MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
<![CDATA[JIFUNZE KISWAHILI - Tamthiliya]]> https://jifunzekiswahili.co.tz/ 2024-04-27T15:15:30Z MyBB MwlMaeda]]> 2022-07-24T05:04:03Z 2022-07-24T05:11:49Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2789 <![CDATA[NYERERE NA SAFARI YA KANAANI]]> Oktoba, 1966 kulizuka mgogoro mkubwa wa kihistoria kati ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Muhimbili. Wanafunzi hawa walifanya maandamano makubwa hadi Ikulu wakipinga vikali sera ya kuwataka wajiunge na Jeshi la kujenga Taifa (JKT). Wasomi hawa walilalama kwa hasira wakisema, "afadhali wakati wa mkoloni kuliko serekali ya Nyerere. Mkitulazimisha basi tutaenda KIMWILI, lakini MIOYO yetu, asilani, haitaenda JKT..." Katika kuukabili upinzani huu, Mwalimu, katika ile hotuba maarufu: "Tanzania itajengwa na wenye moyo" aliwacharaza viboko baadhi ya wasomi hao kadamnasi na kuwafukuza takribani wanafunzi 400 warudi kwao, wakalime! Mwandishi anatudokeza, miongoni mwa masuala mengine kuwa: Mgogoro huu wa 1966, ulichangia katika kukuza mimba ya safari ya Kanaani nchi ya asali na maziwa.Hapana shaka kuwa tamthiliya hii, iliyoandikwa kwa ustadi kabisa, ni kitabu muhimu kwa wanasiasa, wasomi na wapenzi wote wa fasihi ya Kiswahili.]]> false MwlMaeda]]> 2022-02-03T08:24:05Z 2022-02-03T08:24:05Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2386 <![CDATA[CHIMBUKO MABADILIKO NA MAENDELEO YA TAMTHIYA]]>
.pdf   MODULI_YA_PILI_CHIMBUKO_MABADILIKO_NA_MA (1).pdf (Size: 31.72 KB / Downloads: 3) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-12-27T06:29:28Z 2021-12-27T06:29:28Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1835 <![CDATA[CHIMBUKO LA TAMTHILIYA NA HISTORIA FUPI YA TAMTHILIYA YA KISWAHILI]]> CHIMBUKO LA TAMTHILIYA NA HISTORIA FUPI YA TAMTHILIYA YA KISWAHILI
Kabla ya mwambao wa Pwani ya Afrika Mashariki kuingiliwa na athari za kigeni zilizotoka ng’ambo, fasihi ya Kiswahili, kama fasihi nyinginezo za kiafrika, ilikuwa ni ya kusimuliwa tu (pasi na kuandikwa) na ilikuwa na tanzu kama vile ngano, sanaa za maonyesho, vitendawili, methali na kadhalika. Utanzu wa tamthiliya haukuwa na taswira kama iliyokuwanayo sasa, bali palikuwa na maigizo ambayo yalitolewa mbele ya hadhira kwa minajili ya kuongoa na kufundisha maadili au hata kutoa sifa kwa vitendo mwafaka vya wanajamii husika. Baada ya majilio ya wageni (Waarabu na Wakoloni) maonyesho haya yalianza kubadilika kwa kuingizwa katika maandishi na kuiga mitindo ya kimagharibi ili kuchukua mkondo wa tamthilia kwa jumla.
Kihistoria, tamthiliya ilianza kwa kutongoa maudhui ya kidini ambayo aghalabu yalikuwa ni uteuzi wa visa fulani kutoka katika Bibilia Takatifu ili kutoa funzo fulani. Pindi mabadiliko yalipoendelea kutokea katika maisha ya mwanadamu, hali hii ilibadilika hadi kuingia katika tamthiliya zilizozingatia maudhui mengine kama vile vichekesho na tanzia. Peck na Coyle (1984:75), wanashadidia maoni haya kwa kusema kuwa katika drama ya Kigiriki, wahusika walikabiliana na matatizo yaliyohusu uhusiano kati ya binadamu na miungu au Mungu. Katika karne ya kumi na sita (16) hata hivyo msisitizo ulitoka katika dini na kuingiza masuala ya kijamii, hivyo tamthiliya zikaanza kuzingatia maadili ya kijamii na kisiasa.
Katika Kiswahili, tamthiliya ya kwanza kabisa kutungwa na mwafrikanakuchapishwani ile ya Henry Kuria (1957) kwa kichwa cha Nakupenda Lakini, ambayo ilitungwa katika enzi ya ukoloni, tamthiiya hii iliigizwa kwa mara ya kwanza mwaka 1954 huko Kenya. Maudhui yake sawa na tungo nyingine nyingi za wakati huo, yaliegemea zaidi upande wa kufurahisha. Huu ni mchezo wa kuigiza unaotongoa maisha ya kijamii, lakini maudhui yake si mazito na hayazingatii hali ya jamii kujisaka na kujitafiti.
Henry Kuria, Kimani Nyoike, Gerishon Ngugi na B.M Karutu ni miongoni mwa wanafunzi wa mwanzo wa Graham Hyslop waliokuwa wakisoma katika shule ya Alliance High School. Hyslop ni mwingereza aliyekuwa katika utumishi wa serikali ya kikoloni nchini Kenya. Hyslop alianzisha kikundi cha maigizo kwa ajili ya askari waliopigana katika vita ya pili ya dunia, miaka ya 1950 alianza kutunga michezo ambayo iliigizwa na kikundi chake. Michezo yake ya mwanzo katika lugha ya Kiswahili ni Afadhali Mchawi (1957), naMgeni Karibu (1957). Inasemekana kuwa Mwingereza huyu (Graham Hyslop) ndiye mtu wa kwanza kuleta tamthiliya kwa lugha ya Kiswahili yenye kufuata kanuni zote za Ki-Arstotle. Mbali na  Henry Kuria, wanafunzi wengine wa Hyslop walioandika tamthiliya kwa Kiswahili ni Kimani Nyoike aliyeandika tamthiliya ya Maisha ni Nini mwaka 1955, B.M Karutu Atakiwa Polisi mwaka 1957 na Gerishoni Ngugi Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi mwaka 1961.
Mulokozi (1996), anadai kuwa kabla ya Graham Hyslop kuchapisha tamthiliya zake tayari kulikuwa na tathiliya za Kiswahili zilizoandikwa kwanza kabla ya kuigizwa jukwaani. Katika kutetea hoja yake Mulokozi anamtaja C. Frank na tamthiliya yake ya Imekwisha iliyochapishwa mwaka 1951, vilevile anadai kuwa tamthiliya nyingi katika kipindi hiki zilizugumzia masuala ya kidini, ziliandikwa na kuigizwa tu mashuleni na makanisani, lakini hazikuchapishwa vitabuni. Mtaala huyu wa fasihi ya Kiswahili anahitimisha hoja yake hii kwa kusema kuwa hadi tulipopata Uhuru, tamthiliya zote za Kiswahili zilizochapishwa ilikuwa zimeandikwa na Wakenya. Madai haya yanaugwa mkono na mtafiti wa utafiti huu.
Kipindi cha Uhuru,Coyle (1984), anadai kuwa, kabla ya miaka ya 1970, tamthiliya za Kiswahili zilikuwa chache sana, na nyingi kati ya chache hizo zilikuwa ni tamthiliya tafsiri, kwa mfano Mfalme Edipode, Mabepari wa Venisi, Julias Kaizari na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Tamthiliya hizi zilitungwa kwa kufuata kanuni za Ki-Aristotle na zilikuwa katika mtindo wa kishairi, nyingine zilizotungwa katika hali ya mazungumzo.
Mulokozi (1996), anaeleza kuwa tamthiliya ya Kizungu na zile za vichekesho ziliendelea kuandikwa na kuigizwa majukwaani. Tamthiliyaandishi ya Kiswahili ilishika kasi sana kipindi hiki, Ebrahim Hussein na Penina Muhando waliongoza katika uandishi wa Tamthiliya ya Kiswahili kwa wakati huu. Tamthiliya za kipindi hiki zilikuwa zikizungumzia masuala mbalimbali kama vile Migongano ya Kitamaduni ( mfano ‘Wakati Ukuta na Kwenya Ukingo wa Thim’), Matatizo ya Kijamii (mfano ‘Lina Ubani, Mke Mwenza, Hatia’), Dini (mfano ‘Aliyeonja Pepo, Maalim, Mukwava wa Uhehe), Ukombozi na Utaifa (mfano ‘Mkwawa Mhinya, Johari Ndogo, Kinjekitile, Tone la Mwisho, Harakati za Ukombozi’), Ujenzi wa jamii mpya (mfano, ‘Kijiji Chetu, Nuru Mpya, Giza Limeingia, Mashetani, Mwanzo wa Tufani, Kilio cha Haki), Uake na matatizo ya Kijamii (mfano, ‘Nguzo Mama, Ngozi, Machozi ya Mwanamke), Falsafa ya Maisha (mfano, ‘Kinjeketile, Kwenya Ukingo wa Thim) na Uchawi, Uganga na Itikadi za Jadi (mfano, ‘Njia panda (muhanika), Ngoma ya Ngw’anamalundi, Kinjeketile na Mafarakano).

 NANI MUASISI WA KUTUMIA KANUNI ZA KI – AFRIKA KATIKA TAMTHILIYA YA KISWAHILI?
Hoja hii ya nani mwanzilishi wa fasihi ya kiswahili ya kimajaribio katika uwanja wa tamthiliya ilianza kujitokeza katika miaka ya 1980 ki mabishano. Wahakiki wa mwanzo kabisa katika fasihi ya Kiswahili kama wakina Nkwera walianza kuizungumzia hoja hii mwishoni mwa miaka ya 1970 pasipo mabishano.
Miaka ya 1980 na kuendelea ilikuwa ni miaka iliyowapambanisha mafahari wawili katika uandishi wa tamthiliya ya kiswahili, Ebrahim Hussein na Penina Muhando walitawala fikra, majukwaa, mijadala na makabrasha ya wahakiki wa kazi za kifasihi.
Baadhi ya mawazo ya wahakiki nguli juu ya“nani muasisi katika matumizi ya kanuni za ki-afrika katika tamthiliya ya Kiswahili?”
Nkwera (1977), anachambua kazi mbalimbali za Ebrahim Hussein na Penina Muhando. Katika kujadili maendelao ya kazi za sanaa za Ebrahim Hussein, muhakiki huyu anamtaja Bretch, mwandishi hodari na wa pekee wa michezo ya kuigiza ya kimashariki. Nkwera anaanza kwa kusema:
“Hapo mwanzo Ebrahim Hussein aliathiriwa sana na Bretch katika utunzi wake. Lakini kadri alivyoendelea kustawi katika uandishi wake wa sanaa za maonyesho Ebrahim Hussein alianza taratibu kuchanganya jadi za kiafrika kama vile masimulizi, utambaji, mianzo pamoja na miisho ya kifomula katika uandishi wake. Hivyo Hussein ndiye mwandishi wa mwanzo kabisa aliyeanza kuzikiuka taratibu za kiuandishi katika tamthiliya zilizofuata kanuni za ki-aristotle kwa kuingiza ujadi wa ki-afrika katika kazi zake”.
Mhakiki huyu anahitimisha hoja yake hii kwa kujenga mazingira yanayoonyesha kuwa mwanzilishi wa fasihi ya kiswahili ya kimajaribio katika tanzu ya tamthiliya ya kiswahili ni Ebrahim Hussein, kwani ndiye mwandishi wa mwanzo kabisa aliyeanza kuzikiuka taratibu za kiuandishi katika tamthiliya zilizofuata kanuni za ki-aristotle. Nkwera ana hitimisha kwa kuchambua tamthiliya ya Mashetani ya Ebrahimu Hussein na Pambo ya Penina Muhando. Nkwera anasema:
“Pambo ni mchezo wa hali ya juu kimuundo. Hapana shaka yo yote kwamba Penina Mlama (hapo awali alijulikana kwa jina la Penina Muhando) ameathiriwa na Ebrahim Hussein kama Ebrahim Hussein alivyoathiriwa sana na Bretcht, mwandishi hodari na wa pekee wa michezo ya kuigiza ya Kimashariki. Nkwera anasisitiza kuwa kwa mtu aliyesoma Mashetani (OUP) hatasita kusema kuwa Mama Mlama kaathiriwa na Ebrahim Hussein katika uandishi wake. Jambo hili liwe ni kweli ama sivyo, Si jambo la msingi bali la maana zaidi nikufahamu tu kwamba waandishi hawa wawili wamejitokeza kuwa mafundi na mabingwa wa kuandika michezo ya kuigiza katika fasihi ya Kiswahili na ile ya kimajaribio”.
King’ei (1987), anamtaja Ebrahim Hussein kama mwandishi wa sanaa ya maigizo aliyefanikiwa katika kuchanganya mbinu za masimulizi ya mapokeo ya fasihi simulizi kama vile ngano na vitendawili, na ufundi wa fasihi andishi ambao ameutumia kutungia hadithi hizi kwa muundo wa maigizo jukwaani. King’ei anaitaja tamthiliya ya Jogoo Kijijini na Ngao ya Jadi ya Ebrahim Hussein kuwa mfano wa tamthiliya iliyoathiriwa sana na kumbo ya fasihi simulizi.
Wafula (1999), anautaja mwaka 1971 kuwa ni mwaka wa mabadiliko makubwa katika tasnia ya tamthiliya ya Kiswahili. Mhakiki huyu anamtaja E. N. Hussein na tamthiliya yake ya Mashetani, kuwa ni moja kati ya tamthiliya za mwanzo kabisa katika harakati za utumiaji wa kanuni za kijadi ndani ya kazi za kifasihi. Wafura anasema:
                            “Hussein alijitokeza tena uwanjani, akathibitisha ameidhibiti bahari ya tamthiliya kwa kutoa Mashetani. Tamthiliya ya Mashetani iliweka tarehe mpya katika utungaji wa mchezo wa kuigiza katika lugha ya Kiswahili. Tamthiliya hii ilionyesha kwa mafanikio makubwa, jinsi mapokeo ya kiafrika yanavyoweza kutumika pamoja na mbinu za kisasa kufanikisha malengo ya kijukwaa”.
Katika kutafuta udhibitisho kwa waandishi wenyewe wanaozungumziwa mvutano huu, utafiti huu ulifanya mahojiano na mama Penina Muhando kutaka kujua mambo kadhaa juu ya suala hili. Mwanafasihi huyu mashuhuri alilizungumzia suala hili kwa ufupi sana. Mama Muhando alisema:
“Vuguvugu la mabadiliko nchini Tanzania lilianza mwishoni mwa miaka ya 1970, katika kipindi hiki wasomi wengi wa kiafrika walianza kupinga taratibu za kimaisha zenye umagharibi (taratibu za watu wa Ulaya). Wasomi hawa waliutaja waziwazi ukoloni kama sababu kubwa iliyopelekea kuharibika kwa utamaduni wa kiafrika. Baadhi ya waafrika walianza kubadili majina yao yenye asili ya ukristo ama uislamu kwenda. Kipindi hicho tukiwa wasomi na wanaharakati vijana tuliadhimia kuleta mabadiliko kwenye sanaa ya kiafrika kwa kuzitumia kanuni za kiafrika hasa katika sanaa za maonyesho, ndipo sasa kanuni za jadi ya ki-afrika kama masimulizi, utambaji, mianzo na miisho ya kifomula zilianza kutumiwa na waaandishi. Ukweli ni kwamba katika kipindi hiki cha vuguvugu la mabadiliko Ebrahim Hussein alikuwa tayari ameanza kuugua maradhi yanayomsumbua hadi sasa, hivyo hakushiriki sana katika vuguvugu la mabadiliko haya”.
Muhando (2013);
“Mimi na wasanii wenzangu kipindi hicho tulitunga michezo mingi na kwenda kuicheza katika maeneo mbalimbali “live”, tuliandika michezo mingi sana yenye kanuni za kijadi na mingi kati ya michezo hiyo haijachapishwa na kwasababu kilikuwa ni kikundi michezo mingine sijui hata ilipo. Na unapozungumzia mageuzi ama mabadiliko katika tasnia hii ya sanaa za maonyesho usitazame kazi zilizoandikwa tu vitabuni na kuwekwa ujadi ndani yake, lengo la mabadiliko yetu kipindi hicho ni kuhakikisha kuwa sanaa za jukwaani zinaigizwa katika maeneo husika ya wanajamii na kuleta mwamko wa kimaendeleo zinakuwa na nguvu kuliko zile zinazoandikwa na kuishia kwenye vitabuni tu”.
Maelezo ya Muhando yanaonyesha mwelekeo kuwa yeye pamoja na wasanii wenzake kipindi hicho ndio walikuwa waanzilishi wa kutumia kanuni za jadi ya ki-afrika katika tamthiliya za kiswahili.
(Williady, 2013) katika Utafiti wake,  anaunga mkono mawazo ya Nkwera (1977), King’ei (1987), Wafula (1999), Sengo (1977), yanayodai kuwa mwasisi wa kutumia kanuni hizi katika tamthiliya za Kiswahili ni Ebrahim Hussein. Uungaji mkono huu umetokana na sababu moja kubwa. Mwaka 1971, Ebrahim Hussein alichapisha tamthiliya yake inayoitwa Mashetani, kama wasemavyo wahahiki kuwa Mchezo huu wa Mashetaniumekaa kishetani shetani ili msomaji au mtazamaji auelewe vizuri inampasa ajigeuze shetani katika ulimwengu wa chukulizi za kifasihi, ndipo atapata kuuelewa. Mwaka 1975, takribani miaka 4 baadaye tangu kuchapishwa kwa mchezo wa Mashetani,  Penina Muhando alichapisha tamthiliya yake inayoitwa Pambo, ama hakika Pambo ni mchezo wa kiwendawazimu wendawazimu, ili msomaji auwelewe vizuri inampasa kujitia katika wendawazimu wa kifasihi. Hakuna tofauti kubwa kati ya michezo hii miwili ya Mashetani na Pambo, inaonekana Penina Muhando alichota baadhi ya misingi ya Hussein katika uandishi wake. Haitoshi, mwaka 1976, Ebrahim Hussein alichapisha michezo yake miwili aliyoiweka katika kijitabu kimoja, Jogoo kijijini na Ngao ya jadi. Michezo hii imeandikwa kwa utaratibu wa fasihi simulizi, kuna ngano, watambaji, hadhira na kuna kuanza na kukamilisha kazi ya fasihi kikanuni (mianzo na miisho ya kifomula). Mwaka (1984), miaka takribani nane (8) baadaye Penina Muhando alichapisha tamthiliya yake inayoitwa Lina Ubani, tamhiliya hii inaonekana kuwa na sifa sawa na zile za Jogoo kijijini na Ngao ya jadi. Kwa hoja hii utafiti huu unaunga mkono mawazo ya Nkwera na wenzake kuwa mwasisi wa michezo yenye kukiuka taratibu za ki-aristotle na kufuata taratibu za jadi ya ki-afrika ni Ebrahim Hussin. Kauli hii ya kumtaja Ebrahim Hussein kuwa ndiye mwasisi wa tamthiliya hizi za kimajaribio haitoi ukweli kuwa Penina Muhando naye anaumuhimu mkubwa sana katika tamthiliya ya Kiswahili.
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-12-12T06:42:38Z 2021-12-12T06:42:38Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1712 <![CDATA[TAMTHILIYA YA MKUTANO WA PILI WA NDEGE]]>
.pdf   TAMTHILIYA YA MKUTANO WA PILI WA NDEGE.pdf (Size: 248.34 KB / Downloads: 3) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-12-12T06:21:33Z 2021-12-12T06:21:33Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1710 <![CDATA[TAMTHILIYA YA NGOMA YA NG’WANAMALUNDI (VIDEO)]]> ]]> false MwlMaeda]]> 2021-11-11T04:32:29Z 2021-11-11T04:32:29Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1445 <![CDATA[UCHAMBUZI WA TAMTHILIYA YA “HAWALA YA FEDHA”]]>
.pdf   UCHAMBUZI-WA-TAMTHILIYA-“HAWALA-YA-FEDHA”.pdf (Size: 148.47 KB / Downloads: 5) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-25T15:04:00Z 2021-06-26T00:23:38Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=268 <![CDATA[UCHAMBUZI WA TAMTHILIYA YA MFALME EDIPODE (NADHARIA YA URASIMI)]]>
1.0 Utangulizi…………………………………………………………………………….
1.1. Sababu za Anguko la Mfalme Edipode……………………………………………
1.2. Athari za Anguko la Mfalme Edipode…………………………………………….
1.3. Hitimisho……………………………………………………………………………..
 
1.4 Marejeleo…………………………………………………………………………………
 
 
1.0  UTANGULIZI
Mfalme Edipode ni tamthiliya iliyoandikwa na Sofokile (Sophocles) na kufasiriwa na Samwel S. Mushi mnamo mwaka 1993; tamthiliya hii imeandikwa kwa kufuata lugha ya ushairi ili kumpa hali ya mvuto msomaji.
Tamthiliya imejikita zaidi katika kuzungumzia anguko la Mfalme Edipode juu ya jamii yake ya Thebe, katika tamthiliya hii kuna wahusika wafuatao; Edipode ambaye ni mhusika mkuu na wahusika wengine kama vile Jokaste, Kreoni, Teresia, Kahini, pamoja na mtumishi, Mfalme Laio, Polibo na wengine.
Katika uchambuzi huu tumeongozwa na nadharia ya urasimi (Classicism). Nadharia hii huzingatia wakati maalumu ambapo misingi ya kazi za sanaa huwekwa na kukubalika kuwa vipimo bora kwa kazi nyingine, hivyo kila jamii ina urasimi wake.  Lakini urasimi wa fasihi ya Kiswahili ulikuwepo kati ya karne ya kumi na nane na kumi na tisa, na ule wa kimagharibi hasa Kigiriki na wa Kiroma ulikuwepo tangu karne ya nne (4) kabla ya Kristo na baada ya Kristo.  Nadharia hii huenda sanjari na tamthiliya ya Mfalme Edipode ambayo imejikita katika urasimi mkongwe kama inavyoelezwa na mwandishi Sofokile: alizaliwa Athens, Ugiriki mwaka 496 kabla ya Kristo na aliishi miaka tisini.  Aliishi nyakati ambazo mambo mengi yalikuwa yakitokea ugiriki. Hivyo michezo ya  kuigizwa ilipendwa  sana na Wagiriki wa nyakati hizo na maigizo hayo yalikuwa ya aina tatu;  Maigizo ya huzuni, maigizo ya vichekesho na maigizo ya huzuni na vichekesho.  Hivyo basi Mfalme Edipode alipata anguko.
Kulingana na TUKI (1990) Anguko ni hali ya kushindwa kwa kuendelea kwa jambo fulani, sasa basi Mfalme Edipode alipata anguko katika jamii ya Thebe na kuwa mwisho wa utawala wake katika jamii hiyo.  Anguko hilo la mhusika mkuu lilitokea kwa kuwepo kwa sababu mbalimbali hususani kuwepo kwa nguvu za kiungu.
1.1  SABABU ZA  ANGUKO LA MFALME  EDIPODE
i. Kuwepo kwa utabiri wa Mungu jua (Apolo) juu ya Mfalme Edipode, Mungu jua (Apolo) alitabiri kwamba mwana wa Mfalme atakayezaliwa atamuua baba yake na kumuoa mama yake. Hali hii ilitimia kwa Mfalme Edipode katika kipindi cha utawala wake ndani ya jamii ya Thebe. Hali hii ilitokea kwa kuwa  Mfalme Edipode hakutambua ukweli. Na nukuu:
  • Mchunga; Ndiyo bwana walisema kuna utabiri mbaya,

  • Edipode; utabiri wa Namna gani?

  • Mchunga; uliosema angelimuua baba yake na kumuoa mama yake (UK. 48)
Ujaala (majaliwa au utabiri) ya Mfalme Edipode; Baada ya utabiri Jaala ilitimia kwa Mfalme Edipode kwa kumuua baba yake na kumuoa mama yake kama mke na mume.  Hivyo basi mambo hayo yalisababisha madhara makubwa katika jamii ya Thebe kama vifo na njaa baada ya Miungu kukasirika na hatimaye kuwa sababu ya anguko la Kiutawala kwa Mfalme Edipode katika jamii ya Thebe.  Na nukuu:
“…Mauti kwenye rutuba na neema, mauti kwenye malisho ya wanyama, mauti kwenye tumbo la uzazi na maradhi yaliyo maambukizi…” (UK 2)
 
ii. Kutokujua historia ya jamii ya Thebe: Mfalme Edipode hakuijua historia halisi ya jamii ya Thebe kwani yeye alilelewa katika nchi ya Korintho chini ya Mfalme Polibo na
mkewe Melope.   Hivyo Mfalme Edipode aliamini kuwa hao ndio wazazi wake na hivyo alitambua vyema historia ya Korintho kuliko jamii ya Thebe. Na nukuu:          “Edipode akakua akawa mtu mzima akapendwa na wazee wake na kumlea na raia wa Korinto.  Wakamstahi kama mwana wa Mfalme wa Korinto lakini Edipode hakufahamu kwamba alikuwa mtoto wa kulelewa…” (XVI)
iii. Mfalme Edipode kutaka kujua juu ya madhara ya nchi yake Sanjari na jamii yake ya Thebe kutokana na madhara yaliyoikumba ikiwemo vifo pamoja na njaa.  Jamii ya Thebe ilikumbwa na madhara mengi ikiwemo kukumbwa na magonjwa najisi, Njaa, Ukame, maumivu ya uzazi, kwa mimea tasa, Barabara za mji zikawa na uvundo (Uk. 8 -9).  Hivyo ilipelekea Mfalme Edipode kutaka kujua madhara hayo yametokana na nini ndipo ukweli ulidhihirika kwamba chanzo cha hayo yote ni yeye mwenyewe juu ya jaala alizopata kutoka kwa Miungu ya Thebe.  Hivyo ilipelekea anguko kwa Mfalme Edipode kwa kuacha utawala ili kuepusha matatizo katika jamii ya thebe.
 
1.2 ATHARI ZILIZOIKUMBA JAMII YA THEBE  BAADA YA ANGUKO LA MFALME EDIPODE.
Kutokana na Anguko la mhusika mkuu Mfalme Edipode athari mbalimbali ziliweza kuathiri jamii nzima ya Thebe, waliohai, waliokufa, mizimu, na miungu.  Athari hizo ni kama ifuatavyo:
i. Watoto wa kike wa Edipode hawataweza kuolewa kwa sababu ni kizazi cha laana. Hii ina maana kuwa watoto wa Mfalme Edipode yaani Usmene na Antigone hawataweza kuolewa kwani ni kizazi cha laana iliyofanywa na Edipode kumuoa mama yake Jakasta ambapo Usmene na Antigone walipaswa kuwa wadogo zake. Na nukuu:
‘’Mtakapopata kuolewa, mtu gani, nani huyo atakuwa shujaa wa kutoijali najisi ambayo itawaletea mkosi wanangu na hata wajukuu wenu? Hivyo hii ni athari kwa waliohai.” (UK. 50-59)
ii. Kifo cha Jokaste,
Kutokana  na  utabiri  kuwa  Mfalme Edipode    atatembea  na mamaye  hivyo  baada  ya  malkia   kujua  ameolewa  na  mtoto wake  ilisababisha  malkia  kujinyonga  na kusababisha  anguko  la Mfalme  Edipode  ambaye  alijitoboa  macho kwa  ajili ya  kuficha  aibu  na kutaka  kutoyaona  mambo  yanayotendeka. Na nukuu:
Mtumishi: kwanza  kwa kifupi  Malkia.. kafa
Wazee:   roho maskini ajali  gani  hiyo?
Mtumishi: ni tendo la mkono wake mwenyewe… (UK. 50)
iii. Wananchi  wa  Thebe  kufa  kwa  njaa na magonjwa: Hii  yote ni kutokana na laana iliyo- wapata watu wa jamii ya thebe kutokana na Mfalme  Laio kuzaa mtoto ambaye alikataliwa na miungu na kusababisha miungu kukasirika.
 
iv. Miungu yao kuwalaani kwa kuwapa ardhi kame. Miungu kama Apolo na wengineo walilaani jamii ya Thebe na kuiathiri jamii hiyo kwa ardhi kuwa kavu na kame. Hivyo hii ni athari iliyokumba walio hai katika jamii ya thebe.
1.3 HITIMISHO
Anguko la Mfalme Edipode ni funzo tosha kabisa kwa viongozi wengi walio madarakani kutojua historia za nchi zao na hatimaye kusababisha athari kubwa ikiwemo vifo kwa jamii nzima.. Pia inatakiwa kufuatilia mawazo ya viongozi wetu waliopita na maonyo ya wazee juu ya uendeshaji wa nchi,. Mambo haya yaliyojitokeza katika tamthiliya ya Mfalme Edipode ni dhahiri kuwa yamejitokeza katika nchi mbalimbali za kiafrika na kusababisha kuanguka kwa utawala.
 
 
 
1.5 MAREJELO
 
Bakhressa S.K (1992); Kamusi ya maana na matumizi Oxford University press, Nairobi.
Njogu K. (2007); Nadharia za uhakiki wa fasihi, Industries Ltd, Nairobi
Njogu  K. (1999); Ufundishaji wa fasihi, Nadharia na mbinu; Autolitho Ltd; Nairobi
Sokofile (1993), Mfalme Edipode
Wamitila K.W (2003); kamusi ya fasihi Istilahi na Nadharia, Focus publications Ltd; Nairobi]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-25T14:39:41Z 2021-06-25T14:39:41Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=267 <![CDATA[NADHARIYA YA TAMTHILIYA NA DRAMA]]>
.pdf   NADHARIYA YA TAMTHILIYA NA DARAMA.pdf (Size: 289.2 KB / Downloads: 4) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-25T14:17:36Z 2021-06-25T14:17:36Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=266 <![CDATA[KIJUE KITABU KILICHOTUMIA MHUSIKA MMOJA TU]]> Karibu katika KAMUSI.
KAMUSINI leo tunaangazia Wahusika katika Fasihi.
Makala ya kamusi inaeleza kwa ufupi ni kwa namna gani lugha humfinyanga muhusika wa kazi ya fasihi.
Tuanze hapa, Lugha ndicho kipengele mahususi ktk taaluma ya fasihi. Ndicho kifanyacho fasihi ijuzu na kukidhi vigezo vya kuwa sanaa.
Lugha ndiyo huyajenga maudhui. Maudhui hayo hufumbatwa na wahusika walio katika kazi ya fasihi.
Kariba, raghba na tajiriba zao huelezwa na lugha kisanaa na kisanii.
Wahusika kama viumbe bunilizi wa msanii huumbwa na kufinyangwa na lugha.
Lugha imfinyangayo muhusika fulani huwa imeteuliwa kwa indhari na tahadhari kubwa na fanani ajuaye kazi yake.
Aghalabu lugha hutumika ktk kumweleza muhusika kiasi cha kumpa hisi hadhira kupata hata taswira ya muhusika mawazoni na akilini.
Lugha humweleza muhusika ukubwa wake , udongo, unyonge , ukali, ucheshi wake, kariba zake, weledi , tajiriba , maarifa , nk. Yote haya hufanywa na lugha.
Kwa hiyo, umbo , taswira , picha za ukubwa wa muhusika fulani, umwamba, ukonki, ushenzi, ufirauni, ukatili, uzwazwa, ujuha , uzuzu , uzezeta , ujasiri , ujemedari , uzalendo , uwanaharakati, unafiki, wema, upendo, uadilifu, na nk yote hayo hufanywa na namna lugha inavyomwelezea muhusika fulani.
Lugha ikimweleza muhusika bila shaka hadhira inaweza kuamua kumtambua kama muhusika fulani kama muhusika mkuu, msaidizi, Kivuli, bapa, mjivuni, shujaa, mkwezwa, duara , kinara, nk.
Yote haya hutegemea ni kwa jinsi gani lugha ilivyotumika kumsana, kumuumba na kumfinyanga muhusika fulani ktk kazi ya fasihi.
Muhusika kupitia lugha inayotumika kumuumbia inaweza kuchagiza hadhira kumpenda au kumchukia , kumtoa maana ama kumfanya kiigizi, au kinyume chake muhusika fulani.
Wahusika huumbwa na lugha kisha wao pia hutumika lugha hiyo kuyajenga maudhui ya kazi ya fasihi.
Kwa hiyo, wahusika ndio sauti halisi ya msanii/ mtunzi / fanani wa kazi ya fasihi. Hadhira/ Msomaji au msikilizaji wa fasihi akipata hisia za ubaya au uzuri wa muhusika fulani kiasi cha kumwaga chozi ati kwa sababu Hurem Sultana ametawafu basi ujue mtumzi wa kazi hiyo amefanikiwa sana.
Ukisoma Tamthiliya ya NJE- NDANI kwa mfano utabaini ni kwa namna muhusika mmoja alivyoumbwa kisanaa na watunzi ameweza kuibeba Tamthiliya hiyo mwanzo hadi mwisho.
NJE- NDANI ndiyo Tamthiliya ya kwanza katika fasihi ya Kiswahili kutumia muhusika mmoja tu. ( Haijapata kutokea kabla hii).
NJE- NDANI sasa ipo Chuo Kikuu cha Dodoma, MuM , Jordan – Morogoro.
Tuandikie : majidkiswahili@gmail.com Au +255 715 83 84 80.
Majid Mswahili
Mchambuzi wa Lugha, Fasihi na Fasaha ya Kiswahili
11/06/2019.
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-25T13:45:14Z 2021-06-25T13:45:14Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=265 <![CDATA[MATUMIZI YA DHANA NA SANAA ZA MAONYESHO ZA JADI KATIKA TAMTHILIYA ZA LEO]]>
.pdf   Matumizi ya Dhana na Sanaa za Maonyesho za Jadi katika Tamthiliya za Leo.pdf (Size: 207.92 KB / Downloads: 1) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-25T13:28:03Z 2021-06-25T13:28:03Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=264 <![CDATA[UWASILISHAJI WA MADA KUHUSU TAMTHILIYA YA KISWAHILI]]>
.pdf   UWASILISHAJI WA MADA KUHUSU TAMTHILIYA YA KISWAHILI.pdf (Size: 169.8 KB / Downloads: 2) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-25T13:07:46Z 2021-06-25T13:08:59Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=263 <![CDATA[MIKONDO YA TANZIA]]> Mikondo Minne ya Tanzia
Kuna mikondo minne ya tanzia, nayo ni: Tanzia ya Urasimi (Classical Tragedy), Tanzia ya Urasimi Mpya (Neo-classical Tragedy), Tanzia ya Kisasa (Modern Tragedy) na Tanzia ya Kikomunisti (Socialist Realism Tragedy).
i) Tanzia ya Urasimi (Classical Tragedy)
Hii iliweza kuwepo kutokana na tabaka la mabwanyenye kufadhili sanaa huko Ugiriki. Hivyo liliitumia tanzia kwa manufaa yake yenyewe. Mengi yanayojitokeza kwenye tanzia hizi ni kwa ajili ya kukudhi matakwa ya tabaka hili. Mambo yanayoonyesha hali hii ni ‘status quo’ ambapo mhusika mkuu sharti awe mtu bora ambaye kutokana na kutokamilika kwake kimatendo kwa ajili ya ubinadamu wake anapata janga ambalo linamtoa katika hali ya juu aliyokuwa nayo na kuwa
duni. Aidha, wakati wa urasimi fikra za watu ziliiweka miungu kama yenye kauli ya wema au uovu katika yote yaliyofanyika duniani; hivyo Soyinka, W. (1976) Myth, Literature and the African World. Cambridge: Cambridge University Press. Kurasa 37 – 608 Yaani ‘hali kama ilivyo’ mawazo haya yamesababisha mhusika mkuu kuangushwa na nguvu hizi za kiungu ambazo hawezi kushindana nazo. Nguvu hizi za kiungu hutawala matendo na matukio ya wahusika. Mawazo ya wakati huu yaliheshimu hadhi ya binadamu na kuyaona maisha yake yenye maana na kuthaminika. Ingawa binadamu si rahisi kueleweka (ni changamano), anahusika kwa njia moja au nyingine na masahibu yanayomkuta.
Katika tanzia hizi binadamu yu huru kufuata ushauri wake mwenyewe na ni katika kufanya hivi ndiyo tabia yake hujitokeza. Ukaragosi hauna nafasi katika tanzia. Karagosi siku zote haaminiki na hudharaulika, hivyo hafai kuwa mhusika mkuu. Anatakiwa mtu ambaye ingawa anakabiliwa na magumu yamshindayo, haonyeshi ukaragosi bali huwa na msimamo maalum. Lugha ilitumika pia kukidhi matakwa ya tabaka tawala. Lugha ya tanzia ilikuwa ya kishairi ambayo ilisababisha mgawanyiko kati ya watazamaji wa hali ya chini na ya juu. Waigizaji kutenganishwa na watazamaji kulisaidia upande mmoja kubugia yale ambayo upande mwingine uliyatoa. kuwepo kwa kiitikio/kibwagizo ilikuwa ishara ya demokrasia au sauti ya wengi. Mfano wa tanzia ya urasimi ni Mfalme Edipode9. Tanzia hii inaanza na hali mbaya ya magonjwa ya kufisha katika mji wa Thebe. Watu wa Thebe wanakusanyika kuzungumza juu ya janga hili. Inabainika kuwa
hali mbaya ya Thebe inatokana na kuuliwa kwa mfalme wa zamani Laio. Ili janga litoweke, sharti muuaji ambaye yu miongoni mwa watu wa Thebe apatikane. Mfalme Edipode anaamua kufuatilia jambo hili mpaka huyo muuaji aliyelaaniwa apatikane. Chanzo cha maovu katika tanzia hii ni utabiri wa hapo kale wa miungu kuwa mfalme Laio atauawa kwa mkono wa mwanawe mwenyewe ambaye pia atamwoa mama yake.
Katika uchunguzi wake anagundua kuwa yeye ndiye aliyemuua Laio na pia kumwoa mama yake. Haya ni matukio maovu ya utabiri ambayo waliohusika walijaribu kuyakwepa na kushindwa. Anapogundua tanzia yake, Edipode anajipofusha na kuhamia ughaibuni. Kabla janga halijamtokea mhusika mkuu, sharti apitie awamu tatu – ‘harmatia, perepeteia na anagnoris’. Tanzia ya urasimi ianzapo, mhusika mkuu anaonyesha dosari katika tabia yake – harmatia. Mara nyingi mhusika mkuu huwa amefikia hali aliyonayo sasa kutokana na dosari. Mhusika mkuu hubadilika pale Tanzia iliyoandikwa na Sophocles kati ya 430 na 425 BK. mambo yaanzapo kumwendea kombo, anapitia awamu ya perepeteia.
Licha ya mambo kumgeukia, anagundua kuwa ana dosari; kitu alichotenda kimesababisha mabadiliko kutoka ya ufanisi na kuwa ya kudidimia – anagnoris. Mhusika mkuu anapaswa kukubali kosa lake na kamwe hafanyi ajizi kwa kulikimbia janga linalomngojea (catastrophe). Janga linalotokea husababisha mhusika kufa au wapenzi wake kufa. Mara kwa mara hata ikiwa mhusika hafi, yanayompata ni mabaya zaidi ya kufa. Awamu zote ni kumfanya mtazamaji kuondokana na hisia (catharsis) ili awe mtu bora zaidi baada ya onyesho la tanzia.
ii) Tanzia ya Urasimi Mpya (Neo-classical Tragedy)
Wakati huu pia tabaka tawala limechangia katika kuifanya tanzia iwe kama ilivyo. Tabaka hili ndilo lililomiliki sanaa hivyo liliingiza mawazo yake katika tanzia. Huu ulikuwa wakati wa utaifa kwa Waingereza hivyo mambo mengi yaliyotokea nje ya taifa hili yaliachwa. Isitoshe, katika kudhamini tamthiliya, Ufalme wa Uingereza ulikataza tamthiliya ya kugusia mambo ya kidini na kitawala. Ufalme ulikuwa tayari kudhamini tamthiliya kama chombo cha kuleta burudani tu. Wakati huu kulikuwepo kwa mwamko wa kifikra uliojulikana kama ‘cartesian rationalism’ – ambao uliweka maanani sana tofauti kati ya umbo la ndani na la nje – hususan kuhusu tabia ya binadamu. Miungu na mashetani waliendelea kuwepo kwenye tanzia hizi na walikuwa na uzito. Ila kutokana na mwamko wa fikra mpya
uliokuwepo watu walifanya uchunguzi wa kina kwanza ili kupambanua kati ya miungu halisi na bandia.
Fikra hizi ambazo zilikuwa uzao wa tabaka tawala zilionekana kwenye tanzia wakati huu. Mhusika mkuu aliendelea kuwa wa tabaka la juu. Lugha iliendelea kuwa ya kishairi isipokuwa wakati mwingine watu wa chini waliongea lugha ya kawaida. Huu ni ubaguzi ambao ulibagua kati ya watazamaji wa kawaida na wale wa hali ya juu ambao walifuatilia vizuri zaidi matukio ya jukwaani.
Mwakilishi mkuu wa wakati huu ni William Shakespeare (1564 – 1616) ambaye licha ya kuona tanzia kuwa ni sababu ya uovu ambao mtu humtendea mwingine, hakwenda mbali kuonyesha undani wa mahusiano haya bali aliishia kwenye kuzingatia dhamira sana. Mara  nyingi mhusika wake kwenye tanzia alitatanishwa na dhamira yake mwenyewe. Mfano mzuri ni tanzia yake ya Hamlet12 ambayo mbali na kuonyesha uovu utendekao katika jamii pia kuna mvutano wa dhamira kati ya mhusika huyo huyo mmoja. Kazi zake nyingine ni kama vile Makbeth, Juliasi Kaizari, Tufani na Mabepari wa Venisi. Izingatiwe kuwa Shakespeare aliliandikia tabaka tawala hivyo katu hakuonyesha mgongano wa kitabaka. Alionyesha mambo kuwa ni ya kudumu na hayabadiliki.
iii) Tanzia ya Kisasa (Modern Tragedy)
Tanzia hii imechipuka kutokana na mabadiliko ya fikra na maisha yaliyotokea Ulaya katika karne ya 18. Huu ni wakati ambao ubepari ulianza kushamiri hasa kutokana na kuvumbuliwa kwa mashine ziendazo kwa mvuke (steam engines). Wakati huu ulijulikana kama Mapinduzi ya Viwanda (Industrial Revolution). Ni wakati ambao watu wengi iliwabidi kwenda mijini kufanya kazi viwandani. Miji ikafurika na hali mbovu za maisha zikajitokeza. Hali hii ikawafanya wafanyakazi hawa wawe na ufahamu wa unyonyaji uliokuwa ukiendelea. Msemo mashuhuri wa wakati huo, ‘watu wote wameumbwa kuwa huru na sawa’ ulichangia kwa kiasi kikubwa katika kujenga mawazo tofauti na yale ya urasimi mpya. Wanafalsafa
Auguste Comte na Charles Darwin walichangia kwa kiasi kikubwa kutokana na kazi zao za ‘Positivism’13 na ‘Origin of species’ zilizoandikwa karne ya 18. Wanafalsafa hawa walihamasisha watu kutumia sayansi kutumia sayansi katika maswala ya jamii kutafuta chanzo cha matatizo na kudhibiti matokeo yake. Walihamasisha watu kutafuta njia za kufanya ili maarifa yote yahudumie matakwa ya wakati uliopo.
Hivyo kila tawi la maarifa likajihusisha katika mambo ya wakati huo. Tanzia nayo ilienda sambamba na mabadiliko haya. Mungu au miungu haikuwa tena na nafasi yoyote kwenye maisha ya binadamu. Yote yaliyomsibu binadamu yalikuwa na chanzo chake katika maisha haya haya yenye kufahamika na milango mitano ya maarifa/hisi/fahamu. Rousseau anasimamia msimamo huu kwa kusema kuwa kiini cha uovu hutokana na jamii na sio nje ya jamii. Mhusika mkuu aliyekumbwa na janga alitoka katika ngazi yoyote ya jamii. Mhusika huyu alisakamwa na: mtu mwingine, nafsi yake na jamii.  Pia Falsafa ya Umbile. Hii ni falsafa inayozingatia tu mambo yanayoonekana na kujulikana vyema na wanadamu. Lugha nayo ikabadilika kutoka ya ushairi hadi ya kawaida ili kurahisisha mawasiliano. Iliunganisha kwa ufanisi zaidi mwigizaji na hadhira yake. Licha ya lugha kuunganisha mwigizaji na mtazamaji, bado kiini kikubwa cha tanzia kilibakia kuwa ‘Catharsis’ kama katika mikondo ya awali. Ingawa mtazamaji alijitambulisha na mhusika mkuu kwa yale magumu yanayompata, Steiner haoni kuangamia kwa mhusika mkuu kuwa ndio mwisho bali kulitoa fundisho kwa jamii kuwa inaweza kubadilika na hatimaye kupata mwisho mzuri. Huu mwisho mzuri ungepatikana aidha kwa kubadilisha hali mbaya ya maisha na kuwa nzuri au kupata mwisho mzuri kutokana na mawazo ya kidini ya maisha baada ya kifo. Henrich Ibsen (1828 – 1906) ndiye aliyeashiria mwanzo wa tanzia ya kisasa kuanzia 1870. Tanzia hizi zilionyesha jinsi misingi potovu ya jamii ilivyoangusha watu. Katika tanzia yake ‘Ghosts’ (Mizuka) mwanamke anashurutishwa kukaa na mumewe ambaye hampendi.
Isitoshe, ni mwanaume ambaye kutokana na tabia yake ametengwa na jamii. Mtoto wa kiume wanayemzaa anarithi kaswende kutoka kwa babake. Mwisho wa tanzia kijana wa kiume anahehuka na mama mtu anapata wenda wazimu. Matukio haya husababishwa kwa kwa sababu jamii hushurutishwa kufuata maadili potovu. Arthur Miller (1915 – ) katika tanzi yake ya ‘Kifo cha Mfanyabiashara’ (Death of a Salesman)16 iliyoandikwa 1949, anazungumzia mhusika mkuu Willy Loman ambaye ni mfanya – biashara. Katika maisha, yeye anataka apendwe, ajulikane na asifiwe. Anafahamu kuwa mambo yote haya anaweza kuyapata ikiwa atapata mafanikio maishani. Kwa Willy mafanikio ni utajiri na anaamini mtu hawezi kupendwa bila kuwa na mafanikio. Willy anadhani watoto wake hawampendi kwa sababu hajafaulu maishani. Watampenda tu kama atafanikiwa. Anaamini kuwa mapenzi ni kitu cha kutafutwa au kununuliwa na hakitolewi bure. Pia anawaeleza wanawake kuwa hawataheshimiwa kama hawatakuwa na mali. Anagundua mtoto wake Biff anampenda kwa dhati ingawa wote hawana mafanikio. Tendo hili linampa fununu kuwa amekuwa akiamini imani potofu. Fununu inatokea mwisho wa tanzia ambapo pia Willy anapata ajali ya gari.
Katika ‘A Doll’s House’, mwandishi Ibsen anaonyesha jinsi mhusika Nora anavyotaka kubadili maisha yake duni na magumu yanayosababishwa na mumewe. Nora anaamua kumwacha mumewe na watoto ili aweze kuamua mambo yake mwenyewe. A Doll’s House ni tanzia iliyoshambulia ndoa na maisha ya familia kuwa chanzo cha hali ngumu kwa wahusika. Hivyo kwa Steiner mhusika wa tanzia hii ya kisasa haangamii kabisa kwa sababu majibu ya matatizo yake yapo na kama ni anguko ni anguko la muda tu. Tanzia za kisasa zina mielekeo tofauti hasa ukizingatia kuwa mawazo ya binadamu hayana mipaka na watu sehemu mbali mbali hawabanwi na mawazo na itikadi za aina moja tu.
iv) Tanzia ya Kikomunisti (Socialist Realism Tragedy)
Tanzia hizi zimetokana na mawazo ya Marx na Ukomunisti ya kutaka kuleta jamii isiyo na matabaka duniani. Tanzia za aina hii ni za matumaini juu ya ushindi wa ujamaa duniani na lazima ziongelee kuhusu hilo tu. Ni mwiko kwa mhusika mkuu wa tamthiliya hizi kushindwa kuutangaza ujamaa duniani. Ni tanzia ionyeshayo jinsi jamii nzima inavyobadilika na kuwa ya kikomunisti. Mwisho wa tanzia hizi
hutakiwa kuwa mzuri kwa ushindi wa ujamaa.
Mawazo yaliyotawala tanzia hizi yalitokana na chama cha Ukomunisti huko Urusi na ni fikra ambazo zililazimishwa kwa wanaotawaliwa hasa ukichukulia kuwa jamii hiyo pia ililazimishwa kuwa ya mfumo wa chama kimoja. Matabaka ya wakati wa Kigiriki na wa Shakespeare hayatofautiani ya kipindi hiki. Wananchi wa Urusi walilazimishwa kubugia mawazo ambayo hawakuyapenda. Huu toka mwanzo ulikuwa ukandamizaji wa haki za binadamu au uwepo wa uovu kama katika matabaka yote yaliyotangulia. Wahakiki wa tamthiliya hii wanaposema tanzia haina nafasi katika jamii yao ni kuwakoga wananchi kuwa wategemee
maisha yasiyowezekana. Lugha iliyotumika ni ya kawaida ili kuleta maelewano bora kati ya waigizaji na watazamaji. Kulikuwepo na mtengano maalumu kati ya
mwigizaji na mtazamaji. Miungu haina nafasi kubwa kabisa kwenye tanzia hizi. Mhusika mkuu wa tanzia hizi ambaye ni mhusika aliyejengwa kipropaganda kwa manufaa ya siasa ya kikomunisti huitwa mhusika mkuu wa matumaini. Naye ana sifa zifuatazo:
o Yeye ni mfano kati ya mifano.
o Amefikia kiwango cha juu zaidi cha ubinadamu, hana ubinafsi.
o Hana makosa yoyote (kama anayo ni madogo sana kama kukasirika hivi wakati fulani fulani). Na anaweza kuwa na mambo yasiyofaa ya kujiosha akielekea kwenye kiwango cha juu cha maisha lakini yasiwe kikwazo kwake.
o Lazima aielewe siasa barabara.
o Awe na akili.
o Awe na moyo wa ushupavu.
o Awe na uzalendo.
o Aheshimu wanawake.
o Awe tayari kujitoa mhanga.
o Ana msimamo mmmoja tu; nao ni kufikia kilele cha ukomunisti. Hachanganyi weupe na weusi.
o Akipatwa na shida anajua ni lazima aikwepe ili afikie lengo lake.
Mfano mzuri wa tanzia hizi ni ‘The Measures Taken’20 ya Brecht. Katika tanzia hii, mhusika mkuu – The Young Comrade – anajitoa muhanga ili wenzake waweze kueneza ukomunisti nchini China. Brecht hakuwa muasisi wa tanzia hizi isipokuwa alikubali kubadili jamii.
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-25T13:00:32Z 2021-06-25T13:00:32Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=262 <![CDATA[TAMTHILIYA YA BIBI TITI MOHAMED NA PROF. EMMANUEL MBOGO]]> Tamthiliya hii inahusu Bibi Titi Mohamed. Titi alikuwa kiongozi shupavu aliyeupipgania uhuru wa Tanganyika kwa ujasiri mkubwa akiwa mwanachama wa TANU na kiongozi wa Umoja wa Wanawake. Wakati wanaume wengi walipokuwa wakiogopa kukata kadi za TANU, wakhofia kufukuzwa kazi na mkoloni, Titi aliwahamasisha wanawake kote nchini kuupigania uhuru wa Tanganyika
Kitabu kinaanza mwaka wa 1970 kwa kumuonesha Bi. Titi akiwa Gereza la Isanga Dodoma, moja ya magereza magumu Tanzania. Kabla yake mwaka wa 1953 mwanasiasa mkubwa sana Tanganyika sehemu za Maziwa Makuu, Ali Migeyo alifungwa gereza hilo na Waingereza kwa kosa la kufanya mkutano wa siasa Kamachumu bila idhini ya serikali. Miaka 17 baadae mpigania uhuru Bi. Titi yuko kifungoni kwa kuhusika na kesi ya uhaini kutaka kuiangusha serikali aliyoipigania wakati wa kudai uhuru.
Akiwa hapo gerezani Bi. Titi anaandika historia ya uhuru wa Tanganyika na anaeleza ushirikiano wake na Nyerere wakati wakiwa katika ofisi ya TANU New Street. Bi. Titi anaeleza katika mswada wake, anaoandika jela vipi yeye na wenzake walipita mtaa kwa mtaa kueneza TANU.
Kitu cha ajabu Gereza la Isanga wanamuomba Bi. Titi watumie historia yeke ile kufanya onyesho la historia ya uhuru wa Tanganyika.
[Image: UaCj2HX7kWcRvzy3Az5CTtgufV1I1FtGPvbT8Xwd...46-h659-no]
Bi. Titi akiwa katika moja ya matawi ya TANU Dar es Salaam tawi hili lilikuwa Magomeni Mapipa nyumbani kwa Ali Msham Mtaa wa Jaribu 1955
[Image: tTRTeOOZOOEnRd4Z5Se7kCkFQvldNUen4fJjA6Ja...77-h659-no]
[Image: 1SoH8DK4E3Rp_beqWUyYroAl-85hb9m-PN4bznGL...70-h526-no]
Picha ya Mwandishi aliyopiga Viwanja Vya Mnazi Mmoja mwaka wa 1966 nyuma yake ni barabara iliyokuja kujulikana baadae kama Titi Street kwa kumuenzi Bi, Titi Mohamed na ukivuka barabara hiyo linaloonekana ni Soko la Kisutu maarufu kama ”Soko Mjinga.”
Tamthilia hii ya Bi. Titi Mohamed ni kazi ya kupigiwa mfano kwani naamini hii ni tamthilia ya kwanza ambayo imejaribu kuhadithia historia ya TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kuwataja wale ambao waliupigania uhuru wa Tanganyika. Kurasa za mwanzo Mwandishi anamleta Schneider Plantan akizungumza na Boi Selemani kuhusu TANU.
Bwana Boi akimlalamikia Schneider kuwa mkewe Bi. Titi hatulii nyumbani kwa ajili ya shughuli za TANU kiasi imekuwa yeye ndiyo mfuaji wa nguo zake na mpishi wa chakula chake.
Boi Selemani alikuwa dereva wa taxi.
Schneider yeye ana historia ndefu katika siasa za Tanganyika. Yeye ndiye aliyesimama kidete kuwaleta vijana wasomi katika TAA ili kuwaondoa wazee waliokuwa wamechoka na kuifanya TAA isifanye siasa za maana kwa ajili ya ukombozi wa Tanganyika.
Hii ilikuwa mwaka wa 1950.
Sasa TANU ilipokuja kuasisiwa mwaka wa 1954 Schneider ndiye aliyemleta Bi. Titi katika TANU pamoja na wenzake akina Tatu Bint Mzee na wanawake wengine kuja kukipa nguvu chama.
Tamthilia inaanza mwaka wa 1955 wakati Bi. Titi na wenzake wako katika hekaheka ya kuhamasisha wananchi kujiunga na TANU na wakati huo ndiyo safari ya Julius Nyerere kwenda UNO inatayarishwa.
Boi katika mazungumzao yake na Schneider anatabiri kuvunjika kwa ndoa yake na mkewe Bi. Titi kwa ajili ya TANU na anamtupia lawama zote rafiki yake Schneider Plantan kwa kumpeleka mkewe TANU.
Boi analalamika hadi kufikia kusema, ”Titi mwanamke wa Kiislam. Kasoma madrasa….Bibi Titi kapanda jukwaani…hana baibui…”
[Image: Z6-fQpBJ-lRfA2xmvcOGq9RAPspFuBFrJ_17576x...79-h659-no]
Bi Titi Mohamed na Julius Nyerere wakihutubia wananchi Uwanja wa Jangwani 1955
[Image: Jk3j6Mf4o1KdhJppiFYzyOyBfPfECav6eFwMT5Ib...91-h659-no]
Kulia ni Bi. Titi Mohamed, Clement Mtamila, Sheikh Suleiman Takadir, Julius Nyerere na nyuma ya Nyerere ni Maria
Nyerere, Rajab Diwani na John Rupia
Kitabu hiki, ”Malkia Bibi Titi Mohamed,” ukikianza hukiweki chini hadi umekimaliza.
]]>
false