MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 17

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 17
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
    
SEHEMU YA 17
"Zaidu hakutaka hata kuyasikiliza maeneo Yale ya Zamda huku akiendelea kumuweka vizuri Zamda. Zamda akasema tena hivi"Zaidu twende ndani aaaaaaa.
Hapana hapahapa.
Ndani bana nimeshapaandaa.
Mda huo Kwakweli huyo wa kuitwa Zamda hafai Yaani ni kalegea  kama Mtoto Mwenye Usingizi.. Huko ndani uwanja wa mashambulizi Kwakweli haukuwa wa utani Kabisa sauti tu zikiwa zinasikika kutoka kwa Zamda.
Zaidu
Zaidu uiiiii aaaaà
Basi ilipofika mishale ya saa Tano na nusu ikabidi Jeni awagongeee Zamda na Zaidu ili zaidu na Jeni waweze kwenda shuleni. Mda huo wanaonekana Jeni na Zaidu wanaongea Jambo. Wakiwa maeneo ya chumbani kwa Jeni.
Hivi wewe Zaidu Yaani Tangu mda wote huo unapiga tu.
Sasa. Ntafanyaje Jamani.
Utafanyaje?!.
Ndiyo, yule mtoto anawashwa inabidi nimkune vizuri. Kwahiyo kama ni kumkuna vzuri lazima nichukue mda mrefu.
Ayaaaa Yaani umejisahau kabisaaaaaaa hata kama kuna Mtihani leo mchana.
Nalijua vizuri sana Hilo suala.kwamba leo tena ndiyo Mtihani wa mwisho.
Kumbe walijua Hilo jambo Kabisa?!.
Sasa Ndiyo yatakikana tuanze msafara mda huu.
Haina shida kama ni kula tayari tumeshabonda.
Ndiyo maana yake,wewe Unataka ukapike,ukanunulie wapi chakula?.
Haya bana,ndiyo ishapita
Basi twendezetu chukua begi tuondoke.
Lakini tukirudi kwa kijana  Tito ambaye ameshaishi mkoani Kihangu kwa mda mrefu sana hadi akafikia Sasa kuwa mwenyeji wa huko kihangu. Basi starehe Kwake Kwakweli ndiyo ilizidi kuwa Kama ibada ya Ijumaa kwa waislam Au jumapili kwa wakristo.Aliendelea kuishi katika Jumba la MAPENZI na huyo mpenzi wake wa kihangu aliyekutana naye aitwaye Kitunda. Tabia za Kitunda alizidi kuzivumilia kweli Kweli.Yote hiyo ni Kwasababu Kitunda kutokana na mofolojia yake tu au umbo lake lilivyo Kwakweli  lilikuwa likimchanganga sana kijana Tito na kujikuta Tito anazidi kung'ang'ania katika penzi kama kupe Kwenye mkia wa ng'ombe Kati yake na Kitunda.
Kitunda naye maisha yake yale Yale ya mapenzi ya wizi aliweza kuyaendeleza wakati akiwa na mahusiano ya Kimapenzi na huyo Tito.
 Basi siku Hiyo ikiwa zimebaki siku chache tu Kwa Tito kuweza kurudi mkoani Kimbu siku hiyo ikiwa ni siku ya jumapili wapenzi hao wawili waliamua kwenda Kujifungia katika Nyumba fulani Hivi ya wageni ili waweze kupanga mipango yao vizuri.
Basi mda huo wakionekana wako kitandani ikiwa ni mishale ya saa Kumi na moja ni baada ya kufanya mautamu huko tayari ndipo wakaanzisha mazungumzo. Basi mazungumzo yao yalikuwa hivi.
ila Kwakweli Jabu penzi letu limedumu sana.
Ndiyo tena sana.
Yaani kwasasa umekaribia kukata kama mwaka Hivi Lakini Bado tupo katika MAPENZI yetu ambayo tuliyaanzisha Mimi na Wewe. Au siyo Jabu.
Ni kweli Kitunda. Unajua Kitunda matarajio yangu kwako Kwakweli ni matarajio mazuri sana.
Hata Mimi Najionea Mpenzi WANGU.
Aaaaaaaaaaaaaaa, kuna Kipindi tuliahidiana tutapelekana nyumbani.
Ndiyo Nakumbuka sana Hiyo ahadi.
Ahaaaaa Sawa kama unaikumbuka.
Natukakubaliana kabisa Kwamba wewe ndiyo utaanza kunipeleka kwenu kwenda kunitambulisha Au sivyo?.
Ndiyo Hivyo.Natumai Ndiyo Wakati wenyewe huu.
Ahaaaaa ndiyo mda wenyewe huu.
Ndiyo.
Sawa.sasa Jabu mpenzi Wangu kuna kahadithi nataka nikuhadithie kidogo Hivi.
Kinahusu Nini.
Aaaaaaa, kinahusu daktari fulani Hivi.
Daktari tena,Mambo ya daktari huku yanafikaje?.
Wewe tulia bana Jabu Unataka hadithi hutaki?.
Aaaa Nataka
 Haya tulia nianze Sasa.Kuna daktari mmoja hivi alikuwa akifanya kazi Kwenye hospitali ya rufaa ya kihangu. Daktari huyo kwakweli hakuna mgonjwa ambaye aliyepita kwake na kuacha kutibiwa.Lahashaa kila mgonjwa alitibiwa kutokana na ugonjwa wake ulivyo. Daktari Huyo upasuaji wake Kwakweli ni wa makini Sana japokuwa hakuwa anatumia nyenzo zozote.
"Jabu alirukia mada kwakumuuliza swali hivi"Kama zipi hizo nyenzo?.
Aaaaaa Subiri nazitaja.
Ndiyo zitaje nahitaji kuzijua Sasa.
Sawasawa. Aaaaaaa nyenzo kama vile kutokuvaa gloves.
Aaaaaa huyo daktari alikuwa noma sana hakuwa anavaa gloves.
Ndiyo Ndiyo. Basi daktari yule pia kila aliyekuja kumuona mgonjwa wake akiangalia tu namna mgonjwa anavyotibiwa na daktari basi hata mtu huyo aliyekuja naye alitamani tu atibiwe.Daktari wala hakuwa na hiyana eti  amsuse Lahasha Bali alimtibu vyema sana hadi kujikuta mtu yule naye anaenda kuelezea huko mtaani na hata wengine si wagonjwa waja tu.
Daaaaa huyo daktari Au malaika?.
Wala si malaika.Yaani huyo ni daktari kabisa kabisa. Hata Mimi alishawahi kunitibu vizuri sana na nikawa nimepona kabisaaaaaaa na madawa nikapewa kabisa.
Ulikuwa unaumwa?.
Ndiyo.
Daaa pole sana mpenzi Wangu.
Asante. Basi daktari yule aliendelea kuwa na ufanisi wake kazini vile vile Lakini waandishi wa habari mbalimbali wakawa wanamuuliza ni kwanini huvai gloves unapotaka mathalani kumfanyia mtu upasuaji?.Aliwapa jibu rahisi sana Ambalo wala halikuhitaji kuandikwa Kwenye madaftari milioni ya baadhi ya waandishi wa habari waliokuwa wakimhoji maswali.
Jibu gani hilo Kitunda.
Aaaaaaaa aliwajibu Kwamba.Ni vyema ngozi ya mtu A na B zikutane Au zigusane ili kuweza kupata au kufanya Kitunda kwa ufasaha wakati wa kazi ya upasuaji.Pia mikono yako imejaaliwa kuwa na kinga ha magonjwa sugu Zaidi ya elfu moja mia yano.
Daaaaaaa huyo Sasa kifaru.
Mwisho wa siku Jamhuri ya Kinani iliweza kumpatia tunzo ya daktari bora na tunzo pia ya Daktari shujaa.
Daaaa hongera kubwa Sana daktari.
Aaaa siku hiyo Kweli alishangaa sana yule daktari kwamba kuna mgonjwa ambaye alishawahi kumtibu tena anataka matibabu kwa mara nyingine. Haijawahitokea kwa daktari huyo amtibu mgonjwa fulani alafu tena arudi,lahashaa.
Hakupona vizuri huyo.
Sasa mgonjwa yule alikuja tena siku Hiyo haikuwa siku ya kazi kwa Daktari Bingwa huyo.Lakini yule daktari ilibidi tu amuingize katika chumba maalumu hiyo ni baada ya kumuona kweli mgonjwa yule alikuwa anahitajika kufanyiwa upasuaji wa Haraka na hakuna daktari mwingine mashuhuri wa upasuaji kama yule.
Ikawaje.Daaaa huyo Daktari Ana roho nzuri sana.
Aaaaa alimfanyia upasuaji kwa mda wa masaa manne.
Daaaa huyo mgonjwa alikuwa anaumwa sana nahisi.
Ndiyo maana yake.Baada ya Hayo masaa manne akawa tayari, Kwahiyo ikabidi daktari akae karibu na mgonjwa huyo. Lakini mgonjwa huyo ilibidi atoe Shukrani Sana kubwa.Kwasababu upasuaji aliokuwa anafanyiwa unahitaji umakini sana. Upasuaji ule Ulikuwa ni katika sehemu yake ya uke.
Aaaaaaaa huyo daktari kwanza alikuwa wa kiume Au wa kike.
Alikuwa wa kiume.
Ohooooo. Noma sana.
Sasa Basi mgonjwa akaanza kusema Hivi ".Daktari nashukuru sana kwa upasuaji ulionifanyia Kwakweli ni msaada mkubwa sana umenifanyie.Basi daktari akajibu kwa madaha sana akisema Hivi. Asante haina shida hizi Ndiyo kazi zetu bana wala usihofu. Kisha mgonjwa yule akasema Hivi. Lakini daktari mbona umenifanyia upasuaji Kwenye sehemu yangu ya uke Lakini nashangaa nimevimbaa tumboni tena ndani."Tito akashtuka kwa kusema hivi".
Alaaaaa huyo daktari vipi tena?.
Ndiyo Hivyo. Daktari Mwenyewe alishangaa sana jambo ambalo mgonjwa aliongea.
Akasemaje Sasa?.
kwanza alishangaa, kisha akamuuliza Hivi. Mbona upasuaji nimekufanyia chini alafu panapovimba ni juu?.
Hiyo Kweli kavimbaa juu.
Bwana Yule mgonjwa akaanza kulia kweli kweli na kuanza kumng'ang'ania Daktari Yule. Hadithi yangu na ikaishia hapa ambayo ilikuwa inamhusu hiyo daktari. Sijui kama umeielewa?.
Ndiyo, nimeielewa kabisa.
Sasa Jabu turudi kwenye uhalisia.
Uhalisia?.
Ndiyo uhalisia.kwani hujui maana ya uhalisia.
Uhalisia wa nini?.
Uhalisia wa kitu nilichokuelezea.
Ahaaaaa.
Iko hivi kote huko nimefanya kuzunguka mbuyu sana ila madhumuni yangu yalikuwa nikutaarifu Kwamba "Kitunda alisita kidogo kuongea kwa sekunde chache kisha akasema Hivi".Jabu nina mimba.
Tito akiwa amejifunika shuka lile hadi akaamua kulitupa shuka na kusema Hivi".Kwamba unasema.
Hujanisikia tuseme?.
Ndiyo,sijakusikia ndiyo maana nimekuuliza.
Umenisikia ila." Tito akamalizia mwenyewe kwakusema Hivi "
ila sijaelewa tu.
Ahaaaaaaaa ungesema tu Hivyo uelezewe vizuri.
Ndiyo niambie vizuri.
Nina mimba tena yako.
Ukimaanisha kuna wengine nao Walikuwa wanachangia hapo Au sivyo?.
Sasa Jabu maswali mengine yanatokea wapi.hapa nimekwambia kwamba nina mimba tena ni ya kwako.Kwasababu wewe ndiyo Mpenzi wangu na kila siku tumefanya bila kutumia kondomu Au kinga yoyote ile.
Aaaaaaaaaaaaaaa, haya Kitunda nitailea Hiyo mimba.
Sawa Mume WANGU Eee."Kitunda alimkumbatia Tito Lakini Tito akawa anafurahi kwa Usoni tu Ila la moyoni mwake alijuae mwenyewe Yaani Hana hamu kabisa ".
Umeenda kupima Lakini?.
Hapana Jabu ila dalili inaonesha tu.Natema mate kwelikweli.
Basi Sawa haina shida wambie Wazazi wako nitalea hiyo mimba.
Sawa.
Basi hata kama wazazi wako watakuzingua jaribu kuwaambia tu vizuri kwamba aliyekupa mimba ni nani?.
Sawa.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)