MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
<![CDATA[JIFUNZE KISWAHILI - Ushairi]]> https://jifunzekiswahili.co.tz/ 2024-04-27T10:02:33Z MyBB MwlMaeda]]> 2022-12-19T03:41:28Z 2022-12-19T03:41:28Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2875 <![CDATA[SHAIRI: HIVI KWA NINI TWAVAA?]]> Wasomi na wasomaji, tujadili hili jambo,
Tusibaki waigaji, kukimbilia mikumbo,
Lisilo na mfumbaji, la mavazi hili fumbo,
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Pengine twajivalia, kuona kama urembo,
Vile tukishika njia, kuyaonesha maumbo,
Tuanze kuwasumbua, wenzetu waende kombo,
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Wazazi wametwambia, nasaa zao ni wimbo,
Hakuna wa kusikia, kuacha mambo ya ng'ambo,
Viwalo twajitupia, Kwa wengine huwa fimbo,
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Fumbuka nakufumbua, mavazi hubeba nembo,
Mvaaji akivaa, twajua ni mwendakombo,
Vema akijivalia, tutasema hiki chombo,
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Mitindo tumeizua, kuweka wazi matumbo,
Yatatoka kwenye pua, kuigaiga wa mombo,
Laiti tungalijua, tungalivaa masombo,
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Mitindo ikiingia, twanata kama ulimbo,
Bila ya kufikiria, thamani ya letu umbo,
Hapo tunang'ang'ania, na kuleta majigambo,
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Uzungu watuzuzua, kwa mitumba yenye shombo,
Jambo ninaloshangaa, hivi tumelewa tembo?
Maungo kujiachia, wanzuki ama zarambo?
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Mtu aliyetimia, kichwa, mabega na tumbo,
Akili akatumia, kung'amua haya mambo,
Hawezi kuangukia, pasipo kuramba bambo,
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Siwezi kuendelea, nanga nakitia chombo,
Jambo hilo shikilia, acha kuiga wamombo,
Mbona wewe twakujua, umezaliwa Matombo?
Dhima ya kwanza mwilini, yatusitiri mavazi.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-08-23T04:52:03Z 2022-08-23T04:52:03Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2808 <![CDATA[SHAIRI: CHOZI]]> Alipokuwa kufani, pumzi ikimkwama,
Aliniita pembeni, maneno akiyasema,
Sijitie kilioni, machozi ukayafuma,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Hata ukilia sana, useme olele mama,
Bure wajitesa mwana, tatizole litakwama,
Kisha macho yatatuna, aibu kujitazama,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Useme uvue nguo, ukaanza kulalama,
Wala hupati funguo, tatizo kuliandama,
Hakina kitu kilio, wajongezea dhahama,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Kwa tatizo yake dawa, uanze kulisakama,
Mwishowe kulitatatua, kwa busara na hekima,
Wako moyo utapowa, furaha ukiifuma,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Wakati tukifiliwa, mfano baba na mama,
Moyo hutaki kutuwa, machozi hujaa pima,
Vipi wanafufuliwa? mwisho vichwa vyatuuma,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Tupatapo mitihani, ya mabonde na milima,
Mikono huwa kichwani, tulie olele mama,
Mwisho tunapata Soni, kulia mtu mzima,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Nilikuwa bado kinda, alipofariki mama,
Kilio sikukishinda, nililia Kama kinda,
Huku kule nilikwenda, yani aamke mama,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Chozi halikubadili, kwa punje au alama,
Sikuziona dalili, aamke wangu mama,
Ndipo likumbuka mbali, maneno aliyosema,
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Siku niliyoamini, chozi halina salama,
Yangu hapo sithamini, kulivisha koja jema,
Machozi ni kitu duni, aminj ninayosema,.
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Kwa heri wanazuoni, ndugu zangu maulama,
Nimefika ukingoni, ndiyo yangu kaditama,
Kulialia ya nini, bure kujitia homa?
Halina thamani chozi, aliniusia mama.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-07-30T10:16:09Z 2022-07-30T10:16:09Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2796 <![CDATA[SHAIRI: HANI NIPO KITANDANI]]> haloo!hanii halo, Rwaka hani wasikia?
Ndio hapo sawa halo, vipi unaendelea?
Tatizo nililonalo, lazizi ninaugua,
Hani nipo kitandani, taabani hali yangu.

Wala sijahama njia, nitafika huko Rwanda,
Ikinijia afia, na wangu mwili kuwanda,
Basi huko nitatua, unione mie kinda,
Sasa nipo kitandani, taabani hali yangu.

Ila ninayo pumzi, bado moyo unahema,
Bora nikweleze wazi, kinifanyacho kukwama,
Matatizo ya uzazi, ndiyo yaloniandama,
Jua nipo kitandani, taabani hali yangu.

Ina machungu dunia, na mie yamenikuta,
Nusu niage dunia, kwa tumbo kunikeketa,
Japo nimeamkia, bado najivutavuta,
Ila nipo kitandani, taabani hali yangu.

Maradhi yanaghasia, Karagama sikiliza,
Yakishakuangukia, dira unaipoteza,
Mwilini nimelegea, vile nimepata siza,
Love nipo kitandani, taabani hali yangu.

Nitahama nikipona, Tanzania sitarudi,
Na wewe tukionana, itatulia fuadi,
Ila sasa raha sina, Darling I feel bad,
Vile nipo kitandani, taabani hali yangu.

Namshukuru Karima, ningali hai mpenzi,
Ninaungoja uzima, japo kutwa nakuenzi,
Ningelikufa mapema, ungelipata simanzi,
Hapa nipo kitandani, taabani hali yangu.

Na mie napata ganzi, nikikukosa kijana,
Heri kunipiga konzi, utosini nitapona,
Sitahimili majonzi, na wewe tukikosana,
Japo nipo kitandani, taabani hali yangu.

Maumivu yamezidi, yanikataza kutunga,
Kuacha imenibidi, utungo huu kufunga,
Ila ninakuahidi, huko Rwanda nitatinga,
Nikitoka kitandani, iwe njema hali yangu.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-07-27T18:17:07Z 2022-07-27T18:17:07Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2793 <![CDATA[SHAIRI: UCHAWI]]> Jamani niambieni, akipatapacho mchawi,
Huko awako gizani, mbona ya Mana hayawi,
Pasi na nguo mwilini, lake baridi mchawi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mchawi hupenda tabu, hapendi mambo rahisi,
Kona anaziharibu, apite kwa wasiwasi,
Mlangoni hajaribu, apite kwa urahisi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Yake kazi kuharibu, akageuza kizazi,
Ili unapojaribu, huoni chako kizazi,
Hapo hawana sababu, mambo yao ni ushenzi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Japo yu mtu mkubwa, chamani kuheshimika,
Tabiaye kama mbwa, anapotaka kuruka,
Na baridi atakumbwa, hana nguo kujivika,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Juzi nilipata kesi, mtu katiwa kifafa,
Matabibu na manesi, wakadhani amekufa,
Mwisho katoa kamasi, tukagundua hajafa,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mchawi akifahamu, una kitu kumzidi,
Jua umejipa sumu, kukuroga hana budi,
Utateswa kwa awamu, ukuishe ukaidi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Msiwaone vichaa, kidhani yote ya Mumba,
Wengine tukashangaa, ovyo waanza kuimba,
Wachawi walishakaa, kuchanganya mitishamba,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mtu umesoma sana, Mara vyeti huvioni,
Kumbe walishagawana, watandike kaburini,
Miaka kazi hauna, uchawi ni ushetani,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Machawi yake hasara, ulie yeye acheke,
Wala haimpi fora, hadharani asifike,
Kiumbe mwenye mikwara, japo asifaidike,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mchawi mtu wa ila, mambo yake ni kinyume,
Usiku sie twalala, yu uchi atutazame,
Na hawi tajiri wala, kiwa wongo na aseme,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Sasa ninafunga beti, utungo siendelezi,
Msijenishika shati, ati nimewapa kazi,
Naona bora niketi, kuandika nimesizi,
Jamani niambieni, akipatapacho mchawi.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-07-25T16:26:50Z 2022-07-25T16:26:50Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2791 <![CDATA[SHAIRI: NAINGOJA SIMU YAKO]]> Nimeamka mapema, nimekaa kitandani,
Mawazoni nimezama, ninakuwaza mwandani,
Fikira zimenihama, nipo kwako ewe hani,
Naingoja simu yako!

Mara nasimama wima, ghafla nakaa chini,
Mpenzi nashika tama, bila wewe mimi nyani,
Wewe wangu maulama, wanitia tulizoni,
Naingoja simu yako!

Usidhani nalalama, nijinadani mnadani,
Moyo wangu unauma, Mimi nicheze na nani?
Au simu ulizima, upo kwea kitandani?
Naingoja simu yako!

Sio mwingi wa lawama, nakuomba samahani,
Kwakowe nimetuama, kama somba mtungoni,
Haki kwako nimekwama, mithili mwiba kooni,
Naingoja simu yako!

Basi uamke vema, pasi mavune mwilini,
Nakungoja mtu mwema, unijuze hali gani,
Hamu bado hijakoma, kukusubiri mwendani,
Naingoja simu yako!

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-07-22T02:23:03Z 2022-07-22T02:23:03Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2787 <![CDATA[SHAIRI: NIMPENDE NANI ?]]>
Mwenzenu nipeni rai kwa haya yalonifika
Moyo wangu haukai, kwa hapa nilipofika
Japo naona nishai,  moyoni nimewatika
Kati ya hawa wawili, Nipende nani zaidi?

Huyu  wa kwanza mpole ,  tena si muongeaji
Kama simba mwenda pole, kwenye ufatiliaji 
Hutembea polepole ,amdake mwiwindwaji
Kati ya huyu nayule jama  nimpende nani?

Huyu wa pili  mweusi , kapanda juu kidogo
Mwenye pua ya kitusi,  mwili mwembamba kidogo
Mtalamu wa kukisi,utadhania mgogo
Kati ya huyu na yule ,jama  nimpende nani?

Akili inanituma , wa pili awe mwandani
Ninategemea mema ,sitotoka asilani
Kama ikiwa salama ,nitasota uvunguni
Kati ya hawa wawili Nimpende nani?

Nilikuwa na furaha,nimefika maskani
Nikayaanza madaha, nikavipata vya ndani
Nilishazika karaha,ninapokuwa chumbani
Alivyokuja wa pili , Moyo wangu umeshindwa

Wa pili yeye mcheshi , muda wote tabasamu
Ni kweli kuwa achoshi ,twacheka kama binamu
Kwangu hamu haiishi, jama mpeni salamu
Kati ya Hawa wawili nimpende nani?

Wa kwanza ananijali, kwa pesa nayo mahaba
Nikimuuzi hajali,  hunilea kama baba
Na hunijulia hali,  upendowe sio haba
Wanagenzi mnijuze nimpende yupi?

Rama  karibu javini ,  unipe  jibu murua
Na wengine karibuni, jibu nataka kujua
Nitomuweka moyoni,  kofuli kumfungia
Kitendawili tegua  Yupi kwangu anafaa?

DINNA ( MOM J )
21/7/22
KUWA TAYARI KUHESABIWA
MPE USHIRIKIANO KARANI WA SENSA??]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-06-13T03:21:04Z 2022-06-13T03:21:04Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2598 <![CDATA[SHAIRI: KUJUWA NI MATATIZO]]>                   KUJUWA NI MATATIZO
 
            Lugha yangu ya asili, niijuavyo si haba, najivuniayo sana
            Lakini hii ya pili, ni Kizungu chanikaba, uwelevu nayo sina
            Ndipo juzi Jumapili, akanitanza swahiba, tukaanza kuvutana
            Aliniambia: Silly!, nikadhani anshiba, kumbe yuwanitukana!
 
            Kuelewa ni kuzuri, hukukinga na kujuta, ukawa hutazozana
            Hukupunguza kiburi, ukadharau kuteta, ukapenda kushikana
            Ja vile kaka Saburi, alivyonitia tata, mpaka nikadangana
            Na nilipomshauri, aliponambia: Better, hapo hapo nikakona
 
            Si mjinga kama gude, huzitumia fikira, nawambia muelewe
            Bao latezwa kwa ndude, na kazi ni za majira, yakupasa uyajuwe
            Nenda skuli 'sidode, ujinga una izara, yasikufike na wewe
            Naliambwa: Hey dude!, nikajibu kwa hasira:, Na wewe dude mwenyewe!
 
           Kujiweka nyumanyuma, jambo hilo likataye, usiwatwe mkiani
           Utafanyiwa hujuma, wenzako wakukimbiye, uulize: Kulikoni?
           Jana mimi nilikwama, nikasema nimwambiye, hanong'ona sikioni
           Akasema: Don't murmur, hasema: Mama nnaye, sijui wateka nini!
 
          Kimombo tulokikopa, kina sisi chatuuma, chatukutisha madhila
          Kisa hiki ningakupa, japokuwa chanitoma, kina funzo la sahala
          Sima twali twaichapa, akaingia Fatuma, akatuona tukila
          Akanita: Juma's papa, hamba: Papa si wa Juma, lakini waweza kula
 
 
         Mohamed Khamis.
         Takaungu, Kenya
          12.6.2022]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-05-05T06:48:50Z 2022-05-05T06:48:50Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2542 <![CDATA[SHAIRI: POLE YAKO MAKANYILA]]> Usifurahi mwanzoni, kauli huikumbuki?
Yule mtunga diwani, alisema kitu hiki,
Sasa umekuwa nyani, umezua taharuki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.

Kutunga nimekawia, kwa shibe sitamaniki,
Juzi ulisimulia, una wengi marafiki,
Sifuri umeambua, na nyumbani hubanduki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.

Yalizidi maakuli, jambo hili liafiki,
Tukajaziwa bakuli, pilau nyama na siki,
Na ule mweupe wali, ukaliwa kwa samaki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.

Wale wapenda mtindi, hawakukosa wanzuki,
Tulikesha kama bundi, hadi mida ya mswaki,
Watu vikundi vikundi, tukaisahau dhiki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.

Mdomo waacha wazi, kwa hili unahamaki,
Wajawe wanakuhizi, vile unavyojinaki,
Na ujuwe siku hizi, marafiki wazandiki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.

Sasa wakuna sharubu, kimepita kitu hiki,
Imekufika taabu, hakuna wakukulaki,
Njaa ilikuadhibu, na kwako vile hupiki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.

Kijiko umenunua, ukiwa mwenye mithaki,
Kesho wenda kujilia, kula kwako hukumbuki,
Mee! sasa unalia, umenuna haucheki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.

Lifika kukusalimu, na hapa kwako sibaki,
Ilivyonifika hamu, viporo vilivyobaki,
Nikale mbuzi kwa ndimu, na leo kwangu sipiki,
Idd tumekula sisi, pole yako Makanyila.



Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-04-15T19:18:53Z 2022-04-15T19:18:53Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2512 <![CDATA[SHAIRI: KEMEENI VIGOMA]]> Ngoma hizi mchezazo, hali wazi maungoni,
Zinaleta angamizo, mnadhani hatuoni?
Basi zitiwe katazo, hivi mwatufunza nini?
Vikemeeni vigoma.

Kina mama hususani, lawama nawangushia,
Nauliza mwafanyani, ngomani mkisogea?
Kujitia fedhehani, nasi tukiangalia,
Hivi twajifunza nini?

Enyi wapiga vigoma, kina baba maarufu,
Sikieni ninasema, acheni huo uchafu,
Mnatutia kilema, tusiwe waadilifu,
Acheni hiyo tabia!

Serikali Mtukufu, uliye chombo imara,
Ondoeni usumbufu, maadili wanopora,
Taifa hulikashifu, adabu ikose dira,
Kamateni wachezaji.

Wachezavyo ni hatari, sikia habari hizi,
Vyote viungo vya Siri, twaviona siku hizi,
Hata nyie mtakiri, walikofika walezi,
Sheria zichukuliwe.

Yanatufika madhila, watoto tutazameni,
Tunalala bila kula, walezi wapo ngomani,
Ndoani amani Wala, tunabaki madharani,
Watoto tunateseka.

Taona barabarani, wameunda misafara,
Watoto nao njiani, hujiunga misafara,
Hivi wanapata nini, kiongezacho fikira?
Washitakini Wazazi.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
Cosmas shukuru]]> 2022-04-07T21:35:13Z 2022-04-07T21:35:13Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2504 <![CDATA[SHAIRI: NANI ATAKUWA WAO?]]> false MwlMaeda]]> 2022-04-04T02:04:34Z 2022-04-04T02:04:34Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2497 <![CDATA[SHAIRI: ROBO FAINALI CAF: NI SIMBA YA TANZANIA]]>
Ni usiku saa nne,
Huu ni mwezi wa nne,
Tumefunga goli nne,
Simba Robo Fainali.

Ndege tutazidi panda,
Jinsi tunazidi shinda,
Hata dau linapanda,
Simba Robo Fainali.

Wachezaji hongereni,
Na makocha hongereni,
Viongozi pongezini,
Simba Robo Fainali.

Katika ukanda huu,
Simba ndiyo timu kuu,
Katika mpira huu,
Hiyo Robo Fainali.

Siyo Kombe la Azam,
Hiyo pokea salam,
Huko kwa wataalam,
Simba Robo Fainali.

Lingekuwa goli moja,
Wangeinuka pamoja,
Sasa waishiwa hoja,
Simba Robo Fainali.

Wamepigwa Form Foo,
Magoli manne goo,
Na wenyeji wao loo,
Simba Robo Fainali.

Walikuwepo wachawi,
Wakidhania hayawi,
Wameshapakazwa kiwi,
Simba Robo Fainali.

Kesho itisha presi,
Wandugu wenye mikosi,
Hii foo jii kasi,
Simba Robo Fainali.

Amsha amsha yetu,
Tunalala roho kwatu,
Acha wenye roho butu,
Simba Robo Fainali.

Simba tunaisifia,
Heshima kwa Tanzania,
Hapo ilipofikia,
Hiyo zaidi ya dili.

Tembelea Tanzania,
Vile watutangazia,
Wengi wataangalia,
Huko Robo Fainali.

Watalii wakifika,
Uchumi ukajengeka,
Sote tunafaidika,
Simba Robo Fainali.

Ni Simba ya Tanzania,
Robo imeshaingia,
Heri tunaitakia,
Izidishe kwenda mbali.

Robo fainali CAF,
Simba timu maarufu,
Ni mpira maradufu,
Chaenea Kiswahili.

Na Lwaga Mwambande (KiMPAB)
lwagha@gmail.com 0767223602]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-04-02T14:18:48Z 2022-04-02T14:18:48Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2494 <![CDATA[SHAIRI: YAMENIGANDA MAPENZI]]> Mapenzi anayejua, kwa hili simshangazi,
Haya yakishakutua, kukung’uta hauwezi,
Vile hukung’ang’ania, kama chawa kwenye vazi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Miaka imekimbia, tutengane na lazizi,
Fikirani hunijia, kumkataza siwezi,
Picha inanirudia, m atukio ya miezi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Heri angekuwa Tanga, Shinyanga kwenda siwezi,
Uchumi unanizinga, huko mbali sikatizi,
Sasa nimebaki bunga, sioni lenye tatuzi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Niliapo ni msiba, hayakatiki machozi,
Uso wangu nauziba, nizuie michirizi,
Haki nimekuwa zoba, mwenyewe ninajihizi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Jambo linaniumiza, mtu huyo ni mzazi,
Ameoa naeleza, na watoto kwa mashazi,
Ijapo najikataza, kufanya makumbukizi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Nikiona zake picha, mimi chali sijiwezi,
Nawaza kila kukicha, nimezidi siku hizi,
Roho yanambia ‘acha’, ila moyo mchokozi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Tatizo wake upole, kufoka huyu hawezi,
Nakumbuka siku zile, mweledi wa mapepezi,
Basi ilikuwa vile, bila yeye sijilazi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Bwana huyu mtalamu, mithili kaenda kozi,
Yake mabo ni matamu, hadharani sielezi,
Ni kama mbuzi kwa ndimu, alikuwa mganguzi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Yana ajabu mapenzi, yakianza hayasizi,
Marefu kama utenzi, wenye beti jozi jozi,
Na ukiwa mwanafunzi, hutaweza piga mbizi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Nilidhani Mjaluo, kwa urefu mchokozi,
Weusi wenye vutio, afaa kwa matumizi,
Nikakiweka kituo, kwake sikupitilizi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Kijana wa Kimanyema, kiliko chake kizazi,
Ni mkoani kigoma, Tabora yake makazi,
Kwa sasa ameshahama, yupo Shinyanga kikazi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Kweli mahaba huua, kwa hili sibishilizi,
Nimekonda hadi pua, sijisifu siku hizi,
Heri zirudi hatua, hadi kwenye mwakajuzi,
Sipendi sasa naumwa, yameniganda mapenzi.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-03-02T02:03:37Z 2022-03-02T02:03:37Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2418 <![CDATA[SHAIRI: MWENDANI]]>
1. Mwendani wako mwendani, ukitaka umjuwe
Ngia naye safarini, mwenende mwendo wa kuwe
Au muate nyumbani, ukatembee ukawe
Akosapo kuwa mwewe, huyo ni wako mwendani

2. Mwendani wako mwendani, ukitaka mjuato
Mpishe ndia zenye mwani, zenye miba na tototo
Au mbwagie zani, ambayo kwamba ni nzito
Akuonyapo mapito, huyo ni wako mwendani

3. Mwendani wako mwendani, ukitaka mfeeli
Moyowo utie kani, utumie yakwe mali
Umuonapo haneni, hakuregeza kauli
Hashabihi hamithili, huyo ni wako mwendani

- Muyaka bin Haji (mshairi wa Mombasa, aliyeishi baina ya mwaka 1776 na 1840).

*mwenende- mwende
*mwendo wa kuwe - mwendo mrefu; masafa marefu
*muate - mwache
*ukawe - uchelewe
*akosapo kuwa mwewe - asipokunyakulia/asipokuibia chako
*ukitaka mjuato - ukitaka kumjua vizuri
*mpishe ndia - mpitishe njia
*tototo - tope
*mbwagie zani - mwangushie balaa; mpe tatizo kubwa
*akuonyapo mapito - akikuonesha njia za kupita (ili kutoka kwenye tatizo hilo)
*ukitaka mfeeli - ukitaka kumtenda/kumjaribu
*moyowo - moyo wako
*hakuregeza kauli - hakusema neno; hakulalamika
*hashabihi hamithili - hakutoa hata ishara ya kulalamika au kukasirika]]>
false
John John]]> 2022-02-15T07:02:47Z 2022-02-15T07:02:47Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2400 <![CDATA[Pendo lidumisheni]]> MTUNZI: JOHN L. JOHN

Mwenzenu nawatafuta, utungo niwaghanie,
Kuna mambo nimepata, nataka niwaambie,
Pendo lenu dumisheni, lisitiwe walakini.

Kwanza, Mola muombeni, yeye ndiye kimbilio,
Awajalie amani, kila iitwapo leo,
Pendo lenu adumishe, lisitiwe walakini.

Pili, msiwe wepesi, yasemwayo kuamini,
Upeni muda nafasi, ukweli kuubaini,
Pendo lenu dumisheni, lisitiwe walakini.

Tatu, shirikianeni, kwani umoja ni nguvu,
Utengano kataeni, hata kama kwa mabavu,
Pendo lenu dumisheni, lisitiwe walakini.

Nne, vumilianeni, hasa nyakati za shida,
Zenye nyingi tafurani, zisokuwa kawaida,
Pendo lenu dumisheni, lisitiwe walakini.

Mti ulio na tunda, ni sawa na lenu pendo,
Wapo watu huliwinda, lianguke kwa kishindo,
Pendo lenu dumisheni, lisitiwe walakini.

 Mtunzi: JOHN LUKAS JOHN

                0788514751/0747225775
Baruapepe: jjohnlukas0788@gmail.com]]>
false
MwlMaeda]]> 2022-01-21T04:10:54Z 2022-01-21T04:10:54Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=2267 <![CDATA[SHAIRI: CHOZI]]> Alipokuwa kufani, pumzi ikimkwama,
Aliniita pembeni, maneno akiyasema,
Sijitie kilioni, machozi ukayafuma,
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Hata ukilia sana, useme olele mama,
Bure wajitesa mwana, tatizole litakwama,
Kisha macho yatatuna, aibu kujitazama,
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Useme uvue nguo, ukaanza kulalama,
Wala hupati funguo, tatizo kuliandama,
Hakina kitu kilio, wajongezea dhahama,
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Kwa tatizo yake dawa, uanze kulisakama,
Mwishowe kulitatatua, kwa busara na hekima,
Wako moyo utapowa, furaha ukiifuma,
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Wakati tukifiliwa, mfano baba na mama,
Moyo hutaki kutuwa, machozi hujaa pima,
Vipi wanafufuliwa? mwisho vichwa vyatuuma,
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Tupatapo mitihani, ya mabonde na milima,
Mikono huwa kichwani, tulie olele mama,
Mwisho tunapata Soni, kulia mtu mzima.

Nilikuwa bado kinda, alipofariki mama,
Kilio sikukishinda, nililia Kama kinda,
Huku kule nilikwenda, yani aamke mama,
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Chozi halikubadili, kwa punje au alama,
Sikuziona dalili, aamke wangu mama,
Ndipo likumbuka mbali, maneno aliyosema,
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Siku niliyoamini, chozi halina salama,
Yangu hapo sithamini, kulivisha koja jema,
Machozi ni kitu duni, aminj ninayosema,.
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Kwa heri wanazuoni, ndugu zangu maulama,
Nimefika ukingoni, ndiyo yangu kaditama,
Kulialia ya nini, bure kujitia homa?
Halina thamani chozi, alinihusia mama.

Mtunzi Filieda Sanga
Mama B
Mabibo Dsm
0753738704]]>
false