MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : MAPIGO YA MOYO **SEHEMU YA 09**

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : MAPIGO YA MOYO **SEHEMU YA 09**
#1
SIMULIZI : MAPIGO YA MOYO
**SEHEMU YA 09**
Dar es salaam;
 Woga ulitoweka kabisa, tabasamu likaipamba sura yangu kwa mala nyingine tena. Pumzi ndefu ilinitoka kupitia mdomo wangu, tofauti na awali nilipokua nikitumia mdomo wangu kupumua. Kitendo cha mzee Jastin kuondoka nyumbani kwake bila kugundua uwepo wangu mahali pale, ndio jambo pekee ambalo liliweza kunifurahisha. Kusema ukweli nilipona kifo! kifo ambacho kingenikuta kama mzee yule katili angenitia machoni pake.
“Thanks God, aim safe! (Asante Mungu, niko salama) .Hatimaye nilizungumza kizungu, lugha ambayo siku zote niliweza kuiongea kama nikiwa nina furaha. Japokuwa nilikuwa na elimu ya chuo kikuu,elimu ambayo ilinifanya niwe vizuri katika lugha hiyo ya  kimataifa.
“Robert naomba unisaidie kitu!”,msichana mrembo Rose, msichana ambaye nilimpenda kwa moyo wangu wote, japokuwa alikuwa hanipendi kama nilivyokuwa nafikilia.Aliongea kwa upole sana, kichwani mwake alisahau kila kitu kuhusu nia yake mbaya ya kuniua na kulipiza kisasi chake. Jambo pekee ambalo alikuwa akiwaza kwa sasa, ni kujua historia halisi ya maisha yake.
“Nikusaidie kitu gani mpenzi wangu, Harafu baba yako kazungumza kitu kimoja ambacho sijakielewa kwakweli, anasema eti amekuokota!!! lakini naomba usichukie “,nilimweleza Rose bila kutambua kuwa alifahamu kila kitu ambacho baba yake aliweza kukiongea..
“Hilo ndilo jambo mbalo nilitaka unisaidie !pia naomba unisamehe, siku zote nilikuwa nakuongopea kuwa nakupenda lakini nilikuwa nakudanganya tu, nilikuwa nina nia mbaya ya kukuua kabisa kwa sababu nilikuona kama chanzo cha mimi kumkosa Peter, naomba unisamehe kwa yote! lakini mzee Jastin inawezekana mimi sio mwanae wa kumzaa, na kuna siri nzito imejificha ,kwahiyo naomba unisaidie “,moyo wangu ulipasuka mithili ya puto ambalo limejazwa upepo kupita uwezo wake. Sikumwamini tena Rose! nilimuona kama muuaji aliyejivika ngozi ya kondoo.
“Rose nikufanyie nini ujue nakupenda! wazazi wangu walipoteza maisha sababu yako, umenigonga na gari na kunivunja miguu ,isitoshe hujaridhika! bado unajifanya unanipenda ili uniue kirahisi! Inatoshaaa, Rose inatoshaaa! sina budi kukubali kuwa mimi ni mjinga, umenifanya kichaa wa mapenzi “,niliongea maneno mengi kwa huzuni sana,sikuamini kama kweli Rose alikuwa na roho ngumu kiasi kile mpaka kupelekea kutaka kuniua.
Mapigo ya moyo wangu hayakuwa katika hali ya kawaida, yalikimbia mbio ndefu sana kiasi kwamba Rose aliweza kugundua.
“Please Robert! usipaniki, mapenzi ni ya ajabu sana!  nisamehe bure kipenzi changu “,msichana mrembo sana ambaye angemvutia mwanaume yeyote rijali, aliongea na kunisogelea. Kisha alichuchumaa chini na  kunipiga busu katika paji langu la uso.
Kipenda roho hula nyama mbichi! nilijikuta nikimsamehe Rose baada ya kupigwa busu lile, na kujikuta nikiendelea na ujinga wangu kwani tayali roho yangu ilikua imependa kwa dhati. Mapenzi ndiyo yaliyonifanya nivumilie vitendo vyote vibaya ambavyo nilikuwa nimetendewa na Rose, mapenzi ndiyo yaliyomfanya Rose kufanya mipango ya kuniua ili alipize kisasi kwasababu aliniona kama chanzo cha yeye kumkosa Peter. Hivyo kulaumu kusingenisaidia chochote kile! jambo pekee ambalo nilitakiwa kulifanya nikutoa ushirikiano kwa Rose katika kila jambo, na kumuonesha mapenzi ya kila aina ili upendo wake aweze kuhamishia kwangu na wala sio kunichukia.
“Sawa Rose! nimekusamehe, naahidi kukupenda daima hata kama wewe hautakua tayali kunipenda! “,
“Hapana Robert usiseme hivyo! Nimefuta kisasi chote, na niko tayali kukupenda, nisamehe bure mpenzi “,
“Naomba unipende, nipende kama mimi ninavyokupenda ,nakupenda sana Rose “,
“,Usjali kabisa Robert, Sasa hivi nisaidie kujua ukweli kuhusu maisha yangu, wazazi wangu halisi wako wapi?, harafu baada ya hapo tukaishi zetu Uingereza, akaunti yangu ina pesa za kutosha, hata wewe pia raisi kakupatia pesa nyingi ambazo hazitaisha leo wala kesho “,Rose aliongea huku akinimwagia mabusu mengi mfululizo, mabusu ambayo yalinifanya nifungue kabisa moyo wangu, na kusahau maumivu ambayo Rose alikuwa ananisababishia kila kukicha.
Mombasa _Kenya ;
       Rodgers alikuwa na furaha sana, alijiona mshindi dhidi ya raisi wa Tanzania aliyetuma vijana wake waweze kumkamata bila mafanikio.
Akiwa anaendelea na mazoezi ya karate kama kawaida, lakini kwa wakati huu alifanya mazoezi makali bila kupumzika. Alitambua muda wowote, angeweza kukabiliana na askari wa Kenya au Tanzania ambao walikuwa wanamtafuta kila kona ili aweze kujibu mashtaka ya mauaji aliyokuwa ameyafanya.
“Duuuh! kama wameshindwa kunikamata kwenye ndege, wasitegemee kama watanikamata kirahisi uraiani, tena katika ngome yetu yenye ulinzi makini “,aliongea huku akitabasamu, mala baada ya kukumbuka jinsi alivyojifanya mgonjwa mahututi na kukosa nguvu za kutoka chooni alipokuwa amejificha muda wote ndege ilipokua safarini.
Abiria wote walishuka, lakini muhudumu alishangaa abiria mmoja akiwa haonekani. Alipojaribu kukagua kila sehemu ndani ya ndege hakuweza kuona mtu, lakini alikumbuka mgonjwa aliyekuwa ameelekea chooni tangu ndege ilipoanza safari Dar es salaam. Muhudumu aliamini kutakuwa na tatizo!, haraka haraka alielekea chooni, na kama alivyokuwa akifikilia, alimkuta Rodgers akihema kwa nguvu, huku akiwa hawezi hata kusimama. Bila kupoteza muda, ambulance ilifika na wahudumu wa ndege ile walishirikiana kumnyenyua Rodgers na kumuweka ndani ya gari. Hawakuruhusu mgonjwa kupigwa picha zozote zile, kwani waliogopa kuchafua shirika lao la ndege kwa kutoa huduma mbovu mpaka kupelekea abiria akizidiwa kiasi kile bila kugundulika na kupatiwa huduma ya kwanza.
Wahudumu wale wa ndege hawakujua kuwa Rodgers aliwadanganya, hakuwa anaumwa ugonjwa wowote ule bali aliigiza tu. Ambulance haikuweza hata kukaguliwa na askari, kwani waliamini mgonjwa yule aliyefunikwa mwili mzima mpaka uso wake, hawezi kuwa jambazi waliyekuwa wamepokea taarifa zake za mauaji kutoka Tanzania, mauaji ambayo aliyafanya kwa kumuua mtoto wa raisi aliyeitwa Jacob.
Ndio maana hata cctv camera za uwanja wa ndege wa Mombasa, hazikuweza kuinasa sura ya Rodgers.Jambazi hatari na mzoefu sana, siku zote hakubahatisha bali alijiamini na kufanya kazi zake kwa umakini wa hali ya juu, jambo ambalo lilimfanya apendwe na mabosi wake.
……………………………
Madaktari na manesi ambao walimpokea Rodgers katika hospitali ya Mombasa, walishangaa sana kwani walimfanyia vipimo vya kila aina, lakini hawakuweza kuona ugonjwa wowote. Cha kushangaza, Rodgers alipata nafuu haraka sana na baadaye wakamruhusu kuondoka. Madaktari hawakuwa na haja ya kumuuliza maswali mengi kwani wahudumu wa ndege waliomfikisha hospitalini walitaka jambo lile liweze kuwa siri, hawakutaka kuishushia heshima kampuni yao ya usafiri wa anga ya Air Tanzania.
Waliona bora Rodgers kapona haraka sana na kuondoka, kabla vyombo vya habari havijainasa sura ya Rodgers na kuichafua kampuni hii ya Kitanzania. Rodgers alikua ameibalisha sura yake kwa kujifunga kiremba mithili ya mpemba wa Zanzibar, na kuvaa miwani iliyomfanya awe na mwonekano tofauti kabisa. Hivyo ndivyo Rodgers alivyoepuka kukamatwa na askari waliotumwa kumkamata kwenye uwanja wa ndege wa Mombasa Kenya.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)