MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
ETIMOLOJIA YA MANENO ' FADHAA' na 'FAZAA' - Printable Version
JIFUNZE KISWAHILI
ETIMOLOJIA YA MANENO ' FADHAA' na 'FAZAA' - Printable Version

+- JIFUNZE KISWAHILI (https://jifunzekiswahili.co.tz)
+-- Forum: My Category (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=1)
+--- Forum: Majadiliano ya Wadau wa Kiswahili (https://jifunzekiswahili.co.tz/forumdisplay.php?fid=16)
+--- Thread: ETIMOLOJIA YA MANENO ' FADHAA' na 'FAZAA' (/showthread.php?tid=1794)



ETIMOLOJIA YA MANENO ' FADHAA' na 'FAZAA' - MwlMaeda - 12-23-2021

HII NDIYO ETIMOLOJIA YA MANENO ' FADHAA' na 'FAZAA'

Neno *fadhaa* katika lugha ya Kiswahili (kwa mujibu wa Kamusi Kuu ya Kiswahili Sanifu na Kamusi ya Kiswahili ya Karne ya 21) lina maana zifuatazo:

1. *Nomino* : Kosa utulivu wa moyo kutokana na jambo fulani ambalo ama umefanyiwa wewe au umemfanyia mtu mwengine ambalo aghalabu huwa si jema.

2. *Nomino:* Hali ya wasiwasi.

Katika lugha ya Kiarabu, neno hili *fadhaa* (soma: *fadhaun/fadha-an/fadhain فذع* ) ni nomino yenye maana ya ' *jeuri* '.

Ama neno *fazaa* ambalo ni mashuhuri uswahilini na ambalo linachukuliwa kuwa kisawe cha neno *fadhaa* , katika lugha ya Kiarabu ni nomino inayotokana na kitenzi *faza.a/fazi.a* *فزع* ambacho kina maana zifuatazo:

1. *Faza.a فزع* amefazaika/amefadhaika.

2. *Faza.a ilayhi فزع إليه* ameomba hifadhi/amemba msaada.

3. *Faza.aahu  فزعه*  amemnusuru/amemsaidia.

4. *Faza.a min nawmihi فزع من نومه* ameamka kutoka usingizini.

Hiyo nomino *fazaa فزع* katika lugha ya Kiarabu ina maana zifuatazo:

1. Khofu/hofu na wasiwasi.

2. Kuomba hifadhi/ukimbizi.

3. Kuomba msaada.

Kinachodhihiri ni kuwa wataalamu wetu wamelichukua kutoka Kiarabu neno *fadhaa فذع* lenye maana ya ' *ujeuri* ' wakalipa maana ya neno la Kiarabu *fazaa فزع* lenye maana ya khofu/hofu na wasiwasi.

*Shukran sana.*

*Khamis S.M. Mataka.*