MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 14

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 14
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
      SEHEMU YA 14
 
"Mda huo huo Jeni akaamua kumuuliza Zamda swali ambalo hakulitegemea kama angeliuliza.Ilikuwa hivi".Hivi wewe Zamda ushawahi kufikiriaga kwamba iko siku mtafunga ndoa Kabisa wewe na Tito
Mmmh!! Kwakweli Jeni Hilo ni Kama swali gumu sana kwangu.Kwasababu ni swali ambalo sikutegemea kama utaniuliza.
Hapana mbona siyo swali gumu Zamda.
Kwangu ni gumu na kwako ni gumu Ndiyo maana umeniuliza Hilo swali.
Nataka kujua Sasa.
Kwakweli Jeni kuna vikwazo vingi sana hapo. Kwasababu kwanza nikianza na suala la dini.Nakumbuka siku Hiyo mama Tito siku hiyo aliamua kutuuliza maswali kuhusiana na Mambo ya dini.
Wewe na nani?.
Mimi,na Bite Kwasababu Hata Bite hiyo mimba aliyonayo aliyompatia ni muislam swafi kabisaaaaaaa.
Holaaaaa,kumbe hivyo shogaaa sikuwa naelewa.
Ndiyo uelewe Hivyo Sasa.
Alaaaaa hapo kazi ipo.
Kwahiyo mkawa mmemjibu vipi?.
Ndiyo tukamuambia tutampa Majibu siku nyingine.Kwasababu Hayo maswali si ya kujibu jibu tu kiurahisi tu.
Hadi leo hamjawahi kumpa Majibu?.
Ndiyo bado ni mda Sana.Kwasababu Bite alipata mimba Mimi nikiwa na mimba ya miezi mitatu Hivi. Kwahiyo wote kipindi hicho tulikuwa tunajulikana kama mama vijachp.
Ok. Ila hapo Kwenye uchaguzi wa dini Kwakweli Angalia sana.Kwasababu kama baba yako na mama yako ni waislam na sidhani hata kama watapenda kwamba wewe usilimu.Sidhani.
Hili suala sijawahi kumwambia mtu yeyote kule Ngata.
Ahaaaaaaaa, hapo Sawa.
Kwani hata juzi juzi tu hapa ndiyo nimepta namba zao za simu.
Heeeeee,ulizipataje shoga.
Kuna Ndugu yangu Kama bahati nzuri tu siku Hiyo tumeenda sokoni ndiyo nikakutana naye ndiyo nikamgaia namba yangu na Yeye akanipa namba za baba na mama kule Ngata.
Okay. Mimi nakueleza Kwamba kwenye Hilo suala la dini,aaaaa hapo hata usiumize akili,hapo chakufanya ni kwenda mahakamni tu ili kufunga ndoa ya mahakamani kila Mtu awe anafuata dini yake Bali ni mke na mume.Yaani kila mtu na maamzi yake. Wewe utasali kila siku na Ijumaa utaenda msikitini na huyo Tito ataenda kanisani hiyo siku ya jumapili. Simple decisions mbona maamzi rahisi sana haya
Daaaa ikoje ikoje tena Hiyo Jeni!?.
Aaaaaa ni ndoa ya mahakamni tu.Ila kwa maelekezo zaidi kuna mwanasheria hivi namjua pale mahakamani anaishi mitaa ya hapo kati mtaa wa pili hivi ntamuita Au ntampigia ili anieleweshe vizuri Kwasababu informations zako nyingi nazijua Au Vipi?.
Sawa,Itakuwa vyema Sana.
Haina shida, Kwasababu laaa sivyo useme usilimu tu kiurahisi rahisi tu hapana Zamda.Kwasababu hata kama Mimi ni mkiristo siwezi kukushawishi eti uhamie kwenye dini yetu ili tuwe wengi.Kwasababu kumbuka haya Mambo ya dini ni imani tu na kwa ujumal dini ni utamaduni mwingine. Kwahiyo katika kuubadilisha huu utamaduni na imani hiyo ni kweli inaweza kufanyika na ikaleta madhara positive Au negative
Sawasawa Jeni hapo nimekupata.
Basi siku hiyo ikiwa ni siku nyingine kwa wapenzi wakuibia Lakini wenye kuonekana ni wapenzi wenye mapenzi ya dhati dhahiri. Kila mtu anampenda mwenzake nao si wengine ni Zamda na Zaidu. Siku hiyo ikiwa ni siku ya jumapili kama kawaida ya Zaidu kwa siku ya jumapili japokuwa nayo siku hiyo huwa anaenda shule pia kujisomea, Lakini ni uamuzi wake akishamaliza kusoma anaweza kwenda kutembea tembea kidogo.Basi siku Hiyo ikiwa ni mishale ya saa Kumi na nusu alaasiri Mwanadada mrembo Mwenye maamuzi ya kwake ya moyoni akifanya jambo anafanya Kwasababu fulani Yaani ni huyo Zamda.Kwaujumla Zamda afanyapo jambo hufanya kwa sababu fulani. Basi hafanyi kwaajili ya mtu fulani kumuona Au kwa starehe. Hiyo ni falsafa ya mwanadada  Zamda. Mda huo wako na Zaidu katika kochi safi sauti ya Runinga mda huo ilikuwa imepunguzwa kidogo. Basi hiyo ikawa inaonesha Kwamba mazungumzo wanayoyazungumza ni ya muhimu sana
.
"Mda huo akionekana Zamda yuko karibu sana na Zaidu Mkono wake wa kushoto kauweka Kwenye paja la Zaidu, mimba yake ikiwa nayo imezidi kukua kwa miezi na siku zinavyoenda.Kama kawaida yake kajifunga  kanga tu na paja kaliachia wazi nayo hewa kidogo apate.Basi mda huo akawa anamwambia Zaidu hivi".Zaidu Unajua sijui nianzie wapi,Kwasababu nashindwa hata namna ya kuweza kukuelezea jambo Au mambo ambayo moyoni mwangu huwa Nayafikiria Sana.
" mda huo anaonekana Zaidu akiwa amevalia tisheti nyeusi na kofia ya Mungu usione nyeusi suruali nayo iliyokuwa nyeusi na ukichanganya na weupe wake alionekana kama mzungu fulani Hivi kumbe shombeshombe tu.Zaidu akamwambia Zamda Hivi ".aaaa sema tu,itakuwa ni vizuri ukawa unajiamini ukiwa na Mimi. Usiniogope Bali niheshimu kama ninavyokuheshimu.kwa jambo lolote lile wewe  kuwa muwazi tu Mpenzi wangu."mda huo Zaidu akiwa anauchezea chezea mkono wa kushoto wa Zaidu sehemu ya kwenye kiganja".Kwahiyo kuwa huru nieleze.
Aaaaa Zaidu ni mda Kwasasa Tangu tuingie kwenye mahusiano ya Kimapenzi tena mapenzi ya dhati hata kama ingekuwa inafaa tungesema sisi tuko katika uchumba.
Aaaaa Zamda ni kweli. Mmmmu sijajua nini umefikiria hadi kuongea Hivyo Wewe?.
Zaidu una mapenzi ya dhati sana kwangu,Ndiyo maana hata siku moja hivi nilimueleza Jeni nikamwambia kwamba Kwakweli kwasasa mimi kwasasa mawazo ya Tito hayako kichwani mwangu kabisa.
Bali yako kwa nani?.
Kwako.
Kwangu Mimi zaidu kabisaaaaaaa.
Ndiyo.
Nashukuru sana Zamda kwa nafasi hiyo uliyonipatia katika fikra zako.
Sawa na Mimi nikupe shukurani kubwa Sana.
Hivi zaidu hujawahi kufikiri kwamba iko siku Mimi na Wewe tunaweza kuoana?.
" Zaidu alilifikiria hilo jambo kwa sekunde chache hivi kisha akasema ".Aaaaaaa unajua kila Mda una mda wake,na kila mda una matukio yake."Akawa amenyamaza tena kidogo akiwa anamuangalia Zamda machoni kisha akasema Hivi".Aaaaaa nilishawahi kulifikiria Hilo Jambo kwa undani Zaidi.
Kwaundani zaidi ukimaanisha Nini.
Aaaaaa nikimaanisha kwamba iko siku nayo tutakuwa na Watoto wetu ila si Hawa .Lakini kama vipi naweza kuwalea.
Kweli !!??
Ndiyo.
Unajua Zaidu natamani mimba hii ungenipa wewe.
Hapana Zamda usiseme hivyo. Kila jambo ambalo mungu ameamua afanye kwa mja wake katika uso huu wa dunia lina maana fulani.Maana hiyo inaweza kuanza kwa udhuri Au kwa ubaya. Kwahiyo usijekuongea tu hiyo sentensi kwanza ni kama kumkufuru Mungu.
Sawa Mpenzi Wangu nimekuelewa.
Embu nikuulize Jambo fulani.
Uliza tu.
Aaaaaaa vipi Tangu Tito aondoke Kipindi hicho alishawahi kutuma fedha yoyote?.
Hapana.
Anafikiria nini huko alivyokuacha hivi?.
Siku hiyo nilimuuliza Bi mkubwa hapo akasema kwamba hela ndiyo hii ninayoila hapa nyumbani. Yaani chakula na vitu vingine kama vile kufua huko ndiyo Hivyo. Sijui kama ni Kweli ila hajawahi kunitumia fedha yoyote hadi Leo.Ndiyo maana hadi siku ile nikakushukuru sana ulivvyonipeleka hospitali.
Wala usijali Zamda iko siku nayo kwako Chozi unalolitoa kila ukiyakumbuka Mambo unayofanyiwa Chozi hilo litakuja kuwa ni CHOZI LA DHAHABU. Nasema kwa kinywa changu Zamda nitakuoa.
Kweli Zaidu.
Ndiyo Ukweli Lakini japokuwa si leo wala kesho jitahidi kuwa na subra.
Sawa mme wangu.
Sisi Binadamu si kama wanyama wengine. Ujue kwamba pia siyo kama milima kwamba haikutani ni Kwasababu yenyewe imeota bali Sisi tumezaliwa basi ndiyo maana tumeambiwa mwanadamu mizunguko Ndiyo inayomfanya akutane na Maisha mbalimbali na pia na watu wa aina mbalimbali.Kwahiyo ukumbuke tu kwamba Mimi nimesema nitakuoa bali usiulize ni lini.Hii ni nadhiri yangu kwako Basi Natumai nadhiri yangu hii kupitia sauti uliyoisikia ya nadhiri Basi Sauti hii na maneno haya utakuwa unayasikia masikioni na kunikumbuka namna nilichokuwa nimevaa.
Nikiuliza itakuwaje.?
Itakuwa ni swali gumu kwangu. Kwasababu kwasasa kwa wewe ni mchumba wa mtu. Kwasababu miaka mliyoishi mmefikisha kama minne Hivi. Kwahiyo siyo rahisi tu kusema bana Eee tutanye arusi mwezi fulani.ila kwasasa wewe ni mchumba wa Tito.
Laaaa.
Najua utaona ni vigumu Bali elewa kwamba hata mtoto wa yatima anapolelewa na mlezi mwingine hawezisema kwamba yule ndiyo Baba Au mama, ni sawa anaweza kumuita mama Au Baba Bali Ukweli utabaki pale pale tu kwamba wale ni walezi wa mwana huyo.  Sijui kama umenielewa kwa  huo undani.
Nimekuelewa Zaidu.
Ila kwasasa ukijifungua nakushauri usizae tena Yaani Tena.
Sawa.
Yaani Zamda una miaka Kumi na nane kuelekea Tisa unataka kuwa na Watoto wawili. Lahaulaaaeeee.hapana nakwambia usidhae tena.Kwasababu utazeeka haraka.
Sawa Zaidu nimekuelewa.
Mimi miezi si michache nitafanya Mtihani wa Taifa wa kidato cha nne wa elimu ya watu wazima.
Baada ya hapo utaenda wapi Zaidu.
Hapana nitakuwepo tu.
Usiondoke Zaidu.
Nitaangalia na ratiba zinakuwaje ila sintokusahau.wewe ni mwanamke pekee uliyenipa na kunionesha utamu wa mapenzi ulivyo.Mambo mengine Kwenye mapenzi sikuwa nayajua  Bali kupitia wewe nimeyajua sana.
Sawa.
Sasa Zamda nataka niondoke.
Jamani mbona mapema hivyo?.
Hapana si mapema. Nataka nikajiandae vizuri kwaajili ya Mambo ya kesho shule.
Jamani natamani hata ungebaki tu tulale wote leo.
Wala usihofu kuna Kipindi tutalala wote Sana.
Haya bana.
Huyu Jeni naye leo harudi,akija utamsalimu umwambie alale mapema Kwasababu si kwa bata hiyo.
Haya.
"Basi mda huo Zaidu anaonekana anainuka na kumuinua Zamda baada ya kumuinua  Zaidu  akawa anashika shika tumbo la lenye kijacho Zamda na Zaidu huku midomo yao ikikaribiana ikionesha dhahiri ni denda za kuagana. Zaidu ni kijana ambaye Kwakweli kwenye denda amejaaliwa kwelikweli kumpatia mwanamke Yaani mithili ya kusema alienda kusomea.Basi kwa  namna wanavyopeana na Zamda hapo Kwakweli Zamda anajikuta yuko nyuma ya dunia kabisa kwa mambo anayopatiwa zaidu.Basi baada ya kumaliza kupeana denda tayari Zamda ikabidi amsindikize Zaidu hata hadi getini tu Kisha arudi."
Basi ni siku nyingine kabisa na maeneo mengine kabisa wakiwa Jeni na Zaidu ambapo ni maeneo ya shuleni kwao. Kwa mda huo ilikuwa ni mishale ya saa Tano hivi Wakiwa wanaonekana wanapata Chai kidogo ikiwa ndiyo Kama mda wa mapumziko.
Basi Zaidu anaonekana kama kawaida mzee wa kuulamba huku kavaa suruali nyeusi na shati lake la bluu viatu vyeusi vya kufuta tu. Jeni naye Kavaa kama mwanadada wa benkI Basi Walikuwa na maongezi kama yafuatayo.
Aaaaa Unajua Zaidu
Nambie.
Siku zimekaribia kukata tufanye paper tupite Hivi. Au siyo?.
Ndiyo maana Yake.
Kwahiyo umepangaje?.
Kuhusu.
Kuhusu Tena.
Ndiyo.
Aaaaa Zaidu nachomaanisha vipi pale kwa Zamda inabidi ukapige cha mwisho mwisho Kwasababu Hujui ukishamaliza Mambo yatakuwaje unaweza ukabaki au vipi. Kwahiyo inabidi umpatie cha kumuaga.
Kweli.
Alafu ukumbuke miezi ya kuja mchizi wake huyo Tito imeshakaribia.
Alaaaaa,kweli.
Ndiyo maana Yake. Kwani wewe ukajua bado tu.
Duuuu Hatari.Haina shida Jeni sinajua Jeni uko Kwahiyo kila kitu kitanyooka tu. Nampa mautamu ya mwisho pale Pale mageto kwako.
Hamna noma ni wewe mwenyewe tu.
Lazima nifanye Kweli.
Ndiyo Hivyo. Alafu Yaani Sasa Zamda ni anakuwaza wewe tu Yaani sijui akija  huyo jamaa yake itakuwaje kwakweli.
Yaani nakwambia matata sana.Kwasababu hata juzi juzi hivi nilikuwa naongea naye  yaani Mambo aliyokuwa anayaongelea duuuu hadi nikasema huyu Mtoto kweli kaniganda kwelikweli.
Ndiyo Hivyo alafu wote mmekutana waislam wote wakuitwa Zaidu na Zamda hadi Raha nakwambia. Alafu kiumri Bado mdogo tu yule lile ni umbile lake tu ndilo linamfanya aonekane ni mkubwa.Umempita kama miaka mitatu Hivi.
Nimemuahidi iko Siku
Ni vyema kweli kama ikiwezekana tu
Yule mtaishi naye vizuri sana.
Haya Basi nikwambie kitu siku  Ya Jumatatu asubuhi inabidi nije pale mageto kwako mapemaaaaaaa nimpe mautamu yule.
Kwani Jumatatu hakuna paper?.
Liko Lakini si mchana alafu rahistu tu kama kumsukuma mlevi bana.
Haya bana.
Basi Freshi chamsingi ni kujiamini tu.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)