MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO ' HIRIZI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO ' HIRIZI'
#1
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO ' HIRIZI'.

Neno Hirizi katika lugha ya Kiswahili ni nomino yenye maana zifuatazo:

1. Dawa inayojumuisha maandishi, pamoja na uganga mwengine unaofungwa ama kwenye kitambaa au kwenye karatasi, kwa imani kuwa inaweza kufanya kile kinacholengwa mfano kumpa mtumiaji kinga dhidi ya madhara. 

2. Kitu kilichofungwa kwenye ngozi au nguo au kijikaratasi chenye maandishi ya Kiarabu kinachoaminiwa kuwa ni dawa ya kujikinga na madhara ambacho huvaliwa mwilini. 

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *hirizi* ( soma: *hirzun/hirzan/hirzin* *حرز* ) lina maana zifuatazo:

1. Kifaa kilicho ngao ya kujilinda.

2. Eneo lenye ulinzi na amani ambalo watu hupata hifadhi ya maisha yao; ngome.

3. Kitu kinachotoa KINGA dhidi ya madhara.

4. Kanzi ya kuhifadhi vitu vya thamani.

5. Fungu analopata mrithi kutokana na mgawanyo wa mirathi.

6. Kitu kinachoandikwa kwa nia ya kumkinga atakayekibeba dhidi ya shari na maradhi (kama wanavyodai).

Kinachodhihiri ni kuwa neno hili ( *hirizi/hirz* *حرز*  ) lilipoingia katika lugha ya Kiswahili na kutoholewa likawa *hirizi* maana yake katika lugha yake ya asili - Kiarabu - haikubadilika ingawa imejifunga katika mambo ya uganga na kago.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)