MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
<![CDATA[JIFUNZE KISWAHILI - Kiswahili kwa wageni]]> https://jifunzekiswahili.co.tz/ 2024-04-27T11:04:21Z MyBB MwlMaeda]]> 2021-09-06T13:59:11Z 2021-09-06T13:59:11Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1172 <![CDATA[MBINU ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI]]> MBINU ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI
  1. Malengo ya ufundishaji lugha kwa wageni
Lengo kubwa ni kwamba ili mwanafunzi aweze kujua lugha hiyo kwa stadi zote za lugha ile. Stadi za lugha ni 1. Kusikiliza 2.kuzungumza 3. Kusoma 4.kuandika 5. Sarufi 6. Utamaduni wa lugha ile
Malengo ya jumla ya kufundisha ili ni pamoja na:-
1)      Kumwezesha mwanafunzi ili aweze kumudu lugha.
2)      Kumwezesha mwanafunzi aweze kuwasiliana na wazawa wa lugha husika
LUGHA YA KWANZA
Stern (1983) anasema kwamba “lugha ya kwanza lugha ambayo mtoto hupata kutoka kwa mama yake mzazi angali mchanga.
LUGHA YA PILI
Stern (1983) anasema kwamba “ lugha ya pili si lugha ambayo mtoto/mtu aliipata alipoanza kukua na kupata lugha. Hii ni lugha ya kujifunza,kwa maana ya kwamba mtu huyu huwa tayari ana lugha nyingine.mfano. hapa Tanzania Kiswahili ni lugha ya pili kwa watu wengi
LUGHA YA KIGENI
Ni ile lugha ambayo unajifunza na kuitumia lakini wazungumzaji wake wako nje ya nchi au mbali na jamii anapokaa mwanafunzi huyo. Mfn lugha ya kiingereza ni lugha ya kigeni hapa Tanzania
MALENGO YA JUMLA YA UJIFUNZAJI NA UFUNDISHAJI WA LUGHA YA KIGENI
Mara nyingi hii hutegemea taaasisi yenyewe lakini kuna malengo ambayo ni ya jumla:
1)      Kutaka kuwasiliana na wenyeji wa sehemu /nchi husika
2)      Kujiandaa kusafiri kwenda nchi nyingine kwa shughuli mbalimbali
3)      Kwa ajili ya kufanya biashara
4)      Kukidhi vigezo vya masomo
5)      Kufanya utafiti katika taaluma husika
6)      Ili kupata ajira nchi za ng’ambo
KITU GANI KIANZE KUFUNDISHWA SASA?
Onyo: usijaribu kumfundisha mwanafunzi sarufi za lugha hiyo kwanza, utamfundisha ikibidi lakini isiwe kipaumbele chako
W      Anza na salamu za kawaida, salamu katika utamaduni wa mwafrika ni kitu cha muhimu sana, hivyo fundisha salamu,maana lengo ni kwamba huyo mtu aweze kuwasiliana.
MALENGO YA UJUMLA YA UFUNDISHAJI LUGHA YA KISWAHILI KWA WAGENI
a)      Ili mwanafunzi wa Kiswahili ajue mambo yafuatayo:
i.            Aweze kumudu lugha ya Kiswahili
ii.            Aweze kuwasiliana na watumiaji wa lugha ya Kiswahili
iii.            Ili wanafunzi waweze kung’amua mambo yafuatayo:- Namna ya kusema jambo gani? Mfano anataka kwenda chooni Asemee wapi? Kwa nini aseme? Kwa nani aseme? Mazingira gani aseme?
iv.            Ili kuwapa wanafunzi mbinu mbalimbali za kujifunza lugha ya Kiswahili. Wanafunzi wafanye kwa vitendo ili waweze kujichukulia misamiati ya kutosha
v.            Wanafunzi wang’amue umuhimu wa lugha wanayojifunza
b)     ili wanafunzi waweze kutimiza malengo haya, mwalimu ni lazima wape wanafunzi:
kuchunguza®kugundua®kutalii kuhusu lugha ya Kiswahili
c)      wape uwezo wa kukuza lugha ya Kiswahili kila siku aweze kuongeza msamiati kwa kusoma vitabu mbalimbali vya hadithi
d)     wape nafasi kutumia mbinu mbalimbali lugha ili kukuza uelewa wao
e)      wape uwezo wa kukuza fikra zao na kudadisi
f)       wasaidie kufanya utumbuizi wa vipengele vya mfumo na utamaduni wa lugha ya Kiswahili
NADHARIA KUU ZA UJIFUNZAJI LUGHA
Kuna mambo mawili ambayo waalimu tarajili wanapaswa kujua
1)      mbinu za kujifunza lugha ya pili ni nyingi kama ilivyo waalimu wengi
2)      manzingira halishi wakati wa ujifunzaji. Rogers (2001) anasema kwamba “ wakati wa ufundishaji wa lugha ya kigeni hutumia mbinu mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wafikie malengo yao”
kuna nadharia kuu nne (4)za ujifunzaji lugha:
1)      NADHARIA YA UHULKA
ü  Mwasisi wake ni Noamy Chomsky (1957)
ü  Wazo kuu lake ni kwamba: binadamu huzaliwa akiwa na uwezo lugha. Yaani kwenye ubongo wake ana mfumo ambao huzaliwa nao kwa ajili ya kujifunza lugha. Ana kifaa kinachoitwa LAD (Kifaa cha upataji lugha)
ü  Naye Brown (2000) aliunga mkono mawazo haya. Mwingine aliyeunga mkono ni Ellis (1997) walikuwa na hoja kwamba kuna kipindi mtu akifikia umri Fulani hawezi kupata lugha sawasawa na wazawa wa lugha husika. Umri huo ni kuanzia 0-miezi 18. Kwa mujibu wa wataalamu hawa mazingira hayana msaada wowote katika ujifunzaji lugha.
2)      NADHARIA YA UTABIA
ü  Kwa mara ya kwanza ilidokezwa na E.Thonilke(1935). Kwa mujibu wa wanatabia ujifunzaji wa lugha ni mwigo
ü  Aliyetafiti zaidi katika nadharia ya ujifunzaji ni B.F SKINNER , Huyu alikubali ni mwigo lakini akaongeza kuwa ni uimarikaji wa tabia, hivyo mtoto mdogo hazaliwi na lugha bali huichota kutoka kwa wazazi wake
  • Nadharia hii inayapa mazingira nafasi kubwa katika ujifunzaji lugha
  • Je mtu akitengwa na jamii anaweza kuwa na lugha? Jibu unalo wewe mwenyewe!
3)      NADHARIA YA UTAMBUZI
ü  Nadharia hii iliasisiwa na Jean Hajet (1954)
ü  Alidai kuwa binadamu anapozaliwa kuna kipindi maalum cha kupata lugha
ü  Alidai kuwa kujifunza lugha ni sehemu ya makuzi ya binadamu, kwa kadiri unavyokua ndivyo unavyozidi kupata lugha
ü  Alidai kuwa mtoto hupata lugha kabla ya kuzaliwa.
ü  Arth(2003) anadai kuwa mtoto hupata lugha kabla ya kuzaliwa,kuanzia 0-miezi 18
ü  Nadharia hii haipingani na umuhimu wa mazingira katika ujifunzaji lugha
4)      NADHARIA YA UUMBAJI/ MAUMBILE
ü  Iliasisiwa na Jerome Brunner
ü  Wazo kuu la nadharia hii inasisitiza nafasi ya mama katika upataji lugha ya kwanza
ü  Mtoto hutengeneza lugha kutegemeana na mawasiliano ambayo mama yake anayatumia
ü  Alidai, ili mtoto aweze kupata lugha ni lazima mambo yafuatayo yatimizwe
  • Muktadha
  • Tajiriba (experience)
  • Upangilifu (organization)
  • Kujenga mazingira ya upekuzi (udadisi_
ü  Hukaza zaidi kuhusu mazingira katika ujifunzaji lugha
NJIA ZA UJIFUNZAJI LUGHA YA KISWAHILI
Njia za ufundishaji Kiswahili ni nyingi kama na waalimu nao walivyo wengi, lakini njia hizi itatengemea hali ya wanafunzi, hata hivyo njia zifutazo zinapendekezwa zitumike.
  1. Njia ya majadiliano-njia hii haifai kwa mwanafunzi ambaye ndio kwa mara ya kwanza anasikia Kiswahili. Lakini ni njia nzuri kwa mwanafunzi ambaye amewahi kusikia habari za Kiswahili
  2. Njia ya mahojiano. Mfano mwalimu aandae maswali, awaambie wanafunzi wajipe vyeo mfano mmoja anakuwa daktari mwingine anakuwa mgonjwa n.k
  3. Mchezo wa maswali. Kwa mfano. Kama wewe ungekuwa rais wa marekani ungefanyaje kuhakikisha unakomesha ugaidi duniani? Watajibu na kujipatia msamiati kibao
  4. Njia ya uigizaji-mwli awape wanafunzi mwongozo wa maigizo
  5. Njia ya maswali ya papo kwa papo (ana kwa ana) mfano: mimi ni Seni, wewe ni nani?
  6. Njia ya uwandani. Mfno ukitaka kuwafundisha misamiati ya sokoi wapeleke sokoni.
  7. Njia ya kutumia mazingira mbalimbali. Mfano kama mwalimu anataka kuwafundisha michezo wapeleke uwanja wa mpira
  8. Njia ya usomaji. Mfano kusoma pande nne za dunia,kuwapa matini mbalimbali wanafunzi
  9. Njia ya majadiliano funge. Yaani wanafunzi wanajadili vitu ambavyo vimewekewa mipaka
Angalizo:uteuzi wa njia ipi itumike itategemea aina ya wanafunzi na kazi zao!
HULKA/TABIA YA UANAFUNZI KUJIFUNZA LUGHA
Wanafunzi hutofautiana kulingana na hulka zao, mwalimu anahitaji kuangalia mielekeo ya wanafunzi wake. Baadhi ya tabia zao ni kama vile: ucheshi, hasira, aibu, hasira za kutojua, hapendi kusahihishwa, mkimya nk
ATHARI ZA KIJAMII KUHUSU LUGHA/WANALUGHA
Kila jamii ina mtazamo wake kuhusu ujifunzaji lugha, mtazamo hasi ndio ambao huathiri ujifunzaji lugha na kupelekea kutopata motisha wa kujifunza lugha. Baadhi ya mambo yanayoathiri ni kama vile
i.            Nia au lengo la kujifunza lugha hiyo
ii.            Jinsia
iii.            Umri
iv.            Mazingira
v.            Umilisi wa lugha kama akiwa na umilisi mdogo
Malengo ya mwalimu ni kuhakikisha anafanya mambo yafuatayo:
i.            Kuwatia motisha wa kujifunza lugha
ii.            Kumsaidia kuondokana na hasira
iii.            Kuondoa dhana potofu ya ujifunzaji lugha. Mf. Kuna wanaoamini kwamba Kiswahili ni lugha ya kiislamu
iv.            Kuondoa utata katika vipengele vya kisarufi
v.            Kuwaelezea aina mbalimbail za lugha na mahali zinapotumika
Kuhusu matumizi ya lugha ya ishara ni muhimu sana kujua ishara zinazotumika katika jamii. Hivyo mwalimu anapaswa awaeleze mambo yafuatayo
i.            Baadhi ya utamaduni huangalia usoni, tabasamu na kujiamini
ii.            Matumizi ya mkono wa kushoto au wa kulia
iii.            Kuonyesha vidole-jamii zingine haziruhusu kabisa
iv.            Namna ya kusimama na kuelezea jambo
Ili kutimiza hayo yote mwaimu lazima awe na sifa zifuatazo:
i.            Awe muwasilishaji mzuri
ii.            Awe na mpangilio mzuri
iii.            Awe mstahimilivu
iv.            Awe na ujuzi wa kufundisha
v.            Awe na uhusiano mzuri na wanafunzi
vi.            Awe na maarifa ya somo
SIFA ZA MJIFUNZAJI LUGHA
a)      Awe na utayari wa kujifunza lugha ya Kiswahili bila kulazimishwa
b)     Afanye mazoezi ya kuitumia lugha hiyo
c)      Atumie akili kupambanua dhana mbalimbali ili kugundua mambo ambayo jamii Fulani inayafanya
d)     Awe na uhuru wa kuzungumza lugha hiyo
e)      Awe na ratiba ya kujifuza
f)       Aweze kulinganua na kulinganisha lugha anayojifunza
g)      Awe na ukarimu ili aweze kuwa na uhusiano na jamii husika
h)     Awe mtendaji
i)        Azingatie ubora ili aweze kujifunza zaidi
MOTISHA
Ni tabia au msukumo katika kutimiza malengo Fulani. TUKI (2004) wanadai kuwa motisha ni kitu kama fedha inayotolewa ili kumtia mtu hamasa kujifunza jambo.
Hata hivyo, si lazima umpe kitu bali unamtia moyo mwanafunzi na kumsaidia. Mwalimu anapaswa kutumia motisha chanya sio hasi. Mfn hutakiwi kuchapa fimbo
Brown (1994) anasema kuwa motisha:
a)      Ni kiwango cha uchaguzi ambacho unafanya kuhusu lengo unalotaka kufikia
b)      Jitihada atumiazo mtu kufikia malengo hayo
SKINNER &WATTSON-hawa wanaangalia zawadi na uhimizaji kwa wanafunzi pamoja na adhabu ili kufifisha na kujenga hali Fulani
AINA ZA MOTISHA
  1. Mwamko wa mjifunzaji mwanyewe
  2. Mazingira mazuri ya kufundishia Kiswahili mfano, darasa, nje n.k
  3. Jamii inayomzunguka ni motisha pia
  4. Mwalimu anaweza kuwa motisha kwa mwanafunzi
  5. Zana/vifaa vya kujifunzia pia ni motisha
  6. Motisha wa ndani-
MOTISHA IPO KATIKA MAKUNDI MIWILI
ü  Haitegemei vitu vya nje ya yenyewe
ü  Hiki ni kile kinachoonekana kwa mjifunzaji lugha mwenyewe
ü  Hii haibadiliki kulingana na muktadha wowote ule
  1. Motisha wa nje
ü  Ni aina ya motisha ambayo mwanafunzi hutegema kupewa, kupata, kusikia au kuona
ü  Hivi vitamsaidia katika kujifunza lugha
Mwalimu wasaidie wanafunzi kutumia lugha kulingana na muktadha. Hapa kuna mambo ya kuzingatia:-
a)      Akili ya mwanafunzi: lazima utambue tofauti zao katika akili zao ili kujifunza lugha
b)     Kipaji chao-kuna wengine wana vipaji vya kujifunza lugha
c)      Umri-watu wazima huchelewa kujifunza lugha
d)     Jinsia-inasemekana wanawake wanaweza kupata lugha haraka kuliko wanaume
UFUNDISHAJI LUGHA KIMAWASILIANO
ü  Ni muhimu kuhakikisha kwamba katika kujifunza lugha ufundishaji uwe wa mawasiliano
ü  Ni mbinu ya kufundisha lugha ngeni na lugha ya pili
ü  Husisitiza mwingiliano maathiriano kama mbinu ya kujifunza lugha
KAZI ZA LUGHA
ü  Van (1975) anasema kuwa kazi ya lugha ni:
a)      Kutoa habari
  • Kusimulia
  • Kuuliza
  • Kutoa taarifa
b)      Kutafuta taarifa za kitaaluma
c)      Kuelezea mihemuko na misisimko. Mfno mapenzi, misisimko
d)     Kuelezea masuala ya uadilifu.mfn kuomba msamaha, ibada etc
e)      Kwenye mambo ya ushirikiano. Mfn kuamkia watu, kujitambulisha nk
Angalizo: hata kama mwanafunzi ana malengo mengine ya kujifunza lugha hiyo ni lazima umfundishe umuhimu wa lugha hiyo kulingana na muktadha
MASHARTI YA KUZINGATIA
a)      Azingatie majukumu ya kijamii mfn ataanzaje kuzungumza na mtu asiyemjua? Watu wengine ni wenye mamlaka Fulani, hivyo kuna namna ya kuzungumza nao
b)      Majukumu ya kisaikolojia-mfano asipendelee upande wowote mfn CHADEMA CUF na CCM
c)      Mazingira ya lugha ilipo. Je ni lugha ya taifa? Watu wanaokuzunguka wanatumiaje?
Angalizo: lugha sio sarufi tu au fonolojia bali ni chombo cha mawasiliano, hivyo inahitaji kufundishwa kimawasiliano zaidi
MUKTADHA WA UFUNDISHAJI LUGHA
ü  Haya ni mazingira halisi ambapo tukio la ufundishaji lugha hufanyika kwa kuzingatia wadau wakuu watatu
a)      Mwanafunzi
b)      Mwalimu
c)      Jamii
ü  Pamoja na motisha ufundishaji uzingatie sana mambo yafuatayo:
  • Utoaji wa kazi na mazoezi mengi
  • Tumia lugha katika mazingira halisi na yanayostahili ukilenga kwenye stadi nne za lugha
  • Matumizi ya lugha kwa kuzingatia muktadha
  • Utumizi wa mazingira halisi ya darasa.mfn picha, katuni. Nk
  • Himiza ushirikiano miongoni mwa wanafunzi baina yao na baina yako mwalimu
  • Tumia mbinu zaidi ya moja. Mfn vikundi, majibizano nk (rejea mbinu)
  • Fafanua kwa uangalifu masuala ya kisarufi
  • Ajue maono ya mwanafunzi. Mfn huzuni, ucheshi nk
  • Kuunda mazingira ya utani darasani
UFUNDISHAJI WA DARASA MSETO
ü  TUKI (2013) Mseto ni hali ya kuwa na mchanganyiko wa makabila mbalimbali kutengeneza kitu fulani
ü  Hapa ni mchanganyiko wa darasa lenye wanafunzi wanaotoka sehemu mbalimbali na wenye umri tofauti, malengo tofauti nk
ü  Hivyo mwalimu inakubidi utofautishe sana katika ufundishaji wako na uwe makini ili usije ukawakwaza wanafunzi wengine
NAMNA YA UFUNDISHAJI DARASA MSETO
a)      Lazima mwalimu uwe na maarifa ya wanajamii mfn utamaduni wao. Kama ni wazungu, wachina nk jua utamaduni wao
b)     Uwe na usisitizaji wa lugha lengwa. Kama ni Kiswahili basi pendelea kutumia Kiswahili ili usiwakwaze sana. Hata hivyo lazima wawe na lugha ambayo wewe unaijua
c)      Tumia vitendo halisi, ishara nk
d)     Arika wageni mbalimbali waje waeleze kuhusu lugha na mazingira
e)      Puuza(ignore) malengo ya wanafunzi
f)       Ufundishaji wa masuala ya utamaduni lazima ufungamane na muktadha husika
SIFA ZA MPATAJI LUGHA
Mpataji lugha ni lazima awe na sifa kuu mbili tu:
  1. Umilisi wa kiisimu
ü  Ni uwezo alio nao mjifunzaji lugha ambao unamwezesha kutofautisha viambo, miundo tofauti ya lugha na msamiati wa lugha
ü  pia kuweza kutamka lugha ile.
  1. Umilisi wa kiisimujamii
ü  Ni umilisi ambao mtumiaji wa lugha hupata lugha inayomwezesha kujifunza lugha na kuzingatia muktadha
NADHARIA /MBINU /MIKABALA ZA KUJIFUNZA LUGHA YA KIGENI
ü  Nadharia ni mkondo wa mawazo unaotumika kuelezea jambo
ü  Mtesigwa(2009) anasema “ nadharia ni kiunzi cha mitazamo, mawazo au vitendo vinavyohusisha uchunguzi, mpangilio na uchanganuzi wa matukio katika kukabili suala fulani kisayansi
®kuna mambo mawili ambayo lazima tujikumbushe:
a)      Njia za ufundishaji lugha ya kigeni ni nyingi kama waalimu walivyo wengi
b)      Kumbuka hali ya darasa. Tumia njia mbinu zaidi ya moja darasani, usitumie njia moja tu.
ü  Rogers&Richards (2001)wanasema kuwa tunapojiandaa kwenda kufundisha tunahitaji kujiuliza maswali yafuatayo:-
a)      Malengo ya ufundishaji lugha lengwa(LL) ni yapi? Mfano labda lengo lao linaweza kuwa wanataka kuzungumza tu.
b)      Upi ni msingi asili wa lugha lengwa na unaathiri vipi njia za kufundisha. Mfn kaida za lugha ya Kiswahili ni zipi?
c)      Ni misingi ipi inatumika kuchagua mambo katika ufundishaji lugha?
d)     Ni misingi ipi ya upangiliaji wa mada. Mfano kwa kuzingatia suala la utamaduni, mfano salamu nk
e)      Je lugha mama ya mwanafunzi ina jukumu gani katika kujifunza lugha? Mfano miundo ya lugha mama inafanana na lugha lengwa?
f)       Je wanafunzi binafsi watumie mbinu zipi katika kujifunza lugha hiyo?
g)      Je ni mbinu na vitendo vipi hufanikisha vizuri ujifunzaji lugha ya pili (kigeni)?
NADHARIA ZA KUJIFUNZA
  1. Mbinu ya tafsiri sauti
  2. Mbinu ya moja kwa moja(direct method
  3. Mbinu ya usomaji(reading approach method)
  4. Kusikia na kusimulia (audiolingual method)
  5. Kushirikisha jamii (community langaage learning method)
  6. Mbinu ya ukimya (silence method)
  7. Mbinu ya mawasiliano (communicative language approach)
  8. Mbinu ya mwitiko jumuishi(total physical response)
  9. Mbinu ya utambuzi (communitive code method)
  10. Mbinu ya upendekezi (suggestopidia method)
  1. Mbinu ya tafsiri sarufi
ü  wakati mwingine hujulikana kama mbinu ya kimapokeo. Huu ni mkabala ambao ufundishaji wa lugha ya kigeni umejiegemeza katika sarufi ya lugha ya Kiratini. Iliasisiwa/anzishwa na Meidinger (1783) na Ploetz (1849) wakati ule iliaminika kwamba lugha ya kiratini ndiyo lugha pekee.
ü  Nafasi ya lugha mama ilipuuzwa kwa kiasi kikubwa na ilijikita katika sarufi ya Kiratini, na hivyo mwalimu alipaswa kujikita katika kufundisha sarufi ya Kiratini na vipengele vingine vilipuuzwa
ü  Huu ulikuwa ni mkabala elekezi-yaani unawaelekeza watu namna ya kutumia lugha na sivyo wanajamii wanavyotumia lugha hiyo
  1. Mbinu ya moja kwa moja(direct method)
ü  Iliasisiwa na Gouin(1880)
ü  Nadharia hii inazingatia uzungumzaji wa lugha husika
ü  Mbinu zilizopaswa kufundishia ni zile zilizohamasisha wanafunzi kuzungumza. Mfn mbinu ya majadiliano,uigizaji,maswali katika vikundi
ü  Masomo yalianza kwa hadithi fupi halafu wanafunzi wanauliza maswali kuhusu hadithi waliyosimuliwa na mwalimu aliwaambia watoe maoni yao kuhusu hadithi hiyo.
ü  Matumizi ya vielelezo vilitumika zaidi. Mfano picha, ramani, katuni n.k
ü  Kipengele vya sarufi kilifungushwa kwa kufuata muktadha halisi ambamo lugha inatumika
ü  Kipengele cha utamaduni kilifundishwa kwa uchache sana
  1. Mbinu ya usomaji (reading approach method)
ü  Mbinu hii inatumika kufundishia kwa wanafunzi wanaojifunza lugha ya kigeni ambao hawatarajiwi kutoka nje ya nchi ambapo lugha hiyo inatumika
ü  Malengo yake huwa kuendeleza uwezo wao wa kusoma ile lugha
ü  Vipengele vinavyofundishwa ni vile vinavyohusu usomaji, hivyo vipengele vingine havihusiki. Mkazo wake ni kwamba anayejifunza lugha aweze kusoma vitu vingi kwa wakati mmoja.
ü  Mbinu hii haimpi mjifunzaji lugha uwezo wa kuzungumza lugha husika bali ni kuisoma tu.
  1. Kusikia na kusimulia (audiolingual method)
ü  Nadharia hii ilitokana na haja ya ukarimani nchini marekani miaka 1940.
ü  Iliasisiwa na Bloomfield (1942) na Fries (1945)
ü  Msingi mkubwa wa nadharia hii ni kile kinachosemwa
ü  Maandishi hayakupewa fursa kubwa bali kile kilichosemwa ndicho kilikuwa cha muhimu sana. Bloomfield alisema kuwa lugha si katika maandishi bali ni kile ambacho kinasemwa.
ü  Inahusisha kusimulia mada mbalimbali na kupima uwezo wa kusikia
ü  Walipenda sana kutumia miziki, nyimbo, usimulizi na ughanaji
ü  Walisisitiza stadi ya kusikiliza, kuzungumza, kusoma na kuandika
ü  Waliongeza kitu kingine chakuona
  1. Kushirikisha jamii (community langaage learning method)
ü  Iliasisiwa na curran (1976)
ü  Dai la nadharia hii ni lugha ni watu, kwa maana ya kwamba huwezi kutenga jamii na lugha
ü  Walidai kwamba ili uweze kumfundisha mwanafunzi mgeni basi nenda kwenye jamii husika
ü  Walidai pia kwamba kama utaamua kufundishia darasani bali darasa lako lifanye angalau lifanane fanane na jamii ya lugha husika
ü  Ili uweze kufundisha watu ni lazima ushirikishe watu wanaotumia lugha hiyo.
ü  Mwanafunzi atapata vichocheo vya aina nyingi katika jamii na kubaini ni mambo gani yanafaa na mambo gani hayafai
ü  Nadharia hii inaipa kipaumbele jamii kama chombo muhimu katika kujifunza lugha
  1. Mbinu ya ukimya (silence method)
ü  Nadharia hii inaamini kwamba kila lugha ina mfumo wake tofauti na lugha nyingine, hivyo ufundishaji wa lugha ya pili ulenge kumfanya mjifunzaji wa lugha kuwa mmilisi au kukaribia kuwa mmilisi wa lugha anayojifunza
ü  Nadharia hii inadai kwamba ujifunzaji wa aina yoyote ile unahusisha vitu viwili.
Kichocheo®     Mwitikio®       mgeuko
(Mwalimu)     (mwanafunzi)-(anabadilika)
ü  Ili kuweza kutimiza hili, mwalimu anahitaji kujenga mazingira ya utani katika darasa jambo ambalo litaleta matokeo mazuri ya umilisi wa lugha husika
ü  Nadharia hii inamhitaji mwalimu kufanya tathimini kwa wanafunzi wake ili kubaini kama kuna badiliko
  1. MBINU YA UTAMBUZI (COMMUNITIVE CODE METHOD)
ü  Nadharia hii inatokana na ukosoaji/udhaifu wa nadharia ya mbinu ya sarufi na ile ya moja kwa moja
ü  Ilianzishwa mwaka 1970
ü  Wanadai kwamba mwanafunzi apewe vipengele vyote vya lugha kwa ujumla mwanafunzi kumpa maarifa mapana kuhusu lugha, kumpakanuni za msingi kuhusu lugha, halafu yeye mwenyewe kulingana na utambuzi wake aweze kuielewa lugha.
ü  Uwafundishe kanunu za msingi. Kwa mfano katika lugha ya Kiswahili ni lazima ujue ngeli za majina-hii itakusaidia kutumia nomino katika mazingira tofauti tofauti, vitenzi-waeleze namna ambavyo vinaweza kukaa peke yake kama sentensi
  1. Mbinu ya mwitiko jumuishi(total physical response)
ü  Nadharia hii pia hujulikana kama mkabala asilia.
ü  Iliasisiwa na James na Asher
ü  Inatilia mkazo mfumo na muundo wa lugha.
ü  Kama ilivyo nadharia ya usikizi nadharia hii pia inasisitiza umuhimu wa kumudu mazungumzo kama sehemu ya umilisi wa lugha
ü  Ufundishaji uhusishe mazoezi ya kurudia rudia ambayo angalau unamfanya mwanafunzi kumudu anachojifunza
ü  Nadharia hii inasisitiza matumizi ya vitendo na ishara mbalimbali kama nyenzo mojawapo katika kujifunza lugha.
  1. Mbinu ya upendekezi (suggestopidia method)
ü  Ilianzishwa na Lonzano georgi (1979)
ü  Nadharia hii inayapa mazingira bora ya ujifunzaji lugha kama nyenzo muhimu mojawapo katika kujifunza lugha. Hii inamaanisha kwamba mazingira yanayotumika kujifunzia lugha ni lazima yamkumbushe mwanafunzi kile alichojifunza jana yake
ü  Wanaelezea namna ya mkao wakati wa kufundisha wanafunzi wageni. Mkao katika darasa uwe ni wa kutazamana, maana yake vikae kwa duara.
ü  Wanasisitiza matumizi ya mziki laini na mziki nyororo
  1.                 MBINU YA MAWASILIANO (COMMUNICATIVE LANGUAGE APPROACH)
ü  Inasisitiza maingiliano na maathiriano katika ya mwalimu, mwanafunzi na jamii
ü  Wanakaza kwamba kujifunza lugha ni kujifunza kuwasiliana.
ü  Kujua lugha kwa hakika sio kujua kanuni za lugha ile bali ni kujua namna ya kuwasiliana na watu wa jamii ile kwa kuzingatia mikitadha mbalimbali ambamo lugha hiyo inatumika
ü  Ni nadharia ambayo imeshaididiwa na wataalam wengi akiwamo Noamy Chomsky
ü  Hii ndiyo nadharia ambayo inafaa kutumia kwa ajili ya kujifunza lugha
VIWANGO VYA WANAFUNZI
  • Hapa inamaanisha uwezo alio nao mtu wa kutumia lugha Fulani.
  • Viwango hivi viliwekwa na shirika/taasisi moja isiyokuwa ya kibiashara wala kiserikali liitwalo Interagence Language Round Table (ILRT)
  • Kulingana na shirika hili wajifunzaji lugha wako katika viwango vitatu
a)      Wanafunzi wa daraja la msingi (Kisw.DAMSA) Beginners Level
b)      Wanafunzi wa daraja la kati (DAKATI)Intermediate Level
c)       Wanafunzi wa daraja la juu (DAJUU) Advanced Level
a)                  Wanafunzi wa daraja la msingi (Kisw.DAMSA) Beginners Level
Daraja limegawanyika katika viwango hivi
  • Kiwango cha 0-®mwanafunzi hawezi kabisa kuzungumza lugha
  • Kiwango cha +0-®mwanafunzi amekaririshwa tu mahitaji muhimu akibadilishiwa tu basi Amepotea
  • Kiwango cha 1-®mwanafunzi anaweza kusitahimili mazungumzo ya ana kwa ana ila hawezi kuanzisha mazungumzo
  • Kiwango cha +1-®huyu anaweza kuanzisha mazungumzo yeye mwenyewe, hata hivyo ni kwa ajili ya kukidhi matarajio yake
INTERMIDIATE
  • Daraja la 2-lugha si kamilifu lakini anaeleweka kwa urahisi
  • Kiwango cha 3-anaweza kuzungumza lugha kwa muundo sahihi, ana msamiati wa mazingira fulani fulani tu ili kukidhi mahitaji ya kitaaluma
  • Anaweza kukithi mahitaji ya kitaaluma
b)            Wanafunzi wa daraja la kati (DAKATI)Intermediate Level
c)            Wanafunzi wa daraja la juu (DAJUU) Advanced Level
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-29T17:41:16Z 2021-06-29T17:41:16Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=361 <![CDATA[MAJINA YA SAYARI KWA KISWAHILI]]> 1. Zebaki
2. Zuhura
3. Dunia
4. Mirihi
5. Mshtarii
6. Zohali
7. Sarteni
8. Kausi
9. Utaridi

Chanzo (Kamusi ya Karne ya 21, 2011:614)]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T08:13:56Z 2021-06-28T08:13:56Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=333 <![CDATA[MAJINA YA RANGI KWA KISWAHILI NA KIINGEREZA]]> BOFYA HAPA CHINI KUFUNGUA &t&t&t&t&t&t&t&t&t&t&t


.pdf   MAJINA-YA-RANGI-KWA-KISWAHILI-NA-KIINGEREZA.pdf (Size: 128.4 KB / Downloads: 9) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-27T08:46:56Z 2021-06-27T08:46:56Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=311 <![CDATA[MBINU/NJIA ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI/LUGHA YA PILI]]>
Suala la ufundishaji lilianza miaka mingi tangu muingiliano wa jamii lugha tofauti karne nyingi zilizopita. Jamii moja na nyingine walianza kukubaliana na kukubalinana na lugha ngeni ili wawasiliane nao, na kuibuia haja ya kufundisha lugha ya kigeni. Ufundishaji lugha ya kigeni kitaaluma ilianza karne ya 19 na karne ya 20 ilikomaa sana. Lakini katika kipindi hk chote ufundishaji lgh za kigeni umekuwa ukibadilika kutokana na mabdiliko ya wanafunzi na nadharia za kiisimu na nadharia katika elimu kama taaluma. Hata hivyo ufundishaji lgh za kigeni unazidi kukomaa kutokana namaendeleo ya sayansi na teknolojia, hali hii imeibua mbinu za ufundishaji wa lugha za kigeni.
Mbinu za ufundishaji ni njia za ufundishaji zilizokitwa katika kanuni na miongozo maalumu
  1. Mbinu ya sarufi- tafsiri.
  2. Mbinu ya moja kwa moja.
  3. Mbinu ya usikilizaji.(audialingualism)
  4. Mbinu ya mwitiko kamili wa kivitendo
  5. Mbinu ya utambuzi (cognitive
  6. Mbinu ya ujifunzaji kijumuiya
  7. Mbinu yaupendekezi
  8. Mbinu ya kimawasiliano.
                                                           MBINU YA SARUFI- TAFSIRI.
Hii ni mbinu ya kimapoke kwa kuwa ilianza na ilitawala ufundishaji hata lugha zilizokufa. Hadi sasa inatumika kufundishia watu wengi.
SIFA ZA MBINU HII
  1. Lgh ya utunzi ndiyo inatumika kufundishia
  2. Wanafunzi hupewa orodha za kanuni ya kisarufi ili wakariri (kupewa maneno ya kigeni).
  3. Stadi zinazopewa mkazo ni kusoma na kuandika tu. Mkazo kidogo au hakuna mkazo katika utamkaji wa sauti. Vitabu vilivyoandika kwa ajili ya kufundishia lgh kwa kutumia mbinu hii kwa kiasi kikubwa hufafanua kanuni za kisarufi na kasha kutoa mazoezi mengi ya kutafsiri .
                     MBINU YA MOJA KWA MOJA.
Huzingatiaufundishaji msingi wa uasilia wa lugha. Yaani kumudu lgh ya kigeni kama lugha mama yake. Mbinu hii iliibuka kutokana na kutambua kuwa kutambua lugha ni kuzungumza zaidikuliko kuiandika
SIFA ZA MBINU HII
  1. Lugha lengwa tu ndiyo inayotumika, inachukuliwa kuwa lugha ya kwanza ni chanzo cha makosa katika kujifunza lugha ya pili.
  2. Stadi ya mazungumzo hutawala katika mbinu hii.
  3. Stadi ya kuandika haiwekewi uzito.
MBINU YA USIKILIZAJI.(AUDIALINGUALISM)
Ilijikita katika mbinu ya usikilizaji. Waasisi wa mbinu hii ni wana utabia kama vile Bloomfield 1942, walikabidhiwa mhutasari wa ufundishaji lgh za kigene marekeni na kueleza kuwa kujifunza lugha ni kama kujifunza tabia Fulani ambao wao huona kuwa kujifunza lugha ni kurudiarudia mara kwa mara . lengo la kufundisha lugha ni kuzungumza ni kumwezesha kuzungumza na kukabiliana nayo ana kwa ana kwa kiasi Fulani
SIFA
  1. Kukariri mazungumzo na kufanya mazoezi kuepuka kasoro katika uzungumzaji.
  2. Stadi za lugha hupangiliwa kuanzia stadi ya kusikiliza, kuzungumza, kusoma na kuandika
  3. Hutumia lugha ya kigeni tu kama lugha ya kufundishia/lugha ya pili. Ufundishaji wa ruwaza wa miundo ya lugha uwe wa kurudiarudia.
  4. Hakuna uelezwaji wa sarufi
  5. Msamiati hujifunzwa kutokana namuktadha
  6. Kuna matumizi ya vinasa sauti kama vile cd,video
  7. Msisitizo upo katika utamkaji
  8. Baada ya mwitiko sahihi hutolewa uimarisho/tuzo.
MBINU YA UTAMBUZI
Iliibuka miaka ya 1970 kama mwitiko wa uhakiki ni mbinu rekebishi ya mbinu 2 zilizotamgulia. Watetezi wa mbinu hii ni wanasaikolojia na wanaisimu tambuzi
SIFA ZA MBINU HII
  1. Inatilia mkazo kumpa mwanafunzi uwezo wa kuelewa mfumo wa lugha ya kigeni, kasha kumpa uhuru wa kuweza kujifunza peke yake kwa kutumia msingi aliopewa mbinu hii hupinga kujifunza lugha, baada ya mwanafunzi kupewa mbinu za ujifunzaji mazoezi na msingi mwanafunzi huachiwa huru na kumuachia ajifunze mwenyewe kwa kutumia mbinu zake. Noam Chomsky anaunga mkono mbinu hii. Vitabu vilivyoandikwa kufundishia lugha ya kigeni humsaidia mwanafunzi kutambua misingi ya kisarufi na ufaham na utungajiwa kubuni na kujieleza.
MBINU YA MWITIKO KAMILI WA KIVITENDO
Hii ni mbinu ambayo hitwa pia mkabala asilia wa kujifunza lugha. Mbinu hii iliasisiwa na wanaisimu saikolojia kama James Asher 1969, mbinu hii inalenga utumiaji wa stadi moja ili kuimarisha stadi nyingine.
SIFA
  1. Mwanafunzi humsikiliza na kumtazama mwalimu akitamka amri na kuzitekeleza moja kwa moja na baada ya hapo mwalimu hurudia kila amri na kumtaka mwanafunzi atekeleze baadae mwanafinzi hutekeleza mwenyewe.
  2. Inasisitiza kuwa katika kujifunza lugha ya pili kwa kutumia vitenzi vilivyo katika kauli ya kuamru kama ilivyo kwa watoto wadogo wanapojifunza lugha mama. Mfano mama taka uji.
MBINU YA UJIFUNZAJI LUGHA KIJUMUIYA
Hujulikana pia kama mbinu ya ujifunzaji kwa ushauri. Ni mbinu iliyobuniwa na Charles A na Curran 1976. Ni wana saikolojia bingwa wa masuala ya ushauri na uelekezi. Katika mbinu hii mwanafunzi huzingwatiwa katika mbinu mbili, kwa upande mmoja hisia zake kama binadamu, hupewa nafasi ya kujieleza na kupewa ujuzi wa lugha kwa kiwango kinachotakiwa
SIFA ZA MBINU HII
  1. Mwanafunzi ndiye egemeo la ujifunzaji lugha. Dhima ya mwalimu ni kushauri tu na kuchochea ujifunzaji uendelee, uhusiano baina ya mwalimu na mwanafunzi ni sawa na mshauri na mteja.
  2. Mwanafunzi huchagua wanachotaka kujifunza na kuambiana kwa lugha yao. Mwalimu ambaye ni mshauri huwatafsiria namna ya kukisema katika lugha ya kigeni na wanafunzi hukisema kwa lugha ya kigeni na kukirudiarudia, mchakato huu huendelea katika mada mbalimbali na mazungumzo huhifadhiwa kwa matumizi ya baadae. Katika upande wa hisia za kibianadamu : wanafunzi hupewa nafasi za kukisema kwa kutumia lugha za kigeni. Dai kubwa la mbinu hii ni kuwa lugha ni watu , lugha ni watu kwa kukabiliana pia lugha ni watu kadri ya mahitaji na miitiko yao. Hivyo wanafunzi huwa jumuiya na hujifunza kupitia jumuiya hiyo.
  3. Katika kutumia mbinu hii hakuna mhitasari wala kitabu kinachotumika kufundishia.
                                                         MBINU YA UPENDEKEZI
Mwasisi wake ni Gorge lozanov 1979. Kwa mujibu wa mbinu hii mazingira bora
                                                         SIFA ZA MBINU HII
  1. Darasa hutengenezwa na kuwa mahara pa kuvutia sana kukaa. Wanafunzi wakae kwa muduara katika vikundi vidogo vidogo na kuwe na michoro mziki, picha. Masomo huangwa katika mada kumi na ufundishwaji hupewa masaa manne kila siku kwa siku 6 katika wiki. Wanafunzi hupewa orodha ya msamiati ili kukariri. Mbinu mbalimbali hutumika ikiwa ni pamoja na uigaji, maswali na majibu, uigizaji n.k. vitabu viulivyoandikwa katika mbinu hii husheheni vielelezo mbalimbali ili kumvutia mwanafunzi katika kujifunza. Lengo la mbinu hii ni kupata umilisi wa mazungumzo yaani maneno 230 katika siku 30.

8/04/2014

                                                   MBINU YA KIMAWASILIANO
Mbinu hii iliibuka katika miaka ya 1980 na iliendelea kukubalika katika nchi nyingi duniani kama njia bora ya kufundishia lugha ya pili. Kuibuka kwake kulichochewa na hali ya kutegemeana miongoni mwa nchi za bara la ulaya hasa kiuchumi na soko la dunia kati ya nchi hizo, kama taaluma mbinu hii chimbuko lake lilitokea siku nyingi hata kabla ya 1980, wapo wanaisimu waamirifu kama vile Firth 1968, Halliday 1973 na mwanaisimu jamii Hyrmes 1972, walikuwa na mawazo kuwa lugha ni mawasiliano, wanasema “msingi wa mbinu hii ni mwanafunzi ndilo eneo la mafinzo na kwamba kujifunza lugha ni kujifunzakuwasiliana. Hawa wanatofautiana na Noam chomscky kuwa anayedai kuwa kujua lugha ni kujua umilisi wa mfumo nakanuni na hivyo kuitumia sahihi.
Hivyo tangu siku ya kwanza jitihada za mawasiliano lazima zifanyike katika ujifunzaji na ufundishaji, madhumuni ya mbinu hii n kukuza stadi zote za lgh ambazo hutumika katika mawasiliano.

Maana ya mbinu ya kimawasiliano:-
Ni mbinu iliyokitwa kwa mwanafunzi, hutoa mwanya kwa mwanafunzi si katika umilisi wa sarufi bali pia katika stadi za jamii yaani nini cha kusema, namna ya kusema, lini aseme na wapi aseme ili kuridhika na kile anachohitaji kila siku.
Lengo kuu la mbinu hii ni kumfanya mwanafi=nzi apate umilisi wa mawasiliano na mwalimu kazi yake ni kumwezesha mwanafunzi kupata umilisi wa mawasiliano, na umilisi ni pamoja na
  1. Umilisi wa kisarufi
  2. Umilisi wa uneni
  3. Umilisi wa kiufundi, kv alama za kiuakfishi like koma, nukta nk
  4. Umilisi wa kiisimu jamii. Kv namna ya kusema, wapi nk.
                               MISINGI YA MBINU YA UFUNDISHAJI LUGHA KIMAWASILIANO
  1. Namna ya kutumia lugha
  2. Uamiliaji asilia wa lugha kuwa mwanafunzi ajifunze lugha katika muktadha halisi na wenye uasilia
  3. Ufundishaji uhusishwe na hali halisi ya maisha, ili mwanafunzi aelewe uasilia wa maisha
  4. Lugha ifindishwe kama stadi, lugha isifundishwe kama somo, katika mbinu hii mwal awafanye wanafunzi wake wazungumze ili kujua hali halisi. Hivyoikubalike kuwa lugha ni stadi
  5. Ukuzaji uwezo wa kuwasiliana, katika mawasiliano kuna stadi ndogo 4 ambazo zinapaswa kukuzwa kwa mwanafunzi ili aweze kuwasiliana ambazo ni
(a)    Kuzungumza
(b)   Kusikiliza
©    Kusoma
(d)   Kuandika

SIFA ZA MBINU YA KIMAWASILIANO
  1. Sifa kuu ni mawasiliano, inasisitiza mawasiliano lugha inatumika kwa mawasiliano, hivyo mbinu hii husisitiza mawasiliano katika kufundisha lugha. Husisitiza hali halisi ya maisha na mawasiliano katika muktadha hivyo ujumbe unaoelezwa katika mawasiliano huwa katika muundo wa kidhima.
  2. Inamlenga mwanafunzi kwa sababu kazi ya mwalimu ni mwezeshaji tu, anawezesha kisha anaruhusu mwanafunzi kujifunza mwenyewe.
  3. Muktadha wa kijamii, mbinuhii husisistiza mawasiliano ya kijamii na miktadha halisi, hivyo mwanafunzi hujifunza lugha kwa sababu muktadha wa kijamii hutengenezwa.
  4. Uwezo wa kuzungumza, mbinu hii huwasaidia wanafunzi uwezo wa kuzungumza kitu ambacho ni muhimu katika maisha.
  5. Lugha lengwa hujifunzwa kama lugha ya kwanza katika mbinu hii.
  6. Mbinu hii hukuza stadi za lugha kv, kusikiliza na kuzungumza, kusoma kuandika

                                                           MAHITIMISHO
  1. Mbinu hii haihitajiki kupuuzwa kwa sababu hihitaji mawasiliano ya kila siku.
  2. Utumizi wa lugha wa kila siku ndio msingi wa lugha ya pili na siyo lugha ilivyo katika maandishi, kitendo cha kujifunza lgh kwa kimazingira huitwa
  3. Kama ilivyo ujifunzaji wa mfumo zalishi ni muhimu pia kujifunza raghibaya wanafunzi na kuwapa kiwango Fulani cha kujiamini, mwl awape fursa ya kutumia kile walichojifunza katika mazingira halisi.
  4. Kama uzuri wa mzungumzaji mzawa “ni uzuri huo huo anatakiwa aupate mzungumzaji wa lugha ya pili/asiye mzawa. Vitu vya kuandaa: matini ziwe bora ili mjifunzaji kumudu lugha anayojifunza.
  5. Ni muhimu kwa matini kuwa rahisi ili wanafunzi wasitumia muda mrefu kupata dhana ya matini hiyo, katika hali halisi wanapokutana na matini za namna hii wanachanganya hivyo wapewe muda wa kutosha na mazoezi ya kutosha pia.
  6. Matini hizi zipo si kwa ajili ya kusoma tu bali pia katika kuibua lugha itakavyotumiaka darasani na kuongeza marifa zaidi
  7. Urefu matini sharti ziwe fupi.

UGUMU KATIKA MBINU YA MAWASILIANO
Husababishwa na muktadha ambao lugha hiyo inafundishwa unatakiwa kujua kuwa
  1. Unafundisha akina nani?
  2. Wanajifunzia wapi kwa wazawa au ugenini?
  3. Kwanini wanajifunza?
Hivyo muktadha wa ufundishaji uzingatie mambo makuu manne
  1. Umri mfano watoto, vijana au watu wazima
  2. Viwango, unafundisha katika kiwango gani
  3. Ueledi wao, ueledi wao/kazi zao
  4. Muktadha wa kijamii,
UMRI
(a)    Ufundishaji wa watoto
Inaaminika kuwa watoto hujifunza lugha kirahisi kuliko watu wazima, hujifunza bila kujua jitihada wnazofanya katika kujifunza lugha. Utafiti unaonyesha kuwa waqtu wazima wanaweza kuwa wazuri katika baadhi ya maeneo, wanaweza kurunza misamiati mingi kuliko watoto. Wanaweza kutumia michakato mifupi katika kujifunza michakato ya kisarufi na kiisimu wakati watu wazima wakiwa darasani wana uwezo wa juu wa kujifunza haraka. Hivyo wakati watoto huzungumza katika mzingira halisi bila shida watu wazima wanapata shida. Watoto darasani wanaweza kupata ugumu katika kujifunza lugha ya pili kwa sababu ya tofauti binafsi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa ambazi zio katika ufundishaji wa lugha ya pili. Ili kuwa na ufundishajiwa wenye mafanikio unatakiwa kuwa na stadi maalumu tofauti na zile za watu wazima.

MAMBO MATANO YA KUZINGATIA KUFUNDISHA WATOTO.
  1. Kukuza uwezo wa kufikiri, watoto hujifunza kwa kujikita katika viti au mambo aambayo ni ya papo kwa papo katika matumizi ya lugha. Mambo ya kufanya unapokuwa darasani ili kukuza uwezo wa kufikiri wa watoto:
(a)    Usifafanue sarufi kama ilivyo,
(b)   Dhana za sarufi zifundishwe kwa kutumia ruwaza, mf: nilijifunza kisw, ulijifunza kisw, alijifunza kisw. Tulijifunza kisw-, mlijifunza kisw-
Baadhi ya dhana ngumu zirudiwerudiwe.

  1. Muda wa utayari, hii ni tofauti ya watoto na watu wazima wao huwa na mda mfupi, kazi ya mwl ni kuweka mvuto wa lugha na lifurahishe ili kuonyesha uhalisia. Ni muhimu kuelewa nini maana ya utayari, zingatia yafuatayo:
(a)    Andaa mazoezi ya kuvutia
(b)   Wape aina mabalumbali za mazoezi kuwaandaa
©    Mwl ahuishe , ahaishe na aasilishe kuhusu somo lenyewe, zingatia kuwa mwl ni lazima awe mtendaji kutengeneza utayari wa watoto.
(d)   Ucheshi huwafanya watoto wajifunze.
(e)   Hakikisha unapata udadisi, uchunguzi wa watoto ili kujua mwelekeo wao.
  1. Milango ya fahamu, watoto wanapaswa kutumia milango yote ya fahamu inayochangamushwa, kazi ya mwl ni kujitahidi kuchangamsha hii milango ya fahamu hadi zaidi ya macho na maskio. Mambo ya kufanya
(a)    Fanya michezo hii hupanua milango yao ya fahamu
(b)   Kazi mradi ndogondogo ili kuwafanya wajifunze
©    Misaada ya ufahamu , mf: maua yana harufu gani?
(d)   Tumia lugha ya ishara, n I muhimu kwa sababu watoto wataangalia kwa makini na kutambua lugha.
  1. Athari, haya ni mabo ambayo ni vizuizi katika ujifunzaji lugha. Watoto wana udhaifu kuliko watu wazima, namna ya kuondoa athari za lugha
(a)    Thibiti darasa kutomcheka mtu darasani,
(b)   Uwe mkweli katika kuwajenga,
©    Hakikisha wanashiriki mazungumzo kadri inavyowezekana, wape nafasi kujaribu kufanya kitu kwa kila mmoja.

  1. Uasilia, umaana wa lugha, watoto huingalia lugha mpya kama inaweza kutumika papo kwa papo. Hawajisikii ikiwa lugha haina manufaa kwao mfano lugha isoyo ya asili na isiyo na maana. Kipi cha kufanya:
(a)    usitumie lugha rasmi sana,
(b)   lugha ihusianishwe na mazingira kama vile mazingira, matukio, uhusika mf: motto ahusike kamapolisi, daktari nk.
©    Mbinu ya kuanza na kitu kizima itumike usianze na vipande vipande, weka mkazo katika stadi mablimbali kama kusoma, kusikiliza, kusoma na kuandika
b. ufundishaji watu wazima
watu wazima wanaweza kufundishika kwa urahisi, kiwango chao cha aibu kinaweza kuwa kikubwa hata zaidi ya watoto lakini wao hujiamini. Kuna mambo matano ya kuzingatia katika kufundisha watu wazima.
  1. Kukuza uwezo wa kufikiri, watu wazima wana uwezo wa kutumia data mbalimbali na kanuni, kuwa mwangalifu kufundisha udhahania katika matumizi ya lugha.
  1. Muda wa utayari, watu wazima wana uwezo wa kuwa na utayari kwa muda mrefu hata kama somo haliwavutii,. Lakini kanuni ya kuwapa mazoezi kanuni ni ile ile.
  1. Milango ya fahamu, itumike pia japokuwa watu wazima huongozwa na hisia zaidi.
  1. Athari, jitahidi kuondoa athari zinazotokea katika ujifunzaji na ufundishaji lugha.
  1. Uasilia na umaana wa lugha. Watu wazima wana uwezo wa kufikiri dhana dhahania za lugha na dhana zisizo asilia zinaweza kutumika katika ujifunzaji.
USIMAMIZI WA DARASA LA WATU WAZIMA
  1. MWl uoneshe heshima na nidhamu ili wasijenge dhana ya kuchukia somo au kuwa na mwelekeo hasi wa somo hilo,
  2. Mwl asiwachukulie watu wazima kama watoto
  3. Mwl awape uhuru wa kufanya wanapokuwa katika mazingira yao wanapokuwa nje ya darasa
  4. Mwl asiwafundishe watu wazima nidhamu kama vile watoto
  5. Wachukulie kuwa ni watu wazima hivyo wanaweza kufanya mambo kiutu uzima.

VIWANGO VYA WANAFUNZI
Ufundishaji wa lugha za kigeni huwa katika viwango vitati
(a)    Kiwango cha awali
(b)   Kiwango cha kati
©    Kiwango cha juu


Ufundishajiwa kiwango cha awali
Wanafunzi hawana maarifa kuhusu hiyo lugha hivyo mwl ni mwezeshaji wao katika malengo yao, mwl anapaswakutoa zawadi ili kuwafanya wanafunzi kuweka umakini,
Mambo kumi ya kuzingatia
  1. Mchakato wa ukuzaji akili kwa wanafunzi, wanafunzi washiriki kurudiarudia maneno aktika siku zile za mwanzo. Mwl asichanganyikiwe na wanafunzi kutopata mabadiliko katika kipindi kifupi maana ni lugha ngeni kwao, siku za mwanzo wapatie mazoenzi madogomadogo mf: waweze kutaja majina yao na wanakokaa. Mazoezi yalenge kuwakuza uelewa.
  2. Kazi ya mwl. Mwanafunzi hutegemea mwl katika kila kitu kuhusiana na lugha, kazi za vikundi zitumike katika kujijengea uelewa. Mf picha.
  3. Unenaji wa mwl, mwl aongee kwa sauti ya kutosha, mwl atumie misamiati rahisi kabisa na sarufi rahisi kabisa.
Mwl atumie lugha ya kwanza mara chache sana, si vizuri uwaruhusu wanafunzi kutumia lugha zao za kwanza mara kwa mara. Mwl atumie lugha ya kwanza kwa manufaa ya : kuelezea hoja za sarufi 2. Kuonyesha maneno yaloyowachanganyaau kwenye maneno ya kiutamaduni
  1. Hakikisha lugha inayotumika ni lugha inayotua inafuata kanuni za kimawasiliano hivyo ionyeshe uasilia waa lugha isiwe lugha rasmi sana kwa wako katika hatua za awali mf: salamu na utambulisho, mwl hakikisha kuwa ufundishaji   ni rahisi na mfupi. Mwl usiwakatishe tama wanafunzi wako bali wape muda kujifunza.
  2. Ufasaha na usahihi, ufasaha ni muhimu katika hatua hii hakikisha unakuwa katika semi fupifupi mana ni muhimu kuhimizauzungumzaji , usahihi utiliwe mkazo katika sarufi za lugha. Ni muhimu kuangal;ia mahitaji ya wanafunzi katika kuzungumza bila kukosolewa katika kuzungumza. Wape mazoezi ya kisarufi na kifonolojia.
  3. Ubunifu wa wanafunzi, lengo la kujifunza lugha ni kujenga uelewa na kuzalisha kitu kipya ili kuweka ubunifu na utoaji. Katika kiwango cha awali wanafunzi wanaweza kuwa wabunifu kwa kiwango Fulani usitegemee ubunifu mkubwa sana katika lugha.
  4. Mbinu, mbinu rahisi zitumike, anzisha maswali unayoyamiliki yakifuatiwa na maswali ya wanafunzi, pia mbinu ya makundi ni mbinu nzuri sana.
  5. Malengo ya mzungumzaji na msikilizaji, kazi yake ni uasilia wa mawasiliano hakikisha usikilizaji na uzuungumzaji una maana ya mawasiliano.
  6. Malengo ya usomaji na uandishi, katika kiwango cha awali mada ya kusoma na kuandika inatakiwa iwe fupi inayokidhi matakwa ya wahusika kama vile matangazo, kazi ya kuandika inapaswa kuwa ya kuorodhesha.
  7. Sarufi, inatahusisha vitenzi rahisi, viwakilishi vya nafsi .toa lugha lugha ianyieleweka. mbinu ya kuambukiza sarufi inafaa katika kufundisha sarufi na kuambukiza ruwazA
KIWANGO CHA KATI
Ni mambo yale yale ya kiwango cha awali
  1. Mchakato wa ukuzaji akili kwa wanafunzi, wanafunzi washiriki kurudiarudia maneno aktika siku zile za mwanzo. Mwl asichanganyikiwe na wanafunzi kutopata mabadiliko katika kipindi kifupi maana ni lugha ngeni kwao, siku za mwanzo wapatie mazoenzi madogomadogo mf: waweze kutaja majina yao na wanakokaa. Mazoezi yalenge kuwakuza uelewa.
  2. Kazi ya mwl. Mwanafunzi hutegemea mwl katika kila kitu kuhusiana na lugha, kazi za vikundi zitumike katika kujijengea uelewa. Mf picha.
  3. Unenaji wa mwl, mwl aongee kwa sauti ya kutosha, mwl atumie misamiati rahisi kabisa na sarufi rahisi kabisa.
Mwl atumie lugha ya kwanza mara chache sana, si vizuri uwaruhusu wanafunzi kutumia lugha zao za kwanza mara kwa mara. Mwl atumie lugha ya kwanza kwa manufaa ya : kuelezea hoja za sarufi 2. Kuonyesha maneno yaloyowachanganyaau kwenye maneno ya kiutamaduni
  1. Hakikisha lugha inayotumika ni lugha inayotua inafuata kanuni za kimawasiliano hivyo ionyeshe uasilia waa lugha isiwe lugha rasmi sana kwa wako katika hatua za awali mf: salamu na utambulisho, mwl hakikisha kuwa ufundishaji   ni rahisi na mfupi. Mwl usiwakatishe tama wanafunzi wako bali wape muda kujifunza.
  2. Ufasaha na usahihi, ufasaha ni muhimu katika hatua hii hakikisha unakuwa katika semi fupifupi mana ni muhimu kuhimizauzungumzaji , usahihi utiliwe mkazo katika sarufi za lugha. Ni muhimu kuangal;ia mahitaji ya wanafunzi katika kuzungumza bila kukosolewa katika kuzungumza. Wape mazoezi ya kisarufi na kifonolojia.
  3. Ubunifu wa wanafunzi, lengo la kujifunza lugha ni kujenga uelewa na kuzalisha kitu kipya ili kuweka ubunifu na utoaji. Katika kiwango cha awali wanafunzi wanaweza kuwa wabunifu kwa kiwango Fulani usitegemee ubunifu mkubwa sana katika lugha.
  4. Mbinu, mbinu rahisi zitumike, anzisha maswali unayoyamiliki yakifuatiwa na maswali ya wanafunzi, pia mbinu ya makundi ni mbinu nzuri sana.
  5. Malengo ya mzungumzaji na msikilizaji, kazi yake ni uasilia wa mawasiliano hakikisha usikilizaji na uzuungumzaji una maana ya mawasiliano.
  6. Malengo ya usomaji na uandishi, katika kiwango cha awali mada ya kusoma na kuandika inatakiwa iwe fupi inayokidhi matakwa ya wahusika kama vile matangazo, kazi ya kuandika inapaswa kuwa ya kuorodhesha.
  7. Sarufi, inatahusisha vitenzi rahisi, viwakilishi vya nafsi .toa lugha lugha ianyieleweka. mbinu ya kuambukiza sarufi inafaa katika kufundisha sarufi na kuambukiza ruwaza.
KIWANGO CHA JUU
  1. Mchakato wa ukuzaji akili kwa wanafunzi, wanafunzi washiriki kurudiarudia maneno aktika siku zile za mwanzo. Mwl asichanganyikiwe na wanafunzi kutopata mabadiliko katika kipindi kifupi maana ni lugha ngeni kwao, siku za mwanzo wapatie mazoenzi madogomadogo mf: waweze kutaja majina yao na wanakokaa. Mazoezi yalenge kuwakuza uelewa.
  2. Kazi ya mwl. Mwanafunzi hutegemea mwl katika kila kitu kuhusiana na lugha, kazi za vikundi zitumike katika kujijengea uelewa. Mf picha.
  3. Unenaji wa mwl, mwl aongee kwa sauti ya kutosha, mwl atumie misamiati rahisi kabisa na sarufi rahisi kabisa.
Mwl atumie lugha ya kwanza mara chache sana, si vizuri uwaruhusu wanafunzi kutumia lugha zao za kwanza mara kwa mara. Mwl atumie lugha ya kwanza kwa manufaa ya : kuelezea hoja za sarufi 2. Kuonyesha maneno yaloyowachanganyaau kwenye maneno ya kiutamaduni
  1. Hakikisha lugha inayotumika ni lugha inayotua inafuata kanuni za kimawasiliano hivyo ionyeshe uasilia waa lugha isiwe lugha rasmi sana kwa wako katika hatua za awali mf: salamu na utambulisho, mwl hakikisha kuwa ufundishaji   ni rahisi na mfupi. Mwl usiwakatishe tama wanafunzi wako bali wape muda kujifunza.
  2. Ufasaha na usahihi, ufasaha ni muhimu katika hatua hii hakikisha unakuwa katika semi fupifupi mana ni muhimu kuhimizauzungumzaji , usahihi utiliwe mkazo katika sarufi za lugha. Ni muhimu kuangal;ia mahitaji ya wanafunzi katika kuzungumza bila kukosolewa katika kuzungumza. Wape mazoezi ya kisarufi na kifonolojia.
  3. Ubunifu wa wanafunzi, lengo la kujifunza lugha ni kujenga uelewa na kuzalisha kitu kipya ili kuweka ubunifu na utoaji. Katika kiwango cha awali wanafunzi wanaweza kuwa wabunifu kwa kiwango Fulani usitegemee ubunifu mkubwa sana katika lugha.
  4. Mbinu, mbinu rahisi zitumike, anzisha maswali unayoyamiliki yakifuatiwa na maswali ya wanafunzi, pia mbinu ya makundi ni mbinu nzuri sana.
  5. Malengo ya mzungumzaji na msikilizaji, kazi yake ni uasilia wa mawasiliano hakikisha usikilizaji na uzuungumzaji una maana ya mawasiliano.
  6. Malengo ya usomaji na uandishi, katika kiwango cha awali mada ya kusoma na kuandika inatakiwa iwe fupi inayokidhi matakwa ya wahusika kama vile matangazo, kazi ya kuandika inapaswa kuwa ya kuorodhesha.
  7. Sarufi, inatahusisha vitenzi rahisi, viwakilishi vya nafsi .toa lugha lugha ianyieleweka. mbinu ya kuambukiza sarufi inafaa katika kufundisha sarufi na kuambukiza ruwaza.
MUKTADHA WA KIJAMII
Upo katika namna 2
  1. Kijamii na kisiasa na
  2. Kitaasisi
MUKTADHA WA KIJAMII NA KISIASA
Baadhi ya mambo ya kijamii na kisiasa ni pamoja na usahihi na kufaa
Rejesta na mitindo
Semi zinazokubalika katika jamii
Usanifu wa lugha katika kabila na kitaifa
Sera ya lugha katika taifa
Lahaja ya lugha
Katika kipengele hiki tunaangalia muktadha wa kisw kama lugha ya 2 na katika lugha ya kigeni. Unapofikiria muktadha wa lugha ya 2 na lugha ya kigeni fikiri pia nn kinatokea nje ya darasa wanafunzi wanapotoka darasani.
MUKTADHA WA UJIFUNZAJI WA LUGHA YA PILI
Lugha lengwa ya darasani hupatika nje ya darasa. Wanafunzi huweza kuwasiliana kwa lugha yao nje ya darasa. Mfano: Kiswahili Tanzania , kiingereza marekani
–          Lugha ya kigeni muktadha wa ujifunzaji wake (lugha lengwa inayofundishwa|) haipatikani nje ya darasa, wanafunzi huwa na msamiati wa darasani tu. Mfano: kiingereza Tanzania , japan, ujeruman . pia Kiswahili ni lugha ya kigen nchini marekeni, china nk. Njia za ufundishaji katika muktadha wa lugha ya pili ni tofauti na ule
MUKTADHA WA KISWAHILI KAMA LUGHA YA PILI
Mwalimu unapofundisha lugha ya Kiswahili kama lugha ya pili fanya yafuatayo:
  1. Wape kazi nyingi za nyumbani zenye uzungumzaji mahususi ili wayaone yanayotokea mtaani na walinganishe.
  2. Wahimize wanafunze kufanya mazoezi na wazawa
  3. Kusanya makala na magazeti
  4. Wahimize kupata mrejesho sahihi kutoka kwa wazawa.
  5. Wasisistize wanafunzi kutunza kumbukumbu sahihi walizojifunza darasani.
  6. Weka mpango wa kutembelea nyanjani (field trips)
  7. Kuwepo kwa ushirikiano wa wazawa wa lugha. Karibisha hata wazawa darasani
UFUNDISHAJI WA KISWAHILI KAMA LUGHA YA KIGENI
Kunakuwepo na shida katika ufundishaji wa kisw kama lugha ya kigeni kwa kuwa nje ya darasa kunakuwepo na lugha isiyopatikana nje ya darasa.
Muda wa kujifunza ni mdogo katika lugha.
MAMBO YA KUFANYA (MWALIMU)
  1. Mwalimu atumie uasilia wa lugha na mbinu shirikishi.
  2. Hakikisha unatoa motisha mara kwa mara kila utoapo zoezi ili kuwahamasisha wanafunzi.
  3. Wasaidie sana wanafunzi wako ili waone umhimu wa lugha hiyo.
  4. Wape majaribio ya kufanya kazi na usisitize kuyafanya.
  5. Toa fursa za ziada darasani kama radio, tv, magazeti, vitabu, makala nk.
  6. Fanya michezo ya uigizaji na usumuliaji
  7. Leta wazawa waje kuzungumza nao
  8. Weka mbinu za nje kuzitumia nje ya darasa
  9. Unda klabu za lugha.
  1. Ueledi wao
Hapa tunaangalia je ni wanadiplomasia, wanataaluma, wamisionari nk.

MADA YA 4: UTAYARISHAJI WA MUHTASARI (SYLABUS) NA VIFAA VYA KUFUNDISHIA
  1. Utayarishaji wa syalabus katika ufundishaji wa Kiswahili
Syllabus ni muhatasari wa mada zinazokwenda kufundishwa katika kiwango Fulani cha elimu
Mambo ya kuzingatia katika kuandaa syabus
(a)    Malengo ya kozi
(b)   Mada zizingatie uelewa wa wanafunzi kwa kila kiwango: mf, kiwango cha juu, chini au kati
©    Mada zizingatie muktadha wa wanafunzi
(d)   Izingatie uelewa wa wanafunzi, izingatie uelewa wa awali wa wanafunzi.
(e)   Izingatie matakwa na mahitaji ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.
(f)     Izingatie muda katika ufundishaji wa kila kiwango.
VIPENGELE
  1. Malengo ya jumla ya kufundisha Kiswahili kwa wageni.
  2. Matokeo ya ujifunzaji
  3. Mada zitakazofundishwa kwa kiwango Fulani
  4. Mbinu za kufundishia mada
  5. Vifaa/zana zitakazotumika katika ufundishaji na ujifunzaji wa lugha.
  1. UTAYARISHAJI WA VITABU VYA KUFUNDISHIA KISWAHILI KWA WAGENI.
(a)    Ni muhimu kuzingatia mtiririko mzuri wa mada / masomo kuanzia somo moja hadi jingine kuanzia rahisi kwenda ngumu. Kuna vipengele vine vya kuazingatia katika uandaaji wa kitabu cha kitabu cha Kiswahili kwa wageni
(i)                  Kurasa za utangulizi, yatolewe maelezo ya utangulizi juu ya historia fupi ya lugha ile ili kusaidia mwanafunzi kujua hali na hadhi ya Kiswahili nchini Tanzania ,
pia sauti za lugha na matamshi lazima zionyeshwe katika utangulizi. Maneno ya lugha mama ya mwnafunzi yatumike kutafsiri maneno ya kigeni kumfanya mwanafunzi kutambua sauti ambazo haziko katika lugha yake.
(ii)                Kurasa zenyewe, Masomo yenyewe yaonyeshe mtiririko wa mada zenyewe
(iii)               Kurasa za mwisho,
(a)    Orodha ya misiamia na semi zilizotumika katika kitabu hicho zionyeshwe na zipangwe kialfabeti kurahisisha uapatikanaji wa msamiati. Ni vizuri orodha hiyo iwe na tafsiri katika lugha ya wanafunzi. Pia kunafaa kuwe na orodha mbili za maneno, maneno ya kigeni na maneno ya lugha mama, lengo la orodha hizo mbili ni kuipa nafasi lugha ya wanafunzi kujifunza lugha ya kigeni. Pia kurasa za mwisho zioneshe majedwali kuonesha sarufi ya lugha inayofundishwa kusaidia upatikanaji wa maneno yaliyo sahihi
  1. UTAYARISHAJI WA SOMO LENYEWE
Mambo ya kufanya
  1. Somo liwe na lengo mahususi kumsaidia mwanafunzi kuwasiliana, mada idokeze nn mwanafunzi atajifunza aweze kuwasiliana na wazawa wa lugha.
  2. Somo liwe na msamiati na sarufi ambavyo vinavyokidhi mahitaji wa mwanafunzi.
Msamiati udhihirike kutokana na mada yenyewe, sarufi imhamasishe mwanafunzi kutaka kuzungumza na si kujua kanuni tu.
  1. Somo lionyeshe lugha inavyozungumzwa na wazungumzaji.
  2. Somo liwe na vielelezo vya mazingira halisi na taarifa muhimu za kiutamaduni wa lugha ambayo mwanafunzi anajifunza. Pia aelezwe kuwa salamu yaweza kuwa fupi au ndefu. Mf: shikamoo: hutolewa na mdogo kwa mkubwa. Kifamilia si mme mke na watoto tu bali hata ndugu wa karibu wa lugha hiyo.
  3. Somo liambatane na vielezo kama vitu halisi kama picha, vielelezo,nyimbo, matangazo magazeti, ramani hasa katika hatua ya kwanza. Nk. Lengo la vielelezo ni kumuingiza mwanafunzi ndani ya lugha, utamaduni wa lugha ili aweze kujieleza.
  4. Kila somo liwe na mazoezi halisi wa stadi za lugha mazoezi hayo yatokane na matini au vielelezo vilivyoandamana na masomo hayo. Mazoezi yamwezeshe mwanafunzi kupata umahiri wa uamilifu wa lugha na kukuza mawasiliano. Baada ya kila somo lielezwe mwanafunzi akafanye nn baada ya somo.
UWASILISHAJI WA DARASANI 22/04/2014 KIPINDI CHA JIONI
Swali: Jadili mbinu ya mawasiliano inavyoweza kutumiwa na mwalimu katika kufundisha Kiswahili kwa wageni.
Richard 1996
Mbinu hii ilikuwa katika bara la ulaya na kupelekea kuongezeka kwa wahamiaji na hivyo kukawa na mahitaji makubwa ya wanafunzi wa lugha za kigeni.
Misingi ya ufundishaji
  1. Kujikita katika uwezo wa kuwasiliana katika lugha wanayofundishwa wanafunzi na usijikite katika sarufi ya lugha.
  2. Wanafunzi wapewe nafasi ya kuzungumza kile wanachokijua kuhusu lugha kwa kutumia uwezo wao.
  3. Mwalimu awe mvumilivu pale wanafunzi wanapokuwa wamekosea kwa sababu hawana misingi ya lugha hiyo.
  4. Ufundishaji lugha uzingatie misingi halisi ya maisha
  5. Umilisi wa mawasiliano kwa kutofautisha wapi pakutumia lugha rasmi na wapi pasipo pa kutumia lugha rasmi. Chanzo&t&t&t&t&t
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-27T08:40:40Z 2021-06-27T08:40:40Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=310 <![CDATA[KISWAHILI KWA WAGENI (VIDEO)]]> KISWAHILI KWA WAGENI]]> false MwlMaeda]]> 2021-06-27T08:30:55Z 2021-06-27T08:30:55Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=309 <![CDATA[KISWAHILI KWA WAGENI (VIDEO)]]> KISWAHILI KWA WAGENI (VIDEO)]]> false MwlMaeda]]> 2021-06-27T08:06:50Z 2021-06-27T08:37:51Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=308 <![CDATA[UFUNDISHAJI WA KISWAHILI MAREKANI: MAENDELEO NA CHANGAMOTO]]> SWAHILI FORUM 15 (2008): 121-133
UFUNDISHAJI WA KISWAHILI MAREKANI: MAENDELEO NA CHANGAMOTO
                                     J. KIARIE WA’NJOGU
1. Utangulizi
Kiswahili ni mojawapo ya lugha za Kiafrika zinazofundishwa nchini Marekani. Lugha zingine ni Kiyoruba, Kizulu, na Kihausa (tukitaja chache tu). Kunazo lugha zingine za Kiafrika ambazo hufundishwa kutegemea mahitaji ya wanafunzi. Lugha hizi ni kama vile Ki-
wolof, Kitwi, Kitigrinya, Kiamharik, Kilingala na kadhalika. Lugha za Kiafrika zimekuwa zikifundishwa Marekani kuanzia miaka ya hamsini, kupitia mswada uliopitishwa na bunge wa Elimu ya Ulinzi wa Taifa (National Defense Education Act – NDEA) wa mwaka 1958 (Bo- kamba 2002). Mswada huo ulipelekea kuanzishwa kwa vituo vya ufundishaji wa mambo ya Afrika na masomo ya maeneo mengine (African and other area study centers). Kuanzishwa kwa vituo hivi kulikuwa kama njia moja ya kujaribu kukabiliana na maenezi ya Ukomunisti.
Pia wakati huo huo, kulikuwa na msukumo kutoka kwa Waafrika-wa-Amerika (Waamerika wa asili ya Afrika) uliosababishwa na kutofundishwa mambo yaliyohusu historia na utamaduni wao. Msukumo huu pia ulichangia katika kuanzishwa kwa lugha za Kiafrika katika
vyuo vya elimu ya juu. Baada ya Vita Baridi kuisha na kuvunjika kwa muungano wa Sovieti, Marekani ilihimiza lugha fulani zifundishwe kwa maslahi ya mahitaji yake ya kiuchumi na usalama. Miongoni mwa lugha zilizofikiriwa kuwa muhimu ni Kiamharik na Kizulu (Mazrui 1997). Kiamharik kilipendelewa kwa sababu ya kuwa karibu na eneo la Arabia, lililo na utajiri mwingi wa mafuta ya petroli. Lugha ya Kizulu ilipendelewa kwa sababu ya utariji wa maadini katika Afrika ya Kusini na nafasi ya nchi hiyo katika siasa za bara la Afrika kwa jumla.
Kutokana na kuanzishwa kwa lugha za Kiafrika katika elimu ya juu, vyuo vinavyofundisha lugha ya Kiswahili Marekani vimeongezaka kufikia zaidi ya hamsini. Kwa sababu ya tofauti katika ufadhili wa lugha za Kiafrika, programu nazo hutofautiana katika raslmali au vifaa vilivyomo vya kufundishia, ujuzi wa kufundisha, mbinu za kufundisha, na hata kukua kwa progamu zenyewe (Folarin-Schleicher na Moshi 2000). Katika makala hii tutaelezea ufundishaji wa lugha ya Kiswahili, utayarishaji wa walimu na vifaa, na matatizo yanayokumba ufundishaji wa Kiswahili (na lugha zingine za Kiafrika kwa jumla) kama lugha ya kigeni. Mwisho tutapendekeza njia za kusuluhisha kwa matatizo haya.
Historia fupi ya Kiswahili Marekani
Kama tulivyotaja hapa juu, lugha za Kiafrika zilipoanzishwa Marekani hazikujisimamia (na bado hazijajisimamia katika vyuo vingi) kama idara. Badala yake zilikuwa kama ‘nyongeza’ katika idara mbalimbali kama vile Isimu, Masomo ya Waafrika-wa-Amerika (African-American Studies), na Idara ya Fasihi, Idara ya Fasihi-Linganish, au Idara ya Masomo ya Kimataifa. Mwanzoni, walimu waliochukua nyadhifa za kusimamia au na kufundisha lugha hizi walifanya hivyo kwa kujitolea au kama kazi ya ziada. Waaafrika wachache waliokwenda Marekani kuendelea na masomo yao katika idara mbalimbali waliweza pia kutumiwa kufundisha lugha zao kwa malipo (ingawa ya chini). Malipo haya yalikuwa kwa kulipiwa karo/ada za shule na mshahara mdogo kila mwezi kugharamia maisha na mahitaji ya shule (Sanneh na Omar 2002).
Wizara ya mambo ya Kigeni ya Marekani ilihitaji wafanyakazi wa kuhudumu katika bara la Afrika na kwa hivyo walichapisha vitabu vya kwanza vya kufundishia lugha za Kiafrika. Swala ambalo lilikabili kuanzishwa na kufundishwa kwa lugha za Kiafrika Marekani lilikuwa la kuamua ni lugha zipi (miongoni mwa zaidi ya 2500) zifundishwe. Mwaka wa 1979 walimu wa lugha za Kiafrika na wawakilishi wa vituo vya masomo ya Kiafrika walikutana katika Chuo Kikuu cha Jimbo la Michigan. Lengo la mkutano huo lilikuwa ni kutoa mwelekeo na kipaumbele ufundishaji wa lugha za Kiafrika. Mkutano huo ulitoa orodha ya lugha za kufundishwa kwa kuzingatia maswala ya ndani ya Afrika, kama vile idadi ya wasemaji na matumizi ya lugha hizo kama lugha za pili. Orodha kamili ilikuwa na lugha ishirini na nne zilizofikiriwa kuwa muhimu kama lugha za taifa na za kimataifa. Orodha hii ilitofautianan kidogo na ile ya Wizara ya Elimu kwa sababu yao iliongozwa na maswala ya ulinzi wa taifa.
Mwaka wa 1980 NDEA ilifutiliwa mbali na badala yake kukawa na Halmashauri ya Elimu ya Juu (Higher Education Act). Kupitia msaada wa halmashauri hii, waratibu wa lugha za Kiafrika huweza kukutana kila mwaka kujadiji njia za kuzipa nguvu lugha hizi. Mswada huu ulitiliwa nguvu zaidi baada ya kuanzishwa kwa vyama vya wataalamu kama Vituo Vya Taifa vya Lugha za Kigeni (National Foreign Language Centers-NFLC) mwaka 1987, na Shirikisho la Walimu wa Lugha za Kiafrika (African Language Teachers’ Association-ALTA) mwaka 1988 (Sanneh na Omar 2002). Wakati huo huo, kwa mara ya kwanza, udhamini wa Fullbright-Hays ulitolewa kwa wanafunzi wa Kihausa na Kiswahili ili kuwawezesha kushiriki katika kujifunza lugha hizi ng’ambo wakati wa kiangazi (Group Projects Abroad-GPA). Kufikia sasa kuna udhamini wa lugha tatu (Kiswahili, Kizulu na Kiyoruba) katika mradi huu. Programu ya Kiswahili huwapeleka wanafunzi Tanzania, progamu ya Kiyoruba huwapeleka wanafunzi Nigeria, na ile ya Kizulu huwapeleka wanafunzi Afrika Kusini.
Katika miaka ya tisini, programu za lugha za Kiafrika zilifanya warsha mbalimbali ili kuwazoesha walimu wa lugha husika mbinu za kufundisha na kutahini usemaji wa lugha hizo. Mbinu hizi zilitayarishwa na kupendekezwa na Baraza la Amerika la Ufundishaji wa Luhga za Kigeni (American Council on the Teaching of Foreign Languages-ACTF). Mapendekezo haya yalikubaliwa na wote waliohusika na utekelezaji wake ukaanza mara moja. Kwa bahati mbaya, utekelezaji huu haukudumu kwa sababu ya kubadilikbadilka kwa walimu wa lugha za Kiafrika. Tatizo hili litajadiliwa hapo chini.
Kutokana na msaada wa Chama cha Taifa cha Mashirika ya Lugha Zisizofundishwa sana (National Council of Organizations of Less Commonly Taught languages- NCOLCTL), ALTA iliweza kugharamia mfululizo wa pili wa warsha za kujadili mpango wa kufundisha lugha hizi. Kuliundwa vikundi vya kushughulikia lugha tatu zilizoonekana zikifundishwa sana. Lugha hizi zilikuwa Kiswahili, Kiyoruba na Kizulu. Baadaye, vikundi hivi vilipanuliwa zaidi na wajibu wake kuongezwa na kuwa vikundi vya kushughulikia lugha za Afrika Kusini, Mashariki na Magharibi (Southern, Easter, and Western Africa Language Task Forces).
Mwaka wa 1993, Taasisi ya Kiangazi ya Ushirika wa Lugha za Kiafrika (Summer Cooperative Afrian language Institute-SCALI) ilifanyika kwa mara ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Yale. Taasisi hii iliweza kutumia rasilmali kutoka vyuo husika na kuleta pamoja wanafunzi kutoka vyuo mbalmbali, ambao, zaidi ya kubadilishana mawazo ya utafiti wao, walijifunza mojawapo wa lugha za Kiafrika zilizofundishwa. Tangu wakati huo, taasisi hii hufanyika kila kiangazi na chuo chochote kinachoamua kuchukua jukumu la kuiandaa, hulazimika kufanya hivyo kwa miaka miwili mfululizo, kisha huhamia katika chuo kingine. Wanafunzi wa shahada ya pili au zaidi wanaweza kuomba msaada wa kifedha wa kushiriki katika programu hii kutoka mfuko unaogharamiwa na Wizara ya Elimu ya Marekani kupitia programu inayoitwa kwa kifupi FLAS (Foreign Language and Area Studies).

Sababu za Wamarekani kutaka Kujifunza Kiswahili
Vihamasishi vya lugha na masomo ya Kiafrika vinaweza kujitokeza kwa njia mbili kuu: sababu za chuo-husika na sababu za wanafunzi wenyewe. Sababu za chuo ni kama vile kuweka mahitaji ya lugha za Kigeni. Vyuo kadhaa huwahitaji wanafunzi kutosheleza mahitaji ya lugha ya kigeni kwa kujifunza lugha nyingine zaidi ya lugha ya kwanza. Katika kiwango hiki, lugha ya Kiswahili hushindana na lugha zingine za kigeni zinazofundishwa. Lugha hizi hutofautiana kutoka chuo kimoja hadi kingine. Lugha ya Kiafrika (kama Kiswahii) pia inaweza kuwa sehemu ya shahada inayotolewa na idara/programu ya masomo ya Kiafrika. Sababu za wanafunzi ni nyingi na hutegemea mwanafunzi mwenyewe. Baadhi ya sababu hizi ni mahitaji ya utafiti, kumwezesha mwanafunzi kupata ufadhali, biahsara ya kimataifa, hata kumwezesha mwanafunzi kuwasiliana na mpenzi wake (Wa_Njogu 2005).
Kunao pia wanafunzi ambao walijaribu kujifunza lugha zingine za Uropa bila mafanikio. Hawa nao huja kujaribu lugha ambayo ni tofauti kabisa la lugha yao ya kwanza au na lugha yoyote ile ambayo huwa wamejaribu kujifunza. Utafiti umeonyesha kwamba baadhi ya ujuzi wa lugha ya kwanza unaweza kutumika katika kujifunza lugha ya pili (Odlin 1989). Kwa sababu Kiswahili hutumia hati za Kirumi, wanafunzi hawahitaji kujifunza hati mpya kama ilivyo katika madarasa ya Kichina, Kiarabu, Kikorea, Kijapani na mangineyo. Baada ya mazoezi machache, wao wanaweza kutumia ujuzi wao wa lugha ya kwanza na kusoma. Ingawa haijathibitishwa kiutafiti, kwa vile Kiswahii huandikwa jinsi kinavyosemwa au kutamkwa inakuwa rahisi kwa mwanafunzi kukuza mbinu za kusema na kuandika kwa wakati mmoja.
Kama inavyojitambulisha, Marekani ni nchi yenye wahamiaji kutoka nchi nyingi. Nchi za bara la Afrika nazo hazikubakia nyuma katika swala hili la uhamiaji. Watoto wa wahamiaji hawa huhiari kujifunza lugha ambayo wanaweza kujihusisha au kujitambulisha nayo, na kwa minajili ya kuendeleza utamaduni wao. Wanafunzi ambao wanaweza kusema Kiswahili, huhimizwa kuchukua madarasa ya juu kama yale ya fasihi, lakini wale ambao wamezaliwa na kukulia Marekani huanza na madarasa ya chini kama Wamarekani wenzao. Kwa sababu ya uwezekano wa kupanuka kwa matumizi ya lugha ya Kiswahili barani Afrika, madarasa ya Kiswahili pia huwavutia wanafunzi kutoka bara Ashia kama vile Wachina, Wajapani, na Wakorea.
Kunao wanafunzi ambao hujifunza Kiswahili kwa sababu wanatarajia kuzuru Afrika ya Mashariki. Licha ya wale ambao wanahusika na usomi, kunao wengine ambao wanajishughulisha na miradi hasa ya kidini na huhitaji ufahamu wa lugha na utamaduni wa Kiswahili. Mara kadha kunapatikana wanafunzi ambao ni watu waliostaafu na wanaotarajia kuzuru Afrika kama watalii. Katika Marekani watu wa umri wa juu wanaruhusiwa kujisajilisha madarasa katika vyuo vya serikali bila malipo yoyote. Kwa hivyo wakati mwingine kunapatikana wanafunzi wazee ambao wanajitayarisha kutembelea Afrika ya Mashariki. Kwa jumla wanafunzi ambao hujiunga na madarasa ya Kiswahili kwa malengo yao wenyewe (zaidi ya maamuzi ya chuo) huwa na ari zaidi ya kujifunza. Jambo hili limethibitishwa na watafiti wanaojishughulisha na msukumo unatokana na mwanafunzai mwenyewe na ule unaotoka nje (intrinsic and extrinsic motivation) (kama vile Gardner (1996)).
Shule nyingi za msingi na sekondari nchini Marekani hazifundishi mambo ya Afrika. Kwa hivyo mambo mengi ambayo wanafunzi wanajua kuhusu Afrika ni yale yanayotokana na vyombo vya habari kama magezeti na televisheni. Mambo mengi huwa si ya kweli, na hayalengi kuonyesha picha nzuri kuhusu Afrika. Mara nyingi huwa ni habari zinazohusu njaa, magonjwa, vita vya kikabila, ukame na kadhalika. Madarasa ya Kiswahili hujalizia mapango haya kwa kufundisha historia, jiografia, siasa, dini na imani mbalimbali za Afrika (miongoni mwa mengine) zaidi ya kufundisha lugha. Pia madarasa ya Kiswahili hutoa nafasi nzuri ya kukosoa na kurekebisha imani hizi potovu miongoni mwa baadhi ya wanafunzi.
Baada ya uvamizi wa kigaidi wa Septemba 11, 2001 umuhimu wa lugha za kigeni umetiliwa mkazo sana na serikali ya Marekani. Kwa sababu hiyo vyuo vinavyoweza kutoa mafunzo ya juu kwa wanafunzi wao katika lugha za kigeni vinapata ufadhili mkubwa kutoka serikalini. Maingilio ya serikali katika kuathiri mafunzo vyuoni hayajachukuliwa vizuri na walimu wengi kwa sababu malengo ya serikali na ya vyuo hayalingani. Kwa kuwa sababu za wanafunzi za kujifunza Kiswahili kama lugha ya kigeni ni nyingi na tofauti, silabsi, vifaa, na mbinu za kufundishia nazo hulenga kutosheleza malengo hayo. Hata hivyo ufundishaji wa Kiswahili kama lugha ya kigeni Marekani hukumbwa na matatizo tofauti. Sasa tutayaangazia baadhi ya matatizo hayo.


Matatizo ya Kufundisha Kiswahili kama Lugha ya Kigeni

Matatizo haya yanaweza kuchunguzwa katika vipengele tofauti kama vile: walimu, vifaa, wanafunzi, na ufadhili.

1. Walimu
Wengi wa walimu wanaofundisha Kiswahili kama lugha ya kigeni hawajachukua mafunzo ya kazi hiyo. Wengi wao ni wanaisimu na hufundisha lugha hizi kwa sababu ya uwezo wao wa kuzisema kama lugha ya kwanza, au kwa sababu ya ujuzi wao katika lugha hizi. Tatizo lingine ni kwamba kazi za walimu hawa ni za muda tu, na wala si za kudumu. Kwa hivyo muda wao mwingi huutumia kujishughulisha na mambo mengine ya utafiti wao badala ya Kiswahili. Walimu hawa basi hutegemea sana uzoefu wao na vipawa vyao (Batibo 2003).
Kulingana na Moshi na Schleicher (2000) chini ya asili mia 10 ya vyuo na vyuo vikuu vinavyofundisha lugha za Kiafrika vina walimu wa kudumu wa kufundisha lugha hizi. Ajabu ni kwamba kati ya vyuo hivi hakuna hata kimoja chenye programu iliyoanzishwa kwa ufadhili kutoka kwa serikali. Sababu ya tukio hili ni kwamba vyuo vilivyo na walimu wa kudumu vilianzisha programu zao bila kutegemea mfuko wa serikali na kwa hivyo vilitenga fedha kwa madhumuni ya kukuza programu zao. Hata hivyo walimu hawa huhitajika kufundisha masomo mengine katika nyanja zao za kitaaluma kama vile isimu au fasihi. Kwa sababu tathmini za kazi zao hutegemea sana masomo haya mengine, walimu hawa huzingatia masomo haya zaidi ya lugha katika utafiti wao.
Asilimia kubwa ya walimu wa Kiswahili huwa pia ni wanafunzi wa shahada za uzamili au uzamifu. Wengi wa wanafunzi hawa huwa wanaendelea na masomo yasiyohusiana na lugha ya Kiswahili au mbinu za ufundishaji wa lugha za kigeni. “Utaalamu” wa walimu hawa huwa ni ule wa kuisema lugha ya Kiswahili tu. Ingawa walimu hawa hujibidiisha kufanya kazi nzuri, huwa wanakumbwa na tatizo la kuishiwa na muda wa kujitayarisha kwa masomo yao wenyewe na kujitayarisha kwa masomo ya kufundisha. Na kana kwamba haya si matatizo ya kutosha, vyuo vingi haviwatambui wanafunzi hawa kama wafanyakazi wa chuo na kwa hivyo mishahara yao huwa duni na hawawezi kujiunga na vyama vya wawakilishi wa wafanyakazi vinavyoweza kuwatetea maslahi yao. Ingawa walimu hawa wanapewa jina la walimu wasaidizi, walimu ambao huwa wanastahili kuwasaidia huwa hawaingii madarasani haya mara nyingi (isipokuwa wakati wa ukaguzi wa kazi).
Kunao pia walimu wengine ambao huwa na shughuli zingine mijini na hupewa kazi ya kufundisha Kiswahili kwa malipo ya masaa hayo tu wanayofundisha. Walimu hawa huajiriwa kwa masaa kwa sababu labda chuo hakina pesa au hakitaki kutumia pesa katika programu ya lugha za Kiafrika, na huishia kuchukua hatua hii kwa sababu ya msukumo wa wanafunzi. Hatua hii inaweza kushusha hadhi ya lugha na masomo ya Kiafrika kwa jumla.
Wanafunzi wanaofundishwa na walimu ambao hawakuhitimu katika masomo yao huwa hawayazingatii sana masomo haya. Pia, kwa sababu ya uhaba katika ujuzi miongoni mwa walimu wasiofuzu, kuna uwezekano wa kuishia kufundisha vitu vilivyo rahisi kwao badala ya kuzingatia mahitaji ya wanafunzi na programu kwa jumla.
2. Rasilmali na Vifaa

Kwa jumla kuna uhaba wa rasilmali na vifaa vya kufundishia Kiswahili kama lugha ya kigeni. Vifaa vinavyotumiwa aghalabu huwa katika hali ya vitabu, kanda za kunasia sauti, kanda za video, visahani vya CD, na tovuti/mtandao. Kila kifaa cha kufundishia huwa kimetengenezwa kukidhi au kutosheleza mahitaji fulani. Kwa vile malengo ya wanafunzi wanaojisajilisha katika madarasa ya Kiswahili ni tofauti, kuna haja ya kuwa na vifaa tofauti ili kutosheleza mahitaji yao. Kwa mfano wanafuzi wa isimu hutaka masomo yapangwe kwa kuzingatia miundo ya sarufi. Wanafunzi ambao wangetaka kuzungumza zaidi huhitaji masomo yapangwe kwa njia ya mazungumzo ili waweze kushirikishwa sana katika mazungumzo. Kuna wanafunzi ambao hutaka kuwa na ufahamu zaidi wa utamaduni na kwa hivyo huhitaji mambo ya utamaduni yapenyezwa katika karibu kila somo. Vifaa vingine pia huzingatia mbinu za wanafunzi za kujifunza. Kuna wanafunzai ambao hutaka kuyatazama mambo kijumla, na wengine hutaka kutazama mambo kwa vipengele vyake. Mpaka sasa hakujatolewa kifaa kinachojisimamia chenyewe katika kutosheleza mahitaji ya mwalimu, wanafunzi, progamu na chuo. Vyuo vingine havina maabara ya lugha za kigeni. Walimu wengine hawana uzoefu wa kutumia vifaa vya kiteknolojia na huhiari kuendelea kutegemea ubao na chaki ilhali wanafunzi wangependelea vifaa vya kisasa kuhusishwa katika madarasa yao ya lugha.

Vitabu 
Katika mwaka wa kwanza kuna vitabu kadha vinavyotumiwa kufundishia Kiswahili kama lugha ya kigeni. Vitabu hivi ni Kiswahili:Msingi wa Kusema, Kusoma, na Kuandika cha Thomas Hinnebusch na Sarah Mirza; Kiswahili kwa Kitenda cha Sharifa Zawawi; Tujifunze Kiswahili cha John Mugane; Tuseme Kiswahili cha Senkoro miongoni mwa vingine. Kuna vitabu vingine lakini hivyo hutumiwa kama vya ziada na marejeleo. Vitabu tulivyotaja vimejaribu kuwasilisha lugha na utamaduni kwa njia mwafaka kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Vitabu hivi vimeanza kwa mambo ya kimsingi kwa kuzingatia kwamba watumizi wa vitabu hivi hawana ufahamu wowote wa maisha katika Afrika ya Mashariki (Biersteker and Bennett 1986). Mazungumzo, ufahamu, sarufi na mazoezi vinatosheleza mahitaji ya kiwango hiki. Udhaifu mkubwa wa vitabu vya mwaka wa kwanza ni kuegemea sana katika sarufi. Maoni ya mwandishi ni kwamba kwa vile waandishi wa vitabu hivi ni wanaisimu, walidhani wanafunzi wote wa Kiswahili ni wanaisimu au wana ujuzi wa isimu au wanastahili kuwa na ujuzi huo. Kwa mfano, kitabu cha Mugane kimejaa maelezo ya migao katika vitenzi na makubaliano ya irabu. Ingawa maelezo haya yanawafaa walimu na wanafunzi wa isimu au wanafunzi walio na elimu ya kiisimu, kwa wanafunzi wengi hizi ni habari za kuwapoteza zaidi. Udhaifu mwingine ni wa kutegemea michoro badala ya picha halisi. Picha halisi huonyesha jinsi kitu kilivyo na hali ilivyo katika uhalisi wake. Michoro inaweza kufikiriwa kama maoni ya mchoraji na ukweli wa mambo unaweza kutojitokeza katika michoro. Udhaifu huu unaonekana sana katika kitabu cha Hinnebusch na Mirza. Kitabu cha Senkoro kimeuepuka udhaifu huu kwa kutumia picha halisi. Hata hivyo kuna picha nyingi ambazo hazikuelezewa zinawakilisha nini na mpangilio wa masomo unakosa mtiririko. Baadhi ya masomo magumu yanakuja mapema mno. Katika mwaka wa pili, walimu huchukua mikondo tofauti. Katika kiwango hiki baadhi ya walimu huwatanguliza wanafunzi wao katika usomaji wa magazeti, vifungu vifupi au na hadithi fupi. Pia masomo mengi huwa yameegemea sana katika utamaduni. Baadhi ya masomo ambayo hufundishwa ni familia, malezi ya watoto, majukumu ya watu tofauti katika familia, masomo ya jadi na ya kisasa, siasa, bishara, uchumi, n.k. Hata hivyo hakuna vitabu vilivyoandikwa kuhitimisha mahitaji katika kiwango hiki. Miongoni mwa vitabu vinavyotumiwa ni: Tuimarishe Kiswahili Chetu na Kiswahili Lugha na Utamaduni vya Lioba Moshi; na Masomo ya Kisasa cha Ann Biersteker. Udhaifu mkubwa wa vitabu hivi ni ukosefu wa mazoezi ya kutosha kupima uwezo tofauti wa wanafunzi. Mengi ya mazoezi yaliyopo ni ya ufahamu. Katika mwaka wa tatu na wa nne (wanafunzi wanapopatikana) walimu huchukua mikondo tofauti kutegemea mahitaji ya wanafunzi. Mkondo mkuu ni wa kuwatanguliza fasihi pamoja na kuendelea na sarufi zaidi. Hata hivyo kumeanza kuzuka fikra kwamba sio wanafunzi wote wanaotaka ujuzi wa kuchambua fasihi. Badala ya kuchukua mkondo huu, mawazo ya kuhusisha taaluma nyingeinezo yameanza kusambazwa na kutekelezwa katika lugha zingine za kigeni.
Kanda za kunasia sauti, Filamu, Video, na Visahani vya CD, VCD na DVD
Matoleo ya kwanza ya Kiswahili: Msingi wa kusoma, kusema, na kuandika na Kiswahili kwa kitendo yaliambatana na kanda za kunasia sauti. Kila somo lilikuwa na ukanda wake. Kanda hizi hazikutoa mafunzo au mazoezi zaidi ya yale yaliyokuwa katika vitabuni vilivyohusika. Kuna kanda zingine zilizotayarishwa kwa madhumuni ya kujifunza Kiswahili, lakini hizi zimewalenga watalii. Kanda hizi zimetayarishwa na wafanyabiashara bila kuzingatia mbinu za kujifunza na kufundisha lugha ya kigeni. Kanda hizi huwa ni mkusanyiko wa vifungu vinavyofikiriwa na watayarishaji kwamba vitahitajika kwa mawasiliano ya kimsingi.
Kuna video chache zilizotengenezwa kwa madhumuni ya kufundishia Kiswahili. Kwa mfano: Kiswahili: Lugha na Utamaduni. Video hizi zilitayarishwa na Lioba Moshi wa chuo kikuu cha Georgia kupitia ufadhili wa Wizara ya Elimu ya Marekani. Video hizi zimelengewa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wa pili na huandamana na kitabu. Kwa jumla kuna video nane zenye masomo ishirini na nne. Mambo mbalimbali yamehusishwa katika video hizi. Kwa mwalimu ambaye hajui jinsi ya kutumia video kufundishia, atakuwa na kazi ngumu kwani hakukutolowa mazoezi katika video wala katika kitabu. Video zingine ziko katika lugha ya Kingereza, kwa mfano, The Africans: A tripple heritage za Ali Mazrui. Video hizi huweza kutazamwa na wanafunzi hujadili katika Kiswahili.
Kuna filamu kadhaa ambazo zinaweza kujumuishwa katika vifaa vya kufundishia. Filamu hizi ni kama Arusi ya Mariamu, Maangamizi, Tusamehe, na Bongoland 1 na 2. Filamu za kwanza mbili zimetumiwa kwa kiasi na walimu katiak viwango mbalimbali. Maoni ya wengi ni kwamba filamu hizi zinaweza kutumiwa kwa wanafunzi wa mwaka wa pili na ziadi.   
Kufikia sasa hakuna visahani vingi vya CD vya kufundishia Kiswahili. Kampuni ya Rosetta Stone imetoa kisahani kimoja cha Kiswahili. Mafunzo na mazoezi ya kisahili hiki yanategemea picha na sauti. Picha karibu zote zilizotumiwa zimepigwa Marekani na kwa hivyo hazitoi uhalisi wa mambo kama yalivyo katika Afrika ya Mashariki. Michezi mingi inayoingizwa na kuonyewha katika runinga za Afrika ya Mashariki (hasa Kenya na Tanzania) sasa inapatikana katika DVD na VCD. Shida ni kuwa baadhi ya visahani hivi haviwezi kuchaza moja kawa moja katika mitambo ya Marekani kawa sababu ya tofauti baina ya mitambo.
Mtandao 

Katika mtandao kuna mafunzo ya Kiswahili si haba yanayotolewa na makampuni, watu binafsi na shule. Kwa sababu ya mahimizo katika matumizi ya kompyuta, walimu wengi wamejibidiisha kuweka kazi zao kwenye mtandao. Wafanya biashara nao wamechukua nafasi ya kuweko kwa kifaa hiki kuenezea biashara zao. Matumizi ya mtandao yanaelekea kuwa na faida kwa sababu wanafunzi wanaweza kufanya kazi zao wakati wowote na mahali popote na kumpelekea mwalimu wao kwa barua pepe. Kwa kufanya hivyo pia inapunguza gharama ya karatasi. Mtandao pia umewawezesha wanafunzi na wapenzi wa Kiswahili kuweza kusema na kusikiliza habari na vipindi mbalimbali katika lugha ya Kiswahili kutoka maeneo mengi Kiswahili kinakotangazwa kama Ujerumani, Wingereza, Ujapani, Afrika-Kusini n.k. Shida iliyopo ni kwamba kurasa nyingi zilizoko kwenye mtandao zinahitaji kuhaririwa kwani zimejaa makosa hasa ya kisarufi. Hata hivyo kuna kurasa chache za mtandao ambazo zinafaa. Kurasa hizi ni kama KAMUSI (ya Ann Biersteker na Martin Benjamin), KIKO (ya Liomba Moshi na Alwiya Omar) na SALAMA (ya John Mugane) miongoni mwa zingine.
Licha ya kuwawezesha walimu na wanafunzi kutazama maneno kutoka Kiingereza hadi Kiswahili au kutoka Kiswahili hadi Kiinereza, KAMUSI huwa na nafasi ya mazungumzo na viungo vya mambo mbalimbali kama habari (kutoka nchi mbalimbali-Afrika na Ulaya), na maonyesho ya picha kutoka Afrika Mashariki. KAMUSI ina maneneo zaidi ya 50,000 na bado haijakamilika. KIKO ina visehemu vya video. Kwa hivyo wanafunzi wanaweza kuona vitendo vikifanyika na kusia sauti. Ukurasa huu pia unaweza kutumiwa na wanafunzi wa Kiswahili mahali popote. Ukurasa wa SALAMA huhitaji idhini kutoka kwa mtayarishi. Masomo ya mwaka wa kwanza na wa pili yamekamilika. Kuna picha na sauti pamoja na kamusi katika ukurasa huu.  
3. Ufadhili 
Kama tulivyoona hapo juu, Kiswahili (na lugha zingine za Kiafrika) hutegemea ufadhili kutoka kwa Wizara ya Elimu ya Marekani. Ufadhili huu huwa ni wa kushindaniwa baina ya vyuo mabalimbali. Kila baada ya miaka minne wanaohusika hupeleka maombi yao. Wanaokosa hulazimika kusubiri mpaka baada ya miaka minne. Vyuo vingi huona ugumu au hukataa kuchukua masomo haya kwa sababu ya gharama, na pia baadhi ya viongozi hawaoni faida ya masomo haya kwa Wamarekani na kwa hivyo huyapinga sana. Hata pale msaada unapotolewa huwa hautoshi kukidhia mahitaji ya usimamizi, ufundishaji, na utengenezaji wa vifaa vya kufundishia lugha hizi. Kuna vyuo kadha ambavyo vimejitahidi kuimarisha programu za lugha za Kiafrika. Baadhi ya vyuo hivi ni Yale, Harvard, UCLA, Chuo kiuu cha Indiana (Bloomington), Chuo kiuu cha Georgia (Athens), Michigan State, na Chuo kiku cha Illinois (Urbana Champaign) miongoni mwa vingine.
4. Uhaba wa Wanafunzi
Siku hizi mambo mengi yanafasiriwa kiuchumi. Kwa sababu ya gharama ya elimu wanafunzi hutaka kujua faida ya kujifunza Kiswahili. Kwa vile Kiswahili hakitumiki kama lugha ya kufundishia elimu ya juu (kama vile Kiingereza, Kifaransa, n.k), huonekana kama lugha duni na ambayo matumizi yake si ya kimsingi katika kiwango cha taaluma za juu. Mradi katika Afrika lugha za kigeni zimepewa kipaumbele, itaendelea kuwa vigumu kukiendeleza Kiswahili kama lugha ya kigeni. Uhaba wa wanafunzi pia huathiri kiasi cha usaidizi unaotolewa na vyuo. Kila mwisho wa mwaka, takwimu za idadi ya wanafunzi waliojisajilisha madarasani huhitajika na madarasa ambayo huwa na wanafunzi wachache huwa na tisho la kufungwa. Ni muhimu kukumbuka kuwa wanfunzi huwa na uwanja mkubwa wa kuchagua ni lugha ipi wajifunze. Pana haja ya kubadilisha sera za lugha barani Afrika ili kuzipa lugha zetu umuhimi zaidi. Kuzikuza huko na kuzipa hadhi ndiko kutazifanya zitambulike na kuwavutia wanafunzi wengi.

5. Maabara 
Ingawa vyuo vingi vina maabara za kompyuta, ni vyuo vichache vilivyo na maabara iliyotengwa kwa maksudi ya lugha za Kiafrika. Mpaka sasa ni Chuo Kikuu cha Wisconsin- Madison na Chuo Kikuu cha Georgia vilivyo na maabara ya lugha za Kiafrika. Vyuo vingine huwa na maabara ya lugha za kigeni na uhitaji huzidi nafasi zilizomo kwa sababu ya wingi wa lugha za kigeni zinazofundishwa. Pia baadhi ya vyuo huwa na wakati maalum wa kufundisha lugha za kigeni. Kwa mfano katika Chuo Kikuu cha Yale madarasa yote ya mwaka wa kwanza ya lugha za kigeni hukutana saa tatu na nusu asubuhi Jumatatu mpaka Ijumaa. Kwa hivyo ili kupata nafasi ya kutumia maabara ni lazima kutuma maombi mapema.
Tatizo lingine ni uhaba wa programu za kompyuta za Kiswahili. Kwa mfano mpaka sasa hakuna programu ya kusahihisha tahajia ya Kiswahili na uakifishaji (punctuation). Baadhi ya vifaa  vya  kufundishia  Kiswahili  kwa  kompyuta  vilivyoko  vimetengenezwa  na wafanyabiashara na nyingi hazifai kwa matumizi ya darasani. Hata kule kuliko na mitambo ya kompyuta, walimu wengi bado wanahitaji mafunzo na uzoefu wa matumizi ya vifaa hivi. Kama vile ni vigumu kwa kipofu kumwongoza kipofu mwingine njia, mwalimu asiye na welendi wa matumizi ya kompyuta hawezi kuwafundisha wanafunzi kwa kutumia kifaa kile.

Mapendekezo ya Suluhisho kwa baadhi ya Matatitzo/Vikwamizi
Kuwa na walimu waliofuzu na wa kudumu kunaweza kusaidia kukua kwa programu kwa njia mbalimbali. Kwanza kunaweza kuwavutia wanafunzi katika madarasa ya lugha za Kiafrika (ya Kiswahili ikiwemo). Wanafunzi wengi wa vyuo Marekani hujua zaidi kuhusu masomo na hasa ya lugha kupitia kwa wanafunzi wengine. Katika utafiti mdogo uliofanywa na mwandishi wa makala hii, wanafunzi walipoulizwa jinsi walivyojua kuhusu lugha ya Kiswahili, wengi (asilimia 60) walisema ni kupitia kwa wanafunzi wengine (Wa’Njogu 2001 na 2005). Kwa sababu ya mafunzo na ujuzi mwalimu aliyefuzu atakuwa na mbinu za kuwavutia na kuwahamasisha wanafunzi na hivyo kuongeza idadi. Walimu waliohitimu na wa kudumu wataipa programu sifa kutokana na kushiriki kwao katika kongamano mbalimbali za taifa na kimataifa. Walimu hawa pia wanaweza kupelekea kushawishika kwa vyuo kugharamia programu za lugha za Kiafrika, na hapo kuondoa kutegemea Wizara ya Elimu.
Ingawa kuna vitabu na vifaa vichache, bado kuna haja ya kuendelea kutayarisha zaidi. Vitabu vinavyotumiwa madarasani havitoshelezi mahitaji ya chuo, programu, walimu na wanafunzi. Kuna haja ya kuchapisha vitabu zaidi vya marejeleo vinavyoelezea dhana na vipengele tofauti vya lugha na utamaduni. Kitabu kilichochapishwa na NALRC (National  African Language Resource center) cha marejeo ni mwanzo mzuri lakini kina udhaifu wake. Kamusi pia zilizoko Marekani, kwa mfano ya Awde, haziwafai sana wanafunzi kwa sababu hazionyeshi matumizi ya maneno. Wanafunzi huvunjika moyo wanapokosa neno fulani katika kamusi, au wakiona maneno yana maana nyingi na hawakutolewa mifano ya matumizi. Kamusi zinazochapishwa na TUKI (Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili) zingefaa sana, lakini mara nyingi hazifiki Marekani na zikifika huwa ghali mno. Wanafunzi walio na bahati ya kufika Kenya au Tanzania huhiari kuzinunua huko. Kamusi ilioko kwenye mtandao (Swahili  Internet Living Dictionary), bado haijakamilika na jitihada bado zinafanywa za kutafuta wafadhili ili mradi huo ukamilishwe.
Kwa vile siku hizi wanafunzi wana kompyuta zao, na madarasa mengi ya kisasa yana huduma za mtandao, itakuwa rahisi kuwahimiza wanafunzi kuzileta kompyuta zao madarasani na kutumia. Pana haja kubwa kwa walimu wa Kiswahili kushirikiana na wataalamu wa mitambo ya kompyuta ili wapangiwe warsha za mara kwa mara na kutolewa mafunzo ya matumizi ya vifaa hivi.
Hitimisho 
Umuhimu wa lugha ya Kiswahili katika elimu ya Marekani hauwezi kudunishwa. Hata hivyo pana haja ya kujitolea zaidi kwa viongozi wa vyuo na taasisi za elimu ya juu katika kuzifadhili programu za lugha hii. Waalimu wa lugha ya Kiswahili (popote walipo) wanastahili kuonyesha umuhimu wa lugha hii kwa wanafunzi wa kigeni. Tusipojitolea katika kuikuza lugha hii na kuipa hadhi barani Afrika, itaendelea kuwa vigumu kuvishawishi vyuo kuendelea kuifundhisha. Kuna haja ya kuwa na usawazishaji wa malengo na shabaha ya mafunzo ya lugha hii. Mambo yalivyo sasa wanafunzi hufundishwa vitu tofauti hata wakiwa katika viwango sawa. Tofauti hii inafanya vigumu kwa wanafunzi wanaohama kutoka chuo kimoja hadi kingine kuendelea na programu ya Kiswahili.
Vifaa vyenye picha na sauti, kama vile kanda za video na visahani vya CD, VCD na DVD, hutoa nafasi na kukuza uwezo wa kufikiri na ubunifu miongoni mwa wanafunzi. Vifaa hivi pia huonyesha mazingira katika uhalisi wake. Zaidi ya kufundishia lugha, vifaa hivi huwa njia rahisi ya kufundishia vipengele tofauti vya utamaduni. Aidha vifaa hivi hutoa nafasi nzuri ya mjadala katika lugha husika kutegemea fasiri za wanafunzi. Kwa hivyo pana haja ya kuendelea kutengeneza vifaa vinavyochukua mwelekeo huu.
Ingawa lugha ya Kiswahili si mojawapo wa lugha kuu za kigeni zinazofundishwa Marekani, si sababu ya kubakia nyuma kitekinolojia. Wengi wa wanafunzi wanaojisajilisha katika madarasa ya Kiswahili huwa wamejifunza lugha nyingine ya kigeni (vyuoni au katika shule za sekondari (Wa_Nogu 2001 na 2005) na huwa wameona vifaa vya tekinolojia vinavyotumiwa na hutarajia lugha zetu nazo ziwe zimejikakamua kwa kiasi fulani katika uwanja huu. Pia masomo mengi sasa yanahusisha matumizi ya tekinolojia, na kwa hivyo Kiswahili ni lazima kijiunge na mkondo huu kama kinataka kushindania wanafunzi na masomo mengine na kushindania nafasi katika lugha kuu ulimwenguni. Ingawa lugha ya Kiswahili (na lugha zingine za Kiafrika) inakabiliwa na shida mbalimbali, kuna uwezekano wa kukikuza na kuwa somo linalojisimamia. Kinachohitajika ni ushirikiano mkubwa mingoni mwa walimu na vyuo Marekani, Ulaya na katika Afrika katika jitihada za kulikuza somo hili.

 
 
Marejeleo 

Awde, N. 2004. Swahili-English & English-Swahili. New York, New York: Hippocrene Books.

Batibo, H.M. 2003. The teaching of Kiswahili as a Foreign Language in Africa: A Case of Study from Eastern and Southern Africa. Journal of the African Language Teachers Association, 3:19-34.

Biersteker, A. and Bennett, P. 1986. On Categorizing Language Courses: Reconciling Language Characteristics and Performance Expectations. The Design and Evaluation of African Language Learning Materials. Proceedings of the Spring 1984 Conference on Developing Guidelines for the Evaluation of African Language Learning Materials, East Lansing, Michigan, April 13-14, 1984, imehaririwa na D. J. Dwyer. East Lansing, MI: Michigan State University. (Microfiche).

Biersteker, A. (22005). Masomo ya Kisasa: Contemporary Readings in Kiswahili. Trenton,NJ: Africa World Press

Bokamba, E.G. 2002. African Language Program Development and Admininstration: A History and Guidelines for Future Programs. Madison, WI: NALRC Press.

Folarin-Schleicher, A. & L. Moshi. 2000. The Pedagogy of African Languages: An Emerging Field. Columbus: The National East Asian Languages Resource Centre, Ohio State
University & Madison: The National African Language Resource Centre, University of Wisconsin-Madison.

Gardner, R.C. 1996. Motivation and L2 Acquisition: Perspectives. Canadian Journal of Psychology, 13: 266-172.

Hinnebusch, T. & Mirza, S. 1998. Kiswahili: Msingi wa Kusoma, Kusema na Kuandika. Lanham, MD: University Press of America.

Mazrui, A. M. 1997. The Future of African languages in the American Academy. Prism, 3, 1:Uk. 1-3.

Moshi, L.J. 1988. Tuimarishe Kiswahili Chetu. Lanham, MD: University Press of America.

Moshi, L.J. 1998. Kiswahili Language and Culture. Kensington, MD: Dunwood.

Mugane, J.M. 1999. Tujifunze Kiswahili. Athens, OH: Aramati Digital Technologies Publications.

Odlin, T. 1989. Language transfer: Crosslinguistic Influence in Language Learning. Cambridge, NY: Cambridge University Press.

Sanneh, S. & A. Omar. 2002. African Language Study in the 21st Century: Expansion through Collaboration and Technology. Unpublished paper presented at the 45th ASA Annual Conference, Washington, DC. December 05.08.2002.

Senkoro, F.E.M.K. 2003. Tuseme Kiswahili: A Multidimentional Approach to the Teaching and Learning of Swahili as a Foreign Language. Madison, WI: NALRC Press.

Wa_Njogu, J.K. 2001. A Descriptive Study of Motivation, Ethnicity, Gender, and Achieve-ment in Kiswahili as a Foreign Language in a College Setting: Students’ Perspectives. Unpublished Ph.D Dissertation, Ohio State University, Columbus.

Wa_Njogu, J.K. 2005. Motivation, Ethnicityy, and Gender versus Achievement in Kiswahili as a Foreign Language in a College Setting: A Correlational Study. Journal of the African Language Teachers Association, 6: 45-66.

Zawawi, S. 1988. Kiswahili kwa Kitendo. Trenton, NJ: Africa World Press.

Filamu 

Kibira, J. 2003. Bongoland. Dar es Salaam: Kibira Films International.

Kibira, J. 2006. Tusamehe. Dar es Salaam: Kibira Films International.

Kibira, J. 2007. Bongoland II. Dar es Salaam: Kibira Films International.

Mazrui, A. The Africans: A Triple Heritage. Washington, D.C.: Annenberg/CPB Project.

Mulvihill, R. & M. Mhando. 2000. Maangamizi. Encino, CA: Gris-Gris Films.

Nangayoma, N. & Mulvihill, R. 1983. Arusi ya Mariamu. Encino, CA: Gris-Gris Films.
Kurasa za Mtandao
Mugane, J. 2007. Salama. http://www.aramati.org/ (Tarehe 2, mwezi wa Januari, 2009).
Moshi, L. & A. Omar. 2000. Kiswahili kwa Kompyuta (KIKO). African Studies Institute, University of Georgia, Athens. http://africa.uga.edu/Kiswahili/doe/ (Tarehe 2, mwezi wa Januari, 2009).
Benjamin, M. &, A. Biersteker. 1994. The Kamusi Project. http://www.kamusiproject.org/ (Tarehe 2, mwezi wa Januari, 2009).
Visahani vya CD
The Rosetta Stone. 2007. The Rosetta Stone V2. Swahili Level 1. CD-ROM. Arlington: Ro- setta Stone Ltd.
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T15:38:28Z 2021-06-26T15:38:28Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=306 <![CDATA[WHY STUDY SWAHILI?]]> Information provided by: 
National African Language Resource Center (NALRC) 
A). Why study Swahili?
Swahili (or Kiswahili as it is called when one is speaking the language) is the most important and widely studied indigenous language of Africa, the National and official language of Kenya and Tanzania. It is spoken as a native language on the East coast of Africa and the islands adjacent to the coast from Southern Somalia in the north down through the Kenyan and Tanzanian coasts.
It is also a Lingua franca of the African Continent spoken as a second language by millions of people mainly in Kenya, Tanzania, Uganda, and East Zaire. There are also speakers in Mozambique, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, Southern Arabian countries such as Yemen and Oman, as well as other parts of the world.
It is aired in radio broadcasts such as the British Broadcast Corporation, Voice of America, and Deutsche Welle. It is heard in songs of famous singers such as Miriam Makeba and in popular films like the Lion King. African-Americans refer to their annual cultural festival as Kwanzaa, which is derived from the Swahili word kwanza or ‘first.’ Swahili is taught in academic institutions from Japan in the East to Mexico in the west. It can be used to fulfill language requirements. The study of Swahili also provides interesting issues regarding language policies and language planning. Whatever the area of research one is in, be it linguistics, anthropology, geography, archaeology, or even sociology, knowledge of Swahili and its many varieties is essential if one is working in the East African region. There are many benefits of knowing the Swahili language, including the fact that it serves as a good vehicle to accessing Swahili culture. Swahili has a long written tradition and remarkable history. Finally, knowing Swahili enhances the credibility of researchers interested in East Africa.
B). Who speaks Swahili?
People and History 
Over 50 million people in eastern and central African speak Swahili. It is widely used in Kenya, Tanzania and Uganda. A little over one million people speak it as their first language. Most others speak Swahili fluently as a second, third or fourth language. Those who speak it as a first language are found along the coast of east Africa stretching from southern Somalia to the border between Tanzania and Mozambique. There are also many native Swahili speakers on the Indian Ocean islands of Unguja and Pemba (which together make up Zanzibar), Lamu, the Comoro Islands and the northwestern part of Madagascar. Many Swahili speakers like to refer to themselves in terms of where they come from. So Swahili speakers from Unguja, for example, will refer to themselves as Waunguja or Wazanzibari, those from Kenya as Wakenya and those from Tanzania as Watanzania.
The East African coast was visited by Arabs and Persians as early as the second century A.D. These visitors settled in Africa and married local people. Many local people modified and adopted the visitors’ traditions. On the island of Unguja, for example, the traditional New Year, Mwaka Kogwa, is celebrated during the month of June. This celebration is similar to the Persian New Year of Neiruz. Later visits by Arabs to the area also introduced the Islamic religion, and today many Swahili speakers throughout East Africa are Muslim. Travelers from Portugal, Germany, England and various Asian countries also went to East Africa. Each group left its mark on both the culture and the language. Lame as a center of Swahili Language and Cultures, would be a place of interest to students.
C). Language and Culture
Swahili is a Bantu language of the Niger-Congo family and has a typical, complicated Bantu structure. For example, Swahili utilizes over 13 noun classes, the equivalence of a romance language having 13 genders. Three full noun classes are devoted to different aspects of space and time. Swahili represents an African World view quite different from that of a European language.
 Nouns are grouped into different classes according to their meaning. Human beings, for example, belong to one class: mtu ‘person’/watu ‘people.’ Trees, on the other hand, belong to another class: mti ‘tree’/miti ‘trees’. Diminutive and augmentative meanings are also expressed using the noun class system. The following forms of the word ndege ‘bird’ indicate different sizes: ndege (regular size bird); kidege (small bird); dege (big bird).
 The word Kiswahili is a general term for many varieties of the language spoken along the East African coast. It comes from the Arabic word sahel, meaning ‘coast.’ Kiis a prefix referring to language. In some varieties of Swahili, the language prefix appears as chi-, as in Chimiini, which is spoken in Somalia, or shi-, as in Shingazija, a variant spoken on the Ngazija island of Comoro. Swahili language has been influences by a variety of other language, including Arabic, Portuguese and German. There are many Swahili words with foreign origins, including the following: sita ‘six’ (Arabic), saba ‘seven’ (Arabic), shule ‘school’ (German), bendera ‘flag’ (Portuguese), kitabu ‘book’ (Arabic) and pesa ‘money’ (Hindi). All Swahili speakers share a unique way of expressing time, day or night. Sunrise or sunset are the two focal points used to tell time. The first hour of the day, therefore, comes after sunrise, not after midnight, and the first hour of the night comes after sunset. Also unique to Swahili speakers is the way they communicate with each other indirectly by use of the popular language, also known as leso. This multi-purpose cloth usually has a caption that conveys a proverbial message to its target audience. Lamu is an ancient Swahili city-state in the Indian Ocean off the north coast of Kenya. It is the main town to the traditional swahilini–the original crucible of Swahili culture. In December 2001, UNESCO granted World heritage status to Lamu’s Old town citing the fact that the old town had retained its traditional functions for over 1000 years.
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T15:34:15Z 2021-06-26T15:34:15Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=305 <![CDATA[MBINU ZA UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI]]>
.pdf   UFUNDISHAJI KISWAHILI KWA WAGENI.pdf (Size: 243.87 KB / Downloads: 5) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T15:25:51Z 2021-06-26T15:25:51Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=304 <![CDATA[LEARN KISWAHILI / JIFUNZE KISWAHILI]]>
.pdf   LEARN SWAHILI.pdf (Size: 98.08 KB / Downloads: 9) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T15:16:58Z 2021-06-26T15:16:58Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=303 <![CDATA[LEARN SWAHILI/JIFUNZE KISWAHILI : LESSON 1: CLASSROOM INSTRUCTIONS]]> Lesson 1: Classroom Instructions
rudia……. repeat
mwalimu….. teacher
profesa …….professor
mwanafunzi …….student
jibu ………..answer; respond
uliza ………ask
unaelewa? ………….do you understand?
mnaelewa? ……………do you all understand?
ndiyo …………………yes
la; hapana ………..no
swali ………………question
mna swali? …………….does anyone have a question?
mwalimu, nina swali………….. teacher, I have a question
sielewi ………………..I do not understand
sikiliza ……………………listen (s. command)
sikilizeni………………. listen (pl. command)
simama ………………..stand
tafadhali, simama…………… please, stand
keti; kaa ………………….sit
tafadhali, keti/kaa ……………..please, sit down
kusanya …………………..collect
karatasi…………………. paper
tafadhali, kusanya karatasi…………. please, collect the papers
leta …………………….bring
tafadhali, leta karatasi …………………please, bring the papers
enda ……………….go
tafadhali, enda …………………please, go
tazama……………………. look
funga kitabu………………….. close the book
fungua kitabu…………………. open the book
tafadhali ……………………..please
tafadhali rudia…………….. please repeat
tafadhali, fungua kitabu …………….please, open the book
tafadhali, nyamaza ……………….please, be quiet (sing.)
tafadhali, nyamazeni ………………..please, be quiet (pl.)
tafadhali, ongea/zungumza/sema katika ……..Kiingereza please, speak in English
tafadhali, jibu katika/kwa Kiswahili………… please, respond in Kiwahili
tafadhali, ongea/zungumza/sema katika Kiswahili ……….please, speak in Kiwahili
polepole……………….. slowly
tafadhali, ongea/zungumza/sema polepole…………….. please, speak slowly
taja ……………mention.
tamka …………pronounce
soma …………..read; study
andika ………..write
Classroom Instructions ………………[maagizo ya darasani]

andika kwa Kiswahili…………………… write in Kiwahili
tafadhali soma……………… please read
kumbuka……………………… remember (sing.)
mnakumbuka ………………..remember (pl.)
jaribu………………………… try
tena ……………………again
jaribu tena……………. try again
tafadhali jaribu ………..please try
karibu ………………..elcome
tafadhali fungua mlango …………please open the door
tafadhali funga mlango…………. please close the door
tafadhali kaa/keti………………. please sit (sing.)
“Crying” ni nini kwa Kiswahili? ……….What is “crying” in Kiwahili?
tafsiri…………………. translate
chemsha bongo ……………….brain teaser
sijui………………. I do not know
kwaheri…………… bye
kwaheri, tutaonana kesho…………… goodbye, hope to see you tomorrow
kwaheri, tutaonana baadaye…………… goodbye, hope to see you later
asante…………. thank you
asante sana……………… thank you very much
njoo ………………….come
tafadhali, njoo…………… please, come
samahani ………………pardon; excuse me
samahani, mwalimu, nina swali…………… excuse me, teacher, I have a question
haraka ……………fast
tafadhali, ongea/zumgumza/sema haraka haraka ……………please, speak quicker
vizuri …………………good
vizuri sana ……………very good
Wewe ni mzuri. …………..You are good.
Wewe ni mbaya. ……………You are bad.
kazi nzuri ………………….good work
kazi ya nyumbani ……….homework
Leo tutasoma ………………..Today we will learn _____.
Jana tulisoma nini? …………..What did we learn/study yesterday?
Leo tumesoma nini? …………What have we learned/studied today?

]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T15:11:35Z 2021-06-26T15:11:35Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=302 <![CDATA[LEARN SWAHILI/JIFUNZE KISWAHILI : LESSON 2 : GREETINGS/MAAMKIZI]]> Lesson 2a:
Greetings

Greetings [maamkizi; salamu]
There are at least five ways of greeting in Kiswahili:
A). Habari gani?
B). Hujambo?
C). U hali gani?
D). Shikamoo.
E). Mambo? / Vipi?
A). Habari gani?
Example 1 ‐ Two people greeting each other
Person A: Habari gani?
Person B: Nzuri!
Sentensi:
a). Nzuri / njema / salama / safi / sawa / poa.
[Good / nice / peaceful / clean / fine / cool.]
b). Nzuri / njema / salama / safi / sawa / poa sana…
[Very good / nice / peaceful / clean / fine / cool.]
c). Nzuri / njema / salama / safi / sawa / poa tu…
[Just good / nice / peaceful / clean / fine /
C). U hali gani?
Example 1 ‐ Two people greeting each other Example 2 ‐ One person greeting many people
Person A: U hali gani? Person A: M hali gani?
Person B: Njema. Persons B, C, & D: Salama.
Sentensi:
1. U hali gani? / M hali gani? What’s your condition? / How are you?]
a). Nzuri / njema / salama / safi / sawa / poa.
[Good / nice / peaceful / clean / fine / cool.]
b). Nzuri / njema / salama / safi / sawa / poa sana…
[Very good / nice / peaceful / clean / fine / cool.]
c).  Nzuri / njema / salama / safi / sawa / poa tu…
[Just good / nice / peaceful / clean / fine / just cool.]
D.) Shikamoo.
Example 1 ‐ A youth greeting an elder person
Youth: Shikamoo.
Elder Person: Marahaba.
Sentensi:
Shikamoo. [I touch your feet.]
Marahaba. [I am delighted.]

E). Vipi? / Mambo?
Example 1 ‐ A youth greeting another youth
Example 2 ‐ A youth greeting another
youth
Youth A: Vipi? Youth A: Mambo?
Youth B: Poa. Youth B: Safi.
Sentensi:
Vipi? / Mambo? [What’s up?]
Poa / Safi / Sawa. [Cool / Clean / Fine.]

1. Hodi!
[Requests permission to enter a
house.]
2.Karibu! [Welcome!]
3.Karibu ndani! [Welcome inside!]
4.Asante. [Thank you.]
5.Asante sana. [Thank you very much.]
6.Kwaheri. [Be blessed. / Goodbye.]
7.Tutaonana baadaye.
8.Habari za asubuhi/
mchana/jioni/usiku?
9.Habari za
mama/baba/kaka/dada/
ndugu/mjomba
[We will see each other later.]
[How is the news of the
morning/afternoon/evening/night?]
[How is the news of
mother/father/brother/sister/
comrade/uncle]
10.Habari za
nyumbani/shuleni/chuoni/
masomo/Amerika
[How is the news at
home/at school/at college/
studies/America]

NAMNA NYINGINE ZA MAWASILIANO
Mifano:
Waambaje?           [How are you doing?]
Salaamaleikum.    [Peace be upon you.]
Upo?                       [Are you there?]
Lala salama.         [Sleep peacefully.]
Tuonane kesho.   [See you tomorrow.]
Ndoto njema.        [Dream well.]
Lala unono.            [Sleep comfortably.]
Usiku mwema.      [Good night.]
Usingizi mwema.  [Sleep well.]
Habari za kutwa?  [How was your day?]
Jioni njema.           [Good Evening]
Uende salama       [Go with peace.]
Sina la kuamba.  [I have nothing to say.]
Aleikumsalaam.  [And also with you.]
Nipo.                     [I am here.]
Nawe pia.             [And you also.]
Inshallah.              [God willing.]
Za mafanikio.       [Of success.]
Nawe pia.             [And you also.]
Wa buraha.          [With tranquility.]
Wa buraha.          [With tranquility.]
Njema/Nzuri.       [Good.]
Salama!                 [Peaceful!]
Tuonane inshallah! [We will see each
.                                 other God willing]

]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T15:05:52Z 2021-06-26T15:05:52Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=301 <![CDATA[LEARN SWAHILI: MSAMIATI WA DARASANI/CLASSROOM VOCABULARY]]> A). Vocabulary
mlango / milango …………..[door/ doors]
dirisha / madirisha………… [window / windows]
taa / taa …………………………[light / lights]
ubao / mbao…………………. [board / boards]
kompyuta / kompyuta …….[computer / computers]
kiti / viti ………………………..[chair / chairs]
meza / meza ………………….[table / tables]
kalamu / kalamu………….. [pen / pens]
penseli / penseli…………… [pencil / pencils]
mkoba / mikoba…………… [bag for books / bags for books]
mfuko / mifuko……………. [bag of books / bags of books]
kitabu / vitabu ……………..[book / books]
daftari / madaftari ……….[notebook / notebooks]
kabati / makabati……….. [cupboard / cupboards]
rula / rula…………………. [ruler / rulers]
ufutio / futio ………………[eraser / erasers]
wino / wino ……………….[ink / inks]
ukuta / kuta……………… [wall / walls]
sakafu / sakafu …………..[floor / floors]
dari / dari…………………. [ceiling / ceilings]
paa / paa …………………..[roof / roofs]
simu / simu……………… [telephone / telephones]
karatasi / karatasi ……..[paper / papers]
jaa / jaa ……………………[litter bin / litter bins]
chaki / chaki ……………[chalk / chalks]
zulia / mazulia………… [carpet / carpets]
swichi ……………………..[switch].
swichi ya feni ………….[fan switch]
swichi ya taa………….. [light switch]
mwanafunzi / wanafunzi ……[student / students]

mwalimu / walimu…………[teacher / teachers]
kalenda/kalenda…………….[calendar / calendars]
saa / saa……………………….[clock / clocks]
saa ya ukuta………………….[wall clock]
ramani / ramani……………[map / maps]
kiyoyozi / viyoyozi……….[air conditioner / air conditioners]
picha / picha……………..[picture / pictures]
mchoro / michoro…….[drawing / drawings]
pazia / mapazia……….[curtain / curtains]
runinga/televisheni…[television / televisions]
video/video……………

kengele / kengele…….[bell / bells]
chati / jedwali……..[chart / charts]
rejesta / rejesta…….[register / registers]
bendera / bendera…….[flag / flags]
bendera ya taifa……….[national flag]
mlinzi / bawabu / walinzi….[security / security]
saa / saa……………..[clock / clocks]
saa ya ukuta………..[wall clock]
chati / jedwali……..[chart / charts]
ramani / ramani……[map / maps]
kalenda / kalenda….[calendar]
majilisi / masjala / ofisi……[office / staff room]
picha / picha………..[picture/ pictures]
deski / dawati………[desk]
gazeti / magazeti….[newspaper / newspapers]
jarida / majarida……[journal / periodical]
habari / habari………[news]
barua / barua………..[letter / letters]
makala / makala…..[article / articles]
insha / insha……….[essay / essays]
kumbukumbu / kumbukumbu…..[record / records]
kabrasha / ripoti maalum……..[pamphlet / meeting documents]

Question Formation
Mifano:
1. Darasa hili lina vitu gani?

[What things does this classroom have?]
Darasa hili lina meza, mkoba, chaki, ubao…
[This classroom has a table, backpack, chalk, board…]
2. Hii ni nini?
[What is this?]
Hii ni meza. [This is a table.]
3. Huu ni nini?
[What is this? (referring to wall)]
Huu ni ukuta. [This is a wall.]
4. (Wewe) Hupendi mapambo gani?
[Which decorations don’t you like?]
(Mimi) Sipendi ________. [I don’t like __________.]

]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T14:59:32Z 2021-06-26T14:59:32Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=300 <![CDATA[WATU MBALIMBALI/ VARIOUS PERSONALITIES]]> Various Personalities [watu mbalimbali]
A). Various Personalities
daktari [doctor]
daktari wa meno [dentist]
daktari wa macho
mhunzi [blacksmith]
mjenzi [construction worker]
mkalimani [interpreter]
mkulima [farmer]
mnajimu [astrologist]
mpishi [cook]
mshairi [poet]
mtafiti [researcher]
mvuvi [fisherman]
mwaguzi [dream interpreter]
mwalimu [teacher]
mhadhiri [lecturer; instructor]
ustadh; ustadhi [professor]
profesa [professor]
padre; kasisi [clergy]
sheha [imam (Islamic leader)]
mpelelezi; jasusi [spy; detective; investigator]
ofisa wa polisi; askari; polisi [police officer]
mekanika [mechanic]
nahodha [sea captain]
nahodha wa meli [ship crewman]
mwashi [mason]
rubani [pilot]
seremala [carpenter]
sonara [jeweler]
mchimba madini [miner]
tabibu [healer; physician]
mchuuzi [retailer]
mfanyakazi; mtumishi [worker]
mhandisi [engineer]
mhariri [editor]
tarishi; mjumbe [postman; messenger]
sogora [drummer]
msajili [registrar]
msusi [hairbraider; beautician]
msasi [hunter]
mlanguzi [smuggler]
mlanguzi wa madawa [drug dealer]
mshenga [matchmaker]
naibu [deputy; assistant; acting officer]
baharia [sailor]
utingo; tanboi [luggage manager]
mbunge [MP; Senator]
diwani [council person]
topasi [janitor]
saisi [one who takes care of horses]
rais; raisi [president]
gavana [governor]
mwakilishi [representative; congress person]
waziri [minister; cabinet secretary]
waziri wa afya [Minister/Secretary of Health]
meya [mayor]
mfalme [king]
malkia [queen]
mganga [healer; physician]
maskini; fukara [poor person]
mwadhini [muezzin]
jumbe [village elder; chief; headman]
mpagazi; mchukuzi; hamali [carrier; porter]
kiranja [student leader]
mshona viatu [cobbler]
dalali [auctioneer]
jemadari [commander in chief; chief of staff]
uledi [cabin boy]
liwali [administrative official; headman]
mwenyekiti [chairman; chairperson]
katibu wa chama [secretary of the association]
mwanachama [member]
mwekahazina [treasurer]
nokoa [farm manager]
yaya [nanny]
kuli [dockworker]
somo [confidante; intimate friend]
mhasibu [accountant]
mtemakuni [firewood fetcher]
mpigaramli [fortune teller]
mtumishi [servant; waiter; worker; laborer]
mkutubi [librarian]
shaibu [old man]
ajuza [old woman]
kikongwe; mzee [old person]
kingori [young man]
mtanashati [teenage boy]
mume; mwanamume; janadume [man]
mwari [young woman]
mwanamwali [teenage girl]
mke; mwanamke; janajike [woman]
tajiri; mkwasi [rich person]
mchawi [witch]
mkuu wa chuo; rais wa chuo [university president]
mwenyekiti idara [head of department]
mkuu wa kitivo [dean]
ofisa wa chuo
mpakaji rangi
muuzaji
mwongo; mlaghai
mjinga
mnafiki
mfitini
msaliti
[university official]
[painter]
[salesperson]
[liar]
[stupid]
[pretender; liar]
[inciter]
[traitor]

B). Personalities that begin with mwana‐ 
Zingatia: mwana [child].
mwanamuziki [musician]
mwanasayansi [scientist]
mwanaanga
mwanahewa
[astronaut]
mwanahisabati
mwanahesabu
[mathematician]
mwanamitindo [fashion designer]
mwanamichezo [sportsman/sportswoman]
mwanasanaa [artist]
mwanamaji [marine]
mwanajeshi [soldier]
mwanaisimu [linguist]
mwanahistoria [historian]
mwanahewa
mwanaanga
[air force]
mwanabayolojia [biologist]
mwanaanthropolojia [anthropologist]
mwanasheria [lawyer]
mwanasiasa [politician]
Zingatia [note]
fanya [do]
sijui [I do not know]
si [is not]
sina
kazi
taka
inategemea
gani
ungependa
ungetaka
[I do not have]
[work/employment]
[want]
[it depends]
[which]
[you would like]
[you would want]

]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-26T14:54:41Z 2021-06-26T14:54:41Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=299 <![CDATA[Modifiers ‐INGI and ‐INGINE]]> Sentensi:
1. Vitabu vingi vimenunuliwa. [Many books have been bought.]
2. Miti mingi itapandwa kesho. [Many trees will be planted tomorrow.]
3. Pahali pengi pameharibika. [A lot of places have been damaged.]
4. Nina rafiki wengi. [I have many friends.]
5. Nilinunua kalamu nyingi. [I bought many pens.]
6. Nina vitabu vingi vya Kiswahili. [I have many Kiswahili books.]
7. Nimepoteza madaftari mengi. [I have lost many notebooks.]
8. Wanafunzi wengi katika darasa la Kiswahili ni wazuri. [Many students in Kiswahili class are good.]
9. Wanafunzi wengi wa KU ni walevi. [Many KU students are drunkards.]
10. Nyumba nyingi katika Lawrence ni za zamani. [Many houses in Lawrence are old.]

Sentensi:
1. Fatuma ameleta kiatu kingine. [Fatuma has brought another shoe.]
Fatuma ameleta viatu vingine. [Fatuma has brought other shoes.]
2. Gari jingine limeharibika. [Another car has been destroyed.]
Magari mengine yameharibika. [Other cars have been destroyed.]
3. John amenunua nyumba nyingine. [John has bought another house.]

John amenunua nyumba zingine. [John has bought other houses.]
4.Nitatafuta rafiki mwengine. [I am searching for another friend.]
5. Tumenunua gari jingine. [We bought another car / vehicle.]
6.Tumenunua nyumba nyingine. [We bought another house.]
7. Nimepoteza simu nyingine. [I have lost another phone.]

8. Tutaenda pahali pengine baada ya darasa la Kiswahili. [We will go to another place after Kiswahili class.]
9. Tutaenda mkahawa mwingine baada ya karamu. [We will go to another restaurant after the party.]
10. Tutaona filamuni nyingine leo usiku. [We will see another film tonight.]
11. Mama yangu amenunua nguo nyingine. [My mother has bought another cloth.]
12. Nitakula vyakula vingine kesho. [I will eat other foods tomorrow.]
13. Nitasafisha nguo zingine kesho. [I will clean other clothes tomorrow.]
14. Ninataka kula chakula kingine. [I would like to eat another food.]
15. Ninataka kula tunda jingine. [I would like to eat another fruit.]

]]>
false