MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 24 SEHEMU YA 24

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 24 SEHEMU YA 24
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU
SEHEMU YA 24
Mama samahani sana mama Mimi nataka kwenda Ngata Nina miaka kama zaidi ya mitano sijafika kwetu.Hata kama nilifukuzwa ila ndiyo hivyo.
Hivi Zamda hunielewi.
Mama.
Mama nini wewe Zamda. Unafikiri hapa nyumbani patabaki na nani?.
Sasa.
Sasa nini Wewe. Nakwambia hapa nyumbani patabaki na nani?.
Mama kwani mimi ndiyo Mlinzi wa hapa Au ?.
Heeeeeeeeeeeeeeeeee mbona kama wanijibu kunya hivyo.
Mama siyo kama ni kunya bali nataka kujua kwani Hapa nyumbani Mimi nina cheo cha ulinzi?.
Nani atadeki hapa nyumbani?.
Heeeeeeeeeeeeeeeeee mama mbona hivyo!!!!.
Nani atafua nguo zangu?.
Samahani mama Yaani hata ufanye nini Kwakweli Mimi kama ni kwenda nyumbani kwetu Lazimaaaaa niende.
Wewe siutakaaa nusu mwaka huko?.
Nitakaaje mda wote huo Wakati kule nyumbani wananijua Mimi ni mke wa mtu.
Ila Hayo maamzi ya kwenda huko Kwakweli Mimi sijayaafiki kabisaaaaaaa.
Ayiiii.Sasa mama kikubwa kabisa unachokataa Mimi kwenda kuwasalimia wazazi wangu huko ni nini ?.
Hutorudi.
Sasa nisirudi Kwanini.
Ndivyo ninavyojua hutorudi wewe.
Mama Yaani nimeishi hapa Kimbu miaka mingapi sijui hiyo alafu kirahisi tu.
Haya.Tito analijua Hilo Suala?.
Bado.
Kwanini wakati Ndiyo mume wako.?
Sawa ila wewe ndiyo mkubwa katika hii nyumba ndiyo maana nimeamua nije kwanza kwako nikuambie Lakini ndiyo hivyo nakutana na majanga tu.
Ila bado sijaliafiki hilo Suala.
Haya ila na Mimi tayari nimeshatoa taarifa.
Malumbano dhidi ya Mama Tito na Zamda yalikuwa yakiendelea Lakini bado tu mama Tito akawa anasimamia katika msimamo wake.
Amakweli mtu kuota ndoto inawezaikawa ni kutokana na mchana mzima kitu ambacho amekiongelea sana mchana au umekiwaza sana mchana.Hivyo ndivyo ndoto huwa zinajitokeza.Lakini kwa ndoto nyingine hujitokeza tu bila kujua imekujaje kujaje.
Ikiwa ni mishale ya usiku wa manani Kabisa. Mwanadada Zamda akiwa katika Usingizi Mtamu kutokana na ndoto aliyokuwa akiiota kwa mda huo.
Ndoto hiyo inaonesha kwamba yuko na wazazi wake wamekaa kibarazani hivi maeneo ya nyumbani kwao.Zamda anaonekana amejisitiri vizuri kweli kweli Yaani ni mtoto wa kiislamu kabisa.
mama Zamda anaonekana yuko pembeni na baba Zamda. Wanaongea mda huo wanafurahi kwelikweli. Basi katika maongezi ya ndoto hiyo yalikuwa hivi.
"Mda huo ni Baba Zamda ndiye anayeongea. Alikuwa akisema Hivi"Mwanangu Zamda ni siku nyingi sana tulikutupa.Ila Mateso mengi uliyoyapata pole Sana.
Asante Baba.
Nilikuwa najua hautarudi.
Kwanini Baba?.
Ni mda  mrefu sana hatujaonana mwanangu.
Ni Kweli ndiyo nimekuja hivyo Baba.
Najua tulikukosea ila ndiyo hivyo hasira hasara tu.
Haina shida baba nyumbani ni nyumbani tu hata pawe pangoni.
" Mama Zamda naye akawa anasema Hivi "Mwanangu umekuwa kwelikweli.
Wala Mama kawaida tu.
Uwe unakuja kutusalimia Bana.
Sawasawa mama.
Zile zilikuwa hasira tu.Lakini huko mnaishi vizuri?.
Ndiyo Hivyo tu wazazi  Wangu kuishi kule Kwakweli yataka moyo.
Kwanini.
Namna kulivyo tu.ila nitarudi wakati mwingine ili tuongee vzuri.
Sasa unaenda Wapi?.
Naenda kwetu.
 Hapa ndiyo kwenu mwanangu.
Sawa.
Ghafla kwa mda ule Zamda alishtuka kutoka ndotoni na kujikuta amekaa kitako kitandani akiwa anafikiria  ndoto ile inamaamisha nini.kwa mda huo Tito hakuweko hapo Kwasababu kwakisingizio alikuwa amesafiri kikazi.
Ni siku nyingine kabisa wakiwa wanaonekana Zamda na Jeni wakiwa wanaangalia Runinga hapo.Jeni na Zamda ni Marafiki wa karibu kweli kweli. Basi siku hiyo ikiwa zimebaki siku chache tu ili Zaidu Sudaysi Zaidu kuweza kurudi  kutoka huko Kwenye mashindano.Basi mda huo Zamda na Jeni walikuwa na mazungumzo ya kimipangilio kwelikweli. Ambapo kwa siku hiyo ilikuwa ni siku ya jumapili. Mazungumzo yao yalikuwa kama ifuatavyo.
Jeni Mimi Nataka nikasherehekee sikukuu ya Idd nyumbani kwetu.
Itakuwa vizuri pia Zamda. Kwasababu ni mda mrefu sana. Japokuwa Wazazi wako walikufukuza wewe nenda tu. Kwasasa hawatokuwa na Shida.
Lazima niende tu.
Vipi umeshamwambia mother?.
Nimeshamwambia.
Anasemaje.
Anakataa.
Anakataa?.
Ndiyo. Yaani Hataki kabisaaaaaaa.ila Mimi Nasema lazima niende.
Yaani huyu mother anazingua kwelikweli.
Eti anasema kwamba nikienda sitorudi.Pia hata Tito aliniambia kwamba nikienda huko nisirudi kabisaaaaaaa.
Heeeeeeeeeeeeeeeeee huyu Tito Vipi. Yaani mbona Hawa watu wana roho mbaya hivyo!.
Yaani Mimi hata siwaelewi kabisaaaaaaa.
Sasa Jeni rafiki yangu. Mimi nakwambia nenda kawasalimie wazee huko home.
Naenda Kweli.
Mama Tito akikuzingua tutajua  cha kufanya.
Sawasawa.
Kwanza siku si chache tu tayari Zaidu anarudi.Kwasababu Jana nimechati naye anasema kwamba siku si chache mshindi wa kwanza kwa awamu ya pili anatangazwa ndiyo atakuwa kama Mshindi wa Dunia.
Ahaaaaa.
Kwahiyo akirudi yule lazima aje ajenge Nyumba na utaishi naye vizuri tu.
Yaani nakwambia namuombea kwa mungu aweze kumaliza Salama na kurudi salama Huku Kinani.
Yaani nakwambia lazima atakuwa anajulikana sana.
Ila Jeni Kweli Zaidu atakubali kuishi na Mimi kweli?.
Kwanini unasema hivyo?.
Aaaaa naona Mimi Yaani kwanza hapa Nina watoto wawili.Sijui Kwakweli kama atakubali na Ndiyo Kama akishinda nakwambia sijui.
Nikwambie Kitu Zamda. Niamini Mimi Hapa. Zaidu namjua in and out Kwahiyo zaidu anakupenda kweli kweli. Zaidu hawezi kukusaliti hata kidogo. Zaidu alikuwa akiniambia sana kwamba nafasi ikipatikana kweli Lazimaaaaa akuoe.Nakuahidi Zamda.
Nipe moyo tu Jeni
Ni Sawa. Kwasababu Unajua Zamda mwanaume ambaye Ana mapenzi ya Kweli anajulikana tu.
Kwahiyo ndiyo Kama Zaidu siyo?.
Ndiyo maana yake Zamda.Mimi nakuahidi Zamda Yaani Zaidu akirudi utafurahi sana.
Haya tusubiri.
Kwani wewe hajawahi kukuelezea maisha yake ya kuhusiana na mapenzi?.
Alishawahi.
Kwahiyo kama alishawahi Kwakweli yule anakupenda kutoka Moyoni na hatokusaliti hata kama akishinda na kushika Nafasi ya 01 kidunia.
Ila Unajua Zamda Yaani mda wowote huo hata kama nikilala na Tito Yaani mawazo na saa nyingine ndoto ni kwa Zaidu basiiiiiii.
Zaidu anakudatisha sana. Yaani nakwambia. Alafu ile kipindi ile mwanzoni ukawa Unajua eti mimi ndiyo natoka naye.
Weeee kwa ule ukaribu ambao mlikuwa nao  ulikuwa unatisha sana.
Kwanini Sasa.
Yaani kama kuna siku hivi mda huo Zaidu alikuwepo chumbani kwako alafu wewe ukawa umeingia na nguo zako za kawaida Lakini nashangaa baada ya sekunde chache hivi umejifunga taulo na huko ndani ilivyokuwa ikionekana hukuwa umevaa chochote kabisaaaaaaa.
Zaidu rafiki yangu Sana. Kwahiyo wala hana hata shida.
Duuuuuuuuuuuu haya Bana.
Kwahiyo wewe Zamda jua kwamba Zaidu kukuoa ni kitu ambacho hakiepukiki.Kwasababu alikuwa ananiambia kwamba kizuizi kikubwa kabisa kilichokuwa kimekuwepo ni huyo Tito.
Ayaaaaa alikuwa anamuwaza huyo Tito Tena?.
Ayaaaa iyo kawaida Mbona. Wewe chamsingi Zamda ukiwa unaondoka jipange utaenda kuwasalimia wazazi wako na kurudi. Ukija huku wakikuzingua hapa kwa mama Tito mimi ntajua cha kufanya.
Haina shida Jeni.
Sasa hapo Ndiyo watajua kwamba Mimi nilikuwa naishi hapa kwaajili ya wewe.
Shukrani Sana Jeni.
Kuna sehemu nilikuwa nategemea hivi naweza kuhamia Kwahiyo kipindi utakachokuwa umeenda Ngata  basi Mimi nitahamisha baadhi ya vyombo vyangu ili nivipeleke huko Kati.
Ahaaaaa Basi itakuwa vizuri Jeni.
Haina shida Zamda. Mimi nakufanyia hivi ili uje kuwa mume mzuri ambaye anajielewa na kujitambua.
Sawasawa.
Kwasababu unaweza kujielewa Lakini usijitambue Kabisaaaaa.kumbuka Zamda kwa Mimi hapa mwenzako nina mchumba  Wangu ambaye ni polisi.
Ndiyo ushawahi kuniambia.
Kwahiyo na Mimi ndiyo Maana nakupigani na Wewe upate mume mzuri ambaye anajielewa.
Kama Zaidu siyo.
Ndiyo maana Yake.
Basi siku nazo hazigandi.Unaweza kuhesabu mwaka ukajikuta wahesabu miezi na mwezi,Baadaye kabisa unaanza kuhesabu siku na masaa.
Ikiwa ni siku ya Jumatatu asubuhi na mapema ambapo bibiye Zamda tayari ameshajiandaa ili kuweza kufanya huo msafara wake wa kwenda huko Ngata Kwaajili ya kwenda kuwasalimia Wazazi wake.
Lakini kwa Hapo nyumbani Kwakweli vurugushani ilikoa sana ambapo na mda huo Mama Tito alikuwepo Lakini Tito hakuwepo. Mda huo anaonekana Jeni yuko hapo nje Ambaye ndiyo Kama anataka kumsindikiza na kumpeleka hadi stendi.
Lakini kwa mda huo ambapo ndiyo mda Zamda alikuwa akimuaga mama Tito kukawa na kutokuelewana kidogo. Ilikuwa hivi.
"mda huo Zamda kambeba mwanaye wa Pili na yule mwingine ambaye Ndiye wa kwanza Ambaye Anaitwa Glady yuko hapo pembeni naye wako katika Maandilizi ya msafara. Zamda akasema Hivi".Mama Mimi ndiyo naenda hivi.
" Mda huo Mama Tito akionekana amejifunga kanga tu huku akiwa ameshikilia mswaki Ukiwa na dawa na taulo Jeupe kaliweka begani mwake.Alikuwa akisema Hivi".Unaenda wapi?.
Naenda Ngata.
Ngata Au sio?.
Ndiyo naenda Ngata. Sinilikuambia.
Unaondoka hata Tito hayupo.Wewe mwanamke huna adabu wewe.
Sasa mama sina adabu kivipi.
Unasafiri bila Tito kuwepo.
Si kasafiri kikazi.
Kikazi Eeeee ndiyo huwezi kumsubiria siyo?.
Hadi lini Sasa.
Ahaaaaa jifanye unamaamzi ya kama Hakimu aliyehongwa.
Mama Mimi ndiyo nakuaga Hivi.
Sasa nikwambie Kitu siunajifanya unaenda kwenu eee. Utajuta kuzaliwa Wewe.
Sasa mama Mimi sininaenda  kwetu kuwasalimia.Heeeee kwani mimi hapa mtumwa?.
Yawezekana.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 2 Guest(s)