05-11-2022, 07:00 AM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'ASHERATI'
Neno *asherati* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: a-/wa-*] yenye maana ya *mtu mwenye tabia ya kujamiiana na mtu au watu wasiokuwa na uhusiano wa kindoa.*
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *asherati* linatokana na nomino ya Kiarabu *ashiirah (soma: ashiiratun/ashiiratan/ashiiratin عشيرة)* lenye maana zifuatazo:
1. Rafiki.
2. Jamaa wa karibu.
3. Mke, *haadhihii ashiiratii هذه عشيرتي* huyu ni mke wangu, *haadhaa ashiirii هذا عشيري* huyu ni mume wangu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *ashiirat* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *asherati* lilichukua maana mpya ya mtu mwenye tabia ya kujamiiana na mtu au watu wasiokuwa na uhusiano wa kindoa.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *asherati* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: a-/wa-*] yenye maana ya *mtu mwenye tabia ya kujamiiana na mtu au watu wasiokuwa na uhusiano wa kindoa.*
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *asherati* linatokana na nomino ya Kiarabu *ashiirah (soma: ashiiratun/ashiiratan/ashiiratin عشيرة)* lenye maana zifuatazo:
1. Rafiki.
2. Jamaa wa karibu.
3. Mke, *haadhihii ashiiratii هذه عشيرتي* huyu ni mke wangu, *haadhaa ashiirii هذا عشيري* huyu ni mume wangu.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *ashiirat* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa neno *asherati* lilichukua maana mpya ya mtu mwenye tabia ya kujamiiana na mtu au watu wasiokuwa na uhusiano wa kindoa.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda