MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
<![CDATA[JIFUNZE KISWAHILI - Je, wajua ?]]> https://jifunzekiswahili.co.tz/ 2024-04-28T19:39:55Z MyBB MwlMaeda]]> 2022-07-13T03:42:23Z 2022-07-13T03:42:23Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2685 <![CDATA[Baba alivyookoa ndoa ya kijana wake]]> Baba alivyookoa ndoa ya kijana wake
Iko hivi, katika familia moja yenye mabinti watatu na kijana mmoja wa pekee wa kiume siku moja paliingia tafrani. Kijana wa familia alipofikia umri wa kuoa wazazi na dada zake walihakikisha kijana mpendwa wao anapata mke wa ndoto zake lakini jukumu la kumtafuta mke mwenyewe likawa la muoaji.
Kijana hatimaye aliamua kumtambulisha binti mmoja aliyekuwa naye katika mahusiano kwa muda uliotosha kuwashawishi wote kujiona kila mmoja ameumbwa kwa ajili ya mwenzake.
Baada ya kutambulishana hatua za kuhalalisha uhusiano wao zilianza na hatimaye wakafunga pingu za maisha wakawa mke na mume halali. Mungu akawajalia watoto wawili katika ndoa yao.
 Kadiri siku zilivyosonga wakazidi kuzoeana na mauzauza ya ndani ya ndoa yakaanza kujitokeza kama ilivyokawaida ya vijana wengi wakishazoeana katika ndoa. Makandokando huwa hayakoseni. Mume akaanza vituko mara kuchati kwingi, kuchelewa kurudi na mwisho hata mapenzi kwa mkewe yakawa haba tofauti na ilivyokuwa awali. Katika hali hiyo mke akagundua dhahiri kuna jambo zi bure.
Uvumilivu ulipomshinda mke naye akaona isiwe tabu bora ajiliwaze kwa namna inayomfaa. Hapo mke naye akajipatia kiben ten wake akawa wanapeana raha duniani. Mapenzi kama kikohozi huwezi kukificha. Wakanogewa mpaka mume akagundua na hapo mfumo dume ukajidhihirisha waziwazi kuwa kuchepuka achepuke mume si mke.
Mume alipojiridhisha kwa Ushahidi alionao, siku ya siku akaikusanya familia yake na kwenda kwa wzazi wake. Kufika huko tena akaitisha kikao, ndugu wote wakakusanyika kusikiliza neno la kijana wao wa pekee mpendwa.
Hatimaye kijana akatumbua jipu na kumwaga ushahidi alionao licha ya ushahidi kuwa wa maneno matupu. Mama wa kijana na dada wa kijana hawakutaka kusikiliza la mkwezi wala mfua madafu macho na vidole vyao vikawa juu ya mke wa kijana wao huku wakimtuhumu na kumshutumu kwa maneno makali. “Unataka kutuulia kaka yetu, malaya mkubwa wewe.” Binti wa watu hakutia neno akaamua machozi yamtetee tu.
Wakati hayo yote yakiendelea baba wa kijana alikuwa kimyaaaaaa akitafakari nini cha kufanya. Waswahili wanasema utu uzima dawa. Baada ya muda baba akasema, haya tumekusikia kijana wetu hebu na wewe bitni yangu tueleze una lipi la kusema juu ya tulichoelezwa? Binti yule kwa sauti ya chini sana akasema baba kama anayoyasema ni kweli basi Mungu atajua.
Baada ya kimya kirefu baba wa kijana akasema haya sasa naomba mnisikilize. Kwanza, wewe kijana wangu urudi kwako huyu mkeo na watoto wabaki hapa. Pili, leo hiihii nitasafiri kwenda kutafuta dawa ya kumaliza tatizo hili. Kisha kusema hayo baba akaondoka kwenda alikokuita safari. Huku nyuma binti yule aliishi pale kwa mateso makali na manyanyaso mengi lakini alivumilia akisubiri muujiza utakaoletwa na baba mkwe wake.
Baada ya siku mbili kupita baba yule alirejea nyumbani na kuita tena familia yake yote. Hapo akatoa rai kuwa huko alikokwenda amefanikiwa kupata dawa ya kumaliza tatizo la ndoa ya kijana wao lakini dawa yenyewe inatakiwa kuandaliwa na mtu “safi” na hasa ndugu wa damu. Hapo akamuomba mama mzazi atayarishe dawa hiyo. Mama mzazi wa kijana aliruka futi mia moja akikataa kutayarisha dawa hiyo kwa kuhofia masharti ya “usafi” uliosemwa na baba.
Mpira ukarushwa kwa dada mkubwa wa kijana, naye akaruka na kukataa kabisa kuandaa dawa hiyo kwa kuhofia madhara yanayoweza kumkuta kwani naye hakuwa “safi” kama sharti la dawa linavyotaka.
Baada ya ndugu wote wa kijana kukataa kuandaa dawa baba wa kijana akaamuru wote waondoke na wamuache yeye na kijana wake. Walipoondoka wote baba akamgeukia kijana wake na kumuuliza, “Vipi mwanangu umejifunza nini?” Kijana akajibu nimegundua kumbe hata wewe ni uvumilivu tu ndio unakuweka na mama bila, kumbe hata mama anachepuka!
Baba akamwambia kijana wake, “mchukue mkeo mkaendelee na maisha yenu”.
Je, na wewe umejifunza nini?
 
]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-07-02T15:50:22Z 2022-07-02T15:52:22Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2638 <![CDATA[JE, UNAFAHAMU ATHARI YA MANENO YAKO KWA WENGINE?]]>
Ijumaa iliyopita, nilikuwa darasani nikiwafundisha wanafunzi wangu ndipo mwanafunzi mmoja wa kike akainua mkono kuuliza swali. Nilimruhusu na akauliza swali rahisi sana ambalo nilidhani anapaswa kujua jibu lake maana tayari nilikuwa nimezungumzia mada hiyo wiki iliyopita.

*"Kaa chini, tafadhari! Na sura yako mbaya! Muone!"* ndilo jibu pekee nililompa. Darasa zima liliangua kicheko na alionekana kufedheheka sana.

Niliendelea na somo langu lakini nilihisi kuwa na hatia kwa sababu ya kile nilichokuwa nimesema. Nilimaliza kipindi changu na kuondoka.

Siku ya Jumapili, nilienda Kanisani. Mhubiri alikuwa akiongea juu ya *nguvu ya ulimi*.

Alizungumza juu ya jinsi unavyoweza *kuwavunja moyo, kuwakatisha tamaa na kuwaangusha kabisa wengine kwa kile unachosema*. Nilikumbuka kile kilichotokea Ijumaa na nikajiona ni mwenye hatia zaidi. Niliapa kuwa nitaenda kumuomba msamaha Jumatatu nikifika darasani.

Jumatatu alasiri, nilienda darasani lakini sikumuona yule mwanafunzi. Nilimuulizia kwa wenzake lakini hawakuonekana kujua ni nani hasa niliyekuwa nikimzungumzia.

Ndipo nikasema *"ninamtafuta mtu niliyemtukana Ijumaa".*

*"Aah, huyo ni Furaha, mwalimu! Hayuko darasani leo"* walijibu.
*Rafiki yake ni nani?* Niliuliza.

*"Aisha",* walijibu. *Lakini Aisha pia hayupo darasani.*

Ghafla, msichana aliye na Hijab aliingia. *"Mwalimu, huyo ni Aisha"* wanafunzi wangu walinijulisha.

*Yuko wapi rafiki yako?* Nikamuuliza.
*"Yupi?"* Alijibu bila kunitazama usoni.
*Furaha!* Nilisema.

*Yuko chumba cha kuhifadhia maiti.* Alijibu.
Jibu hilo lilinishtua! *Chumba cha kuhifadhia maiti ????? Kufanya nini hapo ??* Niliuliza.
*"Alikufa Ijumaa"* Aisha alijibu.
*Imekuaje ??????* Niliuliza.

Baadaye niligundua kuwa baada ya kipindi changu Ijumaa, Furaha aligongwa na gari lililokuwa likienda kwa kasi. Alikuwa akivuka barabara bila tahadhari, labda kwa sababu ya kile nilichosema.

*"Mazishi yake ni Jumamosi na umealikwa pia, mwalimu"* Aisha aliendelea.

Wakati nilikuwa nimesimama nilijaribu kuudhibiti mshtuko niliokuwa nao, Aisha alisema huku akilia, *"Mwalimu, umemuua rafiki yangu".*

Alikuwa sahihi! Ninapaswa kuwa muuaji! Wasichana wengine darasani walikuwa tayari wanalia! Sikujua niseme nini, ikiwa ni kuomba msamaha kwa rafiki wa Furaha au kwa roho ya Furaha.

Niliwasilisha barua yangu ya kujiuzulu siku iliyofuata ikiwa na maneno haya: *Wapendwa Wahadhiri na Walimu, tafadhali acheni kutukana wanafunzi wenu. Wako shuleni ili kujifunza kutoka kwenu. Ingekuwa tayari wanajua, wasingekuwa shuleni!*

Tafadhali fikiria kile unachosema kwa watu wengine. Je! Maneno yako yanaleta uhai au kifo kwa wasikilizaji?

ZINGATIO: HADITHI HII NI LAZIMA ISOMWE NA HAIWAHUSU WALIMU TU BALI SISI SOTE TUNAPOKUWA TUNAWASILIANA NA BINADAMU WENZETU:  *WATEJA, WANAFUNZI, WAZAZI, WENZIO, MARAFIKI NA KADHARIKA*

Yatupasa tuwe waangalifu sana juu ya jinsi tunavyosemezana.

*Asante.*??]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-01-22T15:46:55Z 2022-01-22T15:46:55Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2280 <![CDATA[FAHAMU MAJINA YA SEHEMU ZA MIJI MAARUFU TANZANIA NA MAANA ZAKE]]>
1. KOLOMIJE.
Inasemekana mahali hapo alifika Mzungu aliyeitwa James, hivyo huyu Mzungu akataka watu wamwite "J" badala ya kutamka jina lote. Hivyo akawaambia CALL ME J, wabantu wakatamka KOLOMIJE na kutengeneza jina la eneo hilo.

2. KARIAKOO
Hii ilitokana na neno Carrier_crop ambalo lilikuwa ni jina la wabeba mizigo wa eneo hilo la sokoni, lakini Waswahili walishindwa kulitamka jina hilo hivyo wakasababisha kutokea kwa jina la Kariakoo.

3. MSASANI.
Hili jina lililotokana na Bwana mmoja aliyeitwa Musa Hassan ambaye alikuwa ni Mnyapara aliyekuwa akisimamia mashamba ya katani ambaye asili yake ni Mtwara, wamakonde wengi wakaamua kuja kumuomba kazi na kwa kwa kuwa walikuwa hawajui anapoishi waliuliza kwa Mucha Hachani, na wakaendelea kuunga unga mpaka kusababisha kutokea kwa jina la Msasani.

4. KAWE.
Hili lilitokana na neno Cow_Way, barabara maarufu kwa kuswagwa ng'ombe kufikishwa hapo Tangaynyika Packers kwa machinjo.

5. KIGOGO
Ilitokana na kigogo halisi kabisa cha kuvuka pale kigogo mwisho kila jumamosi walikuwa wanakusanyika kukiweka "jamani leo siku ya kigogo" (leo pamejengwa daraja).

6. TABATA
Palikuwa na Muarabu aliyekuwa ananunua korosho kwa mali kauli na kuwaahidi wachuuzi waje siku fulani watalipwa kwa kuwaambia "hapana tabu tabata (utapata pesa yako) akabatizwa jina la Mwarabau Tabata, na mwishowe mahali hapo napo pakaanza kuitwa Tabata.

7. ILALA
Jina hili linatokana na makaburi ya pale Karume ambako hakukuwa na mengine hivyo kila alasiri watu walikuwa wakienda kuzika na wimbo wa Haila Illallah! na mwishowe mahala hapo pakaanza kuitwa Ilala.

8. UBUNGO
Majina yafuatayo: bungoni, mikoroshini, na mabibo yote haya yalitokana na uwepo wa miti mingi ya matunda hayo kupatikana maeneo hayo.

9. KIBORILONI
Kiboriloni ni neno lililotokana na maneno mawili KIBO na ALONE. Hii ilikuwa sehemu ambapo wazungu walisimama na kuona kilele cha Kibo pekee bila kukiona kilele cha Mawenzi, Kibo na Mawenzi ni vilele vya Mt. Kilimanjaro.

10. KIBOSHO
Lilitokana na maneno KIBO na SHOW, hii ni sehemu ambapo Kibo kilionekana vizuri zaidi.

11. MWANANYAMALA
Hapo kitambo mitaa ya Mwananyamala kulikuwa na mapori na Simba, kwa hiyo kina mama wa kizaramo walipokuwa wakifika mitaa hiyo wakawa wanawaambia watoto wao  wanapolia usiku"Mwana Nyamala" maana yake "Mtoto Nyamaza" ili wasisikiwe na Simba.

12. TABORA
Kambi ya Wafanyabiasha. Walikuwa wakipita na bidhaa zao wanakuta viazi vitamu vilivyopikwa na kukatwakatwa vipande na kuanikwa. Hapo huliwa makavu (Chewing gum) au kupikwa na kuliwa. Haya huitwa Matobolwa au Matovola. Hivyo wakapaita kambi ya Matobolwa au Matovolwa. Hii ilikuwa kugeuka na kuwa Tabora.

13. SUMBAWANGA
Wenyeji wa maeneo hayo walikerwa na vitendo vya ushirikina (tofauti na mtazamo wa watu wengi kwamba wenyeji wanaendekeza ushirikina). Kutokana na kero hiyo waliamua kuwapiga mkwara watu wanaoingia katika mji huo kwamba kama unataka kuja huku, basi Tupa Uchawi i.e Sumba (Tupa) Wanga (Uchawi), ukitupa na kuuacha uchawi wako huko uliko unaruhusiwa kuja hapo Sumbawanga.

14. MTONI KWA AZIZ ALI.
Mtoni kwa Aziz Ali pamepata jina kutokana na mkazi mmoja aliyekuwa maarufu (alwatani) sana marehemu Aziz Ali. Mzee huyu alifariki miaka kadhaa iliyopita.

15. KWA BIBI NYAU.
Kwa Bibi Nyau kulikuwa na ajuza mmoja alikuwa anafuga paka wengi sana.

16. NEWALA.
Waingereza walipofika Mtwara walikuta kisima kilichojengwa na wajerumani ambacho kilikuwa cha kizamani kwa wakati Huo , Hivyo walijenga kisima kipya na kukiita NEW WELL, watanganyika wakatamka NEWALA, hatimaye likawa jina la ile sehemu.

17. CHEKERENI[MOSHI].
Hili ni eneo ambapo barabara inakatiza kwenye reli.Sasa wazungu waliweka alama ya bararani ya tahadhari kabla ya kuvuka reli CHECK THE LINE, watu wakatamka CHEKERENI na kuliita hivyo lile eneo hadi leo.

18 . MAKONGOLOSI
Inatokana na neno la kiingereza MAKING LOSS - Zamani waingereza walipata hasara kutokana na shuguli za uchimbaji wa madini eneo la Makongolosi wilaya ya Chunya mbeya ndipo eneo hilo kubatizwa jina hilo .

19 . GODIMA
Ni kijiji kimoja wapo kilichopo wilaya ya Chunya ambacho jina lake lilitokana na kiingereza ambalo ni GOLD MINE ( Mgodi wa Dhababu

20. MATOMBO
Matombo kwa kiluguru ni matiti. Eneo hilo kuna jiwe lenye mwonekano wa mwanamke mwenye matiti. Ndicho chanzo cha kuitwa matombo.

21. KIPONZERO
Kijiji kilichopo barabara ya Iringa kwenda mbeya ndani ya mkoa wa Iringa.Wakati wa ujenzi wa barabara wapimaji walitumia sana neno KEEP ON ZERO kitu kilichofanya wenyeji wafikiri wale wazungu wanapaita pale keep on zero ambayo wao waliitamka kiponzero.

22.MKONGOTEMA
Kijiji kipo baraba ya Njombe to songea. MKONGO ni mti ,Tema walikuwa na maana ya litema/ matema mashamba ya mazao kama ulezi yanayokuwa milimani. Sasa kutokana na watu kukata miti kwaajili ya matema basi ikawa ukitaka kumwelekeza mtu aliko. Unamweleza " kwavudumula mikongo ya matema kola" kingoni. Basi likaja neno MKONGOTEMA.

23. MBAMBA BAY
Kuna mlima upo hapo unaitwa mlima Mbamba. Kwa kilugha mbamba ni radi. Mlima ule ulikuwa na kawaida ya kupiga sana radi nyakati za masika. Hivyo ukaitwa mlima mbamba. Na kutokana eneo hilo lina ghuba katika ziwa nyasa ( bay) ndipo lilipozaliwa jina Ghuba ya Mbamba yaani MBAMBA BAY.

24. KILOMENI ilitokana na maaguzo wakati wa mapigani mzungu aliagiza askari wakifika pale waue wanaume wote yaani KILL ALL MEN wabongo wakashindwa kutamka ndipo wakaishia KILOMENI

25 GONGO LA MBOTO hili lilitokana na mzee mmoja aliyekuwabakiitwa mzee Mboto alikuwa na kirungu kile chenye kichwa. Alipoenda kuwinda maeneo yale ambayo wakati huo yalikuwa ni porini hakuruni. Wakamtafuta sana lakini hawakumpata mpaka leo isipokuwa waliliona rungo au gongo lake. Ndipo walio liona wakati wa kutafuta wakasema jamanj GONGO LA MBOTO hili hapa. Kuanzia siku hiyo eneo hilo limaitwa GONGO LA MBOTO

26 MIKOCHENI lilitokana na duka la kubadilisha pesa MICRO CHANGE

27 KILIMANJARO limetokana na wazungu kushindwa kutamka KILIMA CHA RUWA

27 MBEZI INN MAGARI SABA ilitokea ajali iliyohusisha magari saba kwa wakati mmoja hapo

28 KIBAHA PICHA YA NDEGE jamaa alitengeneza sanam ya ndege na kuiweka hapo paka pta jina.

29. Sehemu nyungine zinabebe majina ya watu kutokana kwamba wao ndiyo walikuwa maarufu wakati huo au walikuwa wa kwanzq kuhamia maeneo hayo. Mfano Mbezi, Mbezi kwa Yusufu, Kwa Msuguli, kwa Ally Maua, Kwa Tumbo alikuwa na tumbo kubwa, kwa Semangube, kwa Shemsa, Kwa bastola, kwa mfuga mbwa, tegeta kwa ndevu nk

Na wewe ongezea mengine]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-12-12T07:44:00Z 2021-12-12T07:53:25Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1722 <![CDATA[WAZARAMO WALIITAWALA ZANZIBAR KABLA YA MWARABU]]>
Na Maalim Kondo Bungo

Historia zinazofutwa kwa kuficha ukweli ndiyo hizi, kumezuka gumzo mitaani kwa ndugu Hasa A Kingo Mzaramo wa Msanga kuteuliwa kuwa Jaji kule nchini Marekani
Si jambo la kushangaza sana kwani kabila la wazaramo wana mengi waliyowahi kuyafanya makubwa na yenye historia kubwa hapa ulimwenguni
Zanzibar kabla ya kupinduliwa na Waarabu mwishoni mwa karne ya 17 au mwanzoni mwa karne ya 18
Hapo nyuma walitawala watawala weusi akiwemo wa mwisho aliyepinduliwa na Waarabu alikuwa akiitwa Mwinyimkuu ni mzaramo mwenye asili ya Bagamoyo wenyeji wa Zanzibar wanajua eneo la mji mkongwe upo msikiti hasaa unaojulikana wa Mwinyimkuu na pembeni yake kuna Hoteli inayodaiwa ndiyo ilikuwa Ikulu yake.
Ikumbukwe tu Zanzibar uisilamu ulikuja zamani sana kabla Waomani hawajaingia kutawala, uisilamu uliingizwa na Waarabu wa Yemen ambao hawakutaka mambo ya utawa wao ni biashara na Dini tu.
Na walikuja ukanda huo wa Zanzibar na Bagamoyo, kule Bagamoyo wa Yemeni walipewa majina kama Shomvi na Guo kutokana na biashara zao za kuuza chumvi na Nguo wakitembeza mitaani huku wakinadi (Shonvi Shonvi) wakimaanisha Chumvi Chumvi hata kizazi chao walichozaa na waafrika kiliendelea kuitwa Wamashomvi na ukisikia Mzaramo anaitwa Shonvi imetokea huko.
Kwa Zanzibar ilikuwa maamkizi ya wazee wetu mbele ya Mwinyimkuu ni kumwambia: Mwinyi yeye anaitikia Muungwana baada ya kupinduliwa na Waarabu kutoka Oman mwinyi alikuwa mnyonge sana kiasi wafuasi wake walikuwa wakimtembelea wakimwambia: mwinyi yeye akawa anaitikia: mwinyimkuu Said akimkusudia Said Barghash aliyempindua.
Salamu hii inaendelea mpaka leo baadhi ya miji ya pwani hususan uzaramoni Bagamoyo na Kisarawe.
Neno shikamoo na marhaba yalililetwa na mzungu gavana wa Tanganyika na Said Said mtawala wa Zanzibar.
Siku walipokutana Gavana alimpa mkono Sultani Said Said Sultani alipoushika mkono wa Gavana akawa anautikisa Gavana akawa anasema (shake more) akimaanisha tikisa zaidi Sultani akawa anamjibu akitamka (marhabba) kwa maana ya karibu au makaribisho mema wale watu weusi wapambe wa Sultan Said Said wakainasa hiyo ikawa na wao wakija asubuhi wanampa mkono huku wakitamka shake more Sultan anawaitikia vile vile marhabba marhabba, shake more kwa matamshi ya wazee wetu ndiyo ikawa shikamoo na Marahaba ikawa kila unapokutana na mkubwa au kiongozi unamtamkia Shikamoo naye anakuitikia marahaba.

Niwatakie siku Njema]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-11-17T16:19:44Z 2021-11-17T16:19:44Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1500 <![CDATA[7 JULAI SIKU YA KISWAHILI DUNIANI]]>
Habari za kutia moyo. Leo UNESCO imepitisha tarehe 7 Julai kuwa ni  siku ya Kiswahili Duniani.

Ni mwanzo mzuri kwa Kiswahili Kimataifa. Baadaye tunaweza kupata wakalimani kwenye vikao vya kimataifa nasi kuwasilisha masuala Kwa Kiswahili!!!]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-10-10T07:38:34Z 2021-10-10T07:38:34Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1307 <![CDATA[JANDONI KUNA MENGI YA KUJADILI]]>
Dada mmoja alinipigia simu, kabla hata sijamuuliza sababu alianza kunielezea matatizo ya mume wake.

Alinielezea mambo mengi mabaya ambayo mume wake alikua akimfanyia.

Nilimsikiliza sana lakini kwa namna alivyokua anaongea nilihisi kuna kitu.

Niliamua kumsikiliza mpaka mwisho ambapo aliniambia “Kaka mimi nimeamua kuondoka huyu si mwanaume wa kuishi naye!.”

Baada ya kumaliza kuongea nilimuambia sasa hembu niambie mazuri ya mume wako.

Alikaa kimya kwa muda kisha akaniambia “Mimi sikukupigia ili kumzungumzia yeye nilitaka tu unipe ushauri kuwa niondokeje maana nimechoka.”

Niliendelea kumsisitiza aniambie angalau zuri moja la mume wake.

Aliniambia zuri nikwakua tu labda anamsomesha mdogo wake sekondari lakini hakuna kingine.

Nilimuambia wala sihitaji mengi, hilo moja tu linatosha, nilimuuliza unasema mume wako hakujali, hajawahi kukununulia nguo hata siku moja au kukutoa out kama wanawake wengine?

Akanijibu ndiyo, nikamuuliza mshahaara wake ni Shilingi ngapi, akaniambia ni kama laki saba kwa mwezi.

Nikamuuliza chakula anatoa akaniambia ndiyo, nikamuuliza kodi ya nyumba kwa mwezi mnalipa Shilingi ngapi akaniambia laki moja na nusu,  kwa mwaka ni Shilingi ngapi?

Akanijibu milioni moja na laki nane.

Nikamuuliza umeme na maji analipa nani?

Akanijibu mlipaji ni  mume wake.

Nikamuuliza kwa mwezi vinaweza fika shilingi ngapi?

Akasema kama elfu ishirini.

Nikamuuliza kwa mwaka ni shilingi ngapi? Akajibu ni kama laki mbili na arubaini, ukichanganya na kodi ni kama milioni mbili.

Nikamuuliza ada ya mdogo wako Shilingi ngapi?

Akaniambia kwakuwa anasoma shuke binafsi ni kama milioni tatu na laki tano kwa mwaka.

Nikamwambia ukichanganya na zile milioni mbili unapata ngapi?

Tukapiga hesabu ikaja kama milioni tano na laki tano.

Nikamuuliza kwa siku chakula anakuachia Shilingi ngapi?

Akaniambia elfu kumi.

Kwa mwezi ni kama ngapi?  Akasema ni laki tatu kwa mwaka ni  kama milioni tatu na laki sita.

Nikamwambia ukijumlisha na zile tano inakuja kama ngapi?

Tukakuta inakuja kama milioni tisa na laki moja.

Nikamwambia haya sasa tuangalie mshahaara wa mume wako ni Shilingi laki saba kwa mwezi, ambayo kwa mwaka ni Shilingi ngapi?

Tukakuta ni milioni nane na laki nne, nikamwambia kama mnatumia milioni tisa na zaidi tena hapo hamjaumwa, sijajumlisha na ndugu zake, sijajumlisha nauli, sijajumlisha na michango ya harusi na bado unalalamika hakutoi out, wakati matumizi yenu tu ni ziadi ya mshahara wake unataka nini, unataka awe anakupa na damu yake.

Alibaki kimya na kukata simu. Baada ya siku mbili alinipigia simu na kuniambia “Kaka nimeelewa sitaki kuondoka tena kwani nimeona nilikua namchanganya tu mume wangu.
Sikua na shukurani na sikuona mazuri yake kwakua akili yangu niliielekezea katika mabaya tu.”

SOMO
Watu wengi tunawachukia wenza wetu kwakua akili zetu tumezipeleka katika mabaya yao tu na si mazuri hivyo tunajikuta tunawachukia na kudhani kua hawatupendi.

Hebu leo amua kuangalia angalau zuri moja tu la mwenza wako...

Hujachelewa.]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-09-27T03:59:33Z 2021-09-27T03:59:33Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1279 <![CDATA[JIFUNZE KULIPA GHARAMA]]> ACHA KUPENDA VYA BURE !!!!
(Pamoja na urefu wake nakusihi ujipe muda kusoma mpaka mwisho)
Makala aliyoandika Paul Mashauri siku chache kabla ya kifo cha Ally Mufuruki. (Mufuruki the legend).
Miaka 10 iliyopita nilimfuata Mr. Ally Mufuruki, Mwenyekiti, CEO, Round Table ofisini kwake. Nikamwambia Mr. Ally unajua tunavyojaribu kusaidia watanzania wenzetu wapate maarifa kupitia “East Africa Speakers Bureau”. Nakuomba sana uje uzungumze katika kongamano tunaloandaa kwa wafanyabiashara. Akaniambia Paul hakuna tatizo juu ya hilo, lakini ada yangu “speaker fee” ni Tsh. milioni 2. Sikumuelewa kabisa Mr. Mufuruki hasa ukizingatia ukweli kwamba anapenda maendeleo ya watanzania wenzake na angeweza kuongea bure.
Lakini haikunichukua muda kumuelewa Mr. Mufuruki. SIku moja mimi mwenyewe binafsi nikaandaa semina ya bure. Gharama zote nilibeba mwenyewe lakini walifika watu 5 tu. Nilistaajabu ya dunia. Semina ambayo hutoza mshiriki mmoja Tsh. 350,000/= na ukumbi unajaa wamekuja watu 5 tu angali semina hiyo hiyo ni bure. Nikagundua watu hawathamini kitu wanachopata bure. Ndiyo maana Mr. Mufuruki alikataa kuongea bure. Sio kwa sababu ya pesa, ni kwa sababu hana muda wa kupoteza. Vitu vya bure vingempotezea muda wake. Nikajifunza kitu kipya kwenye maisha yangu. Ukitaka jambo lako lithaminiwe acha watu walipe gharama.
Somo nililolipata kwa Mr. Mufuruki likawa sehemu ya maisha yangu. Miaka kadhaa ikapita nikafuatwa na binti mmoja na kaka mmoja. Walikuwa ni watu maarufu sana katika nchi hii. Wenye ushawishi mkubwa kwa vijana “celebrities”. Wote walikuwa na mawazo ya biashara na walitaka niwe “mentor” wao. Nikawaambia sawa. Lakini kabla sijaanza “mentorship” program hii, naomba kila mmoja wenu aandike hilo wazo katika “business plan” na atengeneze mfano au “demo” itokanayo na hilo wazo, kisha atafute angalau wateja 2 ndio tuanze “mentorship”. Waliondoka moja kwa moja hawakurudi tena.
Sikuwaambia wale vijana wafanye yote hayo kwa sababu nilikuwa siwezi kuwatengenezea “business plan” au kuwatafutia wateja. Saa 12 tu kwangu zingetosha kuwapa “business plan” yenye mashiko na ningepiga simu chache tu kwenye “network” yangu kuwaunganisha na wateja. Niliwaambia wafanye yale yote ili walipe gharama. Ili waone thamani ya “mentorship” program wanayoitaka. Ili watilie maanani kile wanachotaka kujifuna kutoka kwangu. Kama Mr. Mufuruki alivyotaka mimi na wale niliokuwa nawaandalia kongamano waone thamani ya muda wake na maarifa aliyonayo na mimi nilitaka hawa vijana waone thamani ya muda wangu na kile wanachohitaji ili kuishi ndoto zao.
Kupenda vitu vya bure, kupenda mteremko ni chanzo cha umasikini. Kwa sababu vitu vya bure vinakuja kirahisi. Hautumii nguvu, hautumii akili wala hautokwi jasho. Ukiangalia duniani jamii ambazo zimefanikiwa sana kiuchumi ni jamii ambazo ili uishi, ili upate chakula, ili upate mahala pa kulala ni lazima utumie nguvu zako, akili zako, maarifa yako. Hakuna vitu vya bure. Hakuna mteremko. Kwa kifupi ni lazima ulipe gharama. Ndiyo maana mataifa kama Uingereza na Marekani, huwezi kuishi kama huna kazi inayoeleweka. Wakati mwingine lazima ufanye kazi zaidi ya moja. Ndiyo maana nchi kama Japan, haina rasilimali nyingi lakini ni moja kati ya mataifa yenye uchumi wenye nguvu. Ni kwa sababu kuna changamoto nyingi sana kiasi kwamba kama huna ubunifu huwezi kuishi. Ndiyo maana watu kutoka nchi kama India na China wamesambaa dunia nzima. Ni kwa sababu huko kwao wako wengi sana kiasi kwamba ili utoke kimaisha ni lazima ufanye kitu cha tofauti.
Na kwa mtazamo huohuo ukiangalia jamii masikini sana duniani ni zile jamii ambazo watu wanapenda vitu vya bure. Wanapenda vya kupewa. Ni jamii ambazo hata kama hutaki kufanya kazi utaishi. Kwa sababu ukiumwa njaa utaenda kwa mjomba atakupa hela, utampiga mzinga shemeji yako atakupa hela, utatafuta mke kutoka familia bora utapata hela, utatafuta mume wa mtu akuweke nyumba ndogo upate hela, au utaingia barabarani kuwa ombaomba upate hela ya chakula. Ni jamii ambazo ombaomba wana akiba ya fedha “savings” kuliko wenye mishahara. Ni jamii ambazo maisha siyo magumu. Ni jamii ambazo watu wazembe wanaona ni wajibu wa wale wanaojituma na kutokwa jasho kuwapa hela za kujikimu angali wao wanakesha baa wanakunywa mbege na wanzuki. Ni maisha yasiyo na utofauti na chawa. Maisha ya kunyonyana damu.
Hakuna ubaya kwenye kusaidiana katika maisha. Wala hakuna ufahari kwenye kufanikiwa kwa kutokwa jasho. Lakini ukweli ni kwamba kula kwa jasho ni amri iliyotoka kwa Mungu mwenyewe. Kula kwa kutumia kazi za mikono mikono yako ni amri iliyotoka kwa Mungu mwenyewe. Asiyefanya kazi na asile ni amri iliyotoka kwa Mungu. Hatukatai! Unaweza ukapewa kitu cha bure lakini usifanye kuwa ni sehemu ya utamaduni wako. Kwa sababu akili yako ikifika hatua ikaona kupata vya bure ni haki yako, utachukia watu pasipo sababu za msingi na utaona ni bore ufe kuliko kuishi. Kumbe uwezo wa kupila gharama na kutoka kimaisha uko ndani yako.
Unapokataa kumpa mtu kitu cha bure haumnyanyasi unamsaidia. Hata mtoto mdogo ana umri wa kutafutiwa chakula na kulishwa. Lakini ukitaka umtafutie mtoto wako chakula na kumrisha maisha yake yote hata akishaota ndevu haumsaidii unamharibu. Hivyo ndivyo nilivyowafanyia wale vijana wawili waliokuja kwangu wanataka “mentorship”. Ningewatengenezea “business plan” na kuwatafutia “wateja” ningekuwa siwasaidii ningewaharibu. Kwa sababu “business plan” na “wateja” ni sehemu ndogo sana ya kufanya baishara. Kuna kuishi na wafanyakazi, kuna kuishi na mabenki, kuna kupambana na changamoto za kuibiwa nk. Zaidi ya hapo, mimi ni binadamu, nina matatizo yangu na ninafamilia inaniangalia. Siwezi kuwa sehemu ya maisha ya wale vijana milele hata kama nina roho nzuri kiasi gani. Lazima waonyeshe kiu na njaa ya kutaka kuishi ndoto yao kabla sijaingiza maarifa na muda wangu katika maisha yao.
Sio mimi tu na Mr. Mfuruki tulio na mtazamo huu. Nakumbuka pia siku moja nilikuwa na rafiki yangu, Partner wa KPMG. Akaniambia wanapotafuta wafanyakazi, moja kati ya vigezo ni kuona “attitude” zao. Hata kama huyu mtu ana akili kiasi gani kama “attitude” yake si nzuri wanaweza wakamuacha. Akasema wakati mwingine unaweza ukamuita mtu kwa ajili ya “interview” lakini unamuacha akae kwanza “reception” muda wa “appointment” yake upite tena sana ili uone uvumilivu wake. Sio kwamba unamtesa au unakuwa “unprofessional”. Hapana, ni sehemu ya “interview”. Kama mtu hawezi kuvumilia masaa 3 mbele ya muda aliopewa wa “interview” ataweza kuvumilia “etra hours” akiwa kazini?
Rafiki yangu wa KPMG akawa ameniongezea kitu ambacho Mr. Mfuruki alinifundisha. Kwamba ukipata kitu kwa mteremko huwezi kukithamini. Hata mtu anayepata kazi kwa mteremko hawezi kithamini ile kazi. Ingekuwa ukimaliza tu chuo unapigiwa simu njoo uanze kazi kwa mshahara wa milioni 30 inawezekana wengi wetu wasingethamini kazi zao. Lakini ule mchakato wa kutembea na bahasha ya kaki, kuomba “interview” na kukosa, kuitwa kwenye “interview”, kufanya “interview” ya kwanza na ya pili na ya tatu inakufanya uiheshimu kazi. Kwa sababu kufuatilia kazi miezi sita ni kulipa gharama. Ni sawa na kumlipa Mr. Mfuruki shilingi milioni 2 aje kuzungumza kwenye kongamano lako. Yale atakayofundisha utayatilia maanani. Kwa sababu umelipa gharama.
Mambo ya msingi kwenye maisha utakutana nayo kila mahali. Kulipa gharama ili utoke maishani ni jambo la msingi ukubali au ukatae. Hata wewe usikubali kutoa ulichonacho bure hata kama ni mawazo. Hata kama hauhitaji chochote weka gharama fulani anayehitaji ulichonacho alipe. Akikipata kwa jasho atakiheshimu. Nililiona hilo kwa Mfuruki, kwa rafiki yangu Partner wa KPMG na nikaja nikaliona tena kwa Dr. Reginald Mengi. Siku moja nikiwa ofisini kwake akaanza kulalamika. Akasema “hebu anagalia hawa vijana wa siku hizi walivyo wa ajabu. Kuna kijana hapo “reception” baba yake amemtuma kwangu nimpe kazi. Mimi nina vikao. Amekaa hapo masaa 2 ameshampigia simu baba yake kwamba mimi nimemueweka tu hapo reception masaa 2. Huyu ameshashindwa “interview”. “He is a baba’s boy”.
Kama ilivyokuwa kwa Mr. Mfuruki Dr. Reginald Mengi alitaka kuuthaminisha mchakato wa yule kijana kupata kazi. Sio kwa sababu baba wa yule kijana anafahamiana na Dr. Mengi basi kazi ipatikane kirahisi. Huo sio utamaduni wa mafanikio. Watu waliopitia michakato ya kufanikiwa kama Mr. Mfuruki na Dr. Mengi wanata
mbua hilo. Ndivyo nchi zilizoendelea zilipotokea. Wanatambua umuhimu wa kulipa gharama. Wanakimbia utamaduni wa kutaka vya bure. Wanaheshimu amri ya kula kwa jasho, kula kwa kazi za mikono yako na asiyefanya kazi na asile.
Nimeandika makala hii kwa sababu hii sio elimu ambayo utafundishwa darasani. Hata mimi sikufundishwa na Professor wangu wa uchumi. Nimefundishwa mtaani. Somo lilipoiingia vizuri na mimi nikaanza mchakato wa kufundisha wengine. Ndio maana hata mimi huwezi kunipata kirahisi. Huwezi kuandika tu msg. facebook naomba kukuona nikasema njoo kesho. Sio Mashauri huyu. Sio kwa sababu sina muda. Muda unatengenezwa na unapatikanika. Kama napata muda wa kuandika kwanini nikose muda wa kuonana na wewe? Lakini nataka nijirizishe kwamba uko tayari kulipa gharama. Nataka nijue kama kweli una njaa na hicho unachokitaka, una kiu ya kukifanikisha au unataka kunipotezea muda wangu.
Hata wale ninaofanya nao kazi au niliowahi kufanya nao kazi watakuambia. Wanalipa gharama. Ndio maana wapo vijana wengi leo hii wamesimama wao kama wao wakiwa na biashara zao lakini watakuambia nilijifunza nilipofanya kazi kwa Mashauri. Wengine ni wakuu wa wilaya na wengine ni mawaziri. Ni kwa sababu sikuwaacha wasubiri kulishwa kama watoto wadogo angali wameshaota meno. Nilihakikisha hawapati mteremko walipokuwa na mimi, nilihakikisha wanatoka jasho, wanapanda milima na mabonde. Nilikuwa nawafundisha kujitegemea. Hilo ndio somo ambalo wengi hawalitaki, lakini hilo ndio somo pekee mbalo linaweza likakuvusha kutoka hapo ulipo kuelekea kule unapotaka kufika.
kama umeweza kusoma makala hii ndefu namna hii na kuimaliza ina maana wewe hupendi mteremko na nataka nikutie moyo ya kwamba utafika mbali kwenye maisha yako. Wengi wakiona makala ndefu kama hii hawasomi. wanaandika chini kwenye-comments “gazeti”. Ni kwa sababu wanapenda mteremko. Wanapenda kusoma vile vitabu vya “How to Get Rich Quicker”. Wanapenda kusoma “tweets” yenye sentensi mbili. Bahati mbaya sana maisha siyo “twitter”, maisha hayana shortcut.
Ndio maana matangazo ya “tender” za biashara na kazi hayako “twitter” yako kwenye magazeti. Kwa sababu ili usome gazeti kama hii makala ni lazima uwe na njaa, uwe na kiu ya kufikia malengo yako. Ndio maana “page” kama zangu haziwezi kuwa na “followers” wengi kwenye “social media” ukilinganisha na “comedy”. Kwa sababu masomo yangu hayana mteremko. Lazima ufikiri ndio uelewe. Unaweza ukasoma “post” yangu usiku ukaitafakari usiku kutwa usielewe ukaelewa subuhi. Yes! Umelipa gharama.
Mungu akubariki sana na sambaza makala hii iwe baraka kwa mwenzako. Lakini ili imsaidie lazima alipe gharama. Lazima aende kinyume na utamaduni wa kutaka kusoma vitu vifupi vifupi. Aanze utamaduni mpya wa kulipa gharama kwa kusoma vitu virefu. Na mtihani wa kwanza na hii makala kama gazeti la Daily News-Paul R.K Mashauri
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-09-23T13:28:52Z 2021-09-23T13:28:52Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1263 <![CDATA[TAFAKARI YA LEO]]>
h͟͟a͟͟k͟͟u͟͟n͟͟a͟͟ h͟͟a͟͟k͟͟i͟͟m͟͟u͟͟ a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟t͟͟e͟͟n͟͟d͟͟a͟͟ h͟͟a͟͟k͟͟i͟͟ k͟͟a͟͟m͟͟a͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟.

1. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟k͟͟u͟͟p͟͟e͟͟n͟͟d͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟.

2. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟k͟͟u͟͟c͟͟h͟͟u͟͟k͟͟i͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

3. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟s͟͟e͟͟m͟͟a͟͟ t͟͟u͟͟k͟͟o͟͟ p͟͟a͟͟m͟͟o͟͟j͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

4. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟r͟͟i͟͟n͟͟g͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

5. m͟͟w͟͟e͟͟n͟͟y͟͟e͟͟ k͟͟i͟͟b͟͟u͟͟r͟͟i͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

6. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟k͟͟u͟͟d͟͟h͟͟a͟͟r͟͟a͟͟u͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

7. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟k͟͟u͟͟f͟͟i͟͟t͟͟i͟͟n͟͟i͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

8. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟j͟͟i͟͟g͟͟a͟͟m͟͟b͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟.

9. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟j͟͟i͟͟o͟͟n͟͟a͟͟ a͟͟m͟͟e͟͟k͟͟a͟͟m͟͟i͟͟l͟͟i͟͟k͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

10. m͟͟w͟͟e͟͟n͟͟y͟͟e͟͟ w͟͟i͟͟v͟͟u͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

11. a͟͟s͟͟i͟͟y͟͟e͟͟k͟͟u͟͟b͟͟a͟͟l͟͟i͟͟ u͟͟s͟͟h͟͟a͟͟u͟͟r͟͟i͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟

12. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟k͟͟u͟͟o͟͟n͟͟e͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟.

13. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟k͟͟u͟͟p͟͟u͟͟u͟͟z͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟.

14. a͟͟n͟͟a͟͟y͟͟e͟͟j͟͟i͟͟f͟͟a͟͟n͟͟y͟͟a͟͟ a͟͟n͟͟a͟͟j͟͟u͟͟a͟͟, m͟͟p͟͟e͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟.

k͟͟w͟͟a͟͟ k͟͟u͟͟w͟͟a͟͟ i͟͟p͟͟o͟͟ k͟͟e͟͟s͟͟h͟͟o͟͟ t͟͟u͟͟s͟͟i͟͟y͟͟o͟͟i͟͟j͟͟u͟͟a͟͟, t͟͟u͟͟e͟͟n͟͟d͟͟e͟͟l͟͟e͟͟e͟͟ k͟͟u͟͟p͟͟e͟͟a͟͟n͟͟a͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟, k͟͟w͟͟a͟͟ k͟͟u͟͟w͟͟a͟͟ m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟ n͟͟i͟͟ m͟͟w͟͟a͟͟l͟͟i͟͟m͟͟u͟͟ m͟͟z͟͟u͟͟r͟͟i͟͟ s͟͟a͟͟n͟͟a͟͟. m͟͟u͟͟d͟͟a͟͟ h͟͟u͟͟w͟͟e͟͟k͟͟a͟͟ h͟͟a͟͟d͟͟h͟͟a͟͟r͟͟a͟͟n͟͟i͟͟ j͟͟e͟͟m͟͟a͟͟ n͟͟a͟͟ b͟͟a͟͟y͟͟a͟͟.]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-08-08T04:51:44Z 2021-08-08T08:37:36Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=800 <![CDATA[Nitawapeleka Mtoni, Nitawalazimisha kunywa maji]]> Nitawapeleka Mtoni, Nitawalazimisha kunywa maji
Siku moja baba alimuamsha kijana wake apeleke ng'ombe machungani.
Mtoto akatoka na kundi la ng'ombe hadi porini. Ilipofika majira ya alasiri akawapitisha mtoni kisha akawarejesha zizini.
Alipofika baba yake akamuuliza;
Baba: Ng'ombe wamekunywa maji?!
Kijana: Niliwapeleka mtoni.
Katika Elimu na mchakato wa kujifunza kuna mambo matatu muhimu:-
1. Kufundisha; Bila shaka mtakubaliana nami kwamba, kuna matendo ya kufundisha (teaching activities) ambayo mwalimu anatakiwa ayafanye.
2. Kujifunza; pia yapo matendo ya kujifunza (learning activities) ambayo mwanafunzi anatakiwa ayafanye.
3. Upimaji na Udhibiti; lengo lake kwa kiasi kikubwa ni kupima ufanisi wa 1 na 2 hapo juu. Anapimwa mwalimu kama amefundisha, na mwanafunzi kama amesoma.
Mwalimu ambaye ameandaa skimu, ameandaa nukuu za somo, amesaini mahudhurio ofisini, ameandaa lesoni plani, amesaini klasi juno, amefundisha, ametoa mazoezi na kazi mbali mbalimbali, anakuwa anatekeleza majukumu ya ufundishaji, sawa na kusema ng'ombe wamepelekwa mtoni.
Ikitokea wanafunzi hawajisomei, hawaadhibiwi, wanafeli mitihani, hawaukizi maswali kwa mwalimu; hii ni sawa na kusema ng'ombe wamefika mtoni hawataki kunywa maji
Baada ya matokeo kutoka;
Stakeholders: Mwalimu kwanini wanafunzi wamefeli. kwanini hawakunywa maji?!
Mwalimu: *_Niliwafundisha_* niliwapeleka mtoni.
Pamoja na ukweli kwamba kujifunza ni jukumu la mwanafunzi, lakini je, tunahakikisha wanafunzi wanafanya matendo ya kujifunza? Wanafunzi wanawajibishwa vipi ikiwa hawatekelezi jukumu lao au wanazembea?!
Siku moja nikiwa darasani, katika mazungumzo na wanafunzi;
Wanafunzi: Naipenda nchi yangu, sitakubali ihujumiwe...(salamu ya sasa kuhimiza uzalendo)
Mimi: Hujuma mwaifahamu!?
Tukapiga hesabu ya pesa ambazo serikali inalipa katika huu mpango wa elimu bure, kama ada na gharama nyingine.
Nikauliza kuna mwalimu wa somo lolote hayupo?!
Walimu wa kila somo wapo, na wanafundisha, walimu wanalipwa, chaki zinanunuliwa, vitabu vipo shuleni, madarasa yanajengwa na Ada hamlipi.
Nikawaambia 'hapo ukifeli basi umehujumu nchi yako ambayo unasema hutakubali ihujumiwe.'
Mimi ni mwalimu. Madarasa ninayofundisha pamoja na kutokosa kipindi changu hata kimoja na kuomba vya ziada, nimekuwa nikiwasisitiza waniletee maswali yanayowatatiza muda wowote. Kwa mwaka sasa hawazidi watatu wanaokuja lakini hasa ni mmoja..
Nakubali wapo baadhi yetu walimu wanaotia doa sehemu ya ufundishaji lakini kama mtaalamu katika nafasi yangu nasema kwa kinywa kipana kwamba upande wa mwanafunzi (kujifunza) kuna mapungufu makubwa.
Andiko hili si lawama kwa yoyote, bali ni kuhamasisha kila mdau atimize yanayomhusu.
Elimu yetu imeingiliwa na siasa, wataalamu wengi wa tasnia yetu wamekuwa wanafanya kazi kisiasa. Wakuu wa shule na maafisa elimu wanaelemea kwenye siasa kuliko utaalamu wao katika utendaji. Huenda miongoni mwa vigezo vya kuhudumu katika nafasi hizo ni kustawisha maslahi ya kisiasa ya mamlaka za uteuzi, badala taaluma na elimu.
Niwakumbushe wote waliopewa dhamana katika nafasi mbalimbali tuwe wazalendo kwa nchi na taifa letu, elimu yetu ni nyenzo muhimu katika ustawi wa taifa hili.
Uzalendo ni kupenda nchi yako kwa mapenzi na wivu mkubwa, na kuweka mbele masilahi ya taifa, na si kupenda serikali.
Tuelewane:
Uzalendo ni kupenda nchi, taifa.
Uzalendo si kupenda chama, serikali.
Ndio maana hata ukiwa mtumishi wa serikali kuna mambo inatakiwa ujifinze kuyakataa kwa maslahi ya taifa lako sababu uzalendo wako sio kwa serikali bali ni kwa taifa na nchi yako.
Ningeweza kugusia sehemu nyingi katika mfumo wetu wa elimu, lakini kwa vile kuna mchakato wa maboresho ya mitaala, tutatoa maoni yetu huko.
Lakini walau niseme kwa ufupi kuhusu somo la hesabu;
Somo hili liwe la lazima hadi kidato cha pili, kisha liwe hiari (optional) kuanzia kidato cha tatu.
Mada kama Statistics, Linear programming na Accounts ziitwe junior O-level mathematics, mahususi kwa kidato I na II ambazo zitakuwa ni lazima kwa wanafunzi wote.
Mada kama logarithms, exponent radical,  zipelekwe kidato cha tatu ili wasome wanaotaka (watakaochagua) kusoma Maths.
Siku moja katika wasaa wa kunasihi wanafunzi, (sisi walimu huwa tunatenga muda wa _kupiga stori_ na wanafunzi kuhusu mambo mbali mbali nje ya mada)..
We spare three to five minutes talking contemporary issues
...nikawasimulia hiki kisa cha mzazi aliyemtuma mwanawe porini kuchunga ng'ombe.
Mwisho nikawaambia professionally ilitakiwa niwapeleke mtoni lakini wakuu wangu wananitaka nihakikishe mnakunywa maji.
Buchu, Hamza O.
+255 715 345 789
10/07/2021
Mwanza
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-07-10T06:44:46Z 2021-07-10T06:44:46Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=490 <![CDATA[Ogopa sana mtu mkimya]]>
1. Wako vizuri kwenye kutunza SIRI

2. Siyo rahisi kuwaelewa.

3. Anaweza kukufanya lolote na usitambue kamwe kwamba yeye ndiye chanzo.

4. Huwa wana ajenda nyingi ndani zilizojificha.

5. Hawatabiriki.

Umakini muhimu kusoma ukimya wa mtu]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-07-07T06:32:25Z 2021-07-07T06:32:25Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=447 <![CDATA[KILA KITU KINA UPANDE WAKE WA PILI KATIKA MAISHA]]> Tunaishi katika dunia ambayo watu wasio na pesa wanatafuta pesa ili wapate furaha, wakati huo watu wenye pesa wala hawana furaha na pesa zao.
Hii ni dunia ambayo maskini anakula chochote anachokipata akisononeka kuwa angekuwa na hela, labda angekula vizuri zaidi. Lakini yupo tajiri anayekula mchicha wa kutandika kwa sababu ya maradhi yanayoushambulia mwili wake.
Kuna mtu yupo hospitali anazungumza na daktari kwa siri amsaidie kutoa mimba, halafu kuna mwingine yupo chumba cha pili anamuomba daktari amsaidie mwaka wa saba huu hajapata mtoto.
Kuna mtu yupo sehemu fulani ya dunia anatia saini hati ya talaka kuwa haitaki tena ndoa yake. Lakini kuna mtu yupo kanisani amepiga magoti anamuomba Mungu ampatie mume.
Nimejionea sana kipindi nasoma, kuna wanafunzi wanatamani kusoma lakini wanaondoka shule kwa sababu wazazi wamekosa ada kama ilivyo kwa Watoto wa Mama N'tilie katika ile riwaya maarufu ya Emmanuel Mbogo, lakini kuna wanafunzi wanaondoka shule kwa sababu wazazi wanawataka wakasimamie biashara zao.
Kuna mtu sasa hivi anaandika barua ya kuacha kazi kwa sababu kazi yake imemchosha. Halafu kuna mtu anabadilisha bahasha ya kuhifadhi vyeti vyake, mwaka wa sita huu hana ajira.
Nimejifunza sana kutoka kwa watu maarufu. Kuna mtu sasa hivi anaumiza kichwa usiku na mchana atakuwaje maarufu afahamike na kila mtu mjini halafu yupo staa anayetamani kushuka kwenye gari aingie japo mtaani kuzurura lakini hana hiyo nafasi tena.
Kuna mzazi sasa hivi anatamani muda urudi nyuma ili akamfunze mtoto wake maadili, halafu kuna mzazi analia amempoteza mwanawe, baada ya kumlipia ada na kumpatia malezi mazuri kwa miaka yote, leo amekunywa sumu kwa sababu ya mpenzi aliyekutana naye mwaka jana.
Nilijionea nilipokuwa shule, kuna mwanafunzi analia kupata "C" akiamini amefeli sana lakini kuna mwanafunzi anayerisiti mwaka wa tatu sasa anaitafuta hiyo "C".
Hata ninapomaliza kuandika haya, kuna mtu anasoma akiamini hiki ni kitu chema kwake lakini yupo anayeona hili andiko ni ujinga na upuuzi tu.
Lakini ninachojaribu kusema hapa ni kuwa, kila kitu kina upande wake wa pili wa maisha. Unachoona bora kwako kwa mwingine kinaweza kuwa takataka. Kinachoweza kuwa takataka kwako kwa mwingine kinaweza kuwa bora. Kwa hiyo, tuishi maisha yetu tuliyopewa na Mwenyenzi Mungu.....?

Imenukuliwa mtandaoni.]]>
false