MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
Matumizi ya Lugha Katika Methali

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
Matumizi ya Lugha Katika Methali
#1
Sitiari
  1. Mgeni ni kuku mweupe.
  2. Ahadi ni deni.
  3. Upweke ni uvundo.
  4. Mgeni ni kuku mweupe.
  5. Ujana ni moshi.
  6. Mapenzi ni kikohozi.
  7. Kukopa arusi kulipa matanga.
Tashbihi
  1. Kawaida ni kama
  2. Riziki kama ajali ijapo huitambui.
  3. Usilolijua ni kama usiku wa giza.
  4. Ufalme kama mvua hupiga na kupita.
Tashhisi
  1. Siri ya mtungi muulize kata.
  2. Paka akiondoka panya hutawala.
  3. Jembe halimtupi mkulima.
  4. Ukupigao ndio ukufunzao.
  5. Adhabu ya kaburi aijuaye maiti.
Takriri
  1. Haba na haba hujaza kibaba.
  2. Chovya chovya humaliza buyu la asali.
  3. Hauchi hauchi unakucha.
  4. Hayawi hayawi huwa.
  5. Mtoto wa nyoka ni nyoka.
  6. Bandu bandu huisha gogo.
Balagha
  1. Pilipili usiyoila yakuwashiani?
  2. Angurumapo samba mcheza ni nani?
  3. Wameshindwa wenye pembe seuze wewe kipara?
  4. Simba mla watu akiliwa huwani?
  5. Mzigo uko kichwani, kwapa lakutokeani jasho?
  6. Mavi usiyoyala wayawingiani kuku?
  7. Mla ni mla leo mla jana kalani?
Taswira
  1. Mpanda farasi wawili hupasuka msamba.
  2. Mti mkuu ukigwa wana wa ndege huyumba.
  3. Mtupa jongoo hutupa na ung`ong`o wake.
  4. Angeenda juu kipungu hafikii mbingu.
Chuku
  1. Mzigo wa mwenzio ni kanda la sufi.
  2. Maji ya kifuu bahari ya chungu.
  3. Usipoziba ufa utajenga ukuta.
Tanakali za sauti
  1. Chururu si ndondondo!
  2. Ndo! Ndo! Hujaza ndoo.
  3. Kiliacho pa kijutie.
Kinaya
  1. Bara Hindi ndiko kwenye nguo na waendao uchi wapo.
  2. Kwenye miti hakuna wajenzi.
  3. Asante ya punda ni mateke.
  4. Kigumba kwa nguruwe kwa binadamu ki uchungu.
  5. Kikiharibika cha fundi kikiongoka cha bwana Sudi.
Kejeli/dhihaka/stihizai
  1. Umekuwa mung`unye waharibikia ukubwani.
  2. Hawi Musa kwa kubeba fimbo.
  3. Ucha Mungu si kilemba cheupe.
  4. Kichwa cha kuku hakistahili kilemba.
  5. Kichwa cha nyoka hakibandikwi mtungi.
Jazanda
Joka la mdimu hulinda watundao
  • Mtu mwovu huwanyima wengine vitu asivyovihitaji.
  • Kupanda mchongoma kushuka ndio ngoma
  • Ni rahisi kujitia katika matata kuliko kujitoa.
Taashira
  1. Kimya kingi kina mshindo mkubwa.
  2. Kuku mgeni hakosi kamba mguuni.
Kweli kinzani
  1. Wagombanao ndio wapatanao.
  2. Ukupigao ndio ukufunzao.
  3. Kuinamako ndiko kuinukako.
  4. Mwenye kelele hana neno.
  5. Kimya kingi kina mshindo mkubwa.
Tanakuzi
  1. Tamaa mbele mauti nyuma.
  2. Mpanda ngazi hushuka.
  3. Usione kwenda mbele kurudi nyuma si kazi.
  • Kuainisha methali kutokana na matumizi ya lugha ni kusema mbinu ambazo imetumia.
Vigezo vya Kuainishia Methali/Kuziweka Pamoja na kuzichambua
Mandhari/mazingira k.m. kilimo.
  • Ukipanda pantosha utavuna pankwisha.
  • Jembe halimtupi mkulima.
    1. Maudhui k.m. ulezi
  • Samaki mkunje angali mbichi.
  • Mcha mwana kulia hulia yeye
  1. c) fani/tamathali k.m. takriri
  • Haba na haba hujaza kibaba
  • Mtoto wa nyoka ni nyoka.
  1. d) Jukumu k.m. kuonye
  • Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
  • Ukiambiwa jiambie usijeishia kumbe.
    1. Maana k.m. sawa
      • Haraka haraka haina baraka.
      • Polepole ndio mwendo.
[*]Vigezo zaidi vya kuchambua methali
Inarejelea vitu gani? K.m. Hindi ndiko kwenye nguo na waendao uchi wapo.
  • Nchi-Hindi
  • Vitu-nguo
  • Watu-waendao uchi
  • Inakupa wazo gani kuhusu jamii husika?
  • Utamaduni na njia za kiuchumi.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)