MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
MyBB Internal: One or more warnings occurred. Please contact your administrator for assistance.
<![CDATA[JIFUNZE KISWAHILI - Tafsiri na Ukalimani]]> https://jifunzekiswahili.co.tz/ 2024-04-27T16:32:12Z MyBB MwlMaeda]]> 2021-12-19T04:25:42Z 2021-12-19T04:34:59Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1769 <![CDATA[UTANGULIZI MUHIMU KATIKA TAFSIRI NA UKALIMANI]]>
.pdf   TAFSIRI NA UKALIMANI(0).pdf (Size: 1.66 MB / Downloads: 23) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-12-03T02:59:16Z 2021-12-03T02:59:16Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1646 <![CDATA[CHANGAMOTO ZA KUTAFSIRI KAZI ZA FASIHI NA ATHARI ZAKE KATIKA ULINGANISHAJI]]> Mwandishi
Sephania Kyungu
Simu: 0756719643
Gmail: Sephaniakyungu1996@gmail.com
Iks UDSM 2019
@masshele swahili.
Iksiri
Katika makala hii tumeabili maana ya tafsiri, historia ya tafsiri hususani katika kazi za fasihi, pia tumeeleza maana ya ulinganishi au fasihi linganishi. Aidha, katika kiini cha makala hii tumechambua changamoto anuai ambazo zinawakumba wafasiri wa kazi za kibunifu pamoja na athari za kazi hizo zinazotafsiriwa katika uga wa fasihi linganishi.
1.0 Utangulizi
Tafsiri, Mwansoko (2015) anaeleza kwamba ni zoezi la uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha moja hadi lugha nyingine. Mwansoko (k.h.j) akimnukuu Catford (1965) anasema kuwa kutafsiri ni kuchukua mawazo yaliyo katika maandishi kutoka lugha moja (lugha chanzi) na kuweka badala yake mawazo yanayolingana kutoka lugha nyingine (lugha lengwa).
Anaendelea kueleza kuwa ili kufanikisha tafsiri ni lazima uzingatie mambo mawili ambayo ni: mawazo yanayoshughulikiwa ni sharti yawe katika maandishi na si vinginevyo, pia ujumbe/mawazo katika lugha chanzi na lugha lengwa sharti yalingane.
Kwa hakika hakuna tafsiri iliyosawa kabisa na matini lengwa ndiyo maana Catford akadai sharti yalingane na siyo mawazo sawa, hii inatokana na changamoto za kiisimu, mtindo, historia, utamaduni na tofauti ya semi na tamathali za semi. Changamoto hizi ndizo zilizochambuliwa katika kiini cha makala haya.
Kwa ujumla fasili ya Mwansoko (k.h.j) imeeleza mambo yote ambayo ni ya msingi katika fasili ya tafsiri.
1.1 Historia ya Tafsiri ya Fasihi
Mwansoko (2015) na Mshindo (2010) wanadai kuwa kumbukumbu zinaonyesha kwamba kutafsiri kulianzia zamani sana hata kabla ya Kristo. Wanaendelea kueleza kuwa sayansi na taaluma nyingi zilianzia Misri kwenye miaka ya 3000 na zaidi kabla ya kuzaliwa Kristo zilienea mataifa ya Ulaya kwa njia ya tafsiri kupitia kwa wataalamu wa Kiyunani. Wataalamu wa Ulaya walitafsiri kwa Kilatini vitabu kutoka kwenye ulimwengu wa Kiislamu vilivyokuwa vimetafsiriwa kwa Kiarabu kutoka kwa Wayunani na kuvipeleka kwao Ulaya na kuchota maarifa yaliyokuwamo ndani yake.
Wanaendelea kueleza kuwa kazi nyingi za kutafsiri ziliibuka karne ya 12 na kushika kasi karne ya 19 na 20. Katika karne iliyopita matini nyingi zilizotafsiriwa zilikuwa za kidini, fasihi, sayansi na falsafa.
Karne ya 20 inajulikana kama karne ya tafsiri kutokana na wimbi kubwa la tafsiri. Mwansoko (2015) anaeleza kuwa Hamziyya ni utenzi wa Kiarabu uliotungwa karne ya 13, anaendelea kwa kusema kuwa karne ya 19 Wamisionari walitafsiri vitabu vingi vya Kikristo kwa Kiswahili na baadhi ya lugha za makabila makubwa ya Tanzania.
Wakati wa ukoloni maandiko mengi ya fasihi ya Ulaya na Asia yalitafsiriwa kwa Kiswahili. Kwa mfano:
Hekaya za Abunuasi
Alfu – Lela – Ulela
Robinson Krusoe na Kisawe Chake
Baada ya uhuru wazalendo walichovya katika tafsiri. Kwa mfano Nyerere alitafsiri tamthiliya mbili ambazo ni Mabepari wa Venisi na Juliasi Kaisari.
1.2 Fasihi Linganishi
Kabla ya kufasili dhana ya fasihi linganishi ni vema tukaanza kwa kueleza dhana ya ulinganishaji. TUKI (2014) ulinganishaji ni kufanya tathimini ya vitu viwili au zaidi ili kujua ubora, kufanana na kutofautiana kwa vitu hivyo.
Hivyo, mlinganishaji anapotaka kufanya shughuli hii sharti awe na ujuzi wa vitu vilinganishwavyo, kuwepo kwa vitu viwili vinavyolinganishwa na kuwepo kwa kigezo au vigezo maalumu vya kulinganisha.
Aidha, fasihi linganishi Boldor (2003) akimrejelea Campbell (1926) anaeleza kuwa ni taaluma inayochunguza uhusiano uliopo baina ya fasihi mbili au zaidi nje ya mipaka ya kitaifa kwa njia ya kulinganisha mfanano na msigano. Kwa ujumla, tunaweza kusema kuwa fasihi linganishi ni taaluma inayojishughulisha na uchunguzi na uchambuzi wa uhusiano na usigano uliopo baina ya fasihi mbili au zaidi zinazohusisha vipengele tofauti vya kiutamaduni, itikadi, historia n.k.
2.0 Kiini
Katika sehemu hii tumeangazia changamoto zinazomkabili mfasiri wa matini za kifasihi na athari zake katika ulinganishaji. Katika sehemu hii tutaanza kwa kuangazia changamoto za kutafsiri matini za kifasihi.
2.1 Changamoto za Kiisimu
Massamba (2004)  anadai kuwa isimu ni taaluma ya ufafanuzi, uchambuzi na uchunganuzi wa lugha kwa kutumia mbinu za kisayansi.
Anaendelea kueleza kwamba lugha zote duniani zina  msingi wa kipekee katika vipengele vyake kiisimu (fonolojia, mofolojia, sintaksia na semantiki) hutofautiana.
Hakuna lugha mbili au zaidi ambazo zina muundo unaofanana kiisimu. Mutie (1997) akimnukuu Newmark (1990) anasema kwamba matatizo yanayohusiana na tafsiri yatakwisha pale muumano wa kiisimu utakapowasilishwa katika nadharia ya tafsiri.
Kwa hiyo, kukosekana kwa muumano wa kiisimu kati ya lugha chanzi na lugha lengwa ndiyo unaosababisha changamoto katika kutafsiri matini za kifasihi. Mathalani, riwaya, tamthiliya na ushairi.
2.1.1 Changamoto y Leksia
Fekih (2018) anadai katika kiwango hiki, tunatazama maneno na msamiati iliyotumiwa na mwandishi wa matini chanzi na visawe vyake katika matini lengwa. Aidha, katika kiwango hiki cha leksia kuna changamoto za aina mbalimbali ambazo mara nyingi hujitokeza wakati wa kutafsiri matini za kifasihi, ambazo ni:
Matumizi ya visawe visivyo sahihi, changamoto hii inasababishwa na kutokuwepo na muumano mzuri katika lugha chanzi na lugha lengwa ama athari au upungufu wa mfasiri husika. Changamoto hii inajidhihirisha katika tafsiri ya Robinson Crusoe.
Kwa mfano:
Na.
Matini Chanzi
Ukurasa
Matini Lengwa
Tafsiri Sahihi
01.
Sand bar
6-8→16-19
Mwambani
Fungu la mchanga
02.
Mountainous waves
6→16
Mawimbi makubwa
Milima ya mawimbi
03.
Tossed
6→17
 Likainua
Likarusha
04.
Thirty foot
6→17
Futi ishirini
Futi thelethini
05.
Good swimmer
6→18
Muogeleaji hodari
Muogeleaji mzuri
Chanzo cha tafsiri sahihi TUKI (2014)
Kwa ujumla, changamoto ya tafsiri katika kiwango cha leksia unajidhihirisha kuwepo kwa uteuzi mbaya wa visawe kutoka katika matini lengwa jambo ambalo huondoa uzuri wa kazi ya fasihi.
Matini za kifasihi zinafungamana sana na utamaduni hivyo, mfasiri anapaswa kuzingatia utamaduni wa jamii ya matini chanzi pia ubunifu wa msanii.
Matumizi ya kisawe kimoja katika maneno zaidi ya moja, hii ni changamoto nyingine katika kutafsiri kazi za fasihi.
Kwa mfano, katika tafsiri ya riwaya ya Robinson Crusoe kisawe kimoja kinatumika kurejelea leksia zaidi ya moja katika matini lengwa. Tatizo hilo linapotosha maana pia, huwafanya hadhira kutatanika katika kupata ujumbe uliokusudiwa.
Mathalani, neno land katika (Uk. 6) lilijitokeza mara mbili na kulitafsiri kwa maneno tofauti tafsiri moja “nchi kavu” (Uk. 17) na tafsiri ya pili “ufukoni” (Uk. 18).
Pia, neno land limejitokeza (Uk. 33) na mfasiri kalitafsiri kama “kisiwa” katika (Uk. 33).
Hivyo, matumizi ya kisawe kimoja kurejelea maneno zaidi ya moja katika matini inasababisha upotofu wa maana. Ikiwa kisawe kinarejelea maneno zaidi ya moja katika matini lengwa husababisha hadhira ishindwe kuelewa kisawe kipi ni sahihi na hata kushindwa kupata maana iliyokusudiwa.
Neno la jumla kulitafsiri kimahususi na neno mahususi kulitafsiri kimajumui, hii ni changamoto kubwa katika kutafsiri matini za kifasihi. Kwa mfano, katika  Robinson Crusoe, mfasiri neno bonds katika (Uk. 62) mfasiri alitafsiri kama “kamba” (Uk. 66) wakati bonds linajumuisha kitu chochote ambacho kinatumia na kufungia kama vile “kamba”, “mnyororo”, “pingu” au “waya”. Aidha, neno mahususi hutafsiriwa kama neno majumui. Kwa mfano, neno crew (Uk. 51) mfasiri kalitafsiri kama “watu” (Uk. 49) wakati neno crew linarejelea wafanyakazi wa melini. Kwa maana hiyo, tafsiri iliyotolewa ni ya kiujumla kwani si kila mtu anaweza kuwa mfanyakazi wa meli lakini kila mfanyakazi wa meli huwa mtu.
Katika changamoto hizo hapo aidha husababishwa na kukosekana kwa kisawe katika matini lengwa au udhaifu wa mfasiri mwenyewe.
2.1.2 Changamoto za Kisintaksia
Feki (2018) anadai kuwa katika kiwango hiki kuna changamoto katika mjengeko wa tungo kati ya lugha chanzi kwenda lugha lengwa, hii inatokana na ukweli kwamba kila lugha ina mjengeko wake wa tungo.
Mathalani, katika Bwana Myombekere na Bi Bugonoka na Ntulanalwo na Bulhwali.
“…tena watoto wasipokuwapo husingizia kwa mbwa.” (Uk. 435)
“Siri isiyokuwemo na jamaa yako atashitukia kifo.”
Chanzo, Mwansoko (2015)
Bila shaka maneno yaliyoandikwa kwa hati ya italiki yanaleta mushkili katika muundo wa sentensi. Ingawa hatuna matini chanzi ya Kikerewe lakini tunaweza kubashiri kuwa maneno yaliyowekwa kwa hati ya italiki ama yanaweza kuondolewa kabisa au kubadilishwa maumbile endapo kungetumika sintaksia ya Kiswahili.
“…tena kama watoto hawapo, husingizia mbwa.”
“Siri isiyokuwemo jamaa yako atashitukia kifo.”
Chanzo, Mwansoko (2015)
Changamoto kama hizi katika kutafsiri matini za kifasihi zinatokana na athari za lugha ya kwanza ya mfasiri. Hii ni changamoto kubwa katika matini nyingi, si tu katika  Bwana Myombekere na Bi Bugonoka na Ntulanalwo na Bulhwali bali hata kazi zingine mathalani, Robinson Crusoe.
 Hii inatokana na ukweli kwamba hakuna umahiri mkamilifu katika lugha mbili.
2.1.3 Kiwango cha Semantiki
Semantiki ni kipengele cha kiisimu kinachochunguza maana katika lugha, kipengele hiki hutafiti maana za maneno katika tungo (Habwe na Karanja, 2004). Fakih (2018) anadai kwamba inapofanyika tafsiri ya matini chanzi kwenda matini lengwa huwa tunahawilisha maana na ujumbe uliokuwepo ndani katika matini chanzi kwenda matini lengwa. Kwa mfano, katika riwaya ya Robinson Crusoe.
Na.
Matini Chanzi
Matini Lengwa
Tafsiri Sahihi
01.
Sand bar
Mwambani
Fungu la mchanga
02.
Tassed
Likainua
Likarusha
03.
Thirty foot
Futi ishirini
Futi thelathini
04.
Dragged
Lilinichukua
Liliniburuta
05.
Jagged
Jabali kubwa
Jabali lenyeincha
Chanzo cha Tafsiri sahihi ni TUKI (2014)
Matokeo ya changamoto hii ni kupotosha maana na ujumbe wa matini chanzi na hata kuondoa ushikamani wa maana na ujumbe wa matini hizo.
2.2 Changamoto za Kiutamaduni
Utamaduni ni mkusanyiko wa mila na desturi za jamii inayotumia lugha moja mahususi kama njia ya mawasiliano (Newmark, 1988), kwa kuongezea zaidi Wanjala (2011) naye anasema kuwa zinatofautiana katika utamaduni na hili ni tatizo kwa mfasiri kuliko tofauti za kiisimu. Kwa mfano, katika riwaya ya Robinson Crusoe, changamoto za kiutamaduni zimejitokeza kwa kukosekana ulinganifu katika kiwango cha neno. Hali hii imetokana na matini lengwa imekosa usawa wa moja kwa moja kwa neno lililojitokeza katika matini chanzi. Hivyo, mfasiri hulazimika kuweka maneno yanayokidhi ujumbe katika mawasiliano kwa hadhira pokezi ijapokuwa maneno hayo siyo msamiati halisi iliyotumika katika matini chanzi.
Mfano 1:
Matini Chanzi
Matini Lengwa
Brandy
Mvinyo
Rum
Mvinyo
Wine
Mvinyo
Chanzo, Fakih (2018)
Tukichunguza katika kifani hicho hapo tunaona kwamba neno brandy, rum na wine ni aina ya pombe ambazo zinapatikana katika utamaduni wa lugha chanzi kwa vile katika utamaduni wa jamii ya lugha pokezi hakuna aina hiyo ya pombe kama hizo husababisha mfasiri kuzipa kisawe cha aina moja, ambacho ni “mvinyo”. Changamoto hii inaikumba kazi nyingi za tafsiri hususani zile fasihi kwani hufungamana sana na utamaduni.
Mfano 2: Song of Lawino – Wimbo wa Lawino
Majina ya mimea: Lugoro, Ober, Lyamo, Ocuga, Omar, Lakara n.k.
Majina ya ngoma: Otele, Moko, Ogodo, Bwola, Orok, Lacucuka n.k.
Majina ya majira: Ager, Pato, Kot, Ondunge n.k.
Mavazi maalumu: Odiye, Lacomi n.k.
Hata mwandishi aliyaacha hivyo katika katibu cha Song of Lawino ingawa kitabu hicho alikitafsiri yeye mwenyewe kutoka katika lugha ya Kiacholi ambayo ndiyo aliyokuwa ametumia kwanza. Maneno hayo yalishindwa kutafsiriwa kwenda lugha nyingine kutokana na ufungamano wa moja kwa moja na kabila la Waacholi.
Chanzo, Mtesigwa (2015)
2.3 Changamoto ya Mtindo
Masoko (2015) mtindo ni changamoto kubwa katika tafsiri, anasema mtindo ndiyo unatia uhai, utamu wa hadithi, hii pia si kavu ina ukwasi mwingi wa tamathali za semi. Kwa mfano, katika riwaya ya  Bwana Myombekere na Bi Bugonoka na Ntulanalwo na Bulhwali.
“Njoo ukale na mgeni, apate kula vizuri, sababu ugali wa kula pekee yako, kama umezao kula pamoja na wengine, huwezi kushiba vizuri, hapana.” (Uk. 221)
“…hakuweza tena kuzidi kutamani kuwa na maisha mendi hivyo duniani hapana.” (Uk. 590)
Katika mifano hiyo hapo, ingawa tunaweza kusema kuwa mbinu hii inasisitiza ukiushi, lakini pia ni tabia ya Kikerewe kuwa na vikanushi katika sentensi. Hali hii imehifadhi uasili wa matini chanzi na kupuuza mtindo wa matini lengwa ambayo ni ya Kiswahili.
2.4 Changamoto za Misemo, Nahau, Methali na Vitendawili
Mwansoko (2015) kwa kawaida misemo au tamathali za semi, nahau, methali na vitendawili husukwa kwa kutumiwa kwa kufungamana sana na utamaduni wa watu fulani. Anaendelea kueleza kuwa uchoraji wa dhana zinazowakilishwa na mafungu haya ya maneno siyo tu hufanywa kwa usanii wa hali ya juu bali pia mila, desturi, imani, historia, mazingira na falsafa ya watumiaji wa lugha wanaohusika. Hali hii husababisha changamoto kubwa kwa mfasiri pindi anapotaka kufanya kazi yake.
Kwa mfano:
       Nahau
Kata mbuga.
Mkono wa birika.
Kuongea kwa herufi kubwa.
      Methali
Mpanda ngazi hushuka.
Haraka haraka haina baraka.
Nazi mbovu ni harabu ya nzima.
       Vitendawili
Mzungu wangu daima hubebwa na watumishi 4.
Wazungu wawili wanachungulia dirishani.
Kuku wangu anatagia mibani.
       Tamathali za Semi
Ujana ni maji ya moto (sitiari)
Kwa mujibu wa Kihore (1991) anaeleza kwamba mafungu haya yana changamoto mbili. Changamoto ya kwanza ni kupatikana kwa visawe vyake kimuundo vya mafungu kama haya katika matini lengwa na kupatikana kwa visawe mwafaka vya dhana au maana yake katika lugha lengwa. Aidha, Mwansoko (2015) anajaribu kueleza namna ya kutanzua changamoto hii ambapo anadai kuwa mfasiri hana budi kutafuta misemo yenye maana zinazokaribiana na zile zilizomo katika matini chanzi bila kuzingatia muundo wake. Hii inatokana na ukweli kwamba katika tafsiri kitu kinachoangaliwa sana ni maana na si muundo.
3.0 Athari za Tafsiri katika Ulinganishaji
Katika sehemu hii tutaangazia athari za tafsiri katika ulinganishi, hususani katika uga wa fasihi.
3.1 Tafsiri Imesaidia katika Kuibuka kwa Nadharia ya Fasihi Linganishi
Ponera (2014) anaeleza kuwa lengo la nadharia ya fasihi linganishi ni kuchunguza na kufanana na kutofautiana kwa kazi ya fasihi ya Tanzania na kazi za mataifa mengine hasa Amerika na Ulaya hususani katika vipengele mbalimbali hasa vya kiutamaduni pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Kwa hiyo, kutokana na maelezo hayo ni wazi kuwepo kwa kazi nyingi za mataifa ya nje zilizotafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili na zile ambazo hazijatafsiriwa, ni sababu tosha ya kuanzisha nadharia hii mpya ya fasihi linganishi. Mfano wa kazi zilizotafsiriwa ni:
Mkaguzi wa Serikali
Mkaguzi Mkuu wa Serikali
Mfalme Edipode
3.2 Tafsiri Inaathiri katika Ulinganisho wa Utamaduni
Newmark (1988) anaeleza kuwa utamaduni ni mkusanyiko wa mila na desturi za jamii moja inayotumia lugha moja mahususi kama njia ya mawasiliano. Tafsiri inaathiri katika ulinganishaji kwani inatusaidia kufanya ulinganishi kati ya jamii/taifa au bara katika kipengele cha utamaduni. Kwa mfano:
Song of Lawino    -       Wimbo wa Lawino
             Majina ya Mimea:
Logoro, Ober, Lyanno, Ocuga, Labwor Omar, Lakura n.k
             Majina ya Ngoma:
Otole, Moko, Ogodo, Bwola, Orak, Lacucuku n.k.
             Vyeo vya Watu, Miungu:
Odure, Agik, Alyker, Ojebu, Nyandyang n.k.
Chanzo, Mtesigwa (2015)
Katika kifani hicho, tunaona mfasiri ameshindwa kufasiri maneno hayo ambayo ni ya utamaduni wa Kiacholi kwenda Kiswahili, hii inatupa ushahidi kuwa utamaduni wa Kiacholi na Kiswahili haufanani.
3.3 Tafsiri Imesababisha Kuongezeka kwa Kazi za Fasihi kwa Kiswahili
Mulokozi (2017) anaeleza kwamba fasihi kwa Kiswahili ni fasihi iliyotafsiriwa kutoka taifa lingine. Tafsiri imesaidia kuibuka kwa kazi za fasihi kwa Kiswahili ambazo kwa hakika zimesaidia sana kuongezeka kwa tafiti za fasihi linganishi. Kwa mfano, utafiti wa Fekih (2018) na Serem (2018).
3.4 Tafsiri Imesaidia Kuenea kwa Fasihi ya Kiswahili Ulimwenguni
Tafsiri imesababisha kuenea kwa fasihi ya kiswahili ulimwenguni kwa mfano Kasri ya Mwinyi Fuadi Dei Sklaverei de Gewiize. Kazi nyingine kama vile Uhuru wa Watumwa kwenda Kiingereza, Rose Mistika, Bwana Myombekere na Bi Bugonoka na Ntulanalwo na Bulhwali. Hizi ni baadhi ya kazi zilizotafsiriwa kwenda mataifa mengine, hivyo na kusaidia kukuza shughuli ya ulinganishaji katika uga wa fasihi.
4.0 Hitimisho
Ulinganishi ambao kwa kiasi kikubwa unategemea taaluma ya tafsiri pia una athari hasi kubwa hususani kwa lugha lengwa na kwa utamaduni wa lugha lengwa. Kwa mfano, baadhi ya tabia ambazo ni za asili ya Kiafrika au utamaduni wa Mwafrika leo haupo tena kama zamani. Hii ni kutokana na athari za kazi zilizotafsiriwa kusomwa na watu wengi na kuona kama utamaduni huo ndiyo faafu kwao kuliko tamaduni zao za awali.
MAREJELEO
Fekih, A. H. (2018). “Changamoto za Kutafsiri Riwaya: Mifano kutoka Tafsiri ya Riwaya ya Robinson Crusoe” Tasnifu ya Uzamili: Chuo Kikuu Huria. (Haijachapishwa)
Habwe, J. na Karanja, P. (2004). Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi: Phoenix Publishers.
Kihore, Y. M. (1991). “Miundo ya Kisarufi Katika Tafsiri: Matatizo na Utatuzi” Makala Yaliyotolewa Katika Semina ya Mafunzo kwa Wafasiri wa Kiswahili. Dar es Salaam 16 – 21.
Massamba, D. P. B. (2004). Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. Dar es Salaam: TUKI.
Mshindo, H. B. (2010). Kutafsiri na Tafsiri. Zanzibar: Chuo Kikuu cha Zanzibar.
Mulokozi, M. M. (2017). Utangulizi wa Fasihi ya Kiswahili: Kozi za Fasihi Vyuoni na Vyuo Vikuu. Dar es Salaam. KAUTTU.
Mutie, E. K. (1997). Sanaa katika Tafsiri: Matatizo na Athari Zake. Tasnifu ya Shahada ya Umahiri: Chuo Kikuu cha Nairobi.
Mwansoko, H. J. M. na Wenzake (2015). Kitangulizi cha Tafsiri: Nadharia na Mbinu. Dar es Salaam: TUKI.
Newmark, P. (1988). A Text of Translation. London: Prentice Hall.
Ponera, A. S. (2014). Utangulizi wa Fasihi Linganishi. Dar es Salaam: Karljamer Print Technology.
Serem, S. P. (2018). “Uhakiki Linganishi wa Fani katika Tasnifu Mintarafu ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (Mwakusaka, 1979) na Mkaguzi wa Serikali (Madumulla, 1999).” Tasnifu ya Uzamivu: Chuo Kikuu cha Moi. (Haijachapishwa).
TUKI (2014). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaamu: TUKI.
Wanjala, S. F. ((2011). Misingi ya Ukalimani na Tafsiri. Serengeti: Serengeti Educational Publish.
Masshele/kiswahili
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-10-31T06:31:03Z 2021-10-31T06:38:18Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=1408 <![CDATA[Kamusi sanifu ya Biolojia, Fizikia na Kemia]]> KSBFK ni kifupi cha "Kamusi sanifu ya Biolojia, Fizikia na Kemia" iliyoandaliwa na wataalamu wa TUKI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1990 chini ya uhariri mkuu wa David P.B. Massamba.
Kamusi hii inakusanya maneno ya kisayansi kwa utaratibu ufuatao:
Mwishowe kuna jedwali la elementi ya kikemia.
Kamusi hii ilichapishwa upya mwaka 2004 na mwaka 2012.
Si rahisi kuipata katika maduka ya vitabu lakini inapatikana katika duka la TATAKI jinsi TUKI inaitwa siku hizi. Mada inafana kiasi na ile ya kamusi Awali wa Sayansi na Teknolojia (KAST) lakini wala istilahi wala tahajia hazilingani sawa.
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T12:59:10Z 2021-06-28T12:59:10Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=345 <![CDATA[TAFSIRI SANIFU YA ISTILAHI (BAKITA)]]>
.pdf   TAFSIRI SANIFU YA ISTILAHI.pdf (Size: 176.54 KB / Downloads: 6) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T12:03:50Z 2021-06-28T12:03:50Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=343 <![CDATA[TOFAUTI KATI YA UKALIMANI NA TAFSIRI: KINADHARIA NA KIVITENDO]]>
Kwa kuanza na maana ya tafsiri. Wataalamu mbalimbali wanaeleza maana tafsiri kama ifuatavyo:
Kwa mujibu wa Mwansoko na wenzake (2006) wanaeleza kuwa tafsiri ni zoezi la uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha moja hadi nyingine. Woa wanatilia mkazo katika zoezi la uhawilishaji na kinachohawilishwa ni mawazo katika maandishi.
Pia Catford (1965) anaeleza kuwa, kutafsiri ni kuchukua mawazo yaliyo katika maandishi kutoka lugha mmoja yaani lugha chanzi na kuweka badala yake mawazo yanayolingana kutoka katika lugha nyingine yaani lugha lengwa. Hapa msisitizo upo katika matini zilizoandikwa na kuzingatia zaidi ujumbe au wazo lililopo katika matini chanzi lijitokeze vile vile katika matini lengwa. Mawazo haya hayawezi kuwa sawa kabisa na ya matini chanzi bali ni mawazo yanayolingana toka matini chanzi na matini lengwa, hii ni kutokana na sababu tofauti kama vile utamaduni, historia, kiisimu na mazingira.
Naye Newmark (1982) anaeleza kuwa tafsiri ni mchakato wa uhawilishaji wa maneno kutoka matini chanzi kwenda matini lengwa.
Pia Nida na Taber (1969) wanaeleza kuwa tafsiri hujumuisha kuzalisha upya ujumbe wa lugha chanzi kwa kutumia visawe vya asili vya lugha lengwa vinavyo karibiana zaidi na lugha chanzi kimaana na kimtindo. Wao wanatilia mkazo uzalishaji upya wa kwa kutumia visawe asili vinavyokaribiana na matini chanzi kimaana na kimtindo. Kutokana na maana hizi tunaweza kusema kuwa tafsiri hufanywa katika ujumbe uliopo katika maandishi, ni jaribio la kiuhawilishaji na wazo linalatafsiriwa huwa na visawe vinavyokaribiana na sio sawa kutokana na tofauti za kiisimu, kihistoria, kiutamaduni na mazingira.
Pia maana ya ukalimani umefasiriwa kama ifuatavyo:
Kwa mujibu wa Wanjala (2011) anaeleza kuwa, ukalimani ni kuhawilisha ujumbe uliopo katika mazungumzo pamoja na uamilifu wake kutoka lugha chasili hadi lugha lengwa kwa kuzingatia isimu utamaduni na muktadha wa jamii husika.
Hivyo tunaweza kusema kuwa ukalimani ni uhawilishaji wa taarifa au ujumbe kutoka kwa msemaji wa lugha chanzi kwenda katika lugha lengwa kwa njia ya mdomo au mazungumzo, kwa kuzingatia isimu ya lugha husika, utamaduni na muktadha katika jamii fulani.
Kinadharia na kivitendo taaluma ya tafsiri na  taaluma ya  ukalimani ni tofauti.
Tofauti hizo zinajitokeza katika vipengele vifuatavyo:
Kwa kutumia kigezo cha maana: tafsiri ni taaluma ya uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha chanzi kwenda lugha lengwa kwa kuzingatia isimu, mukutadha na utamaduni. Lakini ukalimani ni taaluma inayohusika na uhawilishaji wa taarifa au wazo kutoka kwa msemaji wa lugha chanzi kwenda katika lugha lengwa kwa njia ya mdomo au mazungumzo kwa kuzingatia isimu, utamaduni na  muktadha wa jamii. Hapa tunaona tofauti kuwa taaluma ya tafsiri inahaulisha ujumbe katika maandishi na ukalimani unahaulisha ujumbe katika mazungumzo.
Kwa kutumia kigezo cha ukongwe: Taaluma ya tafsiri imeanza hivi karibuni mara baada ya majilio ya maandishi. Hii ina maana kwamba baada ya kuwepo kwa maandishi ndipo taaluma hii ya tafsiri ikaanza. Lakini ukalimani ni taaluma kongwe zaidi kwani mazungumzo yalianza kabla ya maandishi. Ukalimani ulianza baada ya maingiliano ya jamii ndipo haja ya kukalimani ikaanza hususani katika shughuli za biashara, dini na kadhalika ndipo ilipolazimu uwepo wa ukalimani katika jamii ili kukidhi mawasiliano.
Kwa kutumia kigezo cha hadhira: Katika taaluma ya tafsiri huwa na hadhira ambayo haishirikiana moja kwa moja katika mchakato wa tafsiri. Hadhira ya tafsiri husoma tu kazi iliyotafsiriwa. Lakini katika taaluma ya ukalimani huwa na hadhira hai inayoshirikiana katika mchakato mzima wa ukalimani. Hii ina maana kwamba hadhira huweza kuwasiliiana na mkalimani endapo hadhira inahitaji jambo la ziada. Mfano katika ukalimani wa mikutano au makongamano na ukalimani wa kijamii kama vile katika masuala ya afya, maji, ujenzi wa shule , imani/ dini nakadhalika hadhira hushirikiana na mkalimani moja kwa moja.
Kwa kutumia kigezo cha stadi kuu na muhimu za lugha: Taaluma ya tafsiri huhusisha stadi kuu nne za muhimu ambazo ni kusoma, kuandika, kusikiliza na kuzungumza. Mfasiri anatakiwa kuwa na ujuzi wa taaluma hii ili kufanikisha mchakato wa tafsiri kwa ufanisi. Lakini katika taaluma ya ukalimani huhusisha stadi kuu muhimu kama vile kusikiliza kutoka kwa msemaji wa lugha chanzi, na kuzungumza kwenda kwa wasikilizaji, na kutunza kumbukumbu.
Kwa kutumia kigezo cha muda: taaluma ya tafsiri huchukua muda mrefu kuhawilisha ujumbe kwani maandishi huhitaji maandalizi, hela na wakati wa kutosha ili kupata kazi iliyo bora zaidi. Lakini taaluma ya ukalimani huchukua muda mfupi mno wa kuhawilisha ujumbe yaani hapo kwa  papo. Mfano ukalimani wa
mahakamani, ukalimani wa mikutanoni au kwenye makongamano, warisha na semina mkalimani, hukalimani mfululizo kuendana na msemaji wa lugha lugha chanzi.
Kwa kutumia kigezo cha mfumo wa lugha : katika taaluma ya tafsiri hutumia mfumo wa lugha ya maandishi. Lakini katika taaluma ya ukalimani hutumia mfumo wa lugha ya mazungumzo. Mfano ukalimani mfululizo au andamizi ambapo mkalimani huzungumza sambamba na msemaji wa lugha  chanzi hivyo mkalimani hufanya kazi kwa haraka sana ili kuendana na kasi ya mzungumzaji kama mfumo wa lugha ulivyo.
Kwa kutumia kigezo cha uwasilishaji: taaluma ya tafsiri, mfasiri ananafasi ya kudurusu kazi aliyopewa na kuweza kuondoa na kurekebisha au kusahihisha makosa yaliyojitokeza katika tafsiri yake. Lakini katika taaluma ya ukalimani, mkalimani hana nafasi
ya kudurusu hata kama kuna kosa lililojitokeza. Na mara nyingi ukalimani huwa na makosa ya kimatamshi, kisarufi na kiuteuzi wa maneno.
Kwa kutumia kigezo cha utunzaji wa kumbukumbu: Katika taaluma ya tafsiri huwa na kumbukumbu ya kudumu kwani mawazo au ujumbe huifadhiwa katika maadhishi. Lakini katika taaluma ya ukalimani kumbukumbu sio ya kudumu kwani huwa katika mazungumzo kinadharia na kivitendo.
Ingawa taaluma hizi mbili yaani taaluma ya ukalimani na taaluma ya tafsiri zinatofautiana kwa kiwango fulani kinadharia na kivitendo lakini taaluma hizi mbili zinafanana.
Vigezo vinavyofananisha taaluma hizi mbili ni hivi vifuatavyo:
Taaluma zote mbili hushughulika na uhawilishaji wa ujumbe kutoka katika lugha chanzi kwenda lugha lengwa.
Taaluma zote hulenga kufanikisha mchakato wa mawasiliano kati ya watu au jamii mbili au zaidi zinazotumia lugha tofauti.
Taaluma zote mbili huchangiana na kushirikiana katika mambo makuu manne muhimu ambayo ni mtoa ujumbe, ujumbe wenyewe, mhawilishaji ujumbe na mpokeaji ujumbe. Mchango wa kila kipengele ni muhimu katika taaluma zote mbili ili kukamilisha mchakato mzima wa tafsiri na ukalimani.
Kwa kutumia kigezo cha uendeshwaji: taaluma zote mbili huweza kuendeshwa kwa namna mbili, binadamu au mashine zinazotumiwa kuhawilisha ujumbe kutoka katika lugha chanzi kwenda lugha lengwa.
Hivyo tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa licha ya kufanana na kutofautiana kwa dhana au taaluma hizi mbili, mfasili na mkalimani hawana budi kuzingatia isimu yaani sarufi ya lugha husika, utamaduni, muktadha husika na hata historia ya jamii husika.
MAREJELEO
Catford J.C. (1965) A Linguistic theory of Translation: OUP London.
Mwansoko, H.J.M. na wenzake (2006) Kitangulizi cha Tafsiri: Nadharia na Mbinu: TUKI Dar es Salaam.
Newmark, P. (1988) A Textbook of Translaton. : Prentice Hall London.
Nida, A. E. na Charles, R. T. (1969) The Theory and Practice of Translation. The United Bible Societies: Netherlands.
Wanjala S. F (2011) Misingi ya ukalimani na tafsiri: Serengeti Education publisher (T) L.T.D. Mwanza Tanzania.]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T10:40:52Z 2021-06-28T10:41:58Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=342 <![CDATA[MATATIZO YA TAFSIRI KATIKA MATINI ZA KITALII NCHINI TANZANIA]]> Matatizo ya Tafsiri katika Matini za Kitalii Nchini Tanzania
Na: Hadija Jilala
 
Utalii ni miongoni mwa sekta muhimu sana katika maendeleo ya nchi na ni sekta ambayo huliingizia taifa pato la kiuchumi. Sekta hii huhusisha watu wa jamii mbalimbali duniani, watu wenye tofauti za kiutamaduni, kiuchumi, kiitikadi, kijamii na wanaozungumza lugha tofauti. Pamoja na hayo, utalii ni eneo ambalo bado halijafanyiwa kazi vya kutosha na watafiti wa lugha na tafsiri ili kuona ni jinsi gani lugha na tafsiri vina mchango katika ukuzaji wa sekta ya utalii nchini Tanzania. Makala haya basi yanachunguza matatizo ya tafsiri katika matini za kitalii zilizotafsiriwa kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Lengo ni kubainisha matatizo ya tafsiri katika matini za kitalii na kutoa mapendekezo ya namna ya kuyakabili matatizo hayo ili kuleta ufanisi wa mawasiliano.
Utangulizi:
Hali ya Sekta ya Utalii Nchini Tanzania
Kwa mujibu wa TUKI (2004:445) utalii ni hali ya kusafiri mbali au kuvinjari huku na huko ili kufurahia mandhari. Upo utalii wa aina mbalimbali kama vile wa asili, kiutamaduni na mambo ya kale. Makala haya yanaangalia utalii wa kiutamaduni. Utalii wa kiutamaduni unajumuisha mambo mbalimbali kama vile kazi za sanaa, urithi wa fasihi simulizi, majumba ya makumbusho, kazi za mikono, matamasha ya sanaa na majengo ya kihistoria (Bennett, 1995).

Kwa hiyo, makala haya yanashughulikia matini zinazopatikana katika majumba ya makumbusho ambayo yanahusika na kuhifadhi vivutio vya utalii wa kiutamaduni. Kulingana na Benavides (2001) utalii una nafasi kubwa katika uchumi wa Tanzania. Ni moja kati ya vyanzo vikuu vya fedha za kigeni na unatoa nafasi za ajira kwa jamii. Hivyo basi, inaonekana kuwa utalii ni tasnia muhimu sana katika kuongeza upatikanaji wa kazi, kuondoa umaskini na upatikanaji wa fedha za kigeni.

Kufikia mwaka 2015 pato la utalii kwenye uchumi wa taifa la Tanzania linategemewa kufikia dola za Kimarekani milioni 3,699.4. Hata hivyo, serikali inapopanga kuendeleza na kuutangaza utalii wa Tanzania, inatakiwa pia kulinda na kuhifadhi rasilimali za asili na
za kiutamaduni.
Kutokana na umuhimu wa sekta ya utalii nchini Tanzania, ipo haja ya kuwa na na vyanzo vya taarifa ambavyo vinafikisha mawasiliano sahihi kwa wageni ili kutangaza vivutio vya utalii na utamaduni wa jamii kwa ujumla. Kuwepo kwa vipingamizi vya mawasiliano huweza kuharibu mawasiliano na hata kupoteza idadi ya wageni wanaofurahia utalii wa nchi. Moja ya njia ya kufikisha mawasiliano kwa watalii ni tafsiri.

Tafsiri katika utalii hutumika kama daraja la mawasiliano linalounganisha watu wa jamii na tamaduni tofauti. Si kila tafsiri inaweza kufikisha mawasiliano; kwa sababu zipo tafsiri ambazo zinaweza kupotosha ujumbe na maana iliyokusudiwa na hatimaye kupindisha mawasiliano. Kwa maana hiyo, ipo haja ya kuchunguza
ufanisi wa mawasiliano katika tafsiri za matini za kitalii ili kuona ni kwa jinsi gani matini hizo zinafanikisha mchakato wa mawasiliano. Kwa hiyo, makala haya yamelenga kubainisha na kujadili matatizo ya tafsiri katika matini za kitalii zilizotafsiriwa kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza na kutoa mapendekezo ya jinsi gani tunaweza kuyakabili matatizo hayo ili kuwa na ufanisi wa mawasiliano katika utalii.
Data za makala haya zilikusanywa katika utafiti uliofanyika Mei 2012 hadi Oktoba 2012 katika Makumbusho za Taifa, Nyumba ya Utamaduni, na Kijiji cha Makumbusho zote za jijini Dar es Salaam. Vilevile, Makumbusho ya Majimaji yaliyopo Songea na Makumbusho ya Mwalimu J. K. Nyerere yaliyopo Butiama mkoani Mara. Aidha, data za utafiti huu zilikusanywa kwa kutumia mbinu nne ambazo ni: usomaji wa machapisho, usaili, dodoso na uchunguzi ushiriki. Mbinu ya usomaji wa machapisho, ilitumika kukusanya na kuchambua matini za kitalii zilizotafsiriwa kutoka lugha ya Kiswahili kwenda katika lugha ya Kiingereza. Matini hizo ni lebo zilizobandikwa katika vifaa na maeneo yaliyopo Makumbusho, vitabu vya mwongozo kwa watalii na vipeperushi. Kwa upande mwingine, mbinu za dodoso na usaili zilitumika kwa waongozaji wa watalii (12), wafasiri wa matini za kitalii (12) na wanafunzi (15) wa programu ya uzamili wa kozi ya tafsiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Nadharia ya Skopos
Makala haya yanatumia nadharia ya Skopos kama kiunzi cha uchunguzi na uchambuzi wa data za tafsiri ya matini za kitalii. Hii ni nadharia ya tafsiri ambayo ilianzishwa na Hans. J. Vermeer miaka ya 1970 huko Ujerumani. Msingi wa nadharia hii ni kuiona tafsiri kama utekelezaji wa kitendo kwa kuzingatia matini asilia. Wafuasi wa nadharia hii wanaamini kwamba, kila matini hutafsiriwa kwa lengo fulani na kwa hiyo tafsiri lazima itimize lengo hilo. Kwa maana hiyo, tafsiri huzalishwa kwa ajili ya hadhira mahususi, kwa lengo mahususi na muktadha maalumu (Vermeer, 1989a). Nadharia hii hujikita katika kutathmini matini kwa malengo maalumu ambayo yanapelekea kukamilisha dhima sawa katika utamaduni chanzi na utamaduni lengwa. Hivyo, kulingana na mkabala huu, tafsiri nzuri ni ile inayoruhusu hadhira lengwa kupata tafsiri yenye ushikamani na matini chanzi (Lauscher, 2000).
Kulingana na Vermeer (1989a) lengo la nadharia ya Skopos ni kuielezea shughuli ya tafsiri katika mtazamo wa lugha lengwa. Kwa ujumla nadharia hii imejikita katika malengo ya tafsiri ambayo huukilia mbinu na mikakati ya tafsiri inayotumika katika kutoa matokeo stahiki ya kidhima (Nord, 2007). Aidha, nadharia hii inaakisi uhamishaji wa jumla wa kiisimu wa nadharia rasmi ya tafsiri kwenda katika dhana ya tafsiri iliyojikita zaidi kwenye dhima na utamaduni-jamii (Gentzler, 2001).

Nadharia hii ina kanuni mbili: kanuni ya ushikamani na kanuni ya uaminifu. Kanuni ya ushikamani ina maana kuwa matini lengwa lazima iwe na maana kwa hadhira lengwa katika utamaduni wa lugha lengwa na katika muktadha wa kimawasiliano ambao matini lengwa itatumika. Kwa upande mwingine, kanuni ya uaminifu ina maana kuwa lazima kuwapo ushikamani wa kimatini baina ya matini lengwa na matini chanzi ambao ni sawa na usahihi wa matini chanzi.
Sababu ya kutumia nadharia hii ni kwamba, ni nadharia ambayo inaitazama tafsiri kama tendo lenye lengo maalumu kwa hadhira na kwa vile tafsiri ya matini za kitalii hulenga kufanikisha mawasiliano baina ya hadhira ya lugha za tamaduni mbili tofauti, nadharia hii imetumika kuchunguza na kujadili endapo lengo hilo linafikiwa au
la. Aidha, makala haya yametumia kanuni za nadharia ya Skopos, yaani kanuni ya ushikamani na kanuni ya uaminifu, kubainisha na kujadili matatizo ya tafsiri ya matini za kitalii kutoka katika lugha ya Kiswahili kwenda katika lugha ya Kiingereza; na hivyo kuonesha ni jinsi gani ushikamani wa maana ya matini chanzi unafikiwa katika matini lengwa. Nadharia hii pia imetumika katika kupendekeza namna bora ya kukabiliana na matatizo ya tafsiri ili kuwa na ushikamani wa maana na ujumbe baina ya matini chanzi na matini lengwa na hatimaye kufanikisha mawasiliano kwa hadhira lengwa.
Lengo la Kutafsiri Matini za Kitalii
Tafsiri ni zoezi la uhawilishaji wa mawazo yaliyo katika maandishi kutoka katika lugha moja (lugha chanzi) na kuweka badala yake mawazo yanayolingana na hayo katika lugha nyingine (lugha lengwa) (Catford, 1965; Newmark, 1988; Mwansoko, 1996; Ordudary, 2007; Venuti, 2008 na House, 2009). Ukichunguza fasili ya tafsiri inayotolewa na wataalamu hao, utaona kuwa kuna mambo ya msingi ambayo yanajitokeza kujenga fasili hiyo. Haya ni pamoja na suala la ulinganifu, maana na ujumbe. Hii ina maana kwamba, tafsiri inapaswa kuwasilisha kwa hadhira lengwa maana na ujumbe
ulio sawa na ule uliowasilishwa na matini chanzi kwa hadhira chanzi. Tafsiri katika jamii ina dhima mbalimbali: kwanza ni daraja la mawasiliano ambalo linaunganisha jamii mbalimbali za watu wanaotumia lugha zinazotofautiana. Vilevile, ni njia ya mawasiliano, nyenzo ya kueneza utamaduni kutoka jamii moja hadi nyingine, mbinu mojawapo ya kujifunza lugha za kigeni na kiliwazo cha nafsi (Newmark, 1988; Mwansoko, 1996).
Tafsiri katika utalii ni taaluma ya msingi na yenye umuhimu mkubwa. Umuhimu huu unatokana na sababu kwamba, katika maeneo ya utalii matini hutafsiriwa ili kukidhi mahitaji ya kimawasiliano kwa watu wanaotoka katika jamiilugha na tamaduni tofauti. Vermeer (1989a) anasisitiza kwamba mchakato wa kutafsiri matini ya aina yoyote ile, hufanyika kwa lengo maalumu na lazima tafsiri itimize lengo hilo (Reiss na Vermeer, 1984). Matini za kitalii kama ilivyo matini zingine hutafsiriwa kwa lengo la kutoa maelekezo na kutoa taarifa muhimu kwa watalii ili waweze kuelewa vivutio vya kitalii vilivyopo katika nchi waliyoitembelea na kufahamu utamaduni wa jamii hiyo. Tafsiri ya matini za kitalii ni aina mojawapo ya tafsiri za matangazo. Matini za aina hii hufanyika kwa lengo la kutoa taarifa na ujumbe kwa hadhira lengwa, kuelimisha juu ya masuala ya jamii chanzi kwa jamii lengwa na kutoa taarifa za matangazo ya biashara na utamaduni. Matini za kitalii zinatoa taarifa zenye dhima tatu, yaani dhima elezi, dhima arifu na dhima amili (Sanning, 2010).
Kwa hiyo, ili tafsiri iweze kufikia malengo hayo, nadharia ya Skopos inasisitiza kwamba, katika tafsiri lazima kuwepo na ushikamani wa maana na ushikamani wa matini. Kwa maana hiyo, mfasiri hujaribu kuzalisha athari sawa kwa hadhira lengwa na ile iliyozalishwa na matini asilia kwa wasomaji wa lugha chanzi. Mathalani, Jin Di na Nida (1984: 102) wanasema, wasomaji wa Kichina huweza kuelewa matini asilia zilizoandikwa kwa lugha ya Kichina kwa sababu wanachangia na mwandishi wa matini hiyo uelewa wa lugha, uzoefu na maarifa ya utamaduni uliozalisha matini hiyo.

Kwa upande mwingine, tofauti za kiutamaduni huwazuia wasomaji wa kigeni kuelewa vema masuala ya kitalii, vitu na vifaa vilivyopo katika maeneo ya utalii. Kwa mfano, majina ya watu, vitu ama vifaa vya kitalii, taarifa za kihistoria na utamaduni. Kwa maana hiyo, mfasiri lazima atumie mbinu bora za kutafsiri ili kupunguza tofauti hizo kwa lengo la kumsaidia msomaji kuelewa ujumbe unaowasilishwa na vivutio vya kitalii vilivyopo katika maeneo mbalimbali. Maeneo hayo ya kitalii ni kama vile majumba ya makabila ya jamii mbalimbali (aina ya nyumba, vifaa vya ujenzi, mtindo wa ujenzi na dhima ya nyumba), mavazi, vyakula, vinywaji, na vifaa vinavyotumika katika jamii hiyo kama vile: vifaa vya nyumbani, matambiko, uganga, uhunzi, kilimo, ufugaji, silaha za kivita, uwindaji na ulinzi, na fasihi ya jamii hiyo.
Yan na Naikang (2011) wanaeleza kuwa lengo la vifaa vya kitalii ni kuvutia wageni, kuwapa hamu ya kutembelea maeneo ya kitalii na kufurahia matembezi yao. Hivyo basi, dhima arifu ni muhimu sana katika utalii. Hata hivyo, lengo hili linaweza kufikiwa kwa kutoa usuli wa taarifa. Kabla watalii hawajaenda kutembelea vivutio vya kitalii huhitaji kupata taarifa zinazohusiana na makusudio ya utalii. Maelezo toshelevu, angavu na yanayovutia huwapa nguvu watalii ya kutembelea eneo la utalii. Kwa maana hiyo, dhima arifu ni muhimu sana. Kwa upande mwingine, dhima elezi haitakiwi kudharauliwa katika utalii. Kwa kusoma matini za kitalii zilizotafsiriwa, watu wanaweza kuhisi sifa za taifa na makaribisho ya wenyeji wa nchi husika kwenye vitabu vya miongozo ya watalii.

Kutokana na mjadala huu, tunaweza kusema kwamba matini za kitalii hutafsiriwa kwa lengo na dhima maalumu. Ni wajibu wa mfasiri kuhakikisha lengo hilo linatimia kwa walengwa wa matini hizo ambao ni watalii. Kwa hiyo, matini za kitalii zinapaswa kutimiza lengo la kimawasiliano kwa watalii ili waweze kuelewa vivutio vya kitalii vilivyopo nchini.
Tafiti kuhusu Tafsiri katika utalii
Utalii Tafsiri katika utalii ni eneo ambalo limeshughulikiwa na baadhi ya wanazuoni nje ya Tanzania kwa kutumia lugha, muktadha na mitazamo tofauti (Nan, 2005; Su-zhen, 2008; Baolong, 2009; Smecca, 2009 na Mohammad, 2010). Wapo watafiti ambao wamefanya utafiti kuhusu mbinu za kutafsiri matini za kitalii. Kwa mfano, Nan (2005) katika makala yake kuhusu matangazo ya utalii amebainisha mbinu za kutafsiri matangazo ya utalii kuwa ni urudiaji, ukuzaji na unyumbukaji. Mtafiti mwingine, Su-zhen (2008) ameandika makala kuhusu nadharia ya Skopos na mbinu za kutafsiri elementi za kiutamaduni katika matini za kitalii. Katika makala hayo, anapendekeza mbinu za kutafsiri matini za kitalii ikiwa ni pamoja na; mbinu ya tafsiri sisisi, mbinu ya unukuzi, mbinu ya unukuzi na tafsiri sisisi, na mbinu ya unukuzi na muhtasari. Aidha, wapo watafiti ambao wamejadili kuhusu matatizo
ya tafsiri katika matini za kitalii. Kwa mfano, Baolong (2009) alitumia Nadharia ya Skopos kwa lengo la kuchunguza matini za habari kwa kutumia mifano ya matini zinazohusiana na utamaduni wa Shaoxing Mingshi. Kwa kuzingatia Nadharia ya Skopos anajadili kuwa matatizo ya tafsiri yanasababishwa na mfasiri kutokutambua lengo la kutafsiri matini.
Aidha, aligundua kuwa kuna matatizo ya kipragmatiki, kiisimu, kiutamaduni na umahususi wa matini. Kwa kutumia Nadharia ya Skopos anapendekeza kuwa, matatizo hayo yanaweza kukabiliwa kwa kuwa na uelewa wa jumla wa tendo la tafsiri, kusisitiza ushirikiano baina ya mfasiri na mteja, kuhimiza ufahamu wa mfasiri juu ya lengo, uwezo wa lugha zaidi ya moja na viwango vya maadili kwa mfasiri.
Smecca (2009) katika makala yake inayohusu vitabu vya mwongozo kwa watalii na taswira ya ‘Sicily’ katika tafsiri amebainisha matatizo ya kutafsiri matini za kitalii kuwa ni; matatizo ya uhamishaji wa maana, kubadilika kwa mwelekeo na udondoshaji wa maneno ambao unajitokeza katika toleo la Kiitaliano.
Kwa upande wake Mohammad (2010) ameandika makala kuhusu masuala ya kiutamaduni katika tafsiri ya vitabu vya mwongozo kwa watalii nchini Irani, kwa kuangalia matatizo na suluhisho lake kwa kutumia mkabala wa nadharia ya Skopos. Katika makala hayo, amejadili hatua za kutafsiri vitabu vya mwongozo kwa watalii, mbinu, matatizo na jinsi ya kukabiliana na matatizo hayo. Anahitimisha kwamba, kudharau au kutotilia maanani masuala ya kiutamaduni katika kutafsiri vitabu vya mwongozo kwa watalii nchini Irani, ni sababu inayowafanya watalii kushindwa kuelewa utamaduni wa Wairani na pia husababisha tatizo la mawasiliano na upungufu katika kuvutia watalii. Yan na Naikang (2011) katika utafiti wao wamechunguza matatizo ya kutafsiri matini za kitalii kutoka lugha ya Kichina kwenda lugha ya Kiingereza. Katika utafiti huo wamebainisha matatizo yanayozikabili tafsiri za kitalii za Kichina-Kiingereza kuwa ni matatizo ya kiisimu na matatizo ya kiutamaduni. Hivyo basi, makala haya yametumia muktadha wa Kitanzania kuchunguza matatizo ya tafsiri katika matini za kitalii zilizotafsiriwa kutoka lugha ya Kiswahili kwenda lugha ya Kiingereza na hatimaye kutoa mapendekezo ya namna ya kuyaondoa matatizo hayo.
Matokeo ya Utafiti
Katika kuchunguza na kuchambua matini za kitalii ambazo ni lebo, vipeperushi na vitabu vya mwongozo kwa watalii makala haya yalibaini matatizo ya tafsiri katika matini hizo. Matatizo yaliyodhihirika ni matatizo ya kiisimu, kimaana na kiutamaduni. Sehemu inayofuata inajadili matatizo hayo kwa kutumia mifano iliyobainishwa katika matini za kitalii:
Matatizo ya Kiisimu
Matizo ya kiisimu yanatokana na tofauti za kisarufi na kimuundo katika msamiati, sintaksia na nduni za lugha chanzi na lugha lengwa (Nord, 1993: 66). Mfasiri hukumbana na matatizo na makosa ya kiisimu katika vipengele vya kiwango cha msamiati na kiwango cha kisintaksia. Katika utafiti huu, matatizo ya kiisimu yaliyobainika katika lebo, vipeperushi na vitabu ya mwongozo kwa watalii yamejikita katika viwango vitatu ambavyo ni: kiwango cha msamiati, kiwango cha kisintaksia na kiwango cha maana. Sehemu inayofuata inajadili matatizo ya kiisimu kwa kuzingatia viwango vyake na mifano dhahiri kutoka katika matini za kitalii zilizopo Makumbusho kama ifuatavyo:
Kiwango cha Msamiati
Matatizo ya kiisimu katika kiwango cha msamiati yamejikita katika uteuzi wa visawe vya kiutamaduni katika lugha lengwa. Makosa katika uteuzi wa visawe wakati wa kutafsiri matini za kitalii huweza kusababisha matatizo katika uelewa na ufahamu wa maana iliyokusudiwa na matini chanzi. Hivyo basi, kutokana na makosa au tatizo la uteuzi wa visawe, hadhira lengwa hushindwa kupata maana sahihi endapo kisawe kilichoteuliwa kitakuwa si sahihi. Katika utafiti huu ilibainika kuwa tatizo la uteuzi wa visawe huweza kusababishwa na matatizo binafsi aliyonayo mfasiri wa matini za kitalii ambayo ni uwezo na ujuzi wa lugha, uelewa wa utamaduni chanzi na utamaduni lengwa na pengine mfasiri kutokuelewa maneno ya lugha ya Kiswahili. Mbali na matatizo ya mfasiri, utafiti huu uligundua kuwa matatizo mengine ni: tofauti za kiisimu za lugha chanzi na lugha lengwa ambazo husababisha ukosefu wa visawe vya lugha chanzi katika lugha lengwa na kutokuelewa utamaduni wa lugha lengwa. Mifano ifuatayo inaonesha uteuzi mbaya wa visawe ambao wakati mwingine unasababishwa na tatizo la lugha (uwezo mdogo wa lugha wa mfasiri) la kutokuelewa maneno ya Kiswahili, utamaduni lengwa na pengine ukosefu wa kisawe katika lugha lengwa:
[Image: SAM_10.JPG]
Mifano iliyopo katika jedwali namba 1 hapo juu, inaonesha kuwapo kwa tatizo la uteuzi wa visawe mwafaka vya kiutamaduni. Kuna makosa katika kuteua visawe vya Kiingereza wakati wa kutafsiri maneno ya Kiswahili kwenda katika lugha ya Kiingereza. Uteuzi wa
neno ‘container’ kama kisawe cha‘kibuyu’, ‘fireplace’ kama kisawe cha ‘mafiga’, na ‘spoon’ kama kisawe cha ‘upawa’ inadhihirisha kuwapo kwa tatizo la uteuzi wa visawe vya kiutamaduni kutoka katika utamaduni lengwa kurejelea utamaduni chanzi na mapungufu ya uelewa na ujuzi wa lugha alionao mfasiri. Hivyo basi,
kulingana na nadharia ya Skopos tunaona kuwa kanuni ya ushikamani na uaminifu haijafikiwa na hivyo basi, kutofikiwa kwa kanuni hizo kunasababisha mapungufu ya mawasiliano na kutofikiwa kwa lengo la tafsiri ya matini za kitalii. Utafiti huu unapendekeza kuwa tafsiri sahihi ya maneno hayo ingekuwa kama ifuatavyo: neno mafiga lingefaa kutafsiriwa kama ‘firestones’, neno upawa lingefaa kutafsiriwa kama ‘shallow ladle’ na kibuyu lingefaa kutafsiriwa kama ‘gourd’.
5.1.2 Makosa ya Kisintaksia
Matini za kitalii zinaonesha kuwa zinakabiliwa na makosa ya kisintaksia ambayo pia huathiri ufahamu na uelewa wa maana kwa
hadhira lengwa. Wakati wa kutafsiri matini za kitalii, mfasiri anaweza kuathiriwa na sarufi na ruwaza za miundo na mipangilio ya sarufi ya lugha yake na kuihamishia katika lugha lengwa. Kulingana na nadharia ya Skopos, lengo la tafsiri ni kwa ajili ya hadhira lengwa kusoma na kuelewa taarifa za lugha chanzi. Kwa kuzingatia matini za kitalii, lengo la tafsiri ni kuvutia wageni. Inawezekana wasomaji wakawa wageni kutoka nje na siyo Waswahili. Ilielezwa wakati wa usaili na waongozaji wa watalii na wahifadhi mila katika Makumbusho zilizotembelewa kuwa, watalii kutoka nje ya nchi ndio tegemeo kubwa la utalii kwa sababu watalii wengi wanaotembelea Makumbusho huwa ni wageni kutoka nje ya Tanzania. Kwa hiyo, wakati wa kutafsiri ni vema kuepuka tafsiri sisisi na sentensi changamano ambazo zinaweza kuleta utata wa maana na hatimaye
kusababisha upungufu wa mawasiliano kwa watalii ambao huhitaji kupata taarifa sahihi za kile wanachokiona katika maeneo ya utalii. Tazama mifano katika jedwali lifuatalo:
[Image: SAM_9.JPG]
Ukichunguza mifano katika jedwali namba 2 utaona kuwa, katika mfano wa kwanza kuna udondoshaji wa kiunganishi ‘kama’ katika matini lengwa. Matumizi ya kiunganishi ‘kama’ katika matini chanzi kina dhima ya kuelezea aina ya mtungi unaozungumziwa. Hivyo basi, kuondolewa kwa kiunganishi ‘kama’ katika lugha lengwa kunaathiri maana na uelewa wa maana kwa hadhira lengwa. Taarifa ya matini chanzi ambayo imekusudiwa kutolewa kwa hadhira lengwa hupotea na hivyo hadhira lengwa hupata dhana na maana tofauti na ile iliyopo katika matini chanzi. Katika mfano wa pili, lugha chanzi inasema ‘kwa matumizi ya vinywaji’ na lugha lengwa imetafsiriwa kama ‘used to keep different drinks’. Hadhira chanzi wanapata dhana na picha tofauti kwamba kifaa kinachoelezewa kinatumika kwa ajili ya vinywaji. Kwa upande mwingine, tafsiri ya sentensi hiyo imeparaganyika kisarufi katika uteuzi wa msamiati ambao umetumika kutafsiri na hivyo kutoa dhana na picha tofauti kwa hadhira lengwa ‘used to keep different drinks’ ambapo hadhira lengwa itapata picha kwamba kifaa hiki kinatumika kuhifadhi vinywaji tofauti. Kisarufi matumizi ya neno ‘keep’ kama kisawe cha neno ‘matumizi’ na kuongeza msamiati mpya ‘different’ inaleta athari katika kutafsiri maneno ya kiutamaduni na kusababisha dhana na picha iliyokusudiwa kwa hadhira chanzi kupotea. Vilevile
huwafanya hadhira chanzi na lengwa kujenga dhana na picha tofauti. Ukichunguza mfano wa tatu utaona kuwa kuna udondoshaji wa kirai kihusishi ‘kwa kawaida’ na matumizi ya neno ‘while’ katika lugha lengwa badala ya kiunganishi ‘na’ ambacho kipo katika lugha chanzi. Hivyo basi, tunaona kuwa makosa ya kisintaksia huweza kuharibu ujumbe uliokusudiwa katika matini chanzi.
Makosa ya Kimaana
Maana ni kitu cha msingi katika tafsiri na ndicho kitovu cha tafsiri (Mwansoko, 1996). Tunapofanya tafsiri ya taarifa za lugha chanzi kwenda katika lugha lengwa huwa tunahamisha maana ya ujumbe uliokusudiwa katika matini chanzi kwenda katika matini lengwa. Katika matini za kitalii ilibainika kuwapo kwa makosa ya maana. Katika makala haya, matatizo ya maana yamewekwa katika viwango vitatu ambavyo ni upotevu na uhamishaji wa maana, upokezi wa maana na utata wa maana.
Upotevu na Uhamishaji wa Maana
Katika baadhi ya tafsiri ya matini za kitalii, imebainika kuwa kuna upotevu na uhamishaji wa maana na ujumbe wa matini chanzi katika matini lengwa. Maana za kiishara za kiutamaduni na maumbo ya maneno hupotea wakati wa kutafsiri. Kihore (1989)
anasema kwamba ingawa lengo kuu la tafsiri ni kuzalisha athari iliyo sawa ya matini chanzi katika lugha nyingine, inatokea kwamba vipengele vya maana na umbo huathiriwa. Kulingana na kanuni ya uaminifu ya nadharia ya Skopos ambayo inasisitiza ushikamani wa matini chanzi na matini lengwa, tunaweza kusema kwamba kukosekana kwa ushikamani katika matini za kitalii ni tatizo la tafsiri. Kwa mfano, wakati wa kufanya uchambuzi wa maudhui ya matini za kitalii ambazo ni lebo, vipeperushi na vitabu vya mwongozo wa watalii, mtafiti aliweza kubainisha upotevu na uhamishaji wa maana na ujumbe katika maneno ya Kiswahili yanapotafsiriwa kwenda lugha ya Kiingereza. Tazama mifano katika jedwali lifuatalo:
[Image: SAM_8.JPG]
Ukichunguza jedwali namba 3 hapo juu, utaona kuwa kuna upotevu na uhamishaji wa maana ya neno la lugha chanzi katika lugha lengwa. Kwa mfano, katika mfano wa kwanza tunaona neno ‘wanaume’ limetafsiriwa kama ‘elders’ hapa kuna upotevu wa maana kwa sababu ‘mwanaume’ na ‘elders’ ni maneno yenye dhana mbili tofauti na urejelezi tofauti kulingana na utamaduni wa jamiilugha ya Waingereza na Waswahili. Neno ‘mwanaume’ hurejelea mtu wa jinsia ya kiume aliyeoa (TUKI: 235) wakati kisawe kilichotumika katika tafsiri kurejelea neno hilo ni ‘elders’ ambalo lina maana ya ‘wazee’. Hivyo basi, tafsiri sahihi inayopendekezwa kwa neno ‘mwanaume’ ni ‘man’ na ‘elders’ ni ‘wazee’. Mfano wa pili unaonesha neno ‘utawala’ limetafsiriwa kama ‘fight experience.’ Tafsiri hii inapotosha maana na historia ya jamii inayozungumziwa katika matini chanzi. Matini chanzi inaelezea kuhusu utawala wakati matini lengwa inaelezea uzoefu wa kivita. Hivyo basi, tunaweza kusema kuwa matini chanzi na matini lengwa zinatoa taarifa na ujumbe tofauti.
Hii inatokana na kutoa tafsiri ambayo si sadifu. Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba, tafsiri sahihi ya neno ‘utawala’ ingeweza kuwa ‘administration’. Kwa upande mwingine katika mfano wa tatu, neno ‘wavulana’ limetafsiriwa kama ‘youth’. Matumizi ya neno ‘youth’ kama kisawe cha neno la Kiswahili ‘wavulana’ hupoteza na kuhamisha maana ya msingi ya neno. Upotevu wa maana unatokea kwa sababu neno‘youth’ katika lugha ya Kiingereza (lugha lengwa) hurejelea ‘kijana’ ambaye anaweza kuwa mvulana ama msichana. Kwa maana hiyo, hadhira ya lugha lengwa huweza kupata maana na ujumbe tofauti na hadhira chanzi. Pia kutokana na tafsiri hizo kupoteza na kuhamisha maana humfanya hadhira lengwa kupata ujumbe ambao si sahihi kuhusu utamaduni wa jamii chanzi.
Uhamishaji wa Maana ya Msingi
Uhamishaji wa maana ni tatizo ambalo hujitokeza katika tafsiri ya matini za kitalii. Maana ya msingi ya neno huhusisha maana za kiishara ambazo zinakuwa zimebebwa na Matatizo ya Tafsiri katika Matini za Kitalii Nchini Tanzania 37 neno linalohusika. Katika matini za kitalii, uhamishaji wa maana ulionekana kwa baadhi ya maneno ambapo maana zake za msingi zilionekana kuhama kutoka katika maana moja kwenda katika maana nyingine. Jedwali lifuatalo linaonesha mifano ya maneno ya Kiswahili ambayo yamepoteza maana yake ya asili katika lugha lengwa:
[Image: SAM_7.JPG]
Ukichunguza mfano wa kwanza, ‘jiwe la kusagia’ limetafsiriwa kama ‘grinding machine’ tafsiri hii inapoteza dhana ya msingi ya ‘jiwe la kusagia’ ambalo ni jiwe kubwa mahususi kwa kusagia nafaka, likiwa na jiwe dogo ambavyo vyote hushirikiana. ‘Jiwe la kusagia’ si ‘mashine’, hivyo kwa dhana hiyo ya ‘grinding machine’ kutumika kama kisawe cha ‘jiwe la kusagia’ hakileti ulinganifu sadifu wa maana, umbo na matumizi ya jiwe la kusagia. Hivyo basi, inapendekezwa neno ‘Jiwe la kusagia’ lingefaa kutafsiriwa kama ‘grinding stone’. Tafsiri hii ya ‘grinding stone’ ni sadifu zaidi kuliko ‘grinding machine’ kwa sababu ‘jiwe la kusagia’ linalozungumziwa ni jiwe kubwa na siyo mashine. Hivyo basi, tafsiri hii inaweza kumsaidia hadhira lengwa kuweza kuhusianisha kile anachokiona na tafsiri yake. Mfano wa pili na nne, yaani ‘mwiko’ na ‘chungu’ vimetafsiriwa kwa kutumia kisawe kimoja ‘scoop’. Ukichunguza vifaa hivi katika utamaduni chanzi ni tofauti katika maumbo, ukubwa, utengenezaji na matumizi yake.

Hivyo basi, tafsiri hii inaathiri maana ya dhana iliyokusudiwa katika matini chanzi. Kwa mifano hiyo, utafiti huu  unapendekeza kuwa neno ‘mwiko’ lingefaa kutafsiriwa kama ‘wooden spoon’ na ‘chungu’ lingefaa kutafsiriwa kama ‘pot’. Mfano wa tatu na wa sita, yaani ‘makobazi’ na ‘viatu’ vyote vimetafsiriwa kama ‘sandals’. Tafsiri hiyo si sadifu kwa sababu ‘viatu’ ni tofauti na ‘makobazi’, kimuundo na kiuvaaji. Hivyo basi, matumizi ya neno sandals kama kisawe cha ‘viatu’ na ‘makobazi’ yanaathiri dhana ya msingi ya maneno hayo na kuleta utata wa maana. Katika mifano hiyo, utafiti huu unapendekeza kuwa neno la Kiingereza ‘sandals’ linasadifu zaidi kuwa kisawe cha ‘makobazi’ na neno la Kiswahili ‘viatu’ liwe kisawe cha ‘shoes’. Mfano wa tano na wa nane, yaani ‘kibuyu’ imetafsiriwa kama ‘container’, na wakati huohuo mfano wa namba nane ambao ni ‘kibuyu kidogo cha dawa’ umetafsiriwa kama ‘a small calabash’. Mifano hii inaonesha kuwa hakuna ushikamani wa maana baina ya
matini chanzi na matini lengwa. Ukosefu wa ushikamani wa maana unasababisha maana ya dhana ya msingi ya kiutamaduni kupotea katika tafsiri na kuleta utata katika maana ya matini chanzi na matini lengwa. Hadhira lengwa itashindwa kupata dhana na maana halisi ya maneno haya. Katika makala haya inapendekezwa kuwa neno ‘kibuyu’ litafsiriwe kama ‘gourd’ na siyo ‘container’ kwa sababu
‘container’ katika lugha lengwa linabeba dhana tofauti na kibuyu.

Hivyo kutafsiri ‘kibuyu’ kama ‘container’ na wakati huohuo kutafsiri neno ‘kibuyu’ kama ‘calabash’ huleta utata wa maana na uhamishaji wa maana ya msingi.
Utata wa Maana
Utata wa maana ni miongoni mwa matatizo ambayo yamejitokeza katika tafsiri ya matini za kitalii. Mifano ifuatayo inaonesha maneno yenye utata wa maana na ujumbe. Kwa mfano, kibuyu kimetafsiriwa kama ‘container’ na wakati huohuo neno ‘kata’ limetafsiriwa kama ‘water container’. ‘Kijiko’ kinatafsiriwa kama ‘spoon’ na ‘upawa’ umetafsiriwa kama ‘spoon’. Ukichunguza mifano hiyo, utaona pia kunautata wa maana ambapo neno moja linatumika kutafsiri maneno zaidi ya moja. Matumizi ya kisawe ‘container’ yanaleta utata wa maana na kupoteza dhana ya msingi ya maneno hayo.
Upanuzi wa Maana
Upanuzi wa maana ni kitendo cha kulipa neno au maneno maana ya ziada. Maana ya ziada huweza kujitokeza wakati wa kutafsiri matini za kitalii kutoka katika lugha chanzi kwenda katika lugha lengwa. Maana ya ziada huathiri dhana, ishara na ujumbe unaobebwa na neno hilo. Maneno hubeba dhana, ishara na ujumbe wa neno kulingana na utamaduni unaohusika. Hivyo basi, maana ya ziada inayopewa neno hilo katika lugha ya matini chanzi huathiri asili ya neno na pia hudondosha sifa za kiisimu na kiuamilifu za neno hilo. Uziada huu pia huathiri upokezi na utambuzi wa ujumbe kwa hadhira kwa sababu hadhira haipati mtekenyo ulio sawa wa ujumbe.
Mifano ya maneno na sentensi zifuatazo ambazo zilibainishwa katika lebo zinaonesha na kudhihirisha upanuzi wa maana unavyojitokeza katika tafsiri ya matini za kiutamaduni katika utalii.
[Image: SAM_6.JPG]
Mifano iliyotolewa katika jedwali namba 5a, inaonesha kuwapo kwa uongezaji wa maneno ambayo hayapo katika lugha chanzi lakini yanajitokeza katika lugha lengwa. Uongezaji wa neno ‘aid’ (msaada) ambalo halipo katika matini chanzi linatoa ujumbe wa ziada ambao
haupo katika matini chanzi. Ujumbe wa ziada huweza kuathiri ujumbe wa matini chanzi.
[Image: SAM_5.JPG]
Katika jedwali namba 5b, tunaona kuwa kuna uziada wa maneno ambao unatokea katika matini lengwa. Uziada huu unaathiri taarifa za kiutamaduni za matini chanzi ambazo ni shughuli zinazofanywa na jamii hii. Mfano uongezaji wa shughuli kama vile ‘basketry’ yaani ‘usukaji wa vikapu’. Shughuli hii haijaelezewa katika matini chanzi.
Hivyo uongezaji wa shughuli ambazo hazipo katika matini chanzi ni upanuzi wa taarifa za matini chanzi ambazo huathiri taarifa za kiutamaduni za jamii husika. Mfano mwingine ni huu ufuatao:
[Image: SAM_4.JPG]
Katika mfano huo, tunaona kuwa tafsiri ya neno ‘Agriculture’ kurejelea shughuli za kilimo zilizoainishwa katika matini chanzi ni la jumla sana. Kila jamii hushughulika na kilimo cha mazao tofauti na jamii nyingine kulingana na jiografia ya eneo linalohusika. Hivyo, matumizi ya neno ‘agriculture’ yanapanua maana na ujumbe
wa matini chanzi na kuleta pia utata katika utambuzi wa ujumbe. Je, jamii hii hujishughulisha na kilimo cha mazao ya aina zote? Vilevile, matumizi ya neno ‘livestock keeping’ ni ya jumla sana. Hata hivyo, uziada huu unaotokana na tafsiri jumuishi unaathiri ujumbe wa matini chanzi kwa sababu ukichunguza matini chanzi imebainisha mazao na mifugo mahususi.
Ufinyu wa Maana
Ufinyu wa maana hutokea pale ambapo neno huwa na maana finyu katika lugha lengwa tofauti na maana ya matini chanzi. Aidha, katika maneno, vishazi ama sentensi hutafsiriwa kwa ufinyu wake na hivyo kulifanya neno, kishazi ama sentensi kuwa na maana finyu
katika lugha lengwa tofauti na ilivyo katika lugha chanzi. Ufinyu wa maana huathiri tafsiri kwa sababu matini lengwa huwasilisha ujumbe tofauti na matini ya utamaduni chanzi. Hivyo basi, athari hii huweza kusababisha hadhira lengwa kutokuelewa maana na hivyo kuathiri mawasiliano katika utalii. Mifano ifuatayo inaonesha maneno ambayo yametafsiriwa kwa maana finyu: Mfano namba 1 katika jedwali hapo juu tunaona kuwa matini chanzi imetafsiriwa kwa mstari mmoja na tafsiri hiyo tunaona maana na ujumbe wa matini chanzi umefinywa. Ufinyu wa maana unasababisha athari za kiutamaduni kwa sababu dhana za kiutamaduni na taarifa muhimu za kaida mila na desturi za jamii ya matini chanzi hupotea. Katika mfano namba 2, kuna ufinyu wa maana ambapo taarifa zilizopo katika matini chanzi, zimedondoshwa. Kwa mfano, kifungu cha maneno “mchezo huu uliwasaidia vijana kuwa na shabaha na hivyo kuweza kupiga wanyama kwa ajili ya kitoweo” kimedondoshwa na hivyo dhana nzima ya ujumbe wa utamaduni chanzi imepotea. Katika mfano huu, taarifa muhimu ya namna mchezo huo ulivyowasaidia vijana imedondoshwa katika matini lengwa. Hivyo basi, udondoshaji huu unaifanya hadhira lengwa kukosa taarifa za umuhimu wa mchezo wa kulenga shabaha kwa jamii.
[Image: SAM_3.JPG]
Mfano katika jedwali namba 6b unadhihirisha udondoshaji wa neno ‘zawadi’ ambalo lipo katika lugha chanzi lakini halipo katika lugha lengwa. Udondoshaji wa neno hili unaathiri taarifa ya ujumbe wa matini chanzi.
 Matatizo ya Kiutamaduni
Tatizo kubwa linaloweka kipingamizi katika tafsiri ni tafsiri ya dhana mahususi za kiutamaduni. Lugha chanzi inaweza kuelezea dhana ambayo haijulikani kabisa katika lugha lengwa. Utamaduni unaelezwa na Newmark (1988) kuwa ni mkusanyiko wa mila na desturi za jamii inayotumia lugha moja mahususi kama njia yake ya mawasiliano. Wanjara (2011) anasema lugha zinatofautiana sana kiutamaduni na hili ni tatizo kubwa sana kwa mfasiri hata kuliko tofauti za kiisimu. Baker (2000:20) anasema ukosefu wa ulinganifu katika kiwango cha utamaduni husababisha ukosefu wa ulinganifu katika kiwango cha neno, hasa ikiwa lugha lengwa haina ulinganifu wa moja kwa moja wa neno linalojitokeza katika matini chanzi. Matatizo ya utamaduni huweza kujitokeza katika viwango viwili ambavyo ni: tatizo la kutafsiri majina kutoka lugha chanzi kwenda lugha lengwa na tatizo la kutafsiri dhana za kiutamaduni kutoka lugha chanzi kwenda lugha lengwa.
Tatizo la Kutafsiri
Majina Katika utafiti huu ilibainika kuwa tafsiri ya majina ya vitu ama vifaa vya kiutamaduni vilivyopo Makumbusho vina changamoto kubwa. Hii ni kwa sababu kila jamii huelewa vitu na kuvipa majina kulingana na uelewa na namna wanavyofasili ulimwengu unaowazunguka. Mifano ifuatayo inaonesha maneno ambayo yametafsiriwa kama yalivyo kutoka lugha ya Kiswahili kwenda lugha ya Kiingereza:
[Image: SAM_2.JPG]
Chanzo: Matini za kitalii Kijiji cha Makumbusho, Dar es Salaam, Mei-Oktoba, 2012 Ukichunguza mifano iliyopo katika jedwali namba 7, utaona kuwa maneno ya lugha ya Kiswahili yametafsiriwa kama yalivyo katika lugha lengwa. Hii inadhihirisha kwamba ni vigumu kupata visawe rejelezi vinavyorejelea majina ya lugha chanzi katika lugha lengwa kwa sababu kila jamii huwa na maneno ama majina ya vitu kulingana na utamaduni wa jamii mahususi. Makala haya yanapendekeza kwamba, maneno hayo yatafsiriwe kwa kuhamisha neno kama lilivyo na kulitolea ufafanuzi kulingana na jinsi linavyoeleweka katika utamaduni chanzi. Tazama mifano ya tafsiri inayopendekezwa katika jedwali namba 7b hapa chini:
[Image: SAM_1.JPG]
Jedwali namba 7b hapo juu linaonesha mifano ya kutafsiri matini zilizojikita katika uelewa wa utamaduni mahususi. Mbinu hii ya tafsiri inatambulika kama mbinu ya uasilishaji na ufafanuzi wa visawe. Kwa kutumia mbinu hii hadhira lengwa itaweza kuelewa kwa urahisi zaidi maana, ujumbe, dhima na namna neno hilo linavyotumika katika utamaduni chanzi.

6.0 Mapendekezo Makala haya yanapendekeza kwamba katika kutafsiri matini za kitalii mfasiri anahitaji kuwa na stadi, ujuzi, maarifa ya nadharia na mbinu za tafsiri. Hii itamsaidia kutafsiri matini za kitalii kwa kuzingatia nadharia na mbinu za tafsiri. Kuteua mbinu iliyo bora kutafsiri matini za kitalii kutamsaidia katika uteuzi wa visawe mwafaka kulingana na aina ya maneno aliyonayo katika matini. Aidha, inapendekezwa kwamba ni muhimu kwa mfasiri kuwa na ujuzi na uwezo wa lugha chanzi na lugha lengwa. Ili mfasiri
aweze kutafsiri matini za kitalii ni vema akawa na ujuzi wa lugha zote mbili. Kwa kufanya hivi mtafiti ataweza kuepuka makosa na matatizo ya kiisimu katika tafsiri ya matini za kitalii. Vilevile, mfasiri anatakiwa kuwa na ujuzi na maarifa ya utamaduni chanzi na utamaduni lengwa. Maarifa haya yatamsaidia kuelewa maana za kiishara na za ziada zinazobebwa na neno la utamaduni chanzi na kulihusianisha na neno la utamaduni lengwa.

Hivyo basi, itakuwa rahisi kwa mfasiri kutafsiri matini chanzi kwenda katika matini lengwa. Mfasiri anapokuwa na maarifa hayo, ataweza kuteua mbinu mwafaka za kutafsiri matini ya kiutamaduni kulingana na maarifa na ujuzi alionao kuhusu maana na ujumbe wa
matini hiyo katika utamaduni chanzi na utamaduni lengwa. Makala haya yanapendekeza kwamba, mfasiri anapokumbana na maneno ambayo yamejikita katika utamaduni mahususi na maana zake zinaeleweka kwa jamii mahususi, ni vema kutumia mbinu ya uasilishaji na ufafanuzi wa visawe. Mbinu hii inampa nafasi mfasiri kutafsiri neno kama lilivyo na kulitolea ufafanuzi kuhusu maana, dhima, ujumbe na jinsi linavyotumika katika utamaduni chanzi.
Hitimisho
Makala haya yamejadili juu ya matatizo ya kutafsiri matini za kitalii na kutoa mapendekezo ya namna bora ya kukabiliana na matatizo hayo ili kuwa na ufanisi wa mawasiliano. Imebainika kuwa, tafsiri ya matini za kitalii huwa na matatizo ya kiisimu, kimaana na kiutamaduni. Kutokana na matatizo hayo baadhi ya matini za kitalii
zinashindwa kufikisha ujumbe sahihi kwa hadhira lengwa na hivyo kusababisha matatizo ya kimawasiliano. Matatizo hayo pia yanasababisha ukosefu wa ushikamani wa maana na ujumbe baina ya matini chanzi na matini lengwa. Kwa maana hiyo, hadhira lengwa hushindwa kupata ujumbe asilia uliokusudiwa na matini chanzi. Aidha, makala haya yanajadili kwamba, kulingana na nadharia ya Skopos tafsiri ya matini za kitalii hutafsiriwa kwa lengo maalumu ambalo ni kufikisha taarifa za kitalii zilizopo katika jamii chanzi. Hivyo basi, ili kufikia lengo hilo makala haya yanapendekeza kwamba, mfasiri wa matini za kitalii lazima awe na ujuzi na maarifa ya kutosha katika tafsiri, nadharia na mbinu, ujuzi wa lugha chanzi na lugha lengwa pamoja na uelewa na ufahamu kuhusu utamaduni chanzi na utamaduni lengwa. Aidha, makala haya yanapendekeza kwamba, matini za kitalii hasa zilizojikita katika utamaduni wa jamii mahususi zitafsiriwe kwa kutumia mbinu ya uasilishaji na ufafanuzi wa visawe. Mbinu hii itasaidia kuweka bayana maana, ujumbe, dhima na matumizi ya neno hilo katika utamaduni wa jamii mahususi. Kwa kufanya hivi, hadhira lengwa wataweza kuelewa neno hilo kwa urahisi na upana zaidi na hatimaye kuwa na tafsiri bora zenye kusababisha ufanisi wa mawasiliano katika maeneo ya utalii.
 MAREJELEO
Baker, M. and Malmakjae, K. (2005). Routledge Encyclopedia of Translation Studies. London: Tylor & Francis Group.

Baolong, W. (2009). “Translating Publicity Text in the Light of the Skopos Theory: Problems and Suggestions” katika Translation Journal Volume 13, Na. 1, uk. 29-50.

Benavides, C. and Fletcher C. (2001). Tourism Principles and Practice. New York: Longman.

Bennett, T. (1995). The Birth of The Museums London. London: Routledge.

Catford, J.C. (1965). A Linguistic Theory of Translation. London:

Oxford University Press. Matatizo ya Tafsiri katika Matini za Kitalii Nchini Tanzania

Gentzler, E. (2001). Contemporary Translation Theories. London and New York: Routledge.

House, J. (2009). Translation. Oxford: Oxford University Press.

Kihore, Y. M. (1989). Isimu na Tafsiri Kutoka na Kuingia Katika Lugha za Kiafrika. Makala za Kongamano Kuhusu Matatizo ya Tafsiri Barani Afrika. Dar es Salaam: WAFASIRI, 24-35, “Uzingativu wa Sarufi katika Tafsiri” Swahili Forum, 12, uk. 109-120

Lauscher, S. (2000). Translation Quality Assessment: Where can Theory and Practice meet? The Translator, Juzuu Na. 6, (2), uk.149-168

Mohammad, R.T. (2010). ‘Cultural Issues in the Transalation of Tourist Guidebooks in Iran: Problems and Solutions from a Skopos Theory Pespective’. Translation Journal, Vol. 4 retrieved on July 2011 from http://www.translationdirectory.com/article2183.php

Mwansoko, H.J.M. (1996). Kitangulizi cha Tafsiri: Nadharia na Mbinu. Dar es Salaam:TUKI.

Nan, C. (2005). A Talk on Translation of Tourism Advertisement. Unpublished Master Thesis. Foreign Language College, Zhejiang Wan Li University.

Nan, C. (2005). A Talk on Translation of Tourism Advertisement. Tasnifu ya Umahiri (Haijachapishwa). Chuo cha Lugha za Kigeni. Chuo Kikuu cha Zhejiang Wan Li.

Newmark. P. (1988). A Textbook of Transaltaion. London: Prentince Hall.

Ndlovu, V. (2000). ‘Translating Aspect of Culture in “Cry, The Beloved Country in Zulu’ Language Matter, 31: 1, kur. 72-102

Nida, E. A. (2001). Language and Culture: Context in Translating. Shanghai: Shanghai Foreign Language Ed Press

Nida, E. A. and Taber, C. (1969). Theory and Practice of Translating. Leiden: Brill.

Ngozi, I.S. (1992). “The Role of translation in literature in Kiswahili and its problems”. Federation of international des traducteurs (FIT)
Newsletter, vol. X1, No. 1-2: kur 63-67.


Nord, C. (1991a). “Skopos, Loyalty and Translational Conventions” Target, 3 (1): 91- 109
______ (1991b). The Analysis in Translation. Amsterdam: Rodopi.
 Matatizo ya Tafsiri katika Matini za Kitalii Nchini Tanzania
______ (1997). Translating as a Purposeful Activity: Functionalist Aproaches explained. Manchester: st. Jerome.
_____ (2001). Translating as a Purposeful Activity-Functionalist Approaches Explained. Shanghai: Foreign Language Education Press.

Ordudary, M. (2007). “Translation Procedures, strategies and methods” Translation Journal. Vol.11,no.3 Availale at www.translationdirectory (retrieved 17th June 2011).

Reiss, K. na Vermeer, H. (1984). Groundwork for a General Theory of Translation. Tubingen: Niemeyer.

Sanning, H. (2010). Lost and Found in Translating Tourist Texts. The Journal of Specialized Translation, Juzuu Na. 13, uk. 124-137.

Smecca, P.D. (2009). ‘Tourist Guidebooks and The Image of Sicily in Translation’ katika Perspective, volume 17, issue 2, uk. 109-119.

Su-zhen, J. (2008). Skopos Theory and Translating Strategies of Cultural Elements in Tourism Texts. Retrieved July 21, 2010 from http://www.linguisti.org.n/doc/su20080906.pdf

TUKI. (2004). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. (2nd ed). Nairobi: Oxford University Press.

Venuti, L. (2008). The Translator’s Invisibility: A History of Translation (2nd ed): Routledge 2 Park Square, Milton Park Abingdon, Oxon Ox 14 4RN.

Vermeer, H. (1989a). ‘Skopos and Commission in Translational Action’ katika

Chesterman, A (Ed). Readings in Translation Theory. Pp 99-104.

Wamitila, K. W. (2003). Kamusi ya Fasihi Istilahi na Nadharia. Nairobi: Focus Books.

Wanjala, F. S. (2011) Misingi ya Ukalimani na Tafsiri kwa Shule, Vyuo na Ndaki: Mwanza: Serengeti Educational Publishers (T) LTD.

Chanzo&t&t&t&t&t&t&t&t]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T10:20:22Z 2021-06-28T10:20:22Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=340 <![CDATA[MASWALI YA TAFSIRI NA UKALIMANI (KENYA]]> CHUO KIKUU CHA MAASAI MARA
 
UNIVERSITY EXAMINATIONS 2014/2015
                                                                                                          
REGULAR EXAMS (MAY-AUGUST, 2015)
 
MAIN EXAM
 
SCHOOL OF ARTS AND SOCIAL SCIENCES
 
DEPARTMENT OF LANGUAGES & LITERATURE
COURSE TITLE: THEORY AND PRACTICE OF TRANSLATION AND INTERPRETATION II
 
COURSE CODE: BKS 221
 
MUDA: SAA 2
MAAGIZO:
JIBU SWALI LA KWANZA NA MENGINE MAWILI
1a) Tofautisha tafsiri na ukalimani    (alama 8)
  1. b) Fafanua sifa za mfasiri bora (alama 4)
  2. c) Eleza hatua mbili kuu za kufasiri kwa mashine (alama 4)
d)Onyesha majukumu ya nadharia ya tafsiri  (alama 8)
  1. e) Eleza dhana zifuatazo:
  2. i) Nadharia ya kisemantiki (alama 3)
  3. ii) Nadharia ya Usuluhishi (alama 3)
  4. Tafsiri kwa Kiswahili makala A (alama 20)
  5. Tafsiri kwa Kiingereza makala ya B (alama 20)
  6. Jadili nadharia ya mawasiliano katika tafsiri ilivyodokezwa na Peter Newmark.  (alama 20)
  7. Onyesha uhusiano wa nadharia ya tafsiri na taaluma nyingine (alama 20)
Makala A
NINA:  Jusper, where were you?
JUSPER:  Serving the nation.
NINA:  How could you desert your brother?
JUSPER:  It was an order.
NINA:  What order? You take off that thing and go and put on something descent. The others will soon be here.
JUSPER:  Is Regina with them?
NINA: Perhaps.
JUSPER:  Girlfriend number one; she ought to come.
NINA:  She’s far away in the city. Where is your father?
DOGA:  (Whispering rather loudly.) Do not detain him. Let him go.
JUSPER:  He can’t go; he is dead.
NINA:  My son, please go and put on a clean shirt.
JUSPER:  A clean shirt? No. Not after the murder.
NINA: What shall we do now? The illness creeps back on him. Jusper , do you know what  day today is?
DOGA:  Don’t remind him.
JUSPER:  Come and see for yourself. (Points at the crack.) Do you see this river, all this water? I threw him in there. Don’t tell me he swam away, because he didn’t. He was dead when I threw him there.
NINA:  He thinks he has killed you. Please do something before he spoils the ceremony.
DOGA: I told you to shut that mouth!
JUSPER:  Alright, I will shut up. Nobody need know am a murderer. (throws the sticks away.) After all, it was great fun. Now I know how they feel when they do it. Shall I go and confess I did it?
NINA: Yes my son, go and put on a clean shirt and then you can confess.
JUSPER:  Do you think they will harm me if I address the rally?
NINA:  No, they won’t. Just go and put your shirt first.
JUSPER:  Will they put him in a government coffin, do you think?
NINA:  Good God, what shall we do?
JUSPER:  I will go and recommend a government coffin with many handles so that everybody will help lower him into the grave. (He smiles, stands at attention, salutes, then exits, military style.)
NINA:  He has never behaved like this before.
DOGA:  His eyes were full of sleep.
NINA: Why did he think he had killed you?
DOGA:  It was his brother he thought he had killed.  I saw him address the grave as if Adika sat right on top of it. It was both strange and frightening.
Makala B
Kwa muda mrefu, kumejitokeza majaribio yanayolenga katika kuieleza lugha pasina mafanikio makubwa hadi pale ilipoanza kutumika mikabala ya kisayansi. Mikabala ya kisayansi ikawa mihimili na misingi dhabiti ya kuichunguzia lugha. Wataalamu mbalimbali wameeleza maana ya isimu, mathalan Besha(1994)ambaye anaifafanua isimu kama taaluma ambayo inachunguza na kuweka wazi kanuni ambazo ni msingi wa kila lugha. TUKI (1990) wanaeleza kuwa isimu ni sayansi ya lugha. Basi, tunaweza kusema kuwa isimu ni taaluma inayohakiki lugha kisayansi. Isimu ni sayansi ya matamshi,maumbo,miundo,maana na matumizi ya lugha.
Taaluma hii hutumia mtazamo wa kisayansi katika kuichambua lugha kinyume na ilivyokuwa hapo zamani ambapo watafiti waliathiriwa na hisia na mielekeo yao. Taaluma hii hujaribu kujibu maswali mbalimbali kuhusu lugha.Maswali haya ni pamoja na: Lugha ni nini? Lugha hufanyaje kazi? Huwa unajua nini unaposema unajua lugha fulani? Je, lugha ni sifa ya binadamu pekee? Lugha ya binadamu hutofautianaje na mawasiliano ya wanyama? Asili ya lugha ni ipi? Kwa nini kuna lugha nyingi? Lugha hubadilikaje? Watoto hujifunzaje lugha? Je, lugha na lahaja fulani ni rahisi kuliko nyingine? Mtu huandikaje na kuchanganua lugha isiyokuwemo kwenye maandishi?
Wataalamu ambao wanashughulikia haya masuala kuhusu lugha huitwa wanaisimu. Mwanaisimu ni mtu anayechunguza lugha kisayansi kwani ana ujuzi wa kanuni zinazoitawala lugha. Mwanaisimu huichanganua na kuieleza lugha kwa kurejelea matukio ya kiisimu kama vile mfumo wa irabu na muundo wa vitenzi vilivyoko katika lugha. Labda swali tunaloweza kujiuliza hapa ni: je malengo ya isimu ni yepi? Suala hili linashughulikiwa katika sehemu inayofuata.
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T10:11:29Z 2021-06-28T10:11:29Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=339 <![CDATA[TAFSIRI NA UKALIMANI (SLIDES)]]>

.pdf   TAFSIRI-NA-UKALIMANI.pdf (Size: 1.13 MB / Downloads: 11) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T09:06:19Z 2021-06-28T09:06:19Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=338 <![CDATA[MCHANGO WA KAZI ZILIZOTAFSIRIWA KATIKA KUENDELEZA LUGHA NA FASIHI YA KISWAHILI]]>

.pdf   MCHANGO_WA_KAZI_ZILIZOTAFSIRIWA_KATIKA_K.pdf (Size: 297.35 KB / Downloads: 4) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T08:56:20Z 2021-06-28T08:56:20Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=337 <![CDATA[UZINGATIFU WA SARUFI KATIKA TAFSIRI]]>

.pdf   UZINGATIFU-WA-SARUFI-KATIKA-TAFSIRI.pdf (Size: 131.64 KB / Downloads: 1) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T08:45:12Z 2021-06-28T08:50:04Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=336 <![CDATA[Tathmini ya Hatua za Tafsiri kama Nyenzo ya Ufanisi wa Mawasilino]]>

.pdf   TATHMINI-YA-HATUA-ZA-TAFSIRI.pdf (Size: 501.56 KB / Downloads: 4) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-28T08:39:08Z 2021-06-28T08:39:08Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=335 <![CDATA[TAFSIRI NA UKALIMANI (VIDEO)]]> BOFYA HAPA &t&t&t&t&t]]> false MwlMaeda]]> 2021-06-26T11:27:21Z 2021-06-26T11:27:21Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=284 <![CDATA[TATHIMINI YA MATINI ILI KUTAMBUA UBORA NA UDHAIFU WAKE KATIKA TAFSIRI]]> BOFYA HAPA CHINI KUFUNGUA &t&t&t&t&t


.pdf   TATHIMINI YA MATINI ILI KUTAMBUA UBORA NA UDHAIFU WAKE KATIKA TAFSIRI.pdf (Size: 153.4 KB / Downloads: 8)
]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-19T10:12:26Z 2021-06-19T10:12:26Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=136 <![CDATA[TAFSIRI INAVYOKUZA NA KUSAMBAZA FASIHI]]>
.pdf   TAFSIRI INAVYOKUZA NA KUSAMBAZA FASIHI.pdf (Size: 179.51 KB / Downloads: 4) ]]>
false
MwlMaeda]]> 2021-06-18T10:16:30Z 2021-06-18T10:16:30Z https://jifunzekiswahili.co.tz/showthread.php?tid=115 <![CDATA[NI KWA JINSI GANI TAFSIRI HUSAIDIA KUKUZA NA KUSAMBAZA FASIHI?]]>
.pdf   NI KWA JINSI GANI TAFSIRI HUSAIDIA KUKUZA NA KUSAMBAZA FASIHI.pdf (Size: 148.66 KB / Downloads: 4) ]]>
false