MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
TANZU ZA FASIHI ANDISHI YA KISWAHILI (WATAALAMU MBALIMBALI)

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
TANZU ZA FASIHI ANDISHI YA KISWAHILI (WATAALAMU MBALIMBALI)
#1
Kama ilivyo kwenye tanzu za fasihi simulizi, haijawa rahisi kueleza tanzu za fasihi andishi kutokana na mikinzano inayoonekana
miongoni mwa wanazuoni.Wataalamu wengi wa awali wa fasihi ya Kiswahili walibainisha kuwa fasihi andishi ina tanzu tatu ambazo ni Ushairi, riwaya na tamthiliya.
MBUNDA MSOKILE 1992: Uhakiki wa fasihi
Yeye anasema tanzu za fasihi andishi zipo tatu; nazo
ni:

Riwaya

Ushairi

Tamthiliya
NKWERA 1976:
Sarufi na Fasihi, Sekondari na vyuo
Anafanana na
Msokile, naye anatambua tanzu tatu ambazo ni:

Riwaya

Ushairi na

Tamthiliya
MULOKOZI 1996
Anaanza kuhoji
uhakiki wa tanzu tatu. Yeye anasema tanzu za fasihi andishi si tatu ni nne;
nazo ni:

Ushairi

Riwaya

Tamthiliya na

Kisa
M’NGARUTHI
2008
Yeye
anakubaliana na Mulokozi kuwa tanzu zipo nne lakini hakubaliana katika majina. Yeye
anatambua:

Ushairi

Hadithi fupi

Riwaya na

Tamthiliya
Kinachoitwa Kisa
na Mulokozi M’ngaruthi anakiita Hadithi
fupi. Wataalamu wa Kenya wanakubaliana na M’ngaruthi, hivyo mfumo wa elimu
ya Kenya unatambua tanzu alizoziainisha M’ngaruthi.
Hata hivyo,
wataalamu wengine wameendelea kuhoji juu ya tanzu nne, kwa sababu novela
nazo zinaingia wapi?
Mfano:
WAMITILA, 2008
Yeye anataja:

Riwaya

Tamthiliya

Novela

Insha

Ushairi

Hotuba

Sira

Masimulizi ya wasafiri
Japokuwa Wamitila
hakiri moja kwa moja kuwa ni tanzu za fasihi andishi lakini anachambua
vipengele hivi kama vinavyojitegemea kila kimoja.
SABABU
YA MIKINZANO YA WANAZUONI JUU YA TANZU ZA FASIHI ANDISHI
1.      Hawakubaliani
katika istilahi/majina ya tanzu mf. Mulokozi kuna utanzu anauita Kisa lakini M’ngaruthi anauita Hadithi fupi.
2.      Hawakubaliani
katika idadi mf. Nkwera (1976)
anasema kuna tanzu tatu wakati Mulokozi (1996) na M’ngaruthi (2008) wanasema
zipo tanzu nne.
 
3.      Kuna
utata katika mpangilio. Yaani ni utanzu
upi uanze, mf. Mulokozi (1996) anaanza na Ushairi, riwaya, Kisa na tamthiliya
wakati M’ngaruthi (2008) anaanza na riwaya, tamthiliya, mashairi andishi na
hadithi fupi.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)