MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU ” **SEHEMU YA 08**

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU ” **SEHEMU YA 08**
#1
SIMULIZI : “JENEZA LA AJABU “
**SEHEMU YA 08**
Msitu wa majini;
Jeshi la msituni, wakiwa wanamtafuta adui aliyevamia msitu wao bila mafanikio, ghafla amli inatoka kutoka kwa kiongozi wao, jini mweupe, waweze kurudi nyuma, upande wa pili wa msitu, katika njia ya kuingilia katikati ya msitu wao, njia ambayo waliweza kutega shimo ambalo lingeweza kumkamata adui yoyote yule kama angekanyaga shimo hilo lililofunikwa kwa udongo,shimo ambalo lilitegwa katikati ya barabara..
“Twendeni haraka sana katikati ya barabara tuliyotega mtego wa shimo, tayali adui ameshanasa “,Jini mweupe alitoa amli kwa jeshi lake, na bila kupoteza muda, walipotea  na kisha kutokea eneo ambalo shimo lilikuwepo.Jini mweupe alikuwa sahihi kabisa, kwani walikuta tayali mtego ulishamnasa adui, mtu waliyemtafuta tangu asubuhi, na ilikua tayali imefika majira ya jioni bila kumtia mikononi.
“Fungeni kamba katika mti huo, na kisha dumbukizeni shimoni, harafu ingieni watu wachache mkamkamate,”jini mweupe alizidi kutoa amli na maelekezo, huku majini wale wakiweza kutekeleza maagizo waliyopewa haraka sana. Walishindwa kutumia nguvu za kijini, kumkamata adui yao, jambo ambalo ingekuwa rahisi kumkamata kijana Njoshi, na kujikuta wakitumia njia za kawaida bila kujielewa, njia ambayo isingefanikiwa, bali ingemrahisishia adui yao kutoka ndani ya shimo na kuwaponyoka. Hayo yote yalitokea kutokana na maombi ambayo mama yake Njoshi, aliweza kuomba mizimu iweze kumsaidia mwanae kutoka katika hatari, pamoja na maombi ambayo Njoshi mwenyewe aliweza kuyafanya kila wakati ambapo hatari ilimkabili.
********
Sauti nzito za kutisha, zikiandamana na mwangwi mzito, Njoshi anazisikia akiwa shimoni. Hakuweza kuogopa tena, lolote ambalo lingetokea, alikuwa tayali kukabiliana nalo, kwani aliona akiendelea kuwa muoga, hatoweza kuishinda vita ambayo iko mbele yake.
“Bila shaka watakuwa wamenifuata mimi, waweze kunikamata, hapa lazima nipambane, lazima nife kiume “,Njoshi aliongea huku akiitazama kamba iliyokuwa inashushwa taratibu ndani ya shimo, na kuona kama hiyo ndio ilikua njia pekee ya yeye kutoka shimoni. Na kulishika panga lake kisawasawa katika mkono wake wa kulia, akiwa tayali kuchinja kiumbe chochote kile kitakachoingia shimoni, huku akiwa amebeba kibegi cheusi mgongoni, kibegi kilichotumika kuhifadhia panga pamoja na kitambaa cheusi chenye nguvu za ajabu, kitambaa ambacho kajifunga kiunoni.
“Huyu mshenzi hanioni, hii ndio dawa yake, “Njoshi aliongea huku akimfyekelea mbali jini mmoja, jini ambaye mwili wake uliundwa kwa mifupa tu, baada ya kushuka na kamba ndani ya shimo, na kuangaza huku na huku bila kumwona adui yake. Lakini Njoshi alishangaa sana, kwani baada ya kulitumia panga lake,  jini yule aliyeyuka kama vile kaunguzwa na moto, na kisha kutoweka kabisa.
“Ahaaaa asante sana mama yangu, kumbe ndio maana ulinambia kuwa hii ndio siraha yangu ya kunirudisha nyumbani salama, ndio maana hata hawanioni, inaonekana huu mkanda pia unanisaidia “,Njoshi aliongea huku akitabasamu, na kushika kamba ili apande kuelekea juu, aweze kutoka shimoni, lakini alisita baada ya kusikia kelele za fujo na hasira, huku akihisi kama kuna viumbe wa ajabu, wenye hasira walikuwa wakiitumia kamba kumfata shimoni.
********
Jini mweupe, pamoja na majini wote wa msituni ikiwemo malikia, wanapata maumivu makali sana, maumivu ambayo hutokea katika miili yao, pale tu jini mwenzao anapopoteza maisha. Kutokana na hasira ya kumpoteza mwenzao, baada ya jini mmoja kuingia ndani ya shimo kumkamata adui aliyeuvamia msitu, na kukutana na panga la ajabu shingoni mwake, panga pekee lenye uwezo wa kuangamiza majini.
Baada ya jini huyo kupoteza maisha, maumivu makali yanawakumba majini wote wa msituni, na kupiga kelele nzito za hasira, kelele ambazo zilisikika katika nchi yote ya Mwamutapa, na nchi jirani, kelele ambazo zilimshtua Njoshi shimoni, na kushindwa kupanda juu kwa kutumia kamba, kutoka ndani ya shimo.
 “Huyu binadamu tukimkamata lazima tumle nyama ,lazima alipie maumivu haya “,malikia wa majini akiwa katika ngome yake, alizungumza kauli ya kisasi, kauli ambayo itamghalimu sana baadae kuitengua, kwani malikia wa majini akiongea kitu lazima akitimize, kuepuka kuteketea kwa watu wake, jambo ambalo itangua kwake kumla nyama Njoshi, kwa nini itakua ngumu?  endelea kufuatilia ,
*******
“Siwezi kuumia kiasi hiki ingieni mkamkamate, akiwa hai au amekufa “,ilikua ni sauti ya jini mweupe, kiongozi wa askari wa majini, askari ambao walifanya kazi ya kuulinda msitu wa majini,akiruhusu jeshi lake kuingia shimoni, baada ya mwenzao aliyetangulia mwanzoni kuuawa, kitendo ambacho kilimfanya Njoshi asite kuelekea juu, kwani alihisi kamba ikiwa nzito sana, alipoishika, kitendo kilichoashiria ujio wa kundi kubwa la majini ndani ya shimo, kwa kutumia kamba ile.
Mwamutapa
“Aiweeeh mama nimerudi tena, pole na kazi, nimetoka kwa mfalme lakini sijamkuta Njoshiii, pia nimekuta kilio eti mfalme kafa, unaweza niambia chochote? ,kwani kwanini mfalme alimuua baba yake Njoshi ………”,Ngesha    ,rafiki yake Njoshi, alimuulza mama wa rafiki yake maswali mengi sana baada ya kumfuata shambani, lakini taarifa hiyo haikumshitua mama yake Njoshi, kwani alifahamu kila kitu.
“Baba wa rafiki yako aliuawa kwasababu alishindwa kumtibu mfalme, kwani ni mwezi umepita sasa mfalme anaumwa, na ni siri haitakiwi Wanamutapa wafahamu, na pia ni kweli mfalme kafa lakini atafufuka japo sina uh…aki…ka “,mama Njoshi akiwa ameshika jembe, akipalilia polepole mahindi yake, alimjibu Ngesha na kushindwa kumalizia sentesi yake, baada ya kusikia sauti nzito za kutisha kutoka msituni, sauti ambazo ni adimu sana kuzisikia. Sauti hizo zilimwogopesha Ngesha, kiasi kwamba alitaka kukimbia, kwani ziliogopesha sana.
“Wii…Wii…wiiii……ihiii…hii … hiii”,zilikua ni sauti za mwangwi zikitoweka kwa mbalii, kutokana na sauti za hasira zilizosikika kutoka kwa viumbe wa ajabu wa msituni.
“Kuhusu sehemu alipo Njoshi, nazani umesikia sauti hizo za ajabu kutoka msituni, Njoshi kaelekea huko katika msitu wa majini, na tayali ameshaua  jini mmoja, na kila atakapoua, utazisikia kelele hizo za hasira kutoka kwa majini ,akirudi salama anaweza kuwa mfalme, ” Mama Njoshi aliongea, huku Ngesha akiwa amepigwa na butwaa, amekosa nini afanye kwa wakati ule, kutokana na maneno aliyo yasikia kutoka kwa mama Njoshi.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)