MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 13

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU SEHEMU YA 13
#1
SIMULIZI : CHOZI LA DHAHABU  
      SEHEMU YA 13
      Hadi Zamda kuanza kuchepuka si kwamba niameamua tu bali kuna vitu ambavyo vimemsukuma hadi Yeye kujikuta anajiingiza Kwenye uhusiano wa Kimapenzi na Zaidu. Cha kwanza Kabisa ni jambo la kusema Kwamba kwa mda ambao anao mimba hamna hata mtu wa kukaa nae karibu na hata kumpatia Ushauri nini cha kufanya na kipi si cha kufanya, pia Jambo lingine ni kwamba tangu Tito kusafiri Safari yake ya kikazi nje ya mkoa wa Ngata hajawahi kumpigia simu Huyo Zamda na wala hata kumtumia Zamda fedha yoyote ya kujikimu kimaisha.
Siku hiyo Zamda alikuwa amekaa peke yake Kwenye kochi akiwa  pakee yake Runinga akiwa amefungulia.Mda huo ni ikiwa ni mishale ya saa Tano asubuhi. Kakaa pekee yake akiwa Kwenye Bahari ya mawazo kweli kweli. Mda huo alizidi kuwaza hadi akajikuta anaanza kuongea tu pekee yake mithili ya kichaa.
"Hapo alipokaa ni Kwenye kochi anaonekana amejifunga kanga moja kutoka kifuani kushuka hadi magotini. Alikuwa anaongea Hivi"
"Mume wangu samahani sana ni kosa kubwa Sana nimelifanya huku, nimeishi na wewe kama miaka mitatu hivi waelekea wa nne kabisaa sijawahi kukusaliti ila nashangaa kwasasa nakusaliti.Nisamehe huko uliko mme wangu kwa mambo ninayokufanyia huku ambayo ni mabaya kwelikweli. Ni mambo ambayo sikuwahi kutarajia kuyafanya Kabisa katika Maisha yangu.Ila Lakini wewe Ndiye kama msababishi wa haya yote. Kabisa mume wangu hata siku ile unaondoka nilikuambia kwamba Mimi na mama yako hapa hazipandi.Kwahiyo nikawa najua kweli mme wangu ananipenda Hivyo basi atakuwa amenisikiliza nini nimemwambia,Lakini chakushangaza baada ya kuondoka tu sijui Yale maneno ambayo nilikuambia uliyaachia hapa getini na ndiyo maana hukumbuki hata kitu kimoja nilichokumbia,hunipigii simu,hunitumii Hela ya matumizi, mwanao yuko hapa,kwani Mimi nafanya kazi Jamani. Ingekuwa hata nauza nyanyanyanya hivi hata kwa siku nikipata mia ntajua ni namna gani ntagawa.Lakini sina hata huo mtaji wa kuweza Kuanzisha hata kakibanda kakuuzia hizo nyanya.
Lakini mume wangu mbona kama ni mshahara unapokea mshahara mzuri tu Lakini leo hii ni kama tayari miezi  na masiku hivi hamna chochote huku kwenye simu yangu sijaona hata huo ujumbe wa hela.Au Mimi Ndiyo sijaangalia Jamani."Anaonekana anachukua simu yake na kuanza kuangalia Kwenye sehemu ya ujumbe inawezekana kuna ujumbe wa fedha umetumwa lakini hakukuta chochote kwenye simu yake zaidi tu ni jumbe za Mitandao anayoitumia.aliendelea kuongea".
mshahara unaoupokea Kwakweli si wakukufanya uone maisha nagumu namna hiyo hadi kushindwa hata kunirushia chochote. Ulivyoenda siku ile nikakwambia usijeukatusahau huku,umeaniacha Mimi nikiwa na mwanetu ambaye ni Glady na mwingine huyo kwasasa wananiita mama kijacho.Sasa hii mama kijacho vipi nashindwa kuelewa Je huyo baba aliyesababisha Mimi kuitwa mama kijacho yuko Wapi. Watu hao ni wanetu wanahitaji matunzo mazuri.Sasa mbona hivyo. Sijapenda kuchepuka ila wewe wewe ndiye uliyenisukumia kwenye Hilo janga  ambapo hadi nije kujinasua sidhani kama ni leo Au Kesho.
Mimi ni mwanamke wa kingata mapenzi kwangu ni kama chakula yaani nikikosa tu kama siku ngapi tayari mwili unaanza kuniwasha tu.Uhusiano wa Kimapenzi niliokuwa nao Kwasasa Kwakweli na huyo kijana  Jamani siamini ndiyo nakufuru Hivi Kwakweli yuko vizuri kitandani kwelikweli hadi nasahau shida zote kabisa. Utamu wake waja hadi kisogoni Jamani.Zaidu ananigusa Penyewe hadi najikuta tu mwili mzima sina kazi nao Bali Yeye Ndiyo Ana kazi Kwenye mwili Wangu.
Tito hadi nafikia kuongea hivi Yaani nakufuru kabisaaaaaaa ni wewe ndiyo unayesababisha yote haya.sijui huko uliko wewe Yaani sijui umenifanya mfanyakazi hapa kwenu au vipi Jamani. Mbona nyiye wanaume mko hivyo Jamani."Mda huo anavyoongea Hivyo hadi machozi yanamtoka".Yaani umenitoa kwetu Ngata na kuja kunifanya hapa kama mfanyakazi wa ndani kabisa. Hata kama nyumbani nilifukuzwa Bali si Kwamba nilitoroka. Hapa nilipo hata sijui dira ya nyumbani kwetu ilivyo.
Ingekuwa najua dira ya nyumbani kwetu ilivyo Kwakweli japokuwa  sina nauli hata ningetembea kwa magoti tu polepole kama kobe huku nikiwa nalia hadi nifike nyumbani kwetu naniwaombe Wazazi wangu msamaha kwa kosa la kiudhalimu nililowafanyia.Lakini Ndiyo Hivyo uwezo huo sina kabisa sanaaaaaaaaa.
Tito mwanamke kiuno chake hupenda akizungushe mara kwa mara ndivyo tunavyoamini wanawake wa Ngata.Yaani ingekuwa ndiyo umeniolea kulekule na tukaishi kule kule Kwakweli nigeenda kukushitaki kabisa kwa mambo unayonifanyia.Najikuta naongea pekee yangu Kama kichaa wa kulogwa Jamani eeeeee mola nisaidie mimi mja wako.Najua ninayoyafanya ni makosa ila Sasa ndiyo hivyo kuna visababisha vingi Sana hadi Mimi kufanya Hivi.
Miezi nayo ilizidi kwenda sekunde, dakika,masaa na siku nazo zikiwa zinazidi kuyoyoma tu Tito akiwa amenyamazia kimya huko alikoenda kikazi. Kipindi hicho tayari Miezi kama sita imeshapita.Basi siku Hiyo ikiwa ni siku ya jumapili. Kwa siku kama Hiyo ni siku ambayo Tito huwa anakuwa na nafasi nzuri sana hata ya kuweza kutoka na kwenda maeneo mbalimbali kuvinjari.Basi mda huo Tito anaonekana akiwa sehemu moja Hivi ambapo ni baa akiwa na Mwanadada mrembo kwelikweli. Sehemu walipo mezani kuna mavyakula kedekede na vinywaji vya kilevi vya kutosha.Mwanadada aliyekuwa naye Tito katika meza ile anaitwa kitunda.Kikunda kwa mwonekano wake Kwakweli amejaaliwa umbo rangi yake mweupe  peeee mithili ya Mtoto wa Debey kumbe kazaliwa katika mkoa wa kihangu.Basi mda huo mwanadada huyo alikuwa amevaa suruali na tisheti fulani Hivi nyekundu. kwa kijana Tito naye akiwa na ameulamba wake wa kofia ya Mungu usinione huku suruali akiwa ameitupia ya bei ghali ya rangi nyeusi na tisheti nyeusi. Basi mda huo wakiwa wamekaa kila mtu kwenye kiti chake wakiwa wanaangaliana wakati wanapeana dayalojia.Ilikuwa Hivi.
Kwani kitunda huku ndiyo kwenu Kabisa ulikozaliwa?."Mda huo Tito anaongea huku anamimina kinywaji".
Ndiyo ni Nyumbani kwetu.
Yaani ndiko ulikozaliwa huku kabisa.
Ndiyo.
Unajua siamini amini vile.
Kwanini huamini.
Yaani Unajua Kitunda nikikuangalia ulivyojaaliwa hivi Yaani hadi nakataa Kabisa kwamba wewe siyo mzawa wa huku.
Unajua Jabu wanifurahisha Sana."Kitunda baada ya kukutana na Tito Lakini walipokuwa wakitambulishana Majina Tito hakumtajia jina lake kamili Bali alimwambia kwamba Yeye anaitwa Jabu.Kwahiyo Ndiyo maana Kitunda anamuita Jabu".
Hapana, nakwambia Ukweli.
Kwani Yaani nikoje nikoje Jamani Jabu, mbona Mimi najiona wakawaida sana.
Hapana wewe wakawaida. Weeeee waliosema kioo hakidanganyi hao ni waongo.kinadanganya vizuri.
Aaaaaa kivipi kinadanganya Jamani.
Kinaonesha upande wa Nyuma tu wa  mwili.
Heheeeheheeheh haya bana hakioneshi.
Basi ndiyo Hivyo acha nikuambie tu kwamba Kwakweli Kitunda umejaaliwa Jamani. Sema unachotaka Kitunda Mimi nikupatie ili uwe mke wangu wa milele.
Haina shida Jabu mimi nitakuwa wako wa maisha.
Asante Sana.
Yaani inabidi nikiwa narudi huko kwetu nikuchukue tu tuende wote.
Weeee naogopa Jabu.
Waogopa nini Kitunda mpenzi Wangu.
Mke mwenza.
"Tito akawa ameshituka kidogo baada ya Kitunda kusema mke mwenza na kujiuliza chapuchapu akilini mwake kwamba Kitunda ni kaongea tu Au inawezekana anamjua vizuri tu .Kisha akasema Hivi".Aaaaaaa sina mke bana.
Kweli.
Ndiyo ukweli huu naokwambia kwako kwamba Mimi nataraji nikuoe mda maalumu ukifika.siunajua haya Maisha bila kuyapanga vizuri utajikuta unabaki kuibiwa tu.
Ni Sawa. Ila siamini Kweli kama Jabu utanioa.
Amini tu Kitunda iko siku tutaishi kwa amani Mimi na Wewe na tupande na Watoto wetu kwa mda unaotakikana.kwani wahofia nini.
Sihofii chochote
Bali.
Unajua wanaume wengi wanaweza kukuahidi jambo Fulani kwako Lakini ukajikuta unamsubiria yule aliyekuahidi unawakatalia Hawa wengine, Lakini cha kushangazwa kabisa baadaye hiyo  huyo aliyekuahidi kakutema.
Hapana Kitunda. Kweli Kitunda hata Mimi ni mwanamme Lakini tabia kama hizo za kishwaini hizo Mimi sina Kwakweli. kama Ndiyo Hivyo unafikiri tungekuwa hapa.
Haya nasikiliza maneno yako nakuachia nafasi, Basi tutaenda wote huko kwenu.umeniambia Wapi panaitwa?.
Panaitwa Kimbu.
Ahaaaaa Kimbu. Sasa kabla ya hapo itabidi tuende kwanza nyumbani kwetu nikakutambulishe.
Nyumbani kwenuuuuuu,usihofu tutapanga.siunajua niko taiti sana,nimebanwa sana Yaani siku za jumapili ndiyo huwa napata nafasi kwa siku nzima. Kwahiyo usihofu Mpenzi wangu tutaenda ili tusiwe tunafanya Mambo yetu kwakujifichaficha tu.
Sawa ntafurahi sana ikiwa Hivyo.
Utafurahi sana Kitunda. Mimi napokea mshahara Lakini sina hata mtu wakuniumiza kichwa ili nifanye kazi kwa bidii afadhali kwa Sasa nimekupata wewe utatumia Hela zangu hadi utasema Basi tu.
Haya bana.
Mchezo unaoendelea kati ya Zamda na Tito kwkeli hapa ni kufuata tu msemo wa nzi usemao Kwamba kama Wewe Unajua kwa Mbele Basi mimi najua kwa Nyumba. Kwasababu Tito anafanya Mambo yake huko aliko na pia Zamda anafanya yake huku aliko kila mtu na ujuzi wake.
Ikiwa kipindi hicho tayari Zamda mimba imeshakuwa kubwa Kabisa yakuonekana kabisa. Siku hiyo alikuwa akiongea na rafiki yake hapo nyumbani ambaye ni Jeni.Mda huo anaonekana amekaa kwenye kochi kajiachia kajifunga kanga tu kifuani hadi mapajani.kwa namna alivyokaa mapaja yake kayaacha wazi yaliyojaaliwa weupee kwelikweli ukichanganya na usafi aliokuwa nao.Naye Jeni akiwa amekaa kwenye kochi kama kawaida yake mama wa kujiachia ili apulizwe na upepo vizuri sehemu zote.Mda huo wanapopeana stori za hapa na pale Walikuwa wanaangalia Runinga. Basi mda huo Zamda akawa anamwambia Jeni hivi.
Hivi Unajua Jeni Tito amenitoka kichwani kabisaaaaaaa Yaani Unajua kabisa.
Alafu wewe zamda unachekesha kwelikweli.Kwanini Sasa.
Sijui tu.Yaani mda wote namuwaza tu huyo Zaidu. Yaani kanikoa machoni mwangu kwelikweli. Yaani Alafu hadi Glady anamuita Zaidu kwamba ni Baba.
Duuuu Sasa si kila siku anamuona kabisa unaingia naye chumbani mnalala,Sasa unafikiri asimuite baba Kwasababu gani.
Yaani Jeni natamani Zaidu angenipaga Yeye mimba.Kwakweli ningejikuta wa juu Sana. Zaidu Ana mapenzi ya dhati kwangu. Zaidu huyu Glady siyo mtoto wake Lakini hapa akija anaweza kuja hata na vinguo kidogo,matunda kama vile maembe,mananasi,machungwa na mapeasi.Huwa nafurahi sana Jamani. Hadi nasema Jamani Eeeee mungu kwanini hivi.
Kweli Zaidu huwa namuona ni mvulana ambaye yuko tofauti sana na wavulana wengine. Yaani kwanza kwa namna alivyo na wewe Ndiye uliyemtongoza ingekuwa ni mvulana mwingine tayari angeanza kukutangaza tu huko uswahilini.
Daaaa Jamani Mimi Nasema tu hata kama huyo Tito akija sijui kama nitamsahau Zaidu. Zaidu ananihudumia miye kama mke wake kumbe Mpenzi tu.Lakini ukija kwa Huyo Tito ambaye kaacha Mtoto mmoja hapa na mwingine mtarajiwa Ndiyo Hana huooo mda kabisa. Yaani Tito tena Sasa Ndiyo kazidi kwelikweli.
Kivipi Yaani.
Yaani Sasa hata kama nikimpigia simu anapokea nakusema yuko bize baadaye usiku.Haya huo usiku nikimpigia Ndiyo wala hapokei simu kamba amelala.
Hhahahahahhaha AAA wewe Zamda usiseme amelala sema wamelala.
Labda Ndiyo Hivyo.Ila Kwakweli Jeni zaidu nitamuombeaga sana kwa mungu aje ajaaliwe kupata mke ambaye Kwakweli wataendana naeye.Zaidu ni mtu anayependa kunipa Ushauri kweli kweli Mara kwa mara. Ile mwanzoni tu tulivyoanzaga Yaani tumelala naye kama mara nne hivi nikawa namwambia nitoe mimba.
Haaaaaaa Zamda utoe mimba Kwasababu gani Sasa?.
Weeeee Sasa kama Tito haeleweki nifanyaje?.
Yaani wewe unachekesha.Alafu Zaidu akakuambiaje?.
Akaniambia Kwakweli nitakuwa nimetenda dhambi kubwa Sana ambaye dhambi hiyo hata Zaidu anasema atakuwa ameishiriki kwamba angenikubalia Mimi nitoe mimba.
Zamda kutoa mimba siyo kiurahisi rahisi tu.unaweza kupoteza Maisha unajionea kabisaaaaaaa Yaani chapuchapu. Yaani wewe mshukuru mungu umekutana na mtu ambaye anatumia akili. Japokuwa alikueleza madhara ya kutoa mimba kiimani sana Lakini hata ukija kitaalam haifai kabisa. Kwahiyo mshukuru zaidu.
Daaaa zaidu nitakupenda milele kokote uliko.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)