MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
Mbinu 7 za Kuwa Mwandishi Bora

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
Mbinu 7 za Kuwa Mwandishi Bora
#1
Kama umewahi kuwa na ndoto au matamanio ya kuwa mwandishi mkubwa kama vile Wole Soyinka, Ngũgĩ wa Thiong’o au pengine hata kuwa mwandishi bora kitaaluma au katika blogu yako, basi ni vyema ukajifunza namna ya kuwa mwandishi bora.
Kuwa mwandishi bora si jambo la mzaha; ni jambo linalalowezekana ikiwa utaweka jitihada stahiki.
Ni dhahiri kuwa jitihada utakazozifanya hazitakuwa bure kwani hivi leo kuna fursa mabalimbali zinazohitaji watu wenye uwezo mzuri wa uandishi.
Hivyo basi, fuatana nami nikujuze mbinu zitakazokuwezesha kuwa mwandishi bora kabisa na kufikia malengo yako ya mbeleni.

Soma maandiko bora

Ni dhahiri kuwa ukihitaji kufahamu nini mana ya uandishi bora ni lazima usome maandiko bora yaliyoandikwa na waandishi mahiri. Soma maandiko bora kadri uwezavyo kwani utajifunza mambo mbalimbali yakiwemo mpangilio wa hoja, uwasilishaji, matumizi ya lugha n.k. Kama una tatizo la kifedha unaweza kusoma maandiko mbalimbali yanayopatikana kwenye mtandao kwa gharama nafuu kabisa kuliko kununua vitabu au machapisho mengine.
Jifunze kanuni bora za uandishi
Uandishi una kanuni zake kama ilivyo kwa taaluma nyingine. Unatakiwa kufahamu maswala kama vile matumizi ya lugha, alama za uandishi, upangaji wa hoja, mbinu za uhariri n.k. Kwa kufanya hivi utaweza kuboresha uandishi wako na kuufanya kuwa wa kiwango cha juu kabisa.
Andika sana
Mazoezi hukufanya kuwa mahiri – practice makes perfect. Kadri unavyoandika kwa wingi ndivyo unavyojenga uzoefu wako zaidi. Uzoefu hupatikana kwa kufanya jambo fulani kwa muda mrefu. Hivyo jitahidi kuandika maandiko/matini mengi kadri uwezavyo ili uweze kunoa uwezo wako wa uandishi. Kupitia mbinu hii utaweza kubaini changamoto mbalimbali za kiuandishi na njia ya kuzitatua.
Tenga muda bora wa kuandika
Siyo wakati wote unafaa kwa ajili ya shughuli za uandishi. Ni vyema ukajitengea muda ambao uko vyema kiafya na kiakili. Mara nyingi asubuhi ndipo mtu anapokuwa na nguvu za kimwili na kiakili kufanya kazi mbalimbali. Hivyo ni vyema ukabainisha muda ambao wewe mwenyewe unaona ni bora kwako kufanya shughuli za uandishi bila matatizo.
Ondoa vitu vinavyokuvuruga
Maisha yetu yamejaa vitu mbalimbali. Vingine hutawala sehemu kubwa ya maisha yetu kiasi cha kutaka kuingilia au kuvuruga kila tunachokifanya. Ili kuwa na ufanisi katika uandishi ni vyema ukaodoa vitu mbalimbali vinavyoweza kukuvuruga kama vile mitandao ya kijamii, simu, televisheni, michezo ya kielektroniki, watu n.k. Unaweza kuzima simu au data katika vifaa vyako ili kuzuia kuvurugwa na mambo ya mtandao. Unaweza kutafuta chumba au eneo maalumu lenye utulivu litakalokuruhusu kufanya kazi yako ya uandishi kwa utulivu. Kwa mfano ninapoandika makala hii nimekaa katika chumba cha kusomea ili kuhakikisha ninapata utulivu wa kutosha.
Orodhesha mawazo
Ni jambo zuri ukajizoesha kuorodhesha mawazo kabla ya kuanza kuandika. Kwa kufanya hivi utakuwa umejiwekea mwongozo mdogo utakao kuongoza juu ya yale unayoyandikia. Unaweza kutumia kipande cha karatasi, shajara, au hata programu za kompyuta kama vile MS Word na Google Docs ili kuorodhesha mawazo yako.
Andika tu bila kuacha
Ni vigumu kujikita katika uandishi bila kuacha kama hujajiwekea lengo na kuwa na mtindo anuwai wa uandishi. Ni dhahiri utazamapo karatasi nyeupe au ukurasa mweupe kwenye kompyuta unaweza ukasita au ukakata tamaa ya kuandika mapema. Hivyo, unaweza kufanya haya yafuatayao ili kuweza kuandika bila kuacha.
  • Andika tu mawazo kadri yanavyokuja akilini mwako kwani utayahariri baadaye.
  • Usifanye mambo mengi kwa wakati mmoja; yaani jikite tu kwenye kuandika bila kujihusisha na mambo mengine.
  • Usihariri; unapohariri wakati unaandika utapunguza ufanisi katika uandishi wako. Andika kwanza na utahariri baadaye.
Ukitumia mbinu hii utaweza kuandika mambo mengi kwa muda mfupi kwa urahisi zaidi bila kuacha au kukata tamaa.
Hitimisho
Zilizoelezwa hapa ni mbinu ambazo zitakuwezesha kuwa mwandishi bora. Mbinu hizi zinatumiwa na mwandishi kuandika makala kadha wa kadha katika blogu mbalimbali na zimempa ufanisi mkubwa. Hivyo unaweza kufanya maamuzi magumu ya kubadilika na kuwekeza katika kuboresha uwezo wako wa uandishi. Naamini hutojutia maamuzi utakayoyafanya kwani utakuwa na tija kubwa sana.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 3 Guest(s)