MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
SIFA MSINGI ZA KUTAMBULISHA AINA ZA VITENZI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
SIFA MSINGI ZA KUTAMBULISHA AINA ZA VITENZI
#1
SIFA MSINGI ZA KUTAMBULISHA AINA ZA VITENZI
Vitenzi ni nguzo kuu katika sentensi, jinsi tujuavyo kuwa sentensi hukamilika tu kwa uwepo wa kitenzi.

Hivi ni kusema kwamba, neno moja la kitenzi ndilo hukamilisha sentensi, au tuseme kuwa neno moja ambalo ni kitenzi laweza kuwa sentensi. Mifano:

i) Mwanafunzi anasoma (sentensi kamili kwa sababu ya kusoma)

ii) Anasoma (sentensi kamili)

iii) Mwanafunzi huyu mrefu mwenye tabia nzuri (Si sentensi kamili kwa kuwa kitenzi hakipo)

Ni rahisi kubaini aina za vitenzi kwa kuwa majina yake huongoza kutambua aina hizo.

Fasili

Kitenzi ni neno linalorejelea tendo katika sentensi. Mfano, soma, imba, ruka.

Mifano katika sentensi:

i) Mwalimu anafunza.

ii) Mkulima anaenda shambani.

Aidha, kitenzi huweza kuwa neno linaloshirikisha, au kuonesha uhusiano baina ya vitu viwili. Mifano, alikuwa, angali, si, ni n.k.

Mifano katika sentensi:

i) Yeye ni mwalimu bora.

ii) Mkulima yu shambani.

Aina za vitenzi

Vitenzi vyaweza kutiwa katika makundi matano makuu. Makundi haya yanatokana na uamilifu/utendakazi  wavyo, unaozaa jina la kitenzi hicho. Katika maelezo ya aina za vitenzi, tutatumia Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Toleo la pili, kufasili maana ya maneno hayo.

A) Vitenzi halisi

Neno halisi humaanisha kweli, hasa, barabara (maana ya kamusi). Huku ni kumaanisha kuwa kitenzi halisi ni kitenzi hasa, yaani, tendo kamili.

Ni kitenzi kinachotumiwa kuonesha tendo linalotendeka katika sentensi. Tendo kamili, tendo hasa, tendo barabara. Mifano:

i) Wanafunzi wanasoma vitabu (tendo kamili, hasa au barabara linatukia; la kusoma)

ii) Wakulima wanalilima shamba (tendo kamili la kulima).

B) Vitenzi vikuu

Kitu kikuu ni kilicho kikubwa labda kwa cheo, umri n.k. Hili lina maana kuwa kitenzi kikuu ni kile kikubwa kimaana, kumaanisha kuwa kinatoa wazo kuu katika sentensi. Mifano:

i) Juma anaweza kupita mtihani (kupita ni kitenzi kikuu kwa kuwa dhana kuu ni kupita, wala si weza)

ii) Wakulima walikuwa wakilima (kitenzi kikuu ni wakilima, kwa kuwa ndilo wazo kuu katika sentensi hii).

Sifa za vitenzi vikuu

i) Hutanguliwa na vitenzi visaidizi. (Walikuwa wakilima)

ii) Huwa cha pili katika sentensi; kinatokea baada ya kisaidizi (Wa)
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)