MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
KUHUSU MUHAMMED SAID ABDULLA (BW. MSA)

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
KUHUSU MUHAMMED SAID ABDULLA (BW. MSA)
#1
KUHUSU MUHAMMED SAID ABDULLA
MAISHA YAKE
Muhammed Said Abdulla alizaliwa huko Makunduchi kisiwani Unguja. Elimu yake ya sekondari alipata katika shule ya misioni ya kikristo. Baada ya kumaliza masomo mwaka 1938 aliajiriwa na serikali idara ya afya. Hapo alihamishwa kwa idara ya kilimo alipokuwa mhariri wa jarida la Swahili Bulletin.
Kutoka hapa aliendelea kuwa mwandishi wa habari na kuanzia 1948 akawa mhariri wa gazeti la Zanzibari. Baadaye alikuwa mhariri msaidizi wa majarida ya Al-Falaq, Afrika Kwetu na Al Mahda. Tangu 1958 hadi kustaafu mwaka 1968 alikuwa mhariri wa jarida la Mkulima. Katika kipindi hiki kilitokea mapinduzi ya Zanzibar ambako mke na watoto wake waliuawa.
RIWAYA
Mwaka 1958 Abdulla alishiriki kwenye mashindano ya utunzi wa tungo za Kiswahili (“Swahili Story-Writing Competition”) yaliyoendeshwa na Ofisi ya Fasihi ya Afrika ya Mashariki (East African Literature Bureau). Riwaya yake Mzimu wa Watu wa Kale ilishinda tuzo la kwanza ikachapishwa kitabu 1960. Hapa alimbuni mhusika Bwana Msa aliye mpelelezi wa binafsi anayeshirikiana na polisi na kudhihirisha siri ya uuaji wa mtu tajiri. jina la “msa” ni akronimi ya herufi za kwanza za majina yake mwenyewe Abdulla yaani M-S-A.
Abdulla aliendelea kutunga kwa jumla riwaya ya upelelezi sita ambako Bwana Msa ni mhusika mkuu. Mhusika huyu anafanana katika tabia kadhaa na Sherlock Holmes, mhusika wa riwaya za mwandishi Mwingereza Conan Doyle. Sawa na Sherlock Holmes Bwana Msa anavuta kiko, anapata usulihisho wa kesi kwa kutumia akili yake akishirikiana na msaidizi na rafiki yake Najum (anayefanana na Dr. Watson wa Sherlock Holmes) na kusaidia kazi ya polisi inayowakilishwa na Spekta Seif.
Wahakiki walimshambulia Abdulla kwa kutumia mfano wa kigeni. Hata hivyo hata akitumia nukuu za Conan Doyle aliweka masimulizi kabisa katika mazingira na utamaduni wa Unguja na jamii ya Waarabu na Waafrika kabla ya mapinduzi.
Wahakiki wengine wameona ya kwamba muundo wa kesi katika hadithi za Abdalla ni tata mno, hata hivyo wamemsifu kwa uwezo wake wa kuchora tabia za wahusika kikamilifu katika lugha na imani ya Kiunguja.
KATI YA RIWAYA ZAKE ZA KIPELELEZI NI;
Mzimu wa Watu wa Kale (1966)
Kisima cha Giningi (1968)
Duniani Kuna Watu (1973)
Siri ya Sifuri (1974)
Mwana wa Yungi Hulewa (1976)
Nje ya riwaya za upelelezi aliandika pia Mke Mmoja Waume Watatu (1975) kinachohusu ulaghai katika ndoa na mkusanyo wa hadithi fupi katika “Hekaya za Kuburudisha”.
WASIFU
Abdulla alikuwa ni mhariri na mwaandishi wa vitabu tofauti ambavyo viliinyanyua lugha ya kiswahili katika daraja la juu na kuiongezea umaarufu mkubwa eneo la afrika mashariki. Alifanikiwa kuowa mke na kupata wawili katika maisha yake. Vile vile ni miongoni mwa watetezi wakubwa walifanya utetezi katika kuikomboa nchi ya Zanzibar kutoka mikononi mwa Watanganyika. Na hii ndio ilikuwa sababu ya yeye kuwa katika hatari ya maisha yake. Miongoni mwa beti zake za kuwatupia watanganyika ujumbe utakaoweza kuwapotezea nguvu ya kutaka kuinyakuwa Zanzibar. Njama ilianza kupangwa na watanganyika ili kumuondoa Bwana Msa Katika hii dunia
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)