MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 20

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 20
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
         
SEHEMU YA 20
      Mda huo Zamda anavyoingia chumbani kwa Jeni tayari na Tito naye akaamua kutoka na kuelekea mtaani huko Kwenye vijiwe vyake ambavyo huwa anavipenda.Pia na kwa wapenzi wake wa zamani ambao hakuwaona takribani kama mwaka mzima hivi.Zamda aliingia chumbani kwa Jeni na maongezi yakawa yamekuwa hivi.
"Mda huo Zamda amekaa kitandani huku akiwa amempakata mwanaye na Jeni alikuwa amelala kitandani na kujifunika shuka kabisa.Alikuwa akisema Hivi"Shoga yangu Jeni.
Vipi wewe mbona unakuja huku?.
Sasa unafikiri shoga wangu nije Wapi?.
Siukae na mme wako huko!!.
Atiiiiii,nakwambia Mambo mengine yaacheni kama yalivyo tu.Amakweli ukishangaa ya Musa utasitaajabu ya firaghuni.
Kwanini Zamda unasema hivyo?.
Hivi Unajua huyo Tito anasema hajaja na hela ya kutosha, Yaani Unajua nimeishiwa na nguvu.
Hajaja na hela "Jeni akawa ameinuka Kutoka kitandani kisha akawa amekaa kitako huku akiwa ameegemea mto kwa Upande wa ukutani".
Ndiyo maana yake.Wewe unafikiri hadi Mimi nimekimbilia huku ninini?.
Loooooo.sasa hapo shoga yangu kuwa na akili.Wewe mwanaume mzima Kabisa anasafiri kikazi kama mwaka mzima Kabisa alafu eti unarudi kabisaaaaaaa Ukisema kwamba sina chochote.
Unajua Jeni Mimi nashangaa sana.
Unajua Zamda inawezekana huyu jamaa anapenda kuhonga wanawake Sana. Kwani mimi wanaume wanaopenda kuhonga sinawajua walivyo.
Yaani wakoje Jeni, Embu niambie Kwasababu ndiyo maana hata sielewi kinachoendelea.
Wewe kuna Wanaume wakishapata mshahara wao katika asilimia kubwa zaidi huwa wanautumia kwenye Masterehe tu.
Kama zipi?.
Ndiyo Kama hayo Mambo ya kuhonga wadada wa watu na kuwapeleka kwenye hotel kubwa,pombe kwa Sana. Yaani kwa hapo unajikuta nusu ya mshahara wake anautumia Kwenye Mambo kama hayo ambayo ni yanamaliza Hela Sana .
Yaani mbona ni Hatari sana hii Sasa.
Alafu Jeni kuwa makini.
Kwasababu gani?.
Weee huoni kwamba kama Tito kweli anachepuka huko nje kuna uwezekano wa magonjwa kwa wewe kuyapata.Kwahiyo Kuwa makini Sana.
Ayaaaa kweli Jeni.
Mambo ya kwenda hospitali na kuambiwa una UKIMWI alafu wewe hata michepuko haunaga sana sijui itakuwaje hapo.
Daaa kweli Jeni umenifungua kichwa.
Kwahiyo ndiyo hivyo kuwa makini.
Sawa Jeni.Sasa Jeni Mimi nitafanyaje Jamani. Embu leta simu yako nichati na Zaidu, mume wangu mtarajiwa.
Zamda simu hiyo hapo. Kweli chati  nae hata umfurahishe kwelikweli na yeye atakufurahisha.Alafu Alisema kwamba mda wowote atakaokuwa huko nchi za nje hatokuwa anazima simu yake mara kwa mara na data  hatokuwa anazima.
Kumbe bana huyo Tito alivyotoka hapo na Yeye akawa ameamua kwenda kwa Mpenzi wake wa zamani ambaye ndiyo huyo aitwaye Nunu.Kwakweli Nunu na Tito uhusiano wao wa Kimapenzi ulikuwepo tangu kipindi Zamda alipopata mimba kwa mara ya pili.
Mda  huo wanaonekana wako kitandani kila mtu amekaa kwa Upande. Maongezi yao yalikuwa hivi.
Mmmmh! Kwahiyo Tito. Duuuuuuuuuuuu pole Kwanza na Safari.
Asante.
Umekuja leo kabisaaaaaaa Au lini?.
Leo.Kwanini umeniuliza hivi?.
Kwasababu.
Kwasababu gani sana za wewe kuniuliza swali kama hilo?.
Ahaaaaa. Umekuja tu leo tayari unakuja hadi huku na unamuacha mke wako mtarajiwa Pale.
Nani Huyo?.
Si yule mke wako wa kingata pale nyumbani.
Ahaaaaa yule siyo.
Ndiyo Yeye.
Yule ashachakaa bana.kwasasa inabidi niwafuatilie Watoto kama nyiye.Bado Viuno mchelechele tena Mbele Mbele macho kodooooo.Alafu tena waniambia nini?.
Sasa Tito kwanini unasema ameshachakaa Wakati ni wewe ndiyo umemchakaza mdada wa watu?.
Kwani Yeye si ndiyo kataka.
Sawa ila ni wajibu wako wewe kumhudumia.Kwa mda huu ilitakikana ukae nae Karibu hata uwe una mpa moyo na Yeye kweli anajiona ana mwanaume. Sasa pale hata akichepuka nani atakuwa ana makosa.
Bana Eeeee  Nunu huko hiyo mada embu siitaki.
Huitaki kivipi.Huo ndiyo Ukweli kabisa. Yaani kwanza umepata Mtoto wa kingata mzuri mda wowote yuko ndani kakaa katulia tuliii kama maji ya kwenye mtungi.sijawahi kumuona huku mtaani akiwa na michepuko yake.Kwaujumla sidhani kama atakuwa na mchepuko hapa Loronjo. Labda Wewe ndiyo utakayemfanya mwenzako awe na akili za kuchepuka japokuwa alikuwa hafikirii Hayo Mambo.
Unajua Nunu sikuelewi.
Siyo kwamba hunielewi.unanielewa vizuri tu tatizo ni wewe hutaki tu kufikiria ili uweze kunielewa.
Duuuuuuuuuuuu yashakuwa makubwa Sana.
Ndiyo Hivyo. Mwanzoni Mimi nilikuwa nafurahi sana kwamba wewe kuwa na Mimi kwa mapenzi ya kuiba iba tu Lakini kwasasa najua uchungu wake.
Unamaanisha nini unaposema Unajua uchungu Wake?.
Namaanisha nilichotaka kukisema.
Kitu gani?.
Kipindi kile mdada wa watu umempa mimba sijui ilikuwa ya pili ile ukawa unakuja kwangu.Mimi sikuwa najua ule uchungu.ila kwasasa ule uchungu naujua.
 Upi huo.
Wa kama Kipindi ambacho alikuwa nacho kipindi hicho.
Yaani ukimaanisha Nini?.
Alivyokuwa na mimba.
Nani huyo?.
Si yule mke wako. Mbona kama wajifanya huelewi. Umenielelwa vizuri hapo?.
Kidogo.
Sawa,Unataka vikubwa?..
Ndiyo.
Nina mimba
Duuuuuuuuuuuu Nunu una mimba !!!???.
Ndiyo unashangaa nini Sasa?.
Kwani Nunu tulikubaliana nini mwanzoni.
Hivi  wewe Tito Natumai hujanielewa kabisaaaaaaa kuanzia tulivyoanza kuongea.Nimesema hivi ilifika Wakati nikaona kwamba ninachomfanyia huyu mwanamke mwenzangu si kitu kizuri. Acha na Mimi niwe na wangu wa ubani maalumu basiiiii.Siyo tena Mambo ya kuhangaishana huko siyataki.
Kweli kabisaaaaaaa una mimba ???!!!!!
Ndiyo huamini au kwa vile nimevaa dera ndiyo maana hata huamini. Tulia nikufunulie tumbo langu ulione Kwasababu si ushawahi kuliona tu."Nakweli Nunu anaonekana anainuka na kisha akawa amepandisha dera lake juu hadi kifuani kisha akaanza kumwambia Tito hivi ".Umeshajionea mwenyewe Au siyo.
" Tito kabaki kaduwaaa tu huku Nunu akiwa anajifunika tayari kisha Tito akasema Hivi "Yaani Nunu siamini ulichonionesha hapa.
Ndiyo Hivyo. Huu si mfano na wala si picha Bali na kitu halisi Yaani chenyewe Kabisa. Mimba ya miezi minne.
Kwahiyo kabisa Nunu kwasasa wewe siyo Mpenzi wangu kabisa?.
Ndiyo jibu lake hilo kabisaaaaaaa. Pigia na msitari wa kalamu ya bluu ili nyekundu ipite kusahisha kabisa. Wewe ulikuwa ni Mpenzi wangu Yaani Nimeongea kwa Wakati uliopita.
Sasa mbona ulichukua maamzi ya Haraka Hivyo?.
Ndiyo hivyo maamzi yangu yalifikia hapo.Haina haja ya kumfanyia mtu jambo Fulani ili nifurahishe moyo wangu wakati Kwake namkwanza Yaani naukwaza moyo wake.
Lakini.
Lakini nini Tito ndiyo imekuwa Hivyo. Inabidi hata mda mwingine uwe unakuwa na ile hofu hata ya mungu. Yaani wewe unataka kila mwanamke mzuri utakayemuona umpe mimba.Wewe nani weeeeee.wewe mtoto wa mfalme?.
Jamaa aliyekupa mimba anaitwa nani ?.
Anaitwa Jori
Jori ninayemjua mimi ?.
Ndiyo tena umecheza naye Kipindi cha utotoni.
Daaaa kabisaaaaaaa Jori yule rafiki yangu ndiyo kaamua kufanya hivyo.
Sasa wewe Tito unachotaka ni nini?.Kwasababu msichana wa watu yule pale umemzalisha Watoto wawili Sasa hivi anao.Yaani wewe Unataka uoe kila kona sijui.Angalia Tito nikwambie tu kitu.Usije ukaona mwanamke anachepuka si kwamba ndiyo tabia yake inawezekana wewe ndiyo msababishi.
"Tito alihema vikubwa kama ng'ombe" 
Fuuuuuuuuuuuuuuuuu.
Ndiyo hivyo. Najua leo ulitamani sana nikupatie utamu Lakini ndiyo hivyo tu wewe jua kwasasa mimi ni Mali ya mtu mwingine. Nimeshawekewa alama.
Alama gani.
Huoni mimba hii.
Kwahiyo Nunu leo sikugusi hata kidogo.
Yaani nakwambia hata Kidogo. Wewe toka tu nje.Mbona ni rahisi tu kukubaliana na matokeo. Kila matokeo ni matokeo ila kulingaana na yalivyokuijia hapo hiyo ni juu yako.Twende.nikutoe hapa ndani usijekukutwa na Jori hapa ndani alafu yakawa Mambo mengine kumbe walaaa.
Basi nakweli Tito akawa ametoka pale na kuelekea Bar baada ya kupewa kiperemba kikubwa na huyo Nunu.Maneno ya Nunu ukichanganya na uchovu wa msafara ndiyo ikawa hatari kabisa. Kwakweli huko alikoenda kunywa pombe alikunywa vyakutosha kweli kweli.
Kwa siku ile MamaTito alikuwa na mualiko wa arusi. Kwahiyo kwanzia Mishale ya saa tatu hakuwepo pale nyumbani. Wakawa wamebaki Zamda,Jeni na wadogo zake Tito.Mda huo wamekaa sebuleni wakiwa wanaangalia Runinga.
Basi mishale ya saa nne usiku hivi ndiyo Tito anatoka Bar amelewa nyang'anyang'a.Huko nje kelele za geti zikiwa zinasikika huko nje geti likigongwa.ilikuwa hivi.
Ngongongongo.
Ngongongongo."Inasikika sauti ya Tito akisema "Hivi huko ndani Ni hamsiki sio?." Mda huo Tito amelewa kwelikweli Yaani hafai.Maeneo aliyopita kwa vibaka na mateja tu Kwahiyo hata viatu wamempokonya.Basi ndipo Sasa Kwa mda huo Zamda akainuka na kwenda kumfungulia geti".
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)