MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
Nyimbo Katika Fasihi Simulizi

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
Nyimbo Katika Fasihi Simulizi
#1
Nyimbo ni aina ya sanaa katika fasihi ambayo hutumia lugha teule, sauti na kiimbo maalum.
Aghalabu nyimbo hutumia ala za mziki kama vile ngoma. Nyimbo zinaweza kuimbwa na mtu mmoja au zaidi.
Wimbo hugawanywa katika beti na mishororo. Nyimbo nyingi huwa na kiitikio au mstari ambao hurudiwa rudiwa.
Sifa za Nyimbo
  1. Hutumia kiimbo au sauti maalum
  • Huweza kuendamana na ala za muziki
  • Huimbwa na mtu mmoja au watu wengi; wakati mwingine nyimbo huimbwa kwa kupokezanwa.
  • Hutumia lugha ya mkato
  • Hurudiarudia (kukariri) maneno ili kusisitiza ujumbe katika wimbo
  • Umuhimu wa Nyimbo katika Fasihi Simulizi
    1. Kuburudisha
  • Kuelimisha, kufunza, kuonya, kuelekeza
  • Kuliwaza
  • Kusifia kitu au mtu katika jamii
  • Kuunganisha jamii
  • Kudumisha/kuhifadhi tamaduni za jamii
  • Kukuza talanta na sanaa katika jamii
  • Hutumika katika mbinu nyingine za fasihi kama vile hadithi
  • Vipera/Aina za Nyimbo
    Kulingana na Muundo:
  • Maghani
  • Kulingana na Ujumbe/Maudhui:
    Nyimbo za Ndoa
    Nyimbo za harusi huimbiwa bwana na bibi harusi kuwapongeza na kuwapa heko kwa kufunga ndoa yao. Aidha nyimbo hizi huwapa wawili hao mawaidha ya kutunza familia na watoto wao ili waishi pamoja.
    Nyimbo za Jandoni/Tohara
    huimbwa na vijana wanapopashwa tohara. Nyimbo hizi huonyesha ushujaa, na kuashiria kutoka kwamba anayetahiriwa amekuwa mtu mzima sasa.
    Hodiya/Wawe
    Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa na watu wanapofanya kazi ili kuwatia bidii wafanye kazi bila kuhisi machofu.
    Kimai
    Nyimbo za Mabaharia – Hizi ni nyimbo za wanabahari wanaposafiri baharini.
    Nyimbo za Mazishi/Huzuni/Simanzi
    Hizi ni nyimbo za kuliwaza na kuwapa pole walioachwa na marehemu. Nyimbo hizi huwapa matumaini waombolezaji.
    Nyimbo za Kidini
    Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa kumsifia Mungu, kuomba au kutoa mafunzo ya kidini.
    Nyimbo za Kisiasa
    Hizi ni nyimbo za kuwasifia viongozi wa kisiasa
    Nyimbo za Kizalendo
    Nyimbo za huonyesha uzalendo kwa kusifia taifa/nchi
    Nyimbo za Mapenzi
    Katika nyimbo za mapenzi, mwimbaji huimba kwa kumsifia mpenzi wake hasa kwa urembo na tabia zake.
    Mwl Maeda
    Reply


    Forum Jump:


    Users browsing this thread: 1 Guest(s)