MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 19

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 19
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
         
SEHEMU YA 19
Basi nakweli Kitunda akawa ameamua kugonga geti ili kama kutakuwa na watu huko ndani waje kumfungulia.Akiwa anagonga geti huku akisema.
Hodiiiiiiii..."kimya kimetawala"
Hodiiiiiiii...."kimya kimetawala"
Hodiiiiiiii...."kimya kimetawala"
Hodiiiiiiii....."Kimya kidogo"
Alivyogonga kwa mara ya nne ndipo mpangaji mmoja hivi akawa amesikia sauti ya mtu akiita na kugonga getini. Kwahiyo ikabidi aje.Mpangaji huyo alikuwa ni mwanadada hivi.kwa mda huo alikuwa akifua zake Kwahiyo alikuwa amevaa nguo zake za kufanyia kazi tu nyumbani. Kitunda akamuuliza Hivi.
Vipi dada?.
"kisha mpangaji akasema Hivi"Safi karibuni ndani Jamani.
" Wote Yaani Kitunda na Hanunu wakaitikia kwakusema Hivi ".Asante tumekaribia.
" Kisha Kitunda akasema Hivi ".Aaaaa Dada samahani kuna kijana anaishi chumba cha kwanza hapa yupo Kweli?.
Unamzungumzia Tito?
Haitwi Tito
Bali anaitwa nani?.
Anaitwa Jabu.
Eeeeeeee. Anaitwa Jabu?. Ndivyo alivyokwambia Hivyo.
"Kitunda akiwa anaongea tayari anaanza kukasirika na kusema Hivi"Bana Weee Dada Eee Mimi huyo namjua anaitwa Jabu hilo la Tito labda nyiye hapa ndivyo alivyowadanganya namna hiyo. Kwanza Mimi nataka kujua yuko?.
" Mpangaji yule Alimjibu Kitunda kwa urahisi  kabisa kwa kusema hivi "Aaaa hayupo kasafiri.
" Kitunda alishangaa Sana huku akimjibu kwa kusema hivi "Kasafiri?.
Ndiyo Kasafiri Leo.
Amesema anaelekea wapi?.
Kimbu.
" Hapo Sasa ndipo Kitunda akawa hajielewi kabisa huku akiwa  anasema Hivi "Heeeeee Kasafiri kwenda Kimbu. Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii mbona Jabu umenikimbia Jamani.
" Ikabidi Hanunu amuulize swali Kitunda. akisema "Kwani huko ndiyo kwao huko Kimbu?.
Ndiyo Hanunu.Jabu huko ndiyo kwao.Yaani kwanza kumbe Jabu kanidanganya hadi jina lake anaitwa Tito kumbeeeeeeee uwiiiiiii uso wangu ntauficha Yeeeeeeeeyeeeeee.Hii mimba nitaipeleka wapi eeeeeeee Jamani.
" Mpangaji naye akamuuliza Kitunda hivi".Heeeeeeeeeeeeeeeeee Dada Tito ndiyo kakupa mimba.uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii pole San Dada Yangu kwa hapo umeula wa chuya kabisaaaaaaa.Dada hukuangalia hata mtu Jamani wa kukupa mimba.Pole Sana tena sanaaaaaaaaa.
"Kitunda anaongea huku akiwa analia kwelikweli. Alikuwa akisema Hivi".Dada huyo.......huyo..... mkaka nimekutana....tana.....naye huko.....huko.....mjini tu.Hata .....hata si....sisi...sijui ...sijui kwao kabisa.Aliniahidi atajipanga ili akanitambulishe kwao.Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii ntaenda wapi Sasa Jamani na wanaume Wote nimewaacha na kuwatukana kabisa.
" Hanunu akasema Hivi "Shoga yangu Kitunda hapa ushagonga mwamba,umeshajikwaa na hata kama ukilia hauwezi kufanikisha chochote.
Kwahiyo Sasa Hanunu tufanyaje?.Unanisaidiaje?.
Twende tu nyumbani Kitunda. Hatuna la kufanya.
" Mpangaji naye akasema Hivi "Ni Kweli Shoga zangu nendeni tu.Kwasababu hata ulie vipi shoga AAA ndiyo hivyo Mwenyewe kaishakwea.
Twende tu shoga Wangu.
Sawa Kitunda tunaenda huko nyumbani haya huyo mama atasemaje Sasa.Haya huyo baba atasemaje.
Ndiyo hivyo Mambo yameshajitokeza Sasa Chakufanya nini hapa Sasa.?.Aliyekupa mimba kakimbia.Nini tena kingine Kitunda unataka?.Twende nyumbani.
Nilishawaambia wazazi wangu na nikawa nimewaaminisha kabisaaaaaaa kwamba mtu aliyenipa mimba Hana Matatizo Kwahiyo siku yoyote atakuja tu.Sasa leo hii ndiyo ntaenda Kuanza kuhadisia hii hadithi Kwanzia wapi Sasa.
Yule Mpangaji baada ya kuona kwamba Kitunda atamjazia watu akaamua kumjibu vibaya ili aondoke tu.Alisema Hivi"Heeeeeeeeeeeeeeeeee weeeee Dada huelewi tu kaanzie kuwaelezea hao wazazi wako kuanzia mwisho wa ukurasa. Nendeni zenu huko msijemkanijazia watu Hapa."Kisha akafunga geti kwakusema"Kwaherini.
Mpangaji yule akawa amefunga geti. Lakini ule mpango wa Kitunda kusema eti amfanyiye surprise ukawa umebuma.Kwahiyo Kitunda akaamua kumpigia simu Huyo Tito ili amuulize na kupata uhakika ni wapi aliko.
Basi akiwa anaonekana anatafuta jina la namba ya Tito ili aweze kumpigia simu. Baada ya kuliona jina lile kisha akabonyeza sehemu ya kupigia simu.Mda Huo simu kaiweka kwenye shikio la kushoto. Alivyoweka tu shikioni anasikia kwneye simu sauti ya mhudumu wa mtandao maalumu ujulikanao kama SAKAS.COM .sauti hiyo inasema hivi.
Ndugu mteja ahsante kwakutumia SAKAS.COM .Mpendwa,Mteja unayempigia hapatikana kwa Sasa  jaribu tena baadaye.Asante sana kwakuchagua SAKAS.COM .SAKAS.COM huduma nafuu zenye uhakika.
Kwakweli hapo ndipo Kitunda alizidi kuchanganyikiwa kwelikweli baada ya kusikia sauti ile ya mhuhudumu wa SAKAS.COM akisema kwamba mteja anayempigia kwasasa hapatikani.
Kwakweli kilibaki Kilio kikubwa sana kwa huyo Kitunda.Kwasababu Hana namna yoyote ya kufanya ili aweze hata kujimudu vizuri kwa kuweza kulea hiyo mimba.Pindi Tito alipomuahidi Kitunda kwamba atalea mimba hiyo Kwakweli Kitunda alijipa asilimia mia moja kabisa kwakujua kweli huyo wakuitwa Tito atalea mwana huyo.
Pia kinachomtoa machozi mengi Hivyo ni kutokana na Kwamba Kitunda alishawatolea maneno machafu sana wanaume wengine ambao Walikuwa wakimfuatilia.Sasa hapo ndipo pale wahenga Wanasema kwamba usitukane mamba kabla hujavuka mto na Unamtukana mgumba angali wewe si mgumba natumai iko siku cha mtema kuni utakiona.
Ikiwa ni mishale ya saa moja jioni Tayari kijana Tito alikuwa ameshawasili nyumbani kwao huko kwao mkoani  Kimbu katika mtaa wa Loronjo.Inavyoonekana kwa mda huo ni kama tayari nusu saa imeshapita tangu kuwasili nyumbani kwao.Kwahiyo kama ni Mabegi na vitu vingine tayari vimeshaingizwa ndani.
Mda huo tayari alishasalimiana na mama yake Yaani mama Tito na maongezi kidogo Kwahiyo yuko chumbani pamoja na Zamda.Hapo ndani inaonekana Wote wamekaa kwenye kitanda.Ikionekana Zamda akiwa amempakata mwanae akiwa amevaa nguo fulani tu hivi za kunyonyeshea,Tito akiwa amevaa tisheti ya bluu na suruali nyeusi. Basi mda huo Walikuwa na maongezi yao ambayo Kwakweli ni siku nyingi sana hawajaongea ana kwa ana. Basi maongezi yao yalikuwa hivi.
"Zamda akiwa anaongea huku  akiwa anambembeleza mtoto wake.Alikuwa akisema Hivi"Pole na Safari mume wangu.
Shukrani Sana. Huko nilikotoka ni mbali kwelikweli.
Ndiyo maana nimekupa Pole ya msafara wenu.
Sawa.....mhhh....hmmh afya yako vipi?.
Nzuri,ila siyo kama ulivyoniacha.
Kivipi ?.
Kivipi tena ?
Siuliniacha na mimba leo umenikuta na Mtoto Yaani nimejifungua.Kwahiyo hata kama ni afya Yangu ntumai itakuwa tofauti na ile ya kipindi kile.
Ahaaa sawa...hapo nimekupata.
Vipi,Zawadi gani umetuletea.Kwasababu Mimi zawadi yangu ndiyo hii nimekupatia mtoto ambaye nilishawahi kukuahidi. Sijui kwako wewe.?.
Mmmmh..unajua..... Mhhh kama zawadi gani.
Kwani zawadi unampangia mtu,hapana ni wewe utakavyoamua tu.
Daaa.....kwakweli sidhani hata kama nimekuja na zawadi yoyote.
Kwahiyo wewe ukaona ni bora uje huku Kimbu kama vile unaenda kumsalimia ndugu yako sijui Kwenye kambi ya nini vile.
" Kidogo kwa mda huo inasikika sauti ya Jeni ikiita hapo mlangoni.Ilikuwa hivi ".Hodiiiiiiii" Sauti ya Jeni ikawa imekutana na sauti za watu wakiongea huko ndani Kwahiyo hakusikika.Ikabidi apige hodi tena"
Hodiiiiiiii.
Jeni karibu, sukuma mlango.Ni sauti ya Zamda ndiyo iliyosikika ikimkaribisha Jeni.
Nakweli Jeni akawa ameingia akiwa ameshikilia nguo nguo za Mtoto wa Zamda ili amkabidhi huyo Zamda. Basi ikabidi amsalimie kwanza Tito .Jeni akasema Hivi".
Mambo vipi kaka?.
Safi tu, karibu.
Asante Wew Ndiyo wa kukaribia.
Wala.
Pole na Safari.
Asante.
Natumai Safari ilikuwa Shwari Ndiyo.
"Zamda ikabidi amtambulishe  Tito kwa Jeni. Ilikuwa hivi".Aaaa....huyu Anaitwa Jeni.
OK Jeni karibu Sana.
Asante sana kwa mara nyingine.
Anaitwa Jeni,...Aaaa....Jeni ni rafiki yangu sana na tumejuana naye hapa hapa ambapo Yeye kapangisa hicho chumba cha hapo Hivyo ambapo sister wako alikokuwa akilalai.
Ahaaaaa.Sawa nimekuelewa.
sawa. Aiseeee Jeni Mimi naitwa Tito.
Ahaaaaa Tito nilikuwa nikikusikia sana kwa Zamda akiwa anakutaja taja tu.Kwahiyo ni vyema kwa Sasa nimekuona.
Sawasawa. Karibu Sana.
Aaaaaaa Tito huyu Ndiye aliyekuwa akinihudumia hapa nyumbani.
Sawasawa.
Basi sawa Jeni nimekuletea tu hizi nguo hapa zilikuwa zimeanikwa Kwenye hiyo kamba ya hapo nje.
Ahhaaaa,Shukrani Sana. Ni Mimi nilianika.
Okay, Basi acha nikapumzike zangu huko ndani.Ukiwa na tatizo lolote vile utaniita.
Sawa Jeni.
Nakweli mda huo Jeni akawa  ametoka na kurudi chumbani kwake.Zamda na Tito wakawa wameendelea na maongezi. Ilikuwa hivi.
Tuseme Tito huko ulikoendaga miezi yote hiyo ni kwamba Mitandao haipatikani huko au ni nini tatizo?.
Inapatikana mbona .
Sasa ni kwanini ukimya kuuruhusu utawale nanmna hiyo. Au ulipata Matatizo huko?.
Hapana sikupata Matatizo.
Bali ni umeamua tu.
Si kuamua Zamda .
Bali ilikuwa ni nini?.
Mambo tu yalikuwa yamebana.
Yaani Mambo yamebana hadi hata siku za jumapili?.
Afadhali kwa siku za jumapili kidogo tu.
Ndiyo Hivyo ingekuwa hata unanipigia na kunijalia hata hali yangu tu Jamani. Au Ndiyo hivyo Mimi tayari sina thamani kabisaaaaaaa kwako?.
Hapana Zamda.
Hapana nini.Wakati ndiyo ninavyojionea Hivyo.
Ni Mambo tu nimekwambia yalikuwa yanaingiliana tu
Yaani Kwakweli Tito sijui penzi letu Mimi na Wewe linaenda kuangukia wapi.
Kwanini unaongea hivyo. Yaani kwamba.... unataka kuu....
Nataka kufanyaje Yaani.
Ndiyo ungeacha nimalizie.
Yaani kwanza mwisho wa siku  ukaamua kubadilisha hadi namba zako za simu.
Ilibidi nibadilishe namba zangu.Kwasababu simu yangu ilipotea.
Yaani ilipotea kiurahisi rahisi tu Hivyo?.
Nilivyokuwa kazini.
Sawa achana na hiyo mada tuanze mada ngingine kabisa.kwasababu naona hapa kama vile shetani anataka kutuingiza kwenye ugomvi kabisa.
Mbona ugomvi Mambo ya kawaida tu Hayo.
Ila Kwakweli Tito tuache  utani. Kwa Hela hata za kuishi kidogo kidogo kwa sisi hapa nyumbani umekuja nazo.
Nimekuja na Hela kidogo tu.
Sasa Tito, hujaleta zawadi yoyote Yaani zawadi yoyote ile bado hata na Hela ya matumizi hujaja nayo tena.
Sina nakwambia kazini kule tumeambiwa tutulie kidogo watatunufaisha Kidogo.
Sasa Tito tuseme mda huo wote ulisema uko kikazi huko.Yaani hiyo kikazi gani Jamani unarudi hapa Yaani utafikiri kabisaaaaaaa hujui kwamba huku kuna mtu kajifungua.
Unajua Zamda sikuelewi unacholalamika ni nini haswaaaa kwa Hapa?.
Yaani tuseme... Tuseme mada niliyokuwa nikiongelea haukuwa unaielewa kabisaaaa Au umeamua tu.
Si kwamba nimeaumua tu.
Bali ni
Yaani sielewi tu nini kinachokulalamisha hapa.Mbona nilishakuambiaga mapema sana.
Kuhusu Nini.
Umesahau siyo?.
Ndiyo nikumbushe.
Nilishawahi kukuambia kwamba wewe hapa unaishi, Yaani unalala bureeeee, unakula bureeeee na kila kitu bureeeee alafu unataka nini tena Zaidi ya hapo.
Duuuuuuuuuuuu hapa Kweli nimeula wa chuya, acha Mimi nikakae zangu hata na shoga yangu tu huko ndani kwake.
Hata kama ukilala tu huko haina shida.
Sawa.
Nakweli anaonekana Zamda anatoka chumbani hapo na kuingia chumbani kwa Jeni.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)