MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 31

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 31
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU
SEHEMU YA 31
Taarifa ya habari ile Kwakweli ilimshtusha sana Zamda. Kwasababu japokuwa Kweli Zamda na Tito wameshaachana Lakini alichokuwa akifikiria ni kwamba watoto wake kwasasa watakuwa ni yatima.Mda huo ilibidi Zamda ayatoe yake ya moyoni kwa Zaidu.Zamda Alisema hivi.
Unajua Zaidu huyu jamaa aliyetangazwa kwenye Television Hapo ninamjua.
Unamjua.
Ndiyo.
Heeeee unamjuaje Yaani?.
Ndiyo huyo Tito niliyekuwa nakueleza.
Heeeee ndiyo huyu.alafu kweli kwa Mimi sijawahi kumuona Kabisaaaaaaa.
Ndiyo huyu Sasa.
Ndiyo huyu aliyekuwa akikutishia kwa kisu siku Hiyo ulivyotoka Ngata?.
Ndiyo maana Yake.
Amakweli malipo ni Hapa Hapa Duniani akhera ni mahesabu tu.
Kweli.
Kwasababu angalia alivyokuwa akikutishia Yaani Silaha aliyokuwa akiitumia ndiyo hiyo ambayo imemuua.
Ndiyo hivyo nahisi mungu alimuona naakajua tulia huyu jamaa nimjibu kuchuria kwake kwa wenzake. Ndiyo hadi hapo mageereza na mwisho wa siku kisu alichokuwa akinitishia nacho ndicho kimempotezea maisha yake kwa sekunde Au dakika chache tu.
Kwahiyo utafanyaje ili na wewe uunganike katika mazishi haya.
Hapana.... Hapana Yaani tena hapa Kabisa.
Kwanini hapana?.
Zaidu Mimi staki kwenda kule alafu waje waanze kusema kwamba ooooo eti muangalie huyu aliyesababisha kifo cha Tito amekuja kudai urithi.
Tena hayo!!?.
Ndiyo maana Yake.Zaidu Kwakweli huko Mimi siendi kabisaaaaaaa Yaani kabisa. Kwanza hawa watoto kwasasa wao wanajua kabisaaaaaaa Wewe ndiyo Baba .mfano huyu Glady ameanza kukuona wewe  kitambo sana.Kuanzia tu jamaa alivyoondoka Yaani Kipindi kile alipokuwa amesafiri kikazi.
Kwahiyo Zamda maamzi yako yanakuwa wapi?.
Maamzi yangu ni kwamba nooooo huko siendi kabisaaaaaaa. Yaani noooooo kwenda kabisaaaaaaa huko.nimeteseka sana pale na Unataka tena nirudi katika mahabusu ya Mama mkwe pale.Hapana kabisa.
Basi Sawa. Kama Wewe huendi Basi na mimi lazima mguu wangu uwe mzito.
Haya bana.Embu kwasasa ni mda wa sisi kupanga mipangilio yetu ya  arusi vizuri.
Ni Kweli Zamda ni mda mrefu sana tukiwa tunaishi bila  Baraka za mungu.
Ni vyema sana kabisa tukiwa katika kifungo cha maisha chenye halali.
Unajua Zamda aaaaaaa Yaani Sijui nisemeje kuhusiana na wewe tu Jamani.
Kwanini Zaidu. Ninachekesha sana Au vipi?.
Hapana Hayo Majibu yako tu.
Mmmmh ya kwako ni yapi?.
Ni kwamba Zamda Kwakweli thamani yako naijua Mimi,utamu wako naujua Mimi, sauti yako ya mawada naijua Mimi,Yaani tuseme kila kitu katika mwili wako nakijua Mimi.Kwahiyo ndiyo maana nakwambia kwamba najua thamani yako.
Hata Mimi pia Zaidu najua thamani yako.Tena inawezekana yako ni kubwa Sana kulikoni ya Mimi ya Mambo ya uzuri uzuri tu.
Sawa Zamda ni vizuri Kweli kila mtu kujua thamani ya mwenzie.
Sawa.
Siku nazo zilizidi kuyoyoma kwa mtu anayefanya ya faida basi atavuna ya faida.
Basi ikiwa ni siku ya Ijumaa.ilikuwa ni siku maalumu kwa wapendanao hao ambao ni Zamda na Zaidu.Kwa siku hiyo ilikuwa ni usiku wa ZAIDU & ZAMDA.Yaani siku hiyo ilikuwa Ndiyo siku ya arusi.Ambapo arusi hiyo ilifanyikia katika ukumbi uliokuwa ukijulikana kwa jina KAITA HALL huko Damaresela.
Arusi hiyo Kwakweli ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Waziri wa habari michezo sanaa na utamaduni na wageni wengineo Ambao ni waheshimiwa kutoka serikalini.Pia wengineo kutoka katika taasisi mbalimbali kama vile Taasisi ya Fasihi Kinani (TAFAKI), Taasisi ya Uchambuzi wa Sarufi Kinani (TUSAKI) na taasisi nyingine mbalimbali.
Kwa mda huo panavyoonekana katika ukumbi huo Kwakweli ni Furaha tele kweli kweli. Katika eneo walilokuwa wamekaa Bibi na Bwana arusi Kwakweli Palikuwa pamependeza sana na pakiwa panabadilika rangi za kila aina.Siku hiyo Kwakweli Jeni alikuwa Ana furaha sana kwa Zaidu kuweza kutimiza lengo lake ambalo Tangu mwanzo alikuwa akilitamani sana ambalo ni la kumuoa Bibiye Zamda.
Kwa mda huo ulikuwa ni mda wa kuanza kugawa zawadi mbalimbali kwa bibi na bwana Arusi.Ambapo zawaid hizo zinatoka Popote pale.Ambapo arusi iikuja kuisha mnamo saa saba usiku.
Basi ni siku chache baada ya arusi ya Zaidu na Zamda Kufanyika. Siku Hiyo Zamda na Zaidu walikuwa wakifanyiwa interview Yaani mahojiano katika Runinga moja iliyokuwa ikijulikana kwa jina la SAKAS.COM TV .Mda huo ikiwa ni mishale ya saa Kumi alaasiri.Kwakweli kama ni kupendeza Walikuwa wamependeza kweli kweli.Huyo Bibiye Zamda Kwakweli Muonekano wake Yaani uko tofauti Kabisa na ule ambao alikuwa akionekana Wakati alikuwa akiishi Kimbu kule kwa mama Tito.
Mda huo mtangazaji aliyekuwa katika kipindi alikuwa akisema Hivi.
Aaaaa kama kawaida wanangu wa kudekeree kwenye kipindi cha kijanja,Yaani kipindi kinachowezesha watu kujulikana kwelikweli kwa wakishaamua tu.Kama kawaida hapa ni Mimi hapa Rami Gadi.Leo mjengoni Tuna special guest kwelikweli Ambao they are so beautiful In deed.Wamependeza kwelikweli.Wa kiume huyu Natumai kila mtu kwa anayependa kufuatilia matukio Basi  utakuwa unamjua na kumkumbuka kabisa.Kwa ujumla Tuko hapa na  mshindi wa Dunia katika mashindano ya uandishi wa hadithi za kufikirika na zisizo za kufikirika.Ambapo mashindano haya yalifanyikia huko Denmark na Marekani Yaani huko The United States of America. Aaaa Basi ni vyema nikawapa nafasi moja wapo aanze Basi katika kutoa salaam. Karibu
"Alianza Zaidu kwakusema Hivi".Habarini Jamani. Kwa Majina naitwa Zaidu Sudaysi Zaidu ni Mshindi wa Dunia katika mashindano ya uandishi wa hadithi za kufikirika na zisizo za kufikirika kwa miezi michache iliyopita. Huyu hapa "Akiwa anamgusa Zamda. Zaidu Alisema hivi".....aaaaa huyu hapa ni mke wangu.
" Zamda naye alichukua nafasi kwakusema Hivi ".Hellooo naitwa Zamda huyu hapa ni mme wangu.
" Mtangazaji Alisema "Aaaaaa bwana Zaidu Natumai ni juzijuzi tu Ndiyo mlifunga pingu ya maisha.
Ndiyo maana Yake Rami Gadi. Unajua ni vyema kuishi katika Maisha ya kiamani ya kusema tendo lenu limeruhusiwa.
Aaaaaa ni Kweli kabisaaa Zadiu. Yaani kwa namna tunavyoamini na ni utamaduni sana kwetu kwa wana Kinani kwamba ni vigumu sana Kwa nyota kama wewe kuweza Kuoa.
Aaaaaaa ni kweli watu huwa wanakuwa sana na imani kama hizo.Ila Unajua siku zote maamzi ni maamzi pindi yanapotekelezwa.Hili ni jambo ambalo nilishaweka nadhiri kabisaaa Yaani kitambo sana. Kwamba lazima nioe siyo kuishi kihuni huni tu.
Kwakweli ni maamzi makubwa Sana na ni mazuri sana Hayo maamzi yako.aaaaa eti Zamda hili suala unalichukuliaje?.
Aaaaa Kwakweli Rami Gadi niseme tu kila kitu ni mipango ya mungu. Huyu Zaidu kwakweli Tukianza kuzungumzia kuhusiana na mapenzi yetu anza kuhesabu ukirudi miaka nahisi kama miwili hivi.Kwahiyo kwa Zaidu ni mwanaume ambaye kama ni utofauti Kwakweli ni mkubwa sana anao na huo utamaduni wa mastaa wengi wa Kinani.
Aaaaaaa Zaidu vipi kuhusiana na Mambo ya kitaaluma Kwasasa umesimama Au vipi?.
Aaaaaaa hapana. Kwakweli hapo siwezi kusimama Kwasababu ni moja ya mipangilio ambayo nimeamua kwamba Kwakweli yatakikana niikamilishe kwa mda fulani.
Kwahiyo unasoma.
Ndiyo maana Yake.
Kwa namna gani.
Nasoma kama private candidate.
Ahaaaaa ila ni vyema sana kwa ndugu watazamaji nao wakapata maana nzuri ya unaposema private candidate.
Aaaa sawasawa. Namaanisha kwamba naweza kujiandikisha katika kituo chochote cha kufanyia Mtihani na Mambo ya masomo ukawa unafuatilia kwa mda wako.Kwahiyo katika kituo hicho unaweza kwenda Kwasiku pakiwa na Mtihani wowote ule wa Taifa.
Ahaaaaa. Kwahiyo kwa wewe unasoma five na six kwa mwaka mmoja sio.
Ndiyo maana Yake Rami Gadi.
Aaaaa nakupa saluti kubwa Sana Kwakweli nimekubali harakati zako si zautani utani tu.
Aaaaa Unajua Rami Gadi si vizuri sana kuridhika tu na kiti kimoja nilichonacho.
Aaaaa ni kweli in short kwasasa pia hata umri nao ndiyo Kama huo unazidi kwenda. Kwahiyo ukaamua kupiga mwaka mmoja tu.
Ndiyo maana Yake.
Daaaa hongera Sana kwa maamzi kama hayo.
Shukrani sana.
Aaaa Zaidu tutaraji nini kutoka kwako kwa msimu huu ?.
Aaaaaaa kwa ujumla shabiki zangu chakutaraji kutoka kwangu Kwakweli viko vingi Sana.
Kama vipi?.
Aaaaaa moja wapo ni kwamba kuanzia tarehe sita ya mwezi huu naanza kusambaza kitabu kipya katika maduka mbalimbali ya vitabu.
Kinaitwaje?.
Aaaaa kinaitwa SAFARI ambacho kwa ujumla cover lake nimeshaanza kulitangaza katika Mitandao mbalimbali ya Kijamii.
Ahaaaaa. Kwakweli nikupe hongera Sana kwa mapambano ambayo unayaafanya katika tasnia hii.
Shukrani sana tena Sana.
Kwahiyo hadi Sasa ni vitabu vingapi umeshaviandika japokuwa havijatoka?.
Kuna vitabu Kumi ambavyo viko tayari kwasasa viko vinapitishwa katika mamlaka husika kwa ukaguzi mzuri yaani kufanyiwa uhakiki katika Taasisi ya Fasihi Kinani (TAFAKI).
Ahaaaaa Kwanza vipite katika mamlaka husika.
Ndiyo maana Yake.
Sawasawa.
Basi ikiwa ni mishale ya saa tatu usiku. Mda huo Mama Zamda na Baba Zamda wakiwa katika sebule nzuri kwelikweli ya Jumba la kifahari walilojengena na Zaidu.Siku hiyo hata Mama Zaidu naye alikuwepo hapo ambapo alienda kuwasalimia. Kwakweli Jumba Hilo namna lilivyo siyo kama Kipindi kile Tena. Kwahiyo siku Walikuwa na maongezi kwa mda huo.Mda huo Baba Zamda alikuwa anasema Hivi.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)