MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 23

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 23
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
         
    SEHEMU YA 23
      Sasa Tito utaondokaje wakati huu ndiyo mda wetu kwa Mimi na Wewe kuweza kujadili mambo ya familia.
"Mda huo Tito ameshainuka na akaenda kusimama mlangoni. Anaongea na Zamda huku akiwa anaangalia nje Bali si kumuangalia yule anayeongea naye.Kisha Tito akasema Hivi"Kama vile mambo gani?.
Mambo kama vile haya tunayoyazungumzia.
Yamefanyaje Sasa Zamda?.
Hivi wewe Tito unavyorembwa Yaani utafikiri mtoto wa mfalme anayetawala Bara zima.Mbona hivyo Alaaaaa Eeeeeee mungu Eeeeeeee nisaidie miyeeeee?.
Nakweli Mimi mtoto wa mfalme.
Lakini Kwakweli Tito aliamua kutoka nje na kwenda huko kijiweni kwa Marafiki zake na kwenda kunywa pombe. Nyumbani kamuacha Zamda kabaki analia tu.Zamda akawa anasema Hivi.
Eeeeeee Mungu WANGU nipe uvumilivu tu wa hadi Zaidu arudi kutoka huko aliko.Kwasababu kwa maisha haya ninayoishi hapa utadhani nimeletwa hapa kama mtumwa Yaani vile kumbe mchumba wa Mtu kabisa. Natamani kuyatoa maneno Lakini nahofia wapo nitajihifadhi nikifukuzwa.ila yatakwisa tu.
Ikiwa ni mishale ya saa saba mchana siku ya jumapili. Mda huo wakiwemo nyumbani Zamda,Jeni,Mama Tito na Tito mwenyewe wakiwa wanaangalia Runinga. Kwenye Runinga kuna kiongozi alikuwa akifanyiwa mahojiano na kituo kimoja hivi cha kurusha matangazo. Kituo hicho Kilikuwa kinaitwa SAKAS.COM TV.Kiongozi aliyekuwa akifanyiwa mahojiano alikuwa ni waziri wa habari michezo sanaa na utamaduni Bwana Sinjaro Busunga.Kiongozi huyo ndiyo yuko sanjari katika kuweza kuwaangalia washiriki kutoka Kinani walioshiriki katika mashindano ya uandishi wa hadithi za kufikirika Au zisizo za kufikirika.Kwahiyo siku Waziri huyo wa kitengo hiki alikuwa anahojiwa na mwandishi wa habari wa runinga iliyokuwa ikijulikana kama SAKAS.COM TV .Mwandishi alianza kuongea Hivi.
Aaaaaaaaaaaaaaa Natumai Ndugu mtazamaji na msikilizaji uko bukheri wa afya Kabisa. Aaaaaa pembeni yangu hapa aliyoko ni waziri wa habari michezo sanaa na utamaduni. Yuko hapa kwakuweza kuongea na SAKAS.COM TV machache kuhusiana na washiriki wa mashindano ya uandishi wa hadithi za kufikirika na zisizo za kufikirika. Aaaaa mheshimiwa waziri wa habari michezo sanaa na utamaduni Karibu Sana katika kipindi chetu hiki cha Mada kuu.
Shukrani sana Ndugu mtangazaji.
Aaaaa Mheshimiwa waziri Natumai wewe ndiyo Kama kiungo wa Mambo yote kwasasa kutoka Kinani katika Mambo ya sanaa yanayoendelea kwasasa huko ughaibuni.
Aaaaa. Ni Kweli Ndugu mtangazaji. Kwasababu hiyo Ndiyo Kama nafasi yangu niliyo nayo na ndiyo niliyochaguliwa na Mheshimiwa Rais.Kwahiyo lazima niifanyie kazi hii kama ipasavyo.
Mheshimiwa waziri Aaaaaa embu watu wengi wanataka kujua kwa undani ni namna gani haya mashindano yanafanyika.Kwasababu kwa mda waliotengewa ni mda mrefu Sana. Ambao hata ni kama kombe la dunia linaweza kuchezwa na kumalizika kabisa.
Aaaaaa Ndugu mtangazaji niseme tu mashindano haya ni mashindano ya kiupekee kabisaaaaaaa. Yaani ni mashindano ambayo yako tofauti na mashindano ambayo yalishawahi kutokea miaka ya nyuma.
Aaaaa Kwahiyo Mheshimiwa waziri unapoongelea upekee wa haya mashindano ni upi huo?.
Aaaaa Ndugu mtangazaji. Upekee......aaaaa...upekee wa mashindano haya ni kwamba Kwanza tuseme yako katika sehemu Mbili Yaani awamu mbili.
Samahani Mheshimiwa waziri.
Bila samahani.
Aaaaaa hapo Sasa kwenye sehemu Mbili Au awamu mbili napo ufafanuzi wa ndani unahitajika.
Sawasawa, Ndugu mtangazaji awamu hizi zinajitokeza Kwasababu Kwanza kwa awamu ya Kwanza ya mashindano lazima kutakuwa na mchujo Ambao huo ni ndani ya huo mwezi mmoja na siku kazaa hivi. Kwa mwezi huo na Kwa awamu hiyo inafanyikia huko nchini Denmark na hapo patatakiwa papatikane mshindi wa kwanza hadi wa Kumi.
Embu samahani mheshimiwa waziri. Aaaaaa Yaani kwa washindani wote waliochaguliwa wale.
Ndiyo maana yake.Yaani pale panahitajika ustadi mkubwa sana katika kuweza kuzipata nafasi hizo.
Aaaaa vipi kuhusiana na zawadi kwa wengine.
Aaaaaaa kuhusu suala la zawadi kwa namna walivyopanga kila mshiriki tu wa shindano hili lazima apatiwe Laptop moja na vifaa vyake.Hiyo ni tofauti na kuwa mshindi wa kwanza Au na kuendelea pia.
Ahaaaa hapo kuna kazi kubwa.
Ndiyo ndiyo.
Kwahiyo Mheshimiwa waziri kutangazwa kabisa kwa mshindi wa  kwanza ni ile awamu ya pili ambayo Ndiyo ya mwisho?.
Ndiyo ndiyo. Kwasababu hiyo ni baada ya kupatikana kwa wale washindi kumi. Yaani kuanzia mshindi wa kwanza hadi wa Kumi wote hao wataingia katika dimbwi la Pili au awamu ya pili.
Alaaaaa.Mheshimiwa waziri Kwahiyo kwa awamu hiyo ya pili Ndiyo ya lala salama
Ndiyo ndiyo. Kwasababu hapo patahitajika kupatikana washindi watatu tu.
Yaaani kabisa watatu tu?!."mtangazaji huyo akiwa anaongea kwa kuonesha vidole vyake vitatu.Kisha Mheshimiwa waziri akasema Hivi "
Ndiyo hivyo watatu tu.
Je Mheshimiwa waziri vipi kuna dalili zozote kweli Kwa washiriki kutoka Kinani Ambao wanapasua mawimbi sana huko?.
Ahaaaaa wako.Yaani wako.Kama Jana ndiyo nimetoka Denmark ambako Ndiyo awamu ya Kwanza Walikuwa wakiifunga na washiriki wote wakawa wamezawadia zawadi Hizo ambazo ni laptop.Mshindi wa kwanza ambaye alikuwa katika lile Kumi bora alikuwa ni kutoka Kinani ambaye Yeye ni mzaliwa wa Domado Lakini alikuwa akiishi Kimbu.
Aiseeeee Anaitwa nani huyo?.
Ni kijana mdogo mdogo tu hadi hutoamini ambaye Ndiyo alimaliza masomo yake ya kidato cha nne mwaka Jana na amefaulu ambaye anaitwa Zaidu Sudaysi Zaidu.
"Mda huo Jeni baada ya kusikia vile alifurahi sana kwa rafiki yake kipenzi ambaye ni Zaidu kushika nafasi ya kwanza. Zamda naye furaha ya moyoni ilimwijia na Tabasamu la mbali aliweza kulitoa.Mda huo kwenye Runinga pakawa panaonesha picha ya mshindi wa kwanza ambaye ni Zaidi Sudaysi Zaidu.Ndipo Jeni akawa anasema Hivi ".
Heeeeeeeeeeeeeeeeee mbona kweli Zaidu huyu."mama Tito akawa anasema Hivi".
Huyu si Ndiyo yule kijana ambaye alikuwa anakuja Mara kwa Mara hapa kwako kukusalimia?.
Ndiyo Yeye Huyu.Nakweli amefaulu.
" Lakini mda huo mheshimiwa waziri akawa anaendelea kusema hivi ".Huyo Ndiyo mshindi wa kwanza.
Ndugu mtazamaji hiyo Ndiyo picha ya Zaidu Sudaysi Zaidu ambaye  ndiye mshindi wa kwanza kutoka Kinani kwa awamu hii ya Kwanza. Kwahiyo Mheshimiwa waziri tuseme Zaidu Yeye anajua lugha nyingi sana au Vipi.
Lahashaa.
Bali.
Aaaaaa Kwaujumla kule katika mashindano kuna vifaa ambavyo vinamuwezesha mshiriki kuweza kuandika hadithi yake Kwa lugha yake na baada ya hapo hadithi ile inahifadhiwa Kwenye mahshine ile na inakuwa katika lugha mbalimbali.
Sasa Mheshimiwa waziri nini haswaaaa wanachokiangalia katika kuweza kumpata mshindi Huyo.
Aaaa Ndugu mtangazaji kikubwa kabisa ni katika lugha yako unavyoitumia,Pia mda.
Aaaa mheshimiwa waziri katika mda ni kivipi hapo?.
Hapo wanaweza kusema Kwamba washiriki hao kila mmoja aandike hadithi yoyote ile kwa ndani ya nusu saa nyenye kurasa kazaa ambazo watakuwa wamepangiwa.Kwahiyo mshiriki akishamaliza tu kuandika anaituma katika sehemu ya uhakiki na baada ya hapo inahifadhiwa na mchujo unaanza kufanyika.Yaani hapo kama ni wachambuzi wa kazi hii ya fasihi Kwakweli wako vizuri.
Sawasawa.
Kwa namna navyomuona yule kijana lazima achukue nafasi ya kwanza na Kinani itakuwa na furaha kubwa Sana. Kwakweli Zaidu ni Kijana ambaye kwanza anashangaza watu sana pale Unajua Ndugu mtangazaji.
Ndiyo Ndiyo.
Yaani speed yake Kwakweli ile ni ya supersonic speed Kabisa. Anaandika kwa Haraka na hadithi zake nyingi sana ni za kubuni. Yaani Wakati wa uchambuzi hadi wachambuzi wanashangaa Sana kwa kazi aliyoifanya.Kwa Mimi tu ninaahidi kwamba akishika nafasi ya kwanza kwakweli Tena lazima nitampatia zawadi kubwa Sana ukiachana na hizo tunzo atakazopewa.Kwasababu Yeye Atakuwa ni Mshindi wa dunia.
Kwakweli mheshimiwa waziri hapo utakuwa umeonesha hamasa kubwa Sana kwa vijana wengine kuwa na ujasiri kwa nafasi kama hizi zinapojitokeza.
Kweli kweli.
Kwasababu kijana kama Zaidu Ana kipaji chake kwelikweli pia kutokana na ujasiri wake ndiyo umemfanya hadi kufikia pale.
Ni kweli Ndugu mtangazaji. Kwasababu angeleta uoga uoga Kwakweli asingefikia kuwa katika ngazi hii.
Kwelikweli.
Pia kwa siku ya Jumapili atakuwa anafanyiwa interview na chombo Fulani hivi cha Habari cha Marekani.Nitaenda naye.
Kwahiyo na wewe utarudi huko.
Ndiyo ndiyo. Siku ya Ijumaa nitapanda ndege hapa ili hiyo siku ya jumapili jioni hivi ndiyo muda atakaofanyiwa interview.
Shukrani sana Mheshimiwa waziri kwakutupatia maelezo Zaidi kwa haya mashindano. Kwa Mimi napenda kusema Kwamba ukifika huko Marekani Kwakweli mpe hongera Sana na pia mwambie wana Kinani wanamuombea Sana mungu aweze kupeperusha Bendera ya Kinani.
Sawasawa zitamfikia zote hizo.
Kwakweli kwa mda ule Jeni alifutarahi sana kwakusikia taarifa ile huku Zamda Tabasamu likiwemo kwa mbali na furaha yake moyoni. Kwasababu hapo Tito yuko Kwahiyo ndiyo maana Zamda hawezi hata kuongea chochote.
Ni siku nyingine hivi  Wakiwa wanaonekana Nunu na Tito wamesimama njiani wakiwa na maongezi. Mda huo kuna mwanadada anamsubiria Tito Hapo.Nunu akiwa anaongea kwa sauti ya chini kidogo alikuwa anasema Hivi.
Tito huyu mdada hapo ni nani?.
Aaaaa...huyo mdada sio?
Ndiyo Au nimesemaje?.
Huyu mdada ni rafiki yangu tu.
Rafiki yako sio?.
Ndiyo.
Ukweli Kabisaaaaaaa kwamba ni rafiki yako huyu ?.
Ni Kweli kabisa.
Tito siamini.
Huamini nini Sasa Nunu.Huyu mdada ni rafiki yangu tu anaitwa Chawote.
Amakweli Chawote.Hivi wewe Unajua mme wa mtu kabisa.
Kwani..kwani Nunu wewe unahisije Mimi na huyu mdada tukoje Yaani ?.
Kama mnauhusiano Hivi.
Uhusiano wa nini?.
Wa Kimapenzi au mwingine upi?.
Sidhani....ila ....
ila nini Sasa. unajua Tito unachomfanyia yule mchumba Wako si kitu chema kabisaaaaaaa. Embu mhurumie bana.
Haya bana.
ila huyu mdada mimi najua asilimia mia kabisa ni demu wako.
Bana Weee Nunu mbona kama tunazinguana hivi.
Haya Sasa mnaenda wapi na huyo rafiki yako badala ya kwenda na mke wako Pale.
Hapo kati tu.
Kati wapi wakati unampeleka guest wewe.
Duuuuuuuuuuuu naona kama hunielewi.
Sawa. Ili nijue kama ni rafiki yako Kweli tulia nikukumbatie na nikuchumu.
Acha bana Hayo Mambo Bana.
"Nunu nakweli akawa anamlazimisha kumkumbatia Tito na kutaka kumchumu Ghafla yule mwanadada akamuona alikasirika na kusema".
Tito unafanyaje hapo.wanisaliti hadharani kabisaaaaaaa.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)