MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 21

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 21
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
         
SEHEMU YA 21
Zamda akawa amefungua geti ili Tito aweze kuingia.Lakini chakumshangaza Zamda ni kwamba anakutana na Tito amelewa ile mbaya,Nguo zake hazifai kabisa ndiyo hivyo miguuni huko yuko peku peku tu.Kwasababu kwa njia aliyopita kuna mateja na vibaka wa kutosha kweli.Kwahiyo hawakumwacha salam.
Zamda alibaki akiwa ameshika mdomo tu huku Tito akiwa anaingia ndani anayumba yumba tu.Zamda akamsemesha hivi.
Sasa Tito nani kakunywesha pombe Hivyo?.
"akiwa amesimama mlangoni kajishikiza huku bado anayumba yumba tu.Jeni pamoja na wadogo wa Tito wakawa nao wameinuka wakiwa wanamuangalia huyo Tito namna alivyolewa chakari.Kwahiyo Tito akawa anasema Hivi".Mdomo Wangu Ndiyo umeninywesha pombe yote hii Kwakutumia mikono yangu.
Simaanishi Hivyo.
Ulikuwa Unamaanisha nini Sasa.alafu wewe mwanamke wewe unaleta utani na Mimi."Mda huo Tito anamnyooshea  kidole Zamda naye Zamda akawa amesimama kwa makini asije akapigwa.".
Namaanisha nani kakununulia pombe?.
Kwani nini kinanunua pombe?.
Ndiyo nimekuuliza swali wewe unijibu.
Heeeeeeeeeeeeeeeeee wewe una vituko kweli kweli. Hivi unaitwa Zamda eeee.nimenunua kwa hela yangu Mwenyewe. Yaani Hela kutoka kwenye jasho langu."Mda huo kaamua kwenda kukaa Kwenye sehemu ambako ndiko alikokuwa amekaa Zamda."
"Zamda akawa ameshangazwa na maneno ya Tito kisha zamda akamuangalia Jeni na Jeni akawa ameshangaa. Zamda akamuuliza Tito Hivi".wewe siumekuja leo na ukasema hauna Hela ila umekuja na Hela Kidogo tu Au si wewe ?.
Nahisi una Majibu sahihi.
Ambayo Majibu sahihi ndiyo yapi?.
" mda huo Zamda kakaa karibu na alikokaa Jeni. kisha Tito akawa anasema Hivi ."Siumesema nimekwambia Nina Hela Kidogo?.
Ndiyo.
Kwani nilikuambia sina Hela. Kwani Hela Kidogo haiwezi kununulia pombe?.
Sasa Tito.
Sasa nini wewe embu niache bana Mimi nimechoka zangu. Yaani sitaki makelele kabisaaaaa."Mda huo anaamua kujilaza kwenye kochi alilokuwa amelala".kisha Zamda akawa anasema Hivi ".
Haya viatu viko wapi Au Ndiyo umeviuza ukanywea pombe?.
Hivi wewe Zamda unanichukulia poa Sana Au siyo?.
Nimekuuliza tu kwani ugomvi kwani?.Nimekuuliza viatu viko wapi Basi nijibu Majibu kutokana na swali langu lilivyo tu.Inawezekana umepita njia mbaya.
Ndiyo Majibu yake Hayo.Tena Majibu sahihi Sana.
Heeeee tuseme wamekupokonya viatu ?.
Nahisi nimeshakujibu tayari."mda huo Tito akaanza kutapika tu Hapo hapo sakafuni ikawa tena ni kazi kwa Zamda kuanza kudeki.Wadogo zake Tito mda huo wakawa wamekimbilia ndani kwenda Kulala.
Tukirudi huko mkoani kihangu nyumbani anakoishi huyo Kitunda.Ambapo ndiyo Kama siku iliyofuatia. Siku hiyo Kwakweli ilikuwa ni siku mbaya sana kwa Kitunda hadi alijuta kuzaliwa katika dunia hii yenye wanaadamu wenye kufanya Mambo ya Kharamu.
Siku hiyo ikiwa ni asubuhi asubuhi wazazi wake siku hiyo walimuinukia Kitunda kwa Mkono wa kushoto.Basi wakionekana wakiwa maeneo ya nyumbani. Kitunda kavaa dera fulani hivi,Baba Kitunda mzee wa suruali tisheti nyeupeee na mama kavaa gauni kubwa lililomfanya aonekane kama mchungaji wa ng'ombe katika maeneo ya kwenye majani makubwa na yenye kuwasha.
Maswali yalikuwa yakimlenga huyo Kitunda. Baba Kitunda akawa anamuuliza Kitunda Hivi.
Hivi wewe Kitunda  Tangu umepata Hiyo mimba hatujawahi kumuona huyo mwanaume. Mmmh huyo mwanamme Au anafanya kazi nje ya Nchi?.
Hapana yuko hapa Hapa Kinani.
Kinani kabisaaaaaaa.
Ndiyo Baba .
Sasa nataka leo leo tumuone Hapa. Kwasababu Wewe naona kama Unataka kutuchanganya akili.
Hayupo.
"mama Kitunda na baba Kitunda wakauliza kwa pamoja kwa kusema hivi".Hayupo?.
Ndiyo, hayupo .
" mama Kitunda akasema Hivi ".Unavyosema hayupo Basi itabidi utuambie wapi aliko.
Kasafiri.
" Mama akamuuliza Hivi ".Yaani kakutaarifu kama Kasafiri?.
Hapana Mama.
Kwanini?.
Kwa ujumla tu yule kijana amekimbia na nyumbani kwao ni huko Kimbu.
" Baba Akaamua kuingilia mada kwakusema Hivi ".Kakimbia?.Yaani Kabisaaaaa Kakimbia .
Ndiyo Baba.
Tangu lini.
Jumapili.
Heeeee heeeee Sasa Mwanangu Kitunda nini hiki?.
" Baba Kitunda akasema Hivi "Sasa siulikuwa unaringia huo uzuri wako ndiyo Hivyo Sasa utachoma mahindi hapo mjini mpaka useme YES ndipo utajua kwamba haya Maisha siyo mlegezo legezo tu.
Sasa Kitunda haya Maisha umejitakia Mwenyewe. Mbona mwanzoni ulituambia mwenyewe kwamba huyo mchumba wako Hana shida.
Ndiyo nashangaa.
Wewe na wewe umezidi Mambo ya kishenzi shenzi sana.Sasa utajua wapi huyo mtoto huko tumboni atapatia chakula. Ukajiuze Au  ufanyaje juu yako.Wewe tayari ushakuwa ni mbwa koko ambaye hatulii nyumbani kwao.
Basi ikiwa ni siku nyingine kabisa wakionekana Kitunda na Hanunu wakiwa wamekaa maeneo ya Nyumbani kwa kina Hanunu. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya jumapili. Basi maongezi yao yalikuwa kama ifuatavyo.
Hivi Kitunda kuna kitu wanichanganya akilini mwangu.
Kitu gani hicho.
Wewe kuna siku uliniambia kwamba ukiwa hapa mjini usikaze kiuno kwamba nilegeze kiuno.
Ndiyo nilishawahi kukuambia.
Sasa mbona faida yake siioni kwako.
Kivipi Yaani?.Kama vile sijakuelewa vizuri.
Yaani namaanisha kama ni hela sasa ulikuwa unapeleka wapi?.
Yaaani shoga yangu ndiyo  hivyo nilijua Mimi sitochuja hata siku moja .
Hata siku moja haiwezi kutokea Hivyo Kitunda. Nguo yenyewe imetolewa kiwandani na mwisho wa siku itachuja tu.Sasa Ndiyo ije kuwa wewe.
Mbona kama wanichamba Hanunu?.
Sikuchambi.
Bali unanifanyaje.
Nakwambia tu Ukweli. Haya zile hela za kipindi hicho ziko wapi.
Yaani Hanunu nikwambie tu Ukweli wewe kama shoga yangu. Hela ya mwanaume anayekuhonga sidhani kama inakaa.
Kivipi Yaani?.
Yaani labda uwe tu na akili ya kuzitumia vzuri tu  hizo Hela.Kwasababu tuseme tu ile Ukweli kuna siku niliwahi kuambiwa Kabisa nichague gari ninayoipenda.Huyo jamaa ni ana Hela kwelikweli. Lakini mwisho wa siku nikawa nimechukua Hela.
Alafu Hizo Hela ukazitumiaje?.
Nizitumiaje wapi?.Ndiyo hivyo tu najifanya na Mimi naenda na Wakati Haraka naenda kwenye maduka ya fashion za nguo za bei ghali. Si ninajua kwamba hizo Hela nitapata tu.
Jamani Hivi Unajua Kitunda kama ni kuangushia shilingi chooni ndiyo hivyo uliichezea hiyo shilingi huko chooni na Sasa ndiyo Hivyo imeangukia chooni.
Yaani kwa ujumla Hela za kuhongwa ni sawa na kamari tu.Yaani hapa Hanunu wazee hawaelewi hilo suala la Tito kukimbia na kuniachia huu mzigo. Yaani Wanasema hawatonitolea msaada wowote. Kwahiyo Yaani kwasasa itabidi hata nifungue sehemu ya kuuzia mahindi tu.
Ziko nyingi tu za kuuzia mahindi ila Sasa siutaumia sana Kitunda?.
Sasa nitafanyaje kama Ndiyo hivyo wazee wanazingua?
Amakweli maji ya moto yamekuwa baridi.
Kwakweli hali halisi ya maisha ya Kitunda ndiyo hivyo ilivyoanza kwenda mrama.Pia yote hiyo ni kutokana na kutokuwa na matumizi mazuri tu ya kifedha.Kwasababu kama anavyojitapa kwamba alikuwa akipata fedha sana kwakuwachuna wanaume kama vile Tito Lakini matokeo yake ni kwamba Hela zile za wanaume wote nazo zikamchunia moja kwa moja baada tu ya kupewa mimba na Tito ambaye alimuamini Kweli Kweli.
Basi ikiwa ni Siku nyingine Kabisa ambapo ni siku ya jumapili mishale ya saa Tano asubuhi.kijana Tito anaonekana yuko chumbani akiongea na mtu kupitia simu.Sauti hiyo iliyokuwa ikisikika kwenye simu ilikuwa ni sauti ya kike.Kwahiyo mda huo anavyoongea yuko kitandani.Mtu aliyekuwa akiongea naye alikuwa anamuita Fei.Maongezi yalikuwa hivi.
Sasa Fei lini hata tuende mahali vipi tukapumzike ?.
Yaani tukapumzike kivipi?.
Aaaaaa siku hiyo ndiyo itajulikana vizuri.
Alafu tukienda huko nini kitafuatia?.
Yaani madhumuni ya kwenda huko siyo?.
Ndiyo.
Kikubwa ni tuburudishane tu Yaani tupeane utamu tu.
Aaaaa kama ni hivyo si bora uje tu hapa hapa nilipopangisha au nije hapo kwenu ?.
Hapa kwetu haifai.
Kwanini haifai.
Mother anakuwepugi hapa siku za weekend hivi Kwahiyo itakuwa ni vigumu Sana.
Ahaaaaa. Basi njoo hapa kwangu tu.
Kweli kabisa nije hapo Kwako.
Ndiyo ni wewe tu utakavyoamua Lakini. Kama utaona vibaya twende huko unakotaka.
Haina shida huko huko.
Basi sawa.
Kwahiyo hata kama ni Kulala huko naweza kuja tulale kabisa usiku mzima.
Nakwambia ni wewe tu utakavyoamua Tito.
Sawa.Basi leo hii hii Mimi ntakuja huko."Tito anavyoongea vile ghafla Zamda anajitokeza akiwa amemshika mwanaye anataka kuja kumlaza.Anakuta Tito anaongea na simu na sauti inayosikika Kwenye simu ni ya msichana. Mda huo Tito wala hakuogopa chochote kwamba Zamda atasemaje. Kwahiyo akawa anaendelea kuongea na simu tu. Mda huo Zamda anamlaza mwanaye Kwenye kitanda. Kisha Fei ambaye alikuwa anaongea na Tito akamjibu Tito hivi".
Ni wewe tu utakavyoamua kuja leo hii hii Au leo nyingine.
Haya bana.Mimi ntakuja leo hii hii.
Mida ya saa ngapi?.
Jioni nitakujulisha.
Baada ya hapo Tito akawa amekata simu na kisha Zamda akamuuliza swali bwana Tito. Zamda akiwa amesimama pembezoni mwa kitanda. Alisema.
Tito unaongea na nani?.
Swali gani Hilo wewe unaniuliza bana Weee.
Ndiyo nataka kujua ulikuwa unaongea na nani?.
Mtu Fulani hivi.
Yaani Nataka kujua ni wa kike Au kiume?.
Ndiyo wataka kujua hicho siyo.
Alafu mbona Tito wanifanya Mimi kama mtoto."Mda huo tayari Zamda hasira zamwijia kisha Tito akasema Hivi "
Mtoto,...mtoto kivipi?.Labda wewe ndiyo unahisi kwamba Mimi nakufanya mtoto.
Nakuuliza Tito Huyo  uliyekuwa ukiongea naye ni wa kike Au wa kiume?.
Wa kike.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)