MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
CHANGAMOTO ZINAZOATHIRI MAENDELEO YA KISWAHILI

Thread Rating:
  • 0 Vote(s) - 0 Average
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
CHANGAMOTO ZINAZOATHIRI MAENDELEO YA KISWAHILI
#1
 Pamoja na mafanikio hayo ,zimekuwapo changamoto kadhaa zinazoathiri maendeleo ya Kiswahili. Baadhi ya changamoto hizo ni:
  • Upotoshwaji wa lugha ya Kiswahili.
       Upotwashwaji wa Kiswahili hutokea kwa namna kadhaa mfano ni wa uchanganyaji wa Kiswahili na kingereza na pia kutumia Kiswahili kwa maneno yasio yanifu na pia utumizi wa Kiswahili ulioathiriwa na sarufi ya lugha za kikabila hususan kimatamshi na kimuundo.
  • Athari za lugha za kigeni.
Tatizo la kutokithamini Kiswahili miongoni mwa wanajamii ni changamoto ya kuathiriwa na kasumba za ukoloni ambapo wanajamii huthamini Zaidi lugha za kigeni hususan kingereza.
  • Kutokuwepo uwiano wa kimatumizi.
Hii ni changamoto nyengine ambapo Kiswahili hakina uwiano wa kimatumizi katika nchi nzima, tofauti hizi zipo kutokana na jamii moja na nyingine kuathiriwa na lugha mama.
  • Utafauti wa sera .malengo na mipango ya vyombo vya ukuzaji Kiswahili.
  Juhudi za ukuzaji Kiswahili zinaonekana hazina mashiko kutokana na kuwepo idadi kubwa ya vyombo vya ukuzaji Kiswahili ambayo havina mshikamano wa pamoja kwani kila chombo kina malengo,sera, na mipango ya yake ya uendeshaji wa Kiswahili.
  • Uhaba wa wataalamu.
  Uhaba wa wataalamu katika vyombo vya ukuzaji wa Kiswahili husababisha vyombo kutofanya  na kutekeleza malengo kwa ufanisi.
  • Kutokwepo mpango wa kukitumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia.
   Ni tatizo jengine linalokwanishwa maendeleo ya Kiswahili kwa kutotekelezwa kwa mpango wa kukitumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia katika ngazi zote za elimu nchini, na hivyo kutoa mwanya hasa kwa lugha za kigeni kama vile kingereza kustawi zaidi na hivyo kuathiri nafasi ya Kiswahili katika jamii.
Mwl Maeda
Reply


Forum Jump:


Users browsing this thread: 1 Guest(s)