MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SITI BINT SAAD AMEIFARIKI DUNIA HII LEO JULAI 8

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SITI BINT SAAD AMEIFARIKI DUNIA HII LEO JULAI 8
#1
SITI BINT SAAD AMEIFARIKI DUNIA HII LEO JULAI 8

   

HEMED KIVUYO

"Tazameni tazameni eti alichofanya kijiti,kumchukua mgeni ,kumchezesha foliti,Kenda naye maguguni ,kamrejesha maiti"  Ni baadhi ya Maneno yaliyopo katika moja ya nyimbo za Siti Bint Saad ambao kisa chake nicha kweli.

Kilitokea kisa kimoja Zanzibar ambapo Mwanamama mmoja kutoka Bara alihadaiwa na Mwanaume mmoja Kisha kuuawa.

Vijana wengi hudhani baadhi ya nyimbo za Taarab zilizovuma ziliimbwa na Marehemu Fatma Baraka "Bi Kidude"mfano wimbo huo "kijiti" ambao bi Kidude aliuimba ka ufasaha.

Ndu zangu,Siti Bint Saad ameifariki Dunia leo Julai 8.

SITI NI NANI?

SITI alizaliwa Fumba Zanzibar 1880,na alipewa jina la "Mtumwa kwakuwa alizaliwa kipindi Cha utumwa.

Babake alikuwa Mnyamwezi wa Tabora na Mama alikuwa Mdigo kutoka Yanga .

Mamake alikuwa akiuza Nyungu huku Siti akimsaidia hiyo Ni baada ya kupata umriwakujifahamu.

Mwanzo wangoma nilele,Siti alianza kuonesha kipaji Cha uimbaji angali mdogo mno,kiasi Cha mapafu take kufananishwa na Simba kwakuvuta sauti muruwaa..

1911,Siti alindoka kijijini kwao na kuhamia mjini ndipo alipokutana na kundi la Taarab la Nadi ikhwan safaa"

Kundi hili lilianzishwa na Sultani Seyyid barghashy Said. Said anatajwa kuwa Sultani mpenda starehe".

Kundi hili lilikuwa na wanaume tupu kwakuwa miaka hiyo ,Mwanamke hakuruhusiwa kuimba,ilionekana Ni anasa kwao.

Safaa ilivutiwa na uimbaji wa Siti,hapo akaanza kufananishwa na Ummy Kulthum wa Misri.

Kundi hili lilimpa Siti nafasi akawa mwanamke wa kwanza kuimba Taarab katika Hadhira,umma ukahamanika baadaye ukasisimka na Siti hakuwa nawakufananishwa naye.

SITI alivuma ulimwenguni kote,si Afrika hata Ughaibuni. 1928 kampuni ya Columbia And hs masters voice ya Mumbai India ikamtafuta Siti kwa udi na uvumba.

Hatimaye Kampuni hiyo ikajenga studio visiwani Zanzibar kwaajili ya Siti.

Kwakuwa mwiba wa samaki humchoma hata mnunuzi Basi wasompenda Siti wakaanza "chokochoko".

Wakasema "Siti kawa mtu lini,kaja mjini na Kaniki chini ,Kama si sauti angekula Nini"

SITI hakukaa kimya naye akajibu kwa ubeti " Si hoja uzuri ,na sura jamali,kuwa mtukufu najadi kebeli ,hasara ya mtu kukosa akili" .

Mshairi maarufu Shaaban Robert alikutana na Siti siku kadhaa kabla Siti hajaaga Dunia ,

Alimwandikia Fasihi Bora kuwahi kutokea ulimwenguni "wasifu wa Siti Bint Saad". Wengi walizidi kumjua Siti kwa andiko Hilo.

Miaka ya hivi karibuni kulikuwa na Gazeti linaitwa "SAUTI YA SITI" sijui Kama bado lipo ama laa"

SITI aliaga Dunia tarehe 8 mwezi 7 mwaka 1950.

SITI ndiye aliyefungua ndiya kwa waimbaji wengine wakike wa Taarab,watilia mbali Hawa wajuzi akina Malika na wengineo .

Mola azidi kumrehemu Siti Bint Saad (Mtumwa)
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)