MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 18

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 18
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
         
SEHEMU YA 18
Basi ikiwa ni mishale ya saa mbili asubuhi juu ya alama mwanadada Zamda alikuwa tayari ameshabadilshwa jina na kuitwa mzazi hivyo anahitaji pongezi kwa kujifungua mwana wa pili tena wa kike. Ambapo kwa kipindi hicho Jeni alikuwa ameshamaliza mitihani Lakini akawa hajasafiri Kwasababu tu aweze kumsaidia shoga yake ambaye ni Zamda Katika shughuli mbalimbali.Kwasababu tayari Zamda ndiyo huyo Mwari wa kingata kajifungua  mwana wa pili tena wa kike.
Furaha ilimwijia moyoni kwakujifungua Salama tena bila hata kufanyiwa operesheni yoyote. Lakini tatizo na mawazo kwa Zamda yanakuja ni pale ni Je nani atakuwa akimsaidia kifedha?.Japokuwa alikuwa na furaha kweli ya kujifungua.
Basi ilipofika mishale ya saa saba mchana hivi Zaidu akawa ameshawasili kwa Jeni Lakini ni kwa madhumuni ya kwenda kumuona Zamda kama mama Tito hatokuwepo pia na madhumuni mengine aliyoyapangilia. Na kweli kwa mda ule mama Tito hakuwepo Hivyo ikawa ni rahisi kwa Zaidu kuongea na Zamda na kupanga baadhi ya Mambo.
Sehemu walipo inaonekana kwa pembeni kuna kitanda Lakini Zamda kakaa chini kwenye nguo fulani Hivi iliyokuwa imetandikiwa na kuweka kagodoro fulani Hivi ili aweze kulalia Hapo hapo na mtoto wake.Pia Zaidu anaonekana yuko amekaa kitandani akiwa anamuangalia Zamda kwa huruma wakati akiwa anaongea naye.Kwasababu zaidu naye alikuwa na yake ya moyoni ya kusema ingawa hajui je yatamuingiaje kichwani mwa zamda.Ilikuwa hivi.
Zamda Unajua ni hongera kubwa sana unatakiwa upatiwe.
Kwanini zaidu?.
Aaaaa si utani hadi kujifungua Salama kabisa. Halafu kwa mazingira ambayo ulikuwa ukiishi si ya utani.
Ayaaa mbona kawaida Sana."Mda Huo anaonekana anamtuliza mwanaye akiwa analia huku anaendelea kuongea ".
Zamda Unajua hadi nakuonea huruma. Kwasababu Wewe Yaani unaishi hapa utafikiri hiyo mimba hadi kupata mtoto ulijiwekea peke yako tu.
Sasa Zaidu ni sawa,unafikiri nitafanyaje?.
Zamda kwa mimi Ndiyo ningekuwa kama wewe Wallah nigeenda bata ustawi wa Jamii namshitaki.Kwasababu huu si ubinadamu anaokufanyia kabisa.
Namshitaki nani?.
Huyo aliyekupa mimba.
Tito?.
Ndiyo Au mwingine nani?.
Aaaaa Unajua Zaidu Mimi Nasema tu kuna Mambo mengine hutokea hivi Kwasababu Fulani na fulani. Kwahiyo nisikimbilie mbali sana huko mwisho wa siku ikaja ikahitajika fedha nikawa nimeshindiwa hapo hapo.Umenielewa Zaidu.
Sawasawa Zamda nimekuelewa.
Basi kama Ndiyo Hivyo Mambo mengine tunasema tu malipo ni hapa hapa duniani na akhera ni mahesabu tu.
Duuuuuuuuuuuu haya bana maneno yako hayo mtoto wa kingata umenishinda.Aaaaa tukiachana na hayo kuna vitu nilileta hapa kwaajili ya mwana wako hapo. Kuna Poda hapo na vinguo nguo kidogo hivi kwa uwezo wangu ukaishia Hapo. Kwasababu hata Mimi nahisi nimewajibika katika kujazilishia mashikio pia na vinginevyo.
Ahaaaaa, Shukrani sana Zaidu.Una utani Wewe.
Kawaida yangu tu bana.Sasa angalia huyo jamaa yako wakuitwa Tito asije akaja alafu akaanza kuulizia umevipatia wapi na ukaanza kujing'antang'ata tu.
Wala nitamwambia ni Jeni ndiyo kanizawadia.
OK hapo utakuwa umefanya vizuri. Aaaaa pia nimetoka kuongea na Jeni Hapo chumbani kwake kuna suala nimemjuza ambalo kwake  ni jipya,kwa ujumla sikuwahi kumtaarifu mtu yeyote kuhusiana na taarifa hii.
Zaidu taarifa gani?.Wataka kuniacha!?? Eeeeeeee Au ?!.
Hapana bana tulia Zamda mbona kama una hofu sana.
Hofu Kuwa nayo ni lazima kwa mtu ninayempenda Sana na kunijali kama Wewe.
Wala Zamda tuliza mironjo Msafara uende kama wa tembo anavyotembea Pole pole lakini huacha alama nyuma yaani alikopita na Hivyo Basi watu watajua mzee tembo kapita hapa.
"Zamda akimsikiliza kwa makini Zaidu kitu anachokiongea anamaanisha nini Lakini hakuelewa. akamuuliza Hivi "Mmmh!! Tito Unamaanisha nini kwasababu sijakuelewa hata kidogo Yaani?.
Aaaaa haina shida hii wala haihusiani na mada hii Bali lilikuwa ni kama tangazo tu  ila nitakufafanulia vizuri kwa mda mwingine.
Ahaaaaa, Sawa.
Zamda kitu kikubwa kilichonileta hapa ni kuja kukutaarifu kwamba hutoweza kuniona kwa mda wa miezi mitatu.
" Zamda moyo ulimwenda mbio sana na sura yake ikawa imebadilika kidogo Hasira kama zinamwijia kisha akasema Hivi """".Zaidu Unataka kuniacha mchana kweupee kabisaaaaaaa Jamani. Sasa nitabaki na nani Jamani wa kunijulia  hali na Mimi niseme Nina mume.Zaidu wewe ndiyo mwanaume pekee ninayekutegemea wakunipatia tumaini katika moyo wangu. Zaidu.
Hapana Zamda sikuachi nilishawahi kukuahidi kwamba Zamda penzi letu litadumu milele daima japokuwa ni la wizi Lakini iko siku litakuja kuwa la halali kama litatakiwa kuwa la halali.
Hapana zaidu wewe ndiyo unaniacha kiujanja hivyo.
Hapana Zamda nakuambia Ukweli."Mda huo anaonekana Zaidu anatoka pale kitandani alikokuwa amekaa na kwenda kwa Zamda ili kumbembeleza.Mda huo mwanaye alikuwa amemlaza .Zaidu akiwa amemshika Zamda Mkono wake wa kulia akisema kamba"Zamda Mimi Ndiyo kama mume wako niamini mimi, nakuahidi niendako kote huko nikirudi mbona nitarudi hata na ridhiki yoyote.
Hapana Zaidu, hata Tito ndivyo alivyoniaga tu siku Hiyo Hivi hivi.Lakini mwisho wa siku hadi leo sielewi kama hata yuko  hai Au Laaa.
Zamda nilishawahi tena kukuambia kwamba Mimi usinifananishe kabisaaaaaaa na huyo Tito yaaaani kabisaaaaaaa,hata kama sijui ila usinifananishe naye kabisaaaaaaa. Tabia zangu nazijua milele haziwezi kukaa kwenye mfereji mmoja na tabia za huyo Tito.Umenipata Zamda?.
Sawa Zaidu nimekupata. "Hasira zikiwa zimemshashuka kidogo na kusema Hivi"Haya basi mume wangu niambie Hiyo miezi mitatu unaenda wapi?.
Nasafiri.
Unaenda kijijini kwenu au?
Hapana.
Bali?.
Nchi za Nje.
Aaaaaaaaaaaaaaa "Zamda alishangaa kwelikweli kwakusema Hivi".Nchi za nje?.
Ndiyo nchi za nje.
Nchi gani.
Denmark na Marekani.
Haaaa kote huko Zaidu.
Ndiyo Denmark nitakaa kwa siku arobaini na Tano  na Amerika nitakaa kwa mda pia wa siku arobaini na Tano.
Unaenda na nani ?.
Kuna wazungu Hivi tunaenda nao.
Kufanya nini huko.
Kwenye mashindano ya kuandika hadithi za kubuni au za kweli kwenye kompyuta.
Haaaaaaa, kweli Zaidu.
Kweli nakuahidi, Natumai nikirudi penzi letu litaendelea na litazidi kunawirika.Pia hadi kipindi hicho tayari na matokeo yangu yatakuwa yameshatoka Kwasababu nilikuwa natafuta C moja tu.
Ahaaaaa, hongera Sana.
Shukrani Sana. Kwahiyo Ndiyo maana nakwambia wala usihofu.
Lazima nihofu.Sasa huko mtapewa zawadi gani?.
Tutapewa zawadi nyingi sana kutokana na nafasi ya ushindi wako tu.Kwasababu kutakuwa na mikupuo mbalimbali ya mashindano.
Mnashindana mataifa mangapi?.
Usiseme mataifa mangapi sema mabara mangapi?.
Ahaaaa mabara mangapi?
Manne.
Haaaaaaa manne?.
Ndiyo naninatumai nitashika nafasi ya kwanza kidunia japokuwa Ndiyo mara ya kwanza kushindana kimataifa Hivi.
Ahaaa Zaidu nakuombea kwa mungu ushike nafasi ya kwanza ili hata uje uniokoe na Mimi. Kwasababu nimeshakata tamaa kabisa na huyo Tito.
Wala usihofu mke wangu nitajitahidi kwa hali na Mali.
Kwahiyo mnasafiri lini?.
Kesho saa tatu kamili asubuhi kuanzia uwanja wa ndege wa Kimbu ndipo msafara utaanzia hapo na tutapitia uwanja wa kimataifa wa Reni kisha Sasa hapo ndipo tutatoka nje ya nchi kabisa.
 Hapa Kinani mko wangapi?.
Kwenye nchi yetu tuko  washiriki sitini na moja.
Lahaulaaa mbona wengi hivyo?.
Hapana ndivyo walivyokubaliana Hivyo tu kila Taifa litatakiwa wapatikane washiriki sitini na moja kavu.
Ahaaaaaaaa wengi sana.
Ni kweli ni wengi ila Natumai nafasi ya kwanza nitaichukua Mimi hapa.Najua utanikumbuka sana nikiwa huko ugenini ila jua nitarudi tu.Kwahiyo wewe zidi kuniombea mungu tu.
Sawasawa mume wangu mungu akutangulie.
Inshaallah "Walipeana mikono pale na kuweza kukumbatiana kwa makumbatio ya mwisho Kwasababu kuonana tena ni hadi miezi mitatu ipite na siku kazaa.Kwakweli Zamda alipokuwa akimuaga Zaidu kwakweli Zamda alijikuta machozi yanambubujika tu bila hata kujua yametokea wapi. Yote hii ni kutokana na Upendo wa dhati alionao kwa Zaidu. Kwasababu anajua Kabisa Zaidu ndiyo kama kila kitu Kwake alafu tena leo anataka kumuacha pekee kwa mda wote huo.Walikumbatiana kwa mda wa dakika moja hivi wote wakiwa wamesimama, Zamda maneno yake ya mwisho tu Alisema".
Zaidu nakuombea mungu msafara wenu uwe salama kabisa na mfike salama, pia mashindano yako yawe yana mwendo wa Haraka na wenye ukamilifu. Natumai utashinda Zaidu. Ukishinda usinisahau zaidu.
Inshaallah.sitokusahau Zamda. Kwaheri." Zaidu alimchumu Zamda Kwenye shavu la upande wa kulia na Kwa upande wa shavu la kushoto akamshika kwa Mkono wake  wa kulia kisha baada ya Hapo na kumuacha Zamda akiwa amesimama huku akiwa ameduwaa tu.Haamini kilichotokea kwamba ni kweli kabisaa Zaidu anasafiri kwa mda wote huo ".
Basi kwa mda huo Zaidu alienda kumuaga Jeni.Wakiwa Chumbani wawili tu.wakawa wanamazungumzo.
Mhhh Zaidu, vipi Zamda amekubali wewe kusafiri?.
Ndiyo Hivyo itabidi akubaliane na matokeo tu nitafanyaje Sasa na hali ya maisha ndiyo kama hii unayoiona hapa.
Kweli.
Kwasababu Jeni kumbuka hii ni kama bahati nasibu tu imejitokeza.Je nikikataa nitakuja kupata nafasi kama hii unafikiri?.
Hapana ni vigumu sana. Nafasi kama hizi ni adimu sana kuzipata.Kwasababu kwanza ni watu Kutoka huko nje ya nchi lazima tu kitu kikubalike.
Sawa.
Zaidu Mimi ninachokuomba kuwa na Uaminifu pia nitakuombea sana kwa mungu akutangulie katika mashindano yako haya.Natumai imani yetu,yako na juhudi zako zitakufanya wewe kuchukua nafasi ya kwanza kati ya mabara yote yaliyoshiriki.
Shukrani Sana Jeni.
Pia Zamda nakuomba huyu Zamda usije ukamuacha.Kwakweli Mimi sijui kama hata huyo jamaa yake atakuja.
Sitomuacha.
Kwasababu watu wengi wakishaenda huko nchi za nje huwa wakirudi wanarudi na wachumba wao wapya Kabisa.
Hapana,Sijafikiria Hivyo.
Sawa. Kwahiyo hadi hicho kipindi utakapokuwa unarudi matokeo yatakuwa yameshatoka.
Ndiyo ndiyo.
OK utanikuta tu hapa hapa.
Sawa basi utanijuza kama huyo Tito atakuja.
Sawa Haina shida nitakupatia taarifa zote.
Asante.
Nakwambia Zaidu ukienda huko Yaani utakuwa kama mzungu kabisaaaaaaa.
Kwasababu gani ?.
Yaani ukichanganya na huo Weupe wako Kwakweli Yaani basi tu.
Haya Bana. Sasa Jeni Mimi naenda mahome acha nikajiandae ili kesho nisijenikaanza kuhangaika tu na mda umeenda.
Sasa Zaidu. Rafiki yangu wa karibu, kipenzi changu wa Karibu, mshauri wangu wa karibu, mcheshi wangu wa Karibu, muelekezi Wangu wa karibu."Jeni alimkumbatia Zaidu kwa sekunde chache hivi kisha akasema Hivi ".Kwaheri Zaidu tutaonana.
Sasa Jeni nakuomba uishi na Zamda vizuri, usiondoke kabla sijarudi.
Sawa nitakaa nae hadi ukirudi.
kwakweli siku hiyo Zamda, Jeni walijikuta ni kama wameondokewa na nani vile Kwasababu ya Safari ya nje za nchi ya Zaidu ya siku iliyokuwa ikifuatia.
Kwakweli mama Tito Yeye alizidisha sana ubaguzi mkubwa kwa Zamda. Zamda kama mwari huduma nyingi sana alikuwa hazipati kutoka kwa mama Tito. Kwahiyo msaidiizi mkubwa akawa ni Jeni.
Basi tukirudi katika huko mkoa wa kihangu aliko Tito na mpenzi wake Kitunda. Mda huo anaonekana Kitunda anaelekea sehemu alikopangisha Tito. Mda huo Kitunda yuko na shoga wake huyo Hanunu. Ikiwa ni mishale ya saa Kumi alaasiri, wakiwa wamevaa madera,huyo Kitunda dera lilimkaa kweli kweli ukichanganya na umbo lake lilivyo. Sema ndiyo hivyo nayo mimba inaanza kuharibu umbile lake kidogo.Basi wakiwa njiani wanaelekea huko kwa Tito Walikuwa wanamaongezi kama ifuatavyo.
Unajua Hanunu kama vile tumeshafika tu.
Aaaaa kumbe siyo mbali sana.
Wala.Weee Sasa hivi sitaki wanaume wa mbali sana kama yule wa kipindi kile.
Weeeee kweli yule wa kipindi kile uliula wa chuya kwa yule.
Laaa wee acha tu shoga wangu.
Nakwambia akiniona tu huyo Jabu Hiyo furaha atakayokuwa nayo si ya utani Kwakweli. Yaani kwanza acha leo nimfanyie mshitukizo kidogo Yaani Surprise vile.
Ndiyo maana yake.
Haya tumeshafika ndiyo nyumba hii.
Sawa gonga geti.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)