01-29-2022, 04:26 PM
HII NDIYO ETIMOLOJIA YA NENO 'RUBAA'
Neno *rubaa* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana zifuatazo:
1. Jumuiya ya watu wanaoishi na wanaofanya kazi pamoja kwa sababu wana uhusiano fulani unaowaunganisha; Watu wengi wanaofanya kazi pamoja kwa kuunganishwa na uhusiano fulani.
2. Kitendo cha kuweka mguu mmoja juu ya mwengine hali ukiwa umekaa.
*Mfano* : Mgeni alipopewa kiti alikaa rubaa.
3. Uwanja au uga wa shughuli fulani.
*Mfano* : Jangala siku hizi ni maarufu katika rubaa za michezo.
4. Kikundi cha askari wanaopangiwa na kutekeleza majukumu yao chini ya kiongozi mmoja.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *rubaa*( *soma: rubaau/rubaa-a رباع )* ni nomino ya Kiarabu yenye maana ya kukariri namba 4: nne nne/wanne wanne. Kwa mfano: *Hum Jaauu Rubaa-a هم جاءوا رباعا* Wamekuja wanne wanne.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *rubaa-a رباعا* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa nomino ya Kiswahili ' *rubaa* ' lilibeba maana mpya.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Neno *rubaa* katika lugha ya Kiswahili ni *nomino: [Ngeli: i-/zi-]* yenye maana zifuatazo:
1. Jumuiya ya watu wanaoishi na wanaofanya kazi pamoja kwa sababu wana uhusiano fulani unaowaunganisha; Watu wengi wanaofanya kazi pamoja kwa kuunganishwa na uhusiano fulani.
2. Kitendo cha kuweka mguu mmoja juu ya mwengine hali ukiwa umekaa.
*Mfano* : Mgeni alipopewa kiti alikaa rubaa.
3. Uwanja au uga wa shughuli fulani.
*Mfano* : Jangala siku hizi ni maarufu katika rubaa za michezo.
4. Kikundi cha askari wanaopangiwa na kutekeleza majukumu yao chini ya kiongozi mmoja.
Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *rubaa*( *soma: rubaau/rubaa-a رباع )* ni nomino ya Kiarabu yenye maana ya kukariri namba 4: nne nne/wanne wanne. Kwa mfano: *Hum Jaauu Rubaa-a هم جاءوا رباعا* Wamekuja wanne wanne.
Kinachodhihiri ni kuwa neno la Kiarabu *rubaa-a رباعا* lilipoingia katika Kiswahili na kutoholewa kuwa nomino ya Kiswahili ' *rubaa* ' lilibeba maana mpya.
*Shukran sana.*
*Khamis S.M. Mataka.*
Mwl Maeda