu ulianza mala tu baada ya kumwagiwa kisahani changu cha chipsi siku moja nikiwa katika hoteli iliyoko maeneo ya chuo chetu cha SUA pale main Campus, hakuishia hapo, nilipokea matusi mengi sana kama unavyojua watoto wa kizaramo! wakiamua kukuaibisha, siku hiyo lazima ujute. Aliyenifanyia matendo hayo ya ajabu hakuwa mwingine bali Rose, mala baada ya kuingia hotelini na kunikuta nikiwa nimeketi nikila chipsi zangu. Siku zote alinichukia kwani kwa siku alipokea sms nyingi za kimapenzi kutoka kwangu, sababu pekee iliyomfanya abadili namba yake ya simu kila wakati. Japokuwa alinionya nisimpigie simu wala kumtumia meseji, lakini sikuweza kujali chochote kile!, moyo wangu ulikuwa tayali kupokea maumivu ya kila aina.
“Nimeshakukataza usinipigie simu maskini wewe, huna hadhi ya kuwa na mimi “,ni maneno ambayo Rose aliweza kuyaongea na kisha kunibatiza kwa maji ya Kilimanjaro, chupa ya maji ambayo alikuwa ameishika mikononi mwake.
Rose na kundi lake waliondoka baada ya kuniaibisha, kusema ukweli nilichoka! wenye huruma walinihurumia, lakini maadui zangu hasa wanafunzi wenzangu walionidharau kwa umaskini wangu walinicheka sana baada ya kushuhudia kitendo nilichokuwa nimefanyiwa.
“Pole sana kaka, kula chakula hiki, na niambie mtu gani mubaya kakufanyia hivi “,nikiwa nimeinama nikificha aibu ya kuzomewa, nilishtuka mkono wa mtu ukiwa begani kwangu. Niliinua uso wangu na kushangaa nikikabidhiwa chakula kizuri na mtu ambaye siku zote niliogopa hata kumsalimia ,kwani hakuwa  sawa na mimi. Alikuwa ni mtoto wa tajiri maarufu mkoani Morogoro aliyejulikana kwa jina la Peter, baba yake mzee Mathew alikuwa na pesa nyingi sana hivyo basi sikuwa nina hadhi ya kuwa na urafiki naye. Kwani wazazi wangu walikuwa maskini kiasi kwamba nilivaa nguo moja wiki nzima chuoni mpaka watu walinishangaa .
“Kuanzia leo wewe ni rafiki yangu ,nitahakikisha una mpata binti huyu kama kweli unampenda japo inaonekana hana tabia nzuri kama mke wa kuishi naye “,ni maneno ambayo Peter aliongea baada ya kumsimulia kila kitu,japo Peter alipenda sana wanawake, lakini nilishangaa akitamka jambo moja la muhimu sana ambalo nililipuzia kuwa Rose alikuwa ana tabia mbaya hakufaa kuwekwa ndani kama mke wangu. Ndugu msomaji ,hivyo ndivyo niliweza kumpata Peter kama rafiki mpya chuoni na kuyabadilisha maisha yangu. Shida yangu ilikuwa yake mpaka tukamaliza chuo huku nikiwa ninaheshimika na wanafunzi wenzangu chuoni tofauti na awali. Lakini urafiki wetu ulitoweka ghafla kama jinsi ulivyoanza, kwani Peter baada ya kumaliza chuo alisafiri kwenda nchini Uingereza, na huo ndio ukawa mwisho wangu  mimi na yeye kuwasiliana.
**–****—
“,Sawa Peter asante kwa kunikataa na kuniaibisha, lazima nitalipiza kisasi kwa mtu huyu mpumbavu aliyenifanya nitoe machozi leo hii ” ,Rose aliongea huku akimjibu Peter aliyekuwa akiondoka kwa hasira katika part, part ambayo ilifanyika baada ya mashindano mbalimbali ya sanaa kumalizika katika chuo chetu cha SUA.
Na huo ndio ukawa mwanzo wa visa vikali mimi na Rose, alimwambia baba yake kuhusu mimi mpaka kupelekea wazazi wangu kuuawa. Hakuishia hapo! aliamua kunigonga na gari ili aniue kabisa aliponiona nikivuka barabara kizembe huku nikitembea kwa miguu. Ilikuwa barabara ya Morogoro, karibu na kituo cha mwendokasi cha Ubungo baada ya kufika muda mfupi tu na basi la Abood kutoka kijijini kwetu Mikese mkoani Morogoro, kuja Dar es salaam kutafuta shule ya kufundisha na pia kumtafuta kipenzi changu Rose ambaye nilimfikilia kila muda bila kukoma.
Plani yake ilifeli! alijikuta anashambuliwa na watu waliokuwa eneo lile la mwendokasi mala tu baada ya kutaka kuliondoa gari   .Bila kupenda alijikuta akinifikisha hospitalini, ili kukwepa kichapo kutoka kwa wananchi hawa walioshuhudia ajari ile na kugundua kuwa Rose ndiye aliyekuwa na makosa.
Hakuwa na jinsi kuitafuta plani B ya kulipiza kisasi!, na plani pekee aliyoiona inafaa nikujirahisisha kwangu, na kuniweka karibu yake. Aliona bora kumkosea baba yake aliyekuwa akitaka aolewe na mtoto wa raisi aliyeitwa Jacob ,na kukubali kuolewa na mimi ili tu aweze kuniua kirahisi na kulipiza kisasi kwani nilisababisha aweze kumkosa mtu aliyempenda sana, kijana pekee ambaye alikuwa katika moyo wake ambaye aliitwa Peter.
Kenya;
Hatimaye baada ya saa moja kupita,ndege ndogo ya abiria inayomilikiwa na shirika la ndege la Air Tanzania ilianza kutua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mombasa (MOI).Ilikuwa ni safari ya mateso kwa Rodgers kwani alitumia muda mwingi wa safari hiyo akiwa amejificha chooni baada ya kumuona askari mmoja akimtafuta ndani ya ndege. Kusema ukweli alimanusura akamatwe kama asingewahi kumuona askari yule ,na kweli alipona! kwani Rodgers tiketi yake ilikuwa ya mwisho kukatwa, hivyo alikaa mwishoni siti ya nyuma kabisa.Askari alipojaribu kuulza kwani alikuta siti ya mwisho ikiwa wazi, aliambiwa mtu yule kaelekea chooni anasumbuliwa na tumbo la kuhara! Askari kwa vile alikagua asilimia kubwa ya abiria wote na kumkosa adui yake, aliamini hata mgonjwa aliyeelekea chooni atakuwa siye muhusika.
Dar es salaam;
 Hatimaye honi ya gari la mzee Jastin ilitushtua sana mimi na Rose, kwani sikujua mzee Jastin angenifanyia kitendo gani kama angenikuta ndani kwake.
Rose hakuwa tayali kumuona baba yake akiniua, sio kwamba alinipenda! La hasha, alitaka aniue mwenyewe na kulipiza kisasi kwa mikono yake mwenyewe.
“Piiiii! Piiiii ……”mzee Jastin aliyekuwa anapiga honi nje ya geti lake kwa mara ya kwanza, baada ya siku nne kupita alipojaribu kuniua bila mafanikio huku Jacob akifa badala yangu, aliendelea kupiga honi kwa fujo kwani alitaka kuingia ndani haraka sana aweze kufanya mawasiliano na majambazi wenzie walioko Kisauni, Mombasa nchini Kenya.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)