MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA NENO ' ALHAMISI'

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
ETIMOLOJIA YA NENO ' ALHAMISI'
#1
ETIMOLOJIA YA NENO ' ALHAMISI'.
Alhamisi, katika Lugha ya Kiswahili) ni neno (nomino) lenye maana ya siku ya nne ya wiki kuanzia Jumatatu, siku ya wiki iliyopo baina ya Jumatano na Ijumaa.
Neno hili (Alhamisi) asili yake ni Kiarabu na huko ni 'Alkhamiis الخميس '  neno ambalo mzizi wake ni *nomino ya Kiarabu* *khams* (namba tano #5).
Katika Lugha ya Kiarabu neno (Alkhamiis) lina maana zifuatazo:
1. Sehemu ya tano, moja ya Tano.
2. Siku moja katika wiki, siku ya tano ya wiki kuanzia siku ya Jumapili ambayo Waarabu wanaiita *Al-Ahad* (Siku ya Kwanza).
3. Jeshi lenye idadi kubwa ya wanajeshi, huitwa pia kwa Kiarabu *Al-Jayshu* *Al-Jarrar* *الجيش* *الجرار*. Tunaweza kuliita Jeshi la Pembe Tano kwa kuwa jeshi hili huwa na vikosi vitano: Kikosi cha Mbele, Kikosi cha Kati, Kikosi cha Kulia, Kikosi cha Kushoto na Kikosi cha Nyuma.
4. (Kwa watu) Mkusanyiko wa watu *Khamisun* *Naas* *خميس* *الناس*
5. (Kwa nguo na vitu vingine) ni kile chenye urefu wa dhiraa tano.
Neno hili 'Alkhamiis' lilipoingia katika Lugha ya Kiswahili na kutoholewa na kusanifiwa kuwa (Alhamisi) limejifunga na maana moja tu: siku ya wiki iliyopo baina ya Jumatano na Ijumaa.
Kutumika neno hili (Alhamisi) tunaloweza kulifasiri ' *siku ya tano'* kunafanya ulimwengu wa Kiswahili kuwa na siku mbili ziitwazo 'siku ya tano': siku moja kwa neno lenye asili ya Kibantu (Jumatano) na siku nyingine kwa neno lenye asili ya Kiarabu (Alhamisi/Alkhamis).
Nakusudia kusema kuwa Waswahili wameanza kuhesabu siku za wiki Jumamosi na Waarabu wameanza kuhesabu siku za wiki Jumapili. Muachano huo ndio ulioleta Jumatano (Siku ya 5 ya wiki) na Alhamisi (Siku ya 5 ya wiki).
*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)